<?xml version='1.0' encoding='UTF-8'?><?xml-stylesheet href="http://www.blogger.com/styles/atom.css" type="text/css"?><feed xmlns='http://www.w3.org/2005/Atom' xmlns:openSearch='http://a9.com/-/spec/opensearchrss/1.0/' xmlns:georss='http://www.georss.org/georss' xmlns:gd='http://schemas.google.com/g/2005' xmlns:thr='http://purl.org/syndication/thread/1.0'><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291</id><updated>2011-10-27T08:45:25.770-07:00</updated><category term='Politics'/><title type='text'>Fikra Pevu</title><subtitle type='html'></subtitle><link rel='http://schemas.google.com/g/2005#feed' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/posts/default'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default?max-results=100'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/'/><link rel='hub' href='http://pubsubhubbub.appspot.com/'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><generator version='7.00' uri='http://www.blogger.com'>Blogger</generator><openSearch:totalResults>44</openSearch:totalResults><openSearch:startIndex>1</openSearch:startIndex><openSearch:itemsPerPage>100</openSearch:itemsPerPage><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-2701391337476770184</id><published>2011-10-27T02:57:00.001-07:00</published><updated>2011-10-27T02:57:40.174-07:00</updated><title type='text'>Wako wapi Dk. Salim, Jaji Warioba?</title><content type='html'>Tanzania Daima Septemba 2011&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;NI jambo la kusikitisha na kukatisha tamaa kwamba, wananchi wa Jimbo la Igunga wamekuwa ni Watanzania wa kwanza kupatwa na dhoruba iliyoasisiwa nyuma ya dhana dhaifu na isiyo na mashiko ya kujivua gamba.&lt;br /&gt;Nasema ni jambo la kusikitisha na kukatisha tamaa kwa sababu, wakati wakazi wa Igunga wakishinikizwa kucheza mchezo huo mchafu ulioandamana na kila aina ya vurugu, mwasisi wa dhana hiyo, Rais Jakaya Kikwete anachanja mbuga ndani na nje ya nchi.&lt;br /&gt;Anafanya hivyo si kwa sababu nyingine yoyote eti kwa sababu akiwa mkuu wa taifa changa linalokabiliwa na kila aina ya changamoto, analazimika kubeba mizigo mizito yenye lengo la kutukwamua kutoka hapa tulipo leo. &lt;br /&gt;Ili kuonyesha kwa vitendo kwamba yeye ni mtu wa shughuli na mihangaiko mingi, mwasisi huyo wa dhana ya kujivua gamba ambaye baadhi ya wadadisi wanasema hata yeye mwenyewe ni gamba linalopaswa kuvuliwa, ndiyo kwanza amerejea kutoka ‘kwa mama’ nchini Marekani.&lt;br /&gt;Wakati Kikwete akiwa Marekani ambako pia alipata fursa ya kushiriki katika shughuli mbalimbali za msingi na zisizo na umuhimu au unyeti wowote kwa maendeleo ya nchi yetu, wakazi wa Igunga wamekuwa wakishuhudia kila aina ya vituko ambavyo kwa hakika vingeweza kuepukika iwapo tungekuwa na viongozi makini.&lt;br /&gt;Miongoni mwa matukio ambayo hayana tija kwa taifa hili ambayo yalihusisha ziara ya mkuu wa nchi hii Marekani ni pamoja na lile la kualikwa kwake kugonga kengele ya kuashiria mwisho wa uuzwaji wa hisa katika soko la Nasdaq lililoko New York.&lt;br /&gt;Lakini si hilo tu, tukio jingine ambalo nalo halikuwa na tija si kwa wananchi wa Igunga bali hata kwa taifa hili ni lile la Rais kukutana na kupiga picha na msanii wa muziki wa Hip Hop, 50 Cents anayekumbukwa kuwa miongoni mwa watu mashuhuri wachache waliokataa kumuunga mkono Barack Obama wakati wa harakati zake za urais wa Marekani mwaka 2008. &lt;br /&gt;Ni wazi kwamba, wakati mamilioni ya fedha ambazo zingeweza kuepukika yakimwagwa Igunga, Ikulu ya Kikwete inaweza ikawa imeshaanza kujipanga kuandaa vipindi vingine maalum ambavyo vitarushwa na kituo cha televisheni cha Shirika la Utangazaji la Taifa (BBC) vikionyesha mbwembwe za madaraka ya mkuu wa nchi akiwa ughaibuni.&lt;br /&gt;Ni jambo la kusononesha kwamba, viongozi wa CCM wakiwamo marais wawili na mawaziri wakuu sita wastaafu wote wanaotokana na chama hicho ambao ama ni wajumbe wa Kamati Kuu au Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho wako kimya au wanashangilia kile kinachotokea Igunga.&lt;br /&gt;Miongoni mwa viongozi wakuu wastaafu waliofunga midomo yao kwa staili ya kuonyesha ukomo wa fikra zao tangu Kikwete alipoiasisi dhana ya hovyo ya kujivua gamba ni Benjamin Mkapa.&lt;br /&gt;Wakati baadhi yetu tukifanya juhudi kubwa kutaka kujua mitazamo ya watu wa aina ya Mkapa katika dhana hii ghali kwa CCM na kwa taifa, kiongozi huyo huyo mstaafu akawa mtu wa kwanza tena kwenda Igunga kuzindua kampeni za chama hicho.&lt;br /&gt;Mkapa ambaye hakuna shaka alikwenda Igunga kuweka udongo katika kaburi la CCM akaandamana katika harakati zake hizo hadi jukwaani na mwanasiasa aliyelazimishwa kujiuzulu ubunge wa jimbo hilo hilo la Igunga, Rostam Aziz.&lt;br /&gt;Kitendo alichokifanya Rostam cha kuisaliti nafsi yake yeye mwenyewe tena mbele ya wananchi wale wale ambao aliwaaga siku siku chache tu kabla, kilikuwa kikipalilia kisanii fikra nyepesi zilizofinyangwa ndani ya dhana ya kujivua gamba.&lt;br /&gt;Ni jambo lisiloingia akilini hata kidogo kwa mtu aliyeshika madaraka ya urais kwa miaka 10 na anayelindwa na katiba kwa kiwango cha Mkapa, awe ni mtu wa kwanza kulisaliti taifa na kukubali kuona wananchi wa Igunga wakibebeshwa mzigo mkubwa wa gharama za kampeni katika mazingira ambayo yangeweza kuepukwa.&lt;br /&gt;Udhaifu wa maamuzi ya Mkapa na Rostam wa kuunga mkono upuuzi wa chama chao wa kutojali gharama kubwa za kuendesha kampeni Igunga kwa namna moja au nyingine unaonekana kuwatafuna viongozi wengine wastaafu ambao wanao wajibu wa kuliokoa taifa nyakati ngumu kama hizi.&lt;br /&gt;Katika orodha hii wamo Mzee Ali Hassan Mwinyi, Jaji Joseph Warioba, Dk. Salim Ahmed Salim, Cleopa Msuya, Frederick Sumaye, Edward Lowassa na John Malecela.&lt;br /&gt;Ukimwacha Lowassa ambaye bado anakabiliana na jinamizi la Kikwete la kujivua gamba, viongozi hao wakuu wastaafu nao wamejikuta wakiishia kuwa ama mateka, majeruhi au mashabiki wa mchezo huo mchafu ambao leo unaitesa Igunga.&lt;br /&gt;Nitakuwa mnafiki kwa dhimiri yangu, iwapo nitakaa kimya pasipo kuwasuta viongozi hao ambao naamini wangekuwa watu madhubuti na wanaojali maslahi ya Watanzania kabla ya yale ya matumbo na nafsi zao wangekuwa wameshaweza kudhibiti maamuzi kadha wa kadha ya kipuuzi yanayotolewa na viongozi wanaotokana na chama chao leo. &lt;br /&gt;Ni kichekesho cha fedheha kuona viongozi wastaafu wenye hadhi za kimataifa kama Dk. Salim au Jaji Warioba wakikaa kimya wakati vyama vya siasa vikilazimika kurusha helikopta nne angani kwa ajili ya kutafuta mrithi wa Rostam Igunga, katika kipindi kisichozidi miezi 12 tangu kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu.&lt;br /&gt;Hivi kuna haja gani kuwa na chama tawala ambacho viongozi wake walio madarakani na wale waliostaafu wanashindwa kutoa maamuzi sahihi na kwa wakati muafaka?&lt;br /&gt;Kama Kikwete na jopo kubwa la viongozi wastaafu walishindwa kubaini kwamba Rostam ni gamba miezi 12 tu iliyopita, wanawezaje kutuvusha miaka mine ijayo?&lt;br /&gt;Viongozi wa CCM wana bahati kubwa kwamba, wananchi wa Igunga wameingizwa katika mtego ambao laiti kama wangejua kuwa aliyewatega ndiyo hao hao wanaorusha helikopta mbili leo, wasingeendelea kufanya kosa lile lile la kurudisha jina la mgombea wa chama kile kile.&lt;br /&gt;Ni katika mazingira ya siasa za kinafiki kama hizi ndiyo maana baadhi yetu tumekuwa siku zote tukiungana mkono na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere katika kuliombea taifa lipate upinzani madhubuti ili siku moja liponywe maradhi haya mabaya na yanayokuwa kila siku ya ombwe la uongozi.&lt;br /&gt;Hatuwezi kuwa na viongozi wasioona mbele. Tutakuwa ni taifa la watu wavivu wa kufikiri iwapo tutaendeleza hulka za kushangilia kila ujinga unaotendwa na viongozi eti tu kwa sababu wameshika mamlaka ya kuliongoza taifa hili.&lt;br /&gt;Wito wangu kwa viongozi wetu wastaafu ni kujifunza kutoka kwa Mwalimu Nyerere ambaye hata katika ustaafu wake alithubutu kujitokeza hadharani na kukabiliana na maamuzi aliyokuwa akiamini kuwa ni ya hovyo au ya makosa yaliyofanywa na viongozi waliokuwa madarakani baada yake.&lt;br /&gt;Ni ajabu kubwa kwamba wakati dhana ya kujivua gamba ikichochea mapambano ya udini na kutishia mshikamano na umoja wa kitaifa Igunga, viongozi wastaafu wa kitaifa wamekaa kimya huku wengine wakipigia debe maamuzi ya hovyo kabisa eti kwa sababu tu yana baraka za chama chao au kiongozi mkuu wa dola. Huku ni kukosa uzalendo. Huku ni kukosa ujasiri.&lt;br /&gt;Ni jambo la ajabu kabisa kwamba, Mkapa ambaye zama akiwa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM alikuwa mtu mwepesi kuhubiri ‘ukweli na uwazi’ na ‘ushupavu wa uongozi’ yeye mwenyewe ndiye anakuwa wa kwanza kwenda kinyume cha dhana alizozisimamia.&lt;br /&gt;Mkapa na wastaafu wenzake wanapaswa kutambua kwamba, matokeo ya kushindwa kwao kutimiza ipasavyo wajibu wao wa ulezi wa taifa yamezaa kizazi cha hovyo kabisa cha viongozi walio madarakani ambacho kimekuwa chachu kubwa kabisa katika ongezeko la vijana waliokata tamaa ambao wamekuwa wakijiingiza katika matendo mbalimbali hatarishi.&lt;br /&gt;Tabia yao hii ya viongozi wetu kufurahia ustaafu wao huku wakifikiri kwamba wajibu wao unaishia tu katika kuishangilia serikali au chama chao hata katika mambo yanayoligharimu taifa kama haya ya sasa ya Igunga haipaswi kuachwa yakapita hivi hivi tu.&lt;br /&gt;Ukimya na wakati mwingine hulka za kishabiki za viongozi wakuu wastaafu ambao sijui kama unatokana na udhaifu wao wa kuona mambo, uchovu wao wa kimwili au kiakili au kutotaka kwao kushiriki katika mienendo ya kisiasa au kiuongozi ndiyo ambao umeongeza ukubwa wa ombwe la uongozi katika taifa.&lt;br /&gt;Wazee hawa wanapaswa kutambua kwamba, matokeo ya ukimya wao au hulka za baadhi yao kushabikia mambo yameipa fursa CCM ya Kikwete ianze mapema kuendesha harakati za urais wa mwaka 2015 kwa staili ya kuchafuana, kupakana matope, kuumbuana na kuzushiana.&lt;br /&gt;Mbegu ya siasa za uhasama ambayo imeota na matawi yake kuanza kuonekana waziwazi huko Igunga inapaswa kuwa kichocheo cha kwanza cha kuwatoa mafichoni wazee wetu hao na kulikemea kwa nguvu kubwa vuguvugu la chuki lililozalishwa na CCM ya Kikwete.&lt;br /&gt;Wazee hao wanapaswa kutambua kwamba, ni jambo la bahati kubwa kwa CCM kwamba, angalau inapata fursa ya kutunisha misuli Igunga leo hii kwa sababu tu ya kuwapo kwa ushindani mkali kati ya wagombea wawili wa vyama vya upinzani vya Chadema na CUF.&lt;br /&gt;Ni wazi kwamba turufu pekee ambayo CCM wanajaribu kuitumia ili kushinda uchaguzi mdogo wa Igunga leo si ushawishi wa hoja za mgombea wao, au kupendwa na kuaminiwa kwao na wananchi, bali matumaini ya mgawanyiko mkubwa wa kura kati ya vyama vya Chadema na CUF.&lt;br /&gt;Dalili za wazi kabisa za ushindani Igunga zinaonyesha pasipo shaka kwamba, siku nne kabla ya uchaguzi kufanyika, CCM ishinde au ushindwe imepoteza mvuto miongoni mwa vijana wengi wasomi na wale walio mitaani.&lt;br /&gt;Badala yake viongozi na makada wa chama hicho wanaoongoza harakati za kulibakisha jimbo hilo mikononi mwao wamejikuta wakilazimika kutumia nadharia za kihistoria, nguvu ya fedha na mamlaka ya dola waliyonayo katika kuvuta ushawishi miongoni mwa wapigakura. Zote hizi ni gharama za dhana ya Kikwete ya kujivua gamba.&lt;br /&gt;Mwisho&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-2701391337476770184?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/2701391337476770184/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=2701391337476770184&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/2701391337476770184'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/2701391337476770184'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2011/10/wako-wapi-dk-salim-jaji-warioba.html' title='Wako wapi Dk. Salim, Jaji Warioba?'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-300863743001035794</id><published>2011-10-27T02:54:00.001-07:00</published><updated>2011-10-27T02:55:25.287-07:00</updated><title type='text'>Maradhi ya zidumu fikra za mwenyekiti yanalitafuna taifa</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;HAKUNA shaka hata kidogo kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinaugua maradhi mabaya kabisa ya uongozi ambayo yamekuwa yakikitafuna chama hicho kwa miaka mingi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maradhi haya ya uongozi ambayo CCM inaugua hayakuanza leo na niseme wazi kabisa, hayakuanza wakati huu chama hicho kinapoongozwa na Rais Jakaya Kikwete ambaye ndiye mwenyekiti wake wa taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushahidi wa kihistoria unaonyesha kwamba, maradhi hayo ambayo yamepewa majina tofauti na wachambuzi mbalimbali, yalianza kukitafuna chama hicho wakati kikiongozwa na mwenyekiti wake wa kwanza, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbukumbu zinaonyesha kwamba, mara baada ya Nyerere kuamua kustaafu urais mwaka 1985 aliendelea kushikilia madaraka ya mwenyekiti wa CCM kwa takriban miaka mitano zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati akichukua uamuzi huo, kwa makusudi na kwa kutambua haja ya CCM kujijenga, alifanya ziara nchi nzima akisema anafanya hivyo kwa makusudi mahususi ya kukiimarisha chama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kwamba hatua ya Mwalimu na viongozi wenzake wa CCM wa wakati huo ilichangiwa kwa kiwango kikubwa na kubaini kwao kuwapo kwa nyufa na udhaifu wa kiuongozi ndani ya chama hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata baada ya kufikia hatua ya kuamua kustaafu uenyekiti wa chama hicho na kumwachia aliyekuwa rais wa wakati huo, Ali Hassan Mwinyi, Baba wa Taifa kwa nyakati tofauti alipata kutoa kauli ambazo zilikuwa zikitoa mwelekeo wa wazi uliokuwa ukionyesha kuwapo kwa kasoro kadha wa kadha za kiuongozi ndani ya chama hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miongoni mwa kauli hizo ni pamoja na zile za kukifananisha chama hicho na kokoro ambalo hutumiwa na wavuvi kuvua samaki kwa namna kukusanya kila takataka na wakati mwingine kusababisha uharibifu mkubwa kwa viumbe vinavyoishi majini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si hilo tu, baadhi ya wana CCM wanakumbuka namna Mwalimu alivyofikia hatua ya kusema maneno mazito ambayo yamebandikwa katika kuta za vyumba vya mikutano na ofisi za viongozi wa chama hicho tawala; ‘‘Bila CCM Madhubuti Nchi Itayumba’’.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbukumbu zinaonyesha kwamba, Baba wa Taifa alitamka maneno hayo wakati ule alipokuwa akikinyoshea kidole chama chake hicho hata kufikia hatua ya kukilaani, kukikea na hata kukaribia kabisa kukikana pale aliposema; “CCM si baba yangu wala mama yangu naweza kukihama”.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, hofu, wasiwasi na mashaka yaliyopata kuonyeshwa kwa nyakati tofauti na Baba wa Taifa kuhusu CCM, chama alichokiasisi na akakipigania kwa moyo wake wote havijapata kutoweka au kutafutiwa tiba ya kudumu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maradhi ambayo Baba wa Taifa alipata kuyasema kuwa yanakitafuna chama hicho yameendelea kubakia kama yalivyo na kwa bahati mbaya zaidi mengi kama si yote yamezidi kuota mizizi na kustawi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kwa sababu ya maradhi hayo ambayo Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ameyafananisha na saratani ya damu iliyosambaa katika mishipa, CCM imekuja na dhana mpya ya kujivua gamba iliyovuta hisia zenye ukinzani mkali wa hoja kutoka kwa wachambuzi tofauti wa masuala ya kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kuonyesha namna maradhi hayo yalivyokitafuna na yanavyoendelea kukidhoofisha chama hicho kwa kiwango cha kuwatia hofu viongozi wake, Rais Kikwete akaja na msamiati huo mpya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ili kuweza kujibu maswali ya wadadisi wa mambo wanaoisuta CCM wakisema inakabiliwa na tatizo kubwa la ombwe la uongozi, Kikwete akatumia mamlaka aliyopewa kuunda tume iliyojumuisha jopo la wataalam na wanazuoni wenye mapenzi mema na chama hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tume hiyo iliyojumuisha maprofesa na madaktari wa falsafa ikaongozwa na Wilson Mukama ambaye matokeo ya kazi waliyoifanya kwa muda wa wiki mbili kwa kujifungia katika hoteli moja kubwa ya nyota kadhaa yakamfanya ajikute akiukwaa ukatibu mkuu wa chama hicho.&lt;br /&gt;Matukio haya yote ni kielelezo cha wazi kwamba, maradhi yale yale ya uongozi ambayo yamekuwa yakikitesa chama hicho kwa miaka nenda, miaka rudi yameendelea kukitafuna pasipo kukoma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pasipo kujua au pengine kwa mhemuko wa madaraka, Kikwete ambaye ndiye mwenyekiti wa taifa wa chama hicho akajitwika mzigo mzito wa kuongoza harakati za kukinusuru chama chake.&lt;br /&gt;Huku akijua kuwa chama hicho kimelelewa katika misingi ya ‘zidumu fikra za mwenyekiti’ akajitwisha wajibu wa peke yake wa kuunda tume na kisha ili kuweza kukidhi utashi wake binafsi akajenga hoja ya kuwalazimisha wajumbe sekretarieti na wale wa kuchaguliwa wa kamati kuu kujiuzulu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yaliyofuata baada ya hapo sote tunayajua. Sekretarieti mpya ikaundwa huku nyuma na kwa siri ikibeba ajenda ya kuwalenga watu fulani fulani na wakati mwingine kupoza hasira za baadhi ya watu ambao angeweza kupata wakati mgumu kuwatupa kwa namna jongoo atupwavyo na mti wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kinara katika sekretarieti mpya akawa Mukama, mtu ambaye tume yake ilibeba ajenda ya kuwashughulikia watu ambao tangu Kikwete aingie madarakani wamejikuta wakipita katika karai la moto kinyume kabisa na matarajio makubwa waliyokuwa nayo miaka sita tu iliyopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna ile ile ilivyofanya kazi Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe miaka minne iliyopita, tume ya Mukama nayo ikawalenga watu wale wale na sababu zikiwa ni zile zile: Ufisadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jasiri haachi asili. Kikwete yule yule aliyepata kuwanyoshea kidole ‘marafiki’ zake akisema kwamba urais wake hauna ubia, akakunjua makucha ya mamlaka safari hii akielekeza mashambulizi kwa kundi la watu wale wale ambao miaka kadhaa tu iliyopita walikuwa sambamba katika harakati za kusaka madaraka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi yetu hatukupata shida kuelewa ni kitu gani kilikuwa kikitokea wakati tulipowasikia viongozi wapya wa CCM, Naibu Katibu Mkuu (Tanzania Bara), John Chiligati na Katibu wa Idara ya Uenezi na Itikadi, Nape Nnauye wakitangaza kile walichokiita Maazimio ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taarifa ambazo zilivuja miongoni mwetu hata kabla ya kuanza kwa kikao hicho cha NEC, zilikuwa zikieleza bayana kwamba, wembe ulikuwa ni kuwang’oa fulani na fulani ndani ya CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatukuwa na sababu ya kuuliza sababu za maamuzi hayo kuchukuliwa kwani sote tulijua fika kwamba, makusudi makubwa ya maamuzi hayo yalikuwa ni kinyang’anyiro cha urais cha mwaka 2015.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu tunaoufahamu utamaduni wa CCM wa kuhujumiana kisiasa na kulana wenyewe kwa wenyewe kama njia ya kupata madaraka katika taifa hili tukakumbushwa masahibu yaliyopata kuwakuta wanasiasa wa aina ya John Malecela, Frederick Sumaye, Dk. Salim Ahmed Salim na Iddi Simba wakati wa mchakato wa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo basi, tuliposikia walengwa wa safari hii wakiwa ni watatu tu, miongoni mwao wakiwa ni wale walioratibu ajenda za kuwamaliza wenzao mwaka 2005, tukaona tunao wajibu wa kuwaeleza wasomaji wetu kile ambacho kilikuwa kikiendelea ndani ya chama hicho tawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati tukijifanya kidomodomo kuusema ukweli huo mchungu, tukasahau ukweli kwamba nyuma ya ajenda hii ya leo, wako vinara wawili ambao ndiyo waliokuwa wapishi wakuu wa majungu yaliyowamaliza akina Salim, Simba, Sumaye na Malecela.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jambo baya zaidi, nyuma ya karata yetu hii ya kujifanya tukiwa vimbelembele kusimamia na kuutetea ukweli huu ulio bayana, tukajifanya tukiipuuza nguvu kubwa waliyonayo vinara wa mkakati huo ambao kinara wao ndiye mkuu wa kaya aliyeshika mpini wakati sisi tukiwa tumekamata makali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukweli kwamba wapishi wa ajenda hii walikuwa na timu kubwa ya makachero walio serikalini na walio idarani ukawa silaha kubwa ya kutujeruhi, baadhi yetu vibaya sana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huku wakijua kwamba tulikuwa tumeshang’amua janja yao ya kutafunana wenyewe kwa wenyewe kwa gharama za kufifisha turufu muhimu ya ushindi wa demokrasia ya vyama vingi iliyoanza kuchanua katika uchaguzi mkuu uliopita, makachero hao wa CCM na mawakala wao walio serikalini, wakaja na uzushi ule wa siku zote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa ustadi mkubwa huku wakitumia uzoefu wao wa kupindisha mambo, makachero hao wakafanikiwa kupenya katika mioyo ya baadhi ya viongozi wa kidini na wale wa vyama vya siasa vya upinzani ambao wakajikuta wakishangilia dhana isiyo na mashiko ya CCM kujivua gamba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Walipoona hilo halitoshi, wakarejea ndani ya vyumba vyetu vya habari na wakatumia udhaifu wetu wa kufikiri sawasawa kutulisha uzushi wao wakituaminisha kuwa ni wa kweli ukielekezwa kwanza miongoni mwetu na kisha miongoni mwa walengwa wakuu wa ajenda nzima ya kujivua gamba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, makachero hao wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa kulihadaa taifa kupitia vyombo vyetu vya habari na wakati mwingine kwa kuwatumia viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani ambao hawajui kuwa ile dhana ya zidumu fikra sahihi za mwenyekiti (wa CCM) imeshapenya ndani ya mioyo yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la kukatisha sana tamaa kwamba, japokuwa sote kwa ujumla wetu tunatambua vyema kuwa ajenda nzima ya kujivua gamba iliyoasisiwa na mwenyekiti wa taifa wa CCM ina harufu ya dhuluma, uonevu, kupakana matope na kuua ustawi wa mfumo wa vyama vingi bado tumeendelea kushangilia maamuzi hayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo yake makosa yetu hayo yamesababisha wanahabari tujikute tukiwa mavuvuzela wa ajenda ya kujivua gamba, tukipaza sauti na kuimwagia sifa lukuki pasipo kujua kwamba tunafanya hivyo kwa gharama za ustawi wetu wenyewe wa sasa na wa siku zijazo.&lt;br /&gt;Hitimisho la yote hayo linatufanya sote kama taifa, kwa kujua au kutojua tujikute tukiwa majeruhi wa dhana iliyopitwa na wakati ya zidumu fikra za mwenyekiti wa CCM pasipo kujali usahihi, malengo, makusudi na mwelekeo mzima wa kifalsafa wa fikra hizo. Hatupaswi kwenda huko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwisho&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-300863743001035794?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/300863743001035794/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=300863743001035794&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/300863743001035794'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/300863743001035794'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2011/10/maradhi-ya-zidumu-fikra-za-mwenyekiti.html' title='Maradhi ya zidumu fikra za mwenyekiti yanalitafuna taifa'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-471259956465583266</id><published>2011-10-27T02:43:00.000-07:00</published><updated>2011-10-27T02:45:11.270-07:00</updated><title type='text'>CCM inajiandalia anguko</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kwa mara nyingine tena kimechafua hali ya hewa kisiasa nchini, safari hii kikija na kauli mbiu tata ya kujivua gamba iliyoasisiwa, ikaratibiwa (waswahili wanasema – kimkandamkanda) na kuendeshwa kimafia na mwenyekiti wake wa taifa, Rais Jakaya Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sina shaka hata kidogo kwamba, wasomaji wazuri wa gazeti hili, wakawa wamepata picha halisi ya kile kilichotokea mjini Dodoma hivi karibuni kikianzia katika kikao cha Kamati Kuu (CC) na baadaye Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (NEC).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mchezo. Nauita mchezo kwa kuwa hauna tija wala matokeo yoyote ya mabadiliko ya kimfumo au kifalsafa, ulianza katika Kamati Kuu iliyoketi kwa siku mbili na kuhitimishwa na hatua ya Kikwete kumtumia mmoja wa wanasiasa wanaoheshimika, Abdulrahman Kinana kubeba ajenda yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ajenda katika mchezo huo wa kuigiza na uliokuwa umepangwa mapema kabisa, ilikuwa ni pendekezo la kuwalazimisha wajumbe wote wa sekretarieti na kamati kuu ya chama hicho kujiuzulu nafasi zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maelezo yasiyo ya kisayansi yaliyotolewa na ambayo tayari yalikuwa mitaani wiki mbili kabla ya kikao chenyewe yalikuwa na maelezo dhaifu: Kwamba wajumbe wa vikao hivyo viwili walikuwa wameshindwa kumsaidia Mwenyekiti wao, Rais Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu wenye akili zao ndani ya kikao hicho na nje, walijua fika kwamba, walengwa wakuu katika ajenda hiyo walikuwa ni aliyekuwa Katibu Mkuu, Yussufu Makamba, Rostam Aziz na Andrew Chenge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa muda mrefu hoja dhidi ya Makamba kwamba alikuwa ameshindwa kazi, ilikuwa mtaani muda mrefu na yeye mwenyewe mara kadhaa alishapata kujaribu bila mafanikio kuitolea ufafanuzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande wao, Chenge na Rostam walitakiwa kutemwa, lengo la kwanza likiwa ni kuifanya ile kauli aliyoitoa Rais Kikwete, Februari 5 mwaka huu wakati chama hicho kikisherehekea miaka 34 ya kuzaliwa kwake alipotumia kauli mbiu ya kujivua gamba ionekane ilikuwa halisi na yenye mwelekeo madhubuti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Panga lililowalenga wanasiasa hao watatu, kwa bahati mbaya au kwa kupangwa lilijikuta likimkumba pia Bernard Membe, mmoja wa wanasiasa waliokuwa wakiunda sekretarieti, akiwa Mkuu wa Idara ya Siasa na Mambo ya Nje na mjumbe pia wa Kamati Kuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatua ya Rais Kikwete kutolirudisha jina lake ili lipigiwe kura tena wakati alipokuwa akipendekeza majina mapya ya wajumbe CC baada ya ile ya kwanza kujiuzulu bado imeacha maswali mengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wako wanaoamini kwamba, msingi wa hatua hiyo ya Rais Kikwete ilikuwa ni kuwaweka kando wanasiasa wote ambao tayari walikuwa wameshaanza kukigawa chama katika misingi ya makundi ya urais wa mwaka 2015.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jina la Membe kama yalivyo majina ya wanasiasa wengine kama Profesa Mark Mwandosya, Emmanuel Nchimbi, Edward Lowassa, Samuel Sitta, Frederick Sumaye, Chikawe yanahusishwa na urais na hakuna hata mmoja miongoni mwao ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiliacha hilo na kurejea katika hoja ya ufisadi, ni wazi kwamba tuhuma dhidi ya Chenge na Rostam zilikuwa ni moja ya majibu rahisi yaliyokuwa yakificha maelezo halisi yanayokihusisha chama hicho na swali gumu linaloitaka CCM ieleze kwa kina ni kwa namna gani dhana hiyo nzima ya kujivua gamba itamaliza wingu hilo linalokitafuna chama hicho na serikali yake kwa miaka mingi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la kutia shaka sana kwamba, wakati akina Kikwete, Kinana na wenzao wakikuna vichwa juu juu kutafuta majibu ya haraka haraka ya kukinusuru chama chao na hatima iliyo wazi ya anguko lake linalokuja kwa kujongea kadri muda unavyozidi kusonga mbele, walisahau kabisa kuzigeuza fikra ili zimuelekee mwenyekiti binafsi na kumchambua ni kwa kiwango gani, yeye mwenyewe alikuwa ameshindwa kufanya kazi na sekretarieti na kamati kuu yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna ninavyomfahamu Kinana, ninao uhakika wa asilimia 100 kwamba wakati wote walipokuwa wakijadiliana na wenzake ndani ya chama chake kuhusu hatua wanazopaswa kuzichukua, ukweli kwamba, moja ya matatizo makubwa yanayokikwamisha chama hicho ni Kikwete mwenyewe aliliona.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunapaswa kuomba Mungu katika siku isiyo na jina huko tuendako, tuje kumsikia Kinana kwa maneno yake mwenyewe akikiri kwamba, tatizo la kwanza na la msingi ambalo limekikwamisha chama chao na hususan serikali ya CCM katika kipindi cha miaka mitano iliyopita ni mwenyekiti wake, Rais Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, leo hii unapoandika maneno ya namna hii, yenye mwelekeo wa kumsema vibaya Kikwete, marafiki zake na wale wataalam wa masuala ya intelejensia wanaofanya mambo yao wakitumia kanuni moja tu ya hesabu za kujumlisha na mbinu ya kuoteshwa majibu ya matatizo ya taifa hili huwa wepesi kuzusha na kutunga uongo kwamba fulani ametumwa na fulani ili amchafue fulani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wazushi hawa ambao baadhi yao ni makachero wanaopaswa kujua mapana na marefu ya kufanya upembuzi yakinifu kabla ya kuwahadaa viongozi wetu wakuu ndiyo ambao walikuwa nyuma ya ajenda nzima ya CCM kujitoa gamba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la kusikitisha sana kwamba wazushi hao ambao leo hii wamefikia hatua ya kuwa ndiyo ‘think tanks’ ndani ya CCM na serikali yake wakiongozwa na kachero mmoja mwandamizi aliyeingia katika siasa ndiyo waliokuwa pia nyuma ya hoja ya kuwapa siku 90 baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi walio wajumbe wa NEC ambao kwa muda mrefu majina yao yamechafuka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazushi hao ambao kwa kujua au kutokujua baada ya hoja yao hiyo ya kuwaandama watuhumiwa wachache wa ufisadi kuonekana ikipwaya na hata kufikia hatua ya kushambuliwa katika vyombo vya habari na ndani ya vyama vya siasa, wameanza kupindua maneno.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa wazushi hao wanayatuhumu baadhi ya magazeti, likiwamo hili kwamba eti yanatumiwa na mafisadi ili kumchafua Rais Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kauli hiyo hiyo, wazushi hao wamemlisha ujinga wao, Katibu wa Idara ya Uenezi na Itikadi wa CCM, Nape Nnauye ambaye naye hata kabla ya kufikiri na kuchanganua mambo ameanza kupita akikishambulia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Katibu Mkuu wake, Dk. Willibrod Slaa kwa kutumiwa na mafisadi eti kumchafua Rais Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nape na wazushi wenzake hao wanasahau kwamba, msimamo wa magazeti wanayoyashambulia kama ‘Tanzania Daima’ kuhusu Kikwete na ufisadi wanaojaribu kuufanyia usanii hata kabla hawajabuni nadharia yao ya kujivua gamba haujapata kubadilika na utaendelea kubakia na kuwa ule ule siku zote. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi Nape na makachero wengine wanaoasisi michezo ya kisiasa ndani ya CCM wanapojaribu kuitumia dhana ya kujivua gamba kama mkakati wa kuzima kishindo cha mabadiliko kinacholikumba taifa leo wanadhani Watanzania hawajui kwa mapana na marefu ukweli wote kuhusu ufisadi hapa nchini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi CCM hii inayojaribu leo hii kujiokoa kwa gharama ya kusalitiana, kulana wenyewe kwa wenyewe kisiasa (political cannibalism) na kutoana kafara hata katika kashfa kama za Kagoda na Richmond haijui kuwa tuko wengi tunajua kuwa ushiriki wake ni mpana zaidi na unawagusa wakubwa wengi zaidi ndani ya chama hicho tawala na serikali yake?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Itakuwa ni dharau mbaya dhidi ya Dk. Slaa, Chadema na Tanzania Daima iwapo wanasiasa wa aina ya Nape na wenzao watafikiri kwamba wanaweza kutujumuisha katika kundi la watu wanaoyashangilia mageuzi hewa yanayoendelea kufanywa ndani ya CCM leo kwa lengo la kuwahadaa wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Litakuwa ni jambo la kututia aibu iwapo sisi wa Tanzania Daima pia tutaingizwa kichwa kichwa katika sanaa mpya ya CCM ya ‘kujivua gamba’ hata tukaisahau na kuipuuza orodha ya Mwembe Yanga ya watuhumiwa 11 wa ufisadi iliyosomwa na Dk. Slaa, Septemba 15, mwaka 2007.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yatakuwa ni matusi dhidi ya uwezo wetu wa kufikiri iwapo CCM itafikiri kwamba hiki kiini macho chao kipya wanachokifanya sasa kinaweza kikatufanya tukaweka kando madai yenye harufu ya ukweli yatakaoendelea kuitafuna Serikali ya Awamu ya Nne kwamba iliingia madarakani kwa ushawishi wa nguvu ya fedha iliyopatikana kutoka katika Akauti ya EPA na kupitia katika akaunti ya Kagoda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Itakuwa ni fedheha kwetu iwapo tutaupuuza ukweli ulio dhahiri kwamba tatizo la ufisadi ndani ya CCM na serikali yake haliwezi kumalizwa kwa kuwaruhusu viongozi na makada wa chama hicho wahujumiane kisiasa kwa malengo ya kusaka madaraka tena kwa gharama za kufifisha upepo wa mabadiliko ya kisiasa ambao kwa sasa unaongozwa na Chadema.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais Kikwete na timu yake mpya ya uongozi ya CCM wanapaswa kutambua kuwa, kama walivyokwama wakati walipojaribu kuinunua ajenda ya ufisadi kwa njia mbalimbali kupitia bungeni, mahakamani, Takukuru na kwingineko ndivyo watakavyokwama pia safari hii wanapojaribu kupanda farasi mpya waliyempachika jina la kujivua gamba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo, wanapaswa kuanza kutambua mapema kabisa kwamba, maamuzi waliyofanya Dodoma hivi karibuni, japokuwa leo hii yanashangiliwa na wengi ndani na nje ya chama hicho ni kaburi walilojichimbia wenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nyuma ya mabadiliko hayo ya CCM Dodoma, naona kuzaliwa kwa Maalim Seif mpya. Naona kuibuka kwa Jacob Zuma mwingine na kwa hakika tunaweza tukampata Raila Odinga wetu. Tusubiri tuone. Huko ndiko TUENDAKO.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aprili 2011, Tanzania Daima&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-471259956465583266?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/471259956465583266/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=471259956465583266&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/471259956465583266'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/471259956465583266'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2011/10/ccm-inajiandalia-anguko.html' title='CCM inajiandalia anguko'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-1790983067243470711</id><published>2011-10-27T02:34:00.000-07:00</published><updated>2011-10-27T02:36:37.907-07:00</updated><title type='text'>Hizi ni dalili za kifo cha CCM</title><content type='html'>September 2010&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;TAIFA limeingia katika wiki ya saba ya kampeni za urais, ubunge na udiwani ambazo wagombea wake wamesambaa katika maeneo mbalimbali nchini wakijinadi kwa wananchi huku wakitumia kila aina ya mbinu za ushawishi; halali na batili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa jinsi mambo yanavyokwenda, kwa mara ya kwanza katika historia ya chaguzi kuu za vyama vingi, wagombea wengi wanaosaka nafasi za uwakilishi kutoka katika Chama cha Mapinduzi (CCM) katika ngazi zote tatu za urais, ubunge na udiwani wanaonekana wakikabiliwa na upinzani mkali ambao kwa kiwango kikubwa unatishia fursa zao za ushindi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa katika nchi zilizoendelea na kupiga hatua kubwa katika ushindani wa demokrasia ya vyama vingi ni jambo la kawaida kutarajia mabadiliko ya uongozi kila unapofanyika uchaguzi mkuu, kwa nchi changa kama zetu, matarajio ya kimazoea huyaona matukio ya namna hiyo kuwa ni mambo yasiyoweza kutokea kirahisi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kwa sababu hiyo basi ndiyo maana katika mataifa makubwa kama Marekani baadhi ya marais wa aina ya Jimmy Carter, George Bush (mkubwa) pamoja na kuwa na mafanikio kadha wa kadha wakati wa tawala zao, waliangushwa wakati walipojaribu kutetea nafasi zao katika muhula wao wa pili wa madaraka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali kama hiyo ilimpata pia aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Gordon Brown ambaye hata baada ya kuingia madarakani akipita katika mgongo wa Tony Blair pasipo kufanyika kwa uchaguzi mkuu, alijikuta akishindwa katika uchaguzi na mpinzani wake mkubwa, David Cameron.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la kushangaza sana kwamba, wakati matukio ya namna hiyo ya viongozi walio madarakani kukubali kushindwa katika chaguzi huru na za haki yakitokea katika nchi ambazo kutoka kwao tumeiga mfumo wa ushindani wa vyama vingi, kwenye nchi kama Tanzania, walio madarakani (viongozi na vyama vyao) wanaliona jambo hilo kuwa lisilokubalika na lisilopaswa kutokea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dalili za wazi za viongozi walio madarakani kukataa katakata kushindwa hata katika sanduku la kura, zimekuwa zikionekana kutokea kila zinapofika nyakati kama hizi za kampeni za kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kwa sababu hiyo basi ndiyo maana leo hii wakati upepo ukionekana dhahiri kuvuma dhidi ya CCM katika ngazi ya urais kwa upande wa Zanzibar ambako mgombea kwa tiketi Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad anaonekana kuwa na nguvu kubwa na ushawishi unaojitosheleza dhidi ya mshindani wake wa CCM, Dk. Ali Mohamed Shein bado mazingira yanaendelea kubainisha kuwa watawala wanazidi kuliona tukio hilo kuwa lisilopaswa kutokea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hii ya mambo imeanza kujionyesha hata kwa upande wa serikali ya muungano ambako katika mazingira ambayo si rahisi kuyaeleza kwa haraka haraka, mgombea wa urais kwa tiketi ya Chadema, Dk. Willibrod Slaa anaonekana kila kukicha akizidi kuvuta ushawishi unaoonekana kutishia urais wa Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuongezeka kwa mbwembwe na kujiamini kwa Chadema na Dk. Slaa kwa kiwango cha kulifanya tishio lao hilo kuchukua picha inayoanza kuonekana kuwa ni ya kweli na dhahiri, kumesababisha kuibuka kwa matukio na mambo ya kushangaza ambayo yumkini kwa sababu moja au nyingine yanazidi kukiweka chama tawala katika taswira mbaya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna hiyo hiyo, kustawi na kuzidi kung’ara kwa nyota ya Maalim Seif na CUF yake katika mchuano wa urais Zanzibar kwa kiwango cha kuiweka njia panda CCM, nako kunaonekana kupokewa kwa njia ambazo ni dhahiri zinaanza kujenga mazingira ya kutaka kuchafua hali ya hewa ya kisiasa na dalili njema za ustawi mpya wa ustahimilivu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ili kuweza kuwazuia Dk. Slaa kwa Tanzania na Maalim Seif kwa Zanzibar, CCM na mawakala wake kwa ustadi mkubwa wameamua kuendelea kuvitumia vyombo vya habari kujenga taswira ambayo hakuna shaka hata kidogo lengo lake ni kuhakikisha wapinzani hao wawili na vyama vyao hawafanikiwi kuendelea kupenya mioyo ya wapiga kura walio wengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kupitia vyombo kadha wa kadha vya habari, kwa makusudi na kwa nia ya kupotosha au kukuza mambo, kumeibuka taarifa za ajabu ama dhidi ya Maalim Seif na CUF yake kwa upande wa Zanzibar au Dk. Slaa na Chadema yake kwa upande wa serikali ya muungano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati kwa upande wa Zanzibar mawakala wa CCM wameanza kupenyeza makala za kumpaka matope Maalim Seif kuwa ni mwanasiasa mwenye lengo la kuvunja muungano na kuvitenga visiwa vya Unguja na Pemba, Dk. Slaa na Chadema yake sasa wameanza kuhusishwa na siasa za kutishia amani ya nchi na mshikamano wa kitaifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hiyo haitoshi, mawakala hao wa CCM ambao hakuna shaka wamekuwa wakitumia mbinu za namna hiyo hiyo kila zinapofika nyakati za uchaguzi kama hizi wamefikia hatua ya kuandika habari za kupindisha ukweli zinazoonyesha eti Maalim Seif ameshakubali kushindwa urais wa Zanzibar hata kufikia hatua ya kujisalimisha chini ya Dk. Shein akiomba dua aambulie umakamu wa rais katika serikali ya umoja wa kitaifa inayotarajiwa kuundwa baada ya matokeo kutangazwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kwamba, Maalim Seif mwenyewe, mmoja wa viongozi adhimu na wa mfano ambao taifa hili limepata kuwa nao atakuwa ameshang’amua janja hiyo ya CCM na mawakala wake na hivyo atalazimika kuendelea kupiga kampeni pasipo kulitaja tena jina la Dk. Shein.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati Maalim Seif na CUF wakionekana kung’amua janja ya CCM na mawakala wake inayolenga kuwaondoa katika mstari wa kuendelea kunadi sera na mwelekeo wao wa kiuongozi, hali inaonekana kuwa tofauti kwa Chadema na kwa Dk. Slaa ambao kwa kutojua au kwa makusudi wamejikuta wakijizatiti kujibu kila aina ya mashambulizi yanayoelekezwa kwao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tamko lililotolewa na vikosi vya ulinzi na usalama na kusomwa mbele ya wanahabari na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo mwishoni mwa wiki iliyopita ni kielelezo kimoja cha kishindo na nguvu ya upinzani katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati katika uchaguzi mkuu uliopita, tamko kubwa la vikosi vya ulinzi lilitolewa na aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali, Omar Mahita aliyefikia hatua ya kukihusisha CUF kwa namna ya uzushi wa wazi na jaribio la kuvuruga amani kwa kuingiza nchini visu vyenye rangi ya bendera za chama hicho, mwaka huu hali inaonekana kuwa mbaya kwa kiwango cha kuhusisha vikosi takriban vyote vya ulinzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tamko la mwaka huu mbali ya kutoa kila aina ya mwelekeo kuwa lilikuwa likikilenga Chadema ambacho viongozi wake walikuwa wamekaririwa wakisema walikuwa hawako tayari kuona matokeo ya uchaguzi mkuu wa urais, wabunge na madiwani yakichezewa kwa maslahi ya kuibeba CCM, kwa upande mwingine lilikuwa likionyesha kuwapo kwa hofu ndani ya dola kwamba chama hicho tawala kilikuwa katika hatua ngumu zaidi ambayo haijapata kufikiwa wakati mwingine wowote kabla ya uchaguzi huu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akili za kawaida kabisa zinaonyesha kwamba, uzito wa nafasi ya Jenerali Shimbo ndani ya jeshi na ule wa matamshi aliyoyatoa mbele ya wana habari kwa namna yoyote ile yalikuwa yakibeba uzito wa ujumbe ambao ulikuwa nyuma ya matukio ambayo wanaamini yanaweza kutokea kabla, wakati na baada ya uchaguzi mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kwamba, Jenerali Shimbo na vikosi vingine vya ulinzi na usalama wa taifa vilifikia hatua ya kutoa tamko lile si kwa sababu tu ya kutishwa na kombati zinazovaliwa na makamanda wa kisiasa wa Chadema au maneno makali ya akina Freeman Mbowe na Dk. Slaa bali uzito wa kile ambacho kilikuwa kikitarajiwa baada ya uchaguzi mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbukumbu zinaonyesha kwamba, iwapo vikosi vyetu vingekuwa vikishtushwa na kauli za ama uchochezi au zile zenye mwelekeo wa kutishia amani ya nchi, basi tungepata kuwasikia majenerali wa kabla ya Shimbo wakitoa matamshi ya namna hiyo dhidi ya kauli ambazo kuanzia mwaka 1995 zilikuwa zikitolewa na wanasiasa wa aina ya Christopher Mtikila.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo basi, kwangu mimi kwa viongozi wa upinzani, wagombea wao na kwa wapiga kura, kauli kama zile za Jenerali Shimbo zilipaswa kujibiwa kwa kuandaa mikakati ya kujizatiti kushinda kwa kujenga ushawishi zaidi na kwa njia ya kulinda kura kwa namna ambayo haitakuwa rahisi kuibiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ili kufanikisha hilo, akina Dk. Slaa, Mbowe na wenzao wengine wa ndani ya Chadema walipaswa na kimsingi wanapaswa kuendelea kukifanya sasa ni kuwashawishi wananchi sababu za kuwachagua wao na kuwaweka kando akina Kikwete na wagombea wa CCM badala ya kuendelea kuzozana na majenerali ambao kwao siasa si eneo lao la kujidai.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kwamba, iwapo vyama vya CUF (Zanzibar) na Chadema (Tanzania Bara) vitakuwa na mikakati imara na endelevu ya kisera, kifedha, kimtandao na kioganaizesheni basi safari ya CCM kuendelea kubakia madarakani inaweza ikawa imeanza kukoma mwaka huu kwa upande mmoja wa muungano au kwa pande zote mbili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa hilo linaweza likaonekana kuwa ni ndoto ya alinacha kwa baadhi ya watu, hususan wale walio na maslahi ndani ya CCM, ukweli wa kimazingira umeanza kuonyesha kwamba silaha pekee ambazo chama hicho tawala kimebakiza na ambazo sasa inazitumia kama turufu yake ya ushindi ni nguvu ya fedha (si sera), mtandao na historia yake ambayo inawafanya hata wale ambao walipaswa kuwa wameshakihama chama hicho waendelee kubakia humo humo. Hizi ni dalili za mwanzo za kifo cha CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwisho&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-1790983067243470711?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/1790983067243470711/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=1790983067243470711&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/1790983067243470711'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/1790983067243470711'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2011/10/hizi-ni-dalili-za-kifo-cha-ccm.html' title='Hizi ni dalili za kifo cha CCM'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-3611693037753652964</id><published>2011-10-27T02:26:00.000-07:00</published><updated>2011-10-27T02:33:17.041-07:00</updated><title type='text'>Richmond: Laana ya alama za nyakati</title><content type='html'>Tanzania Daima Jumatano, 29 julai 2009&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;MZIMU wa Richmond umerudi tena bungeni, ikiwa ni mwaka mmoja na ushei tangu ulipotua na kusababisha kuondoka kwa mawaziri wawili, akiwamo aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, Februari mwaka jana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kurejea kwa Richmond ndani ya Bunge kunatokana na serikali kutoa tamko ambalo hatimaye linaweza kusababisha kazi kubwa iliyofanywa na iliyokuwa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mchakato mzima wa mkataba ulioipa ushindi Kampuni ya Richmond kuzalisha umeme wa dharura wakati wa kipindi kigumu cha ukame cha kati ya mwaka 2006 na 2007 kuwa isiyo na maana kubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika tamko la serikali lililotangazwa mwishoni mwa wiki iliyopita bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Adam Malima kwa niaba ya waziri wa wizara hiyo, William Ngeleja likieleza namna serikali ilivyotekeleza maazimio 23 ya Bunge kuhusu kashfa ya Richmond, tayari limesababisha Bunge na pengine taifa kugawanyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, ni wazi kwamba taarifa hiyo ya serikali ambayo hatimaye imewasafisha kutoka katika tuhuma viongozi wakuu wawili wa serikali; Mwanasheria Mkuu, Johnson Mwanyika na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk. Edward Hoseah imetoka ikiacha wazi matamshi yaliyopata kutolewa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika moja ya vikao vya Bunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbukumbu zinaonyesha kwamba, Agosti 28 mwaka jana, Pinda akizungumza bungeni kuhusu hatima ya viongozi hao wawili ndani ya Bunge, alisema suala lao lilikuwa limefikishwa Ikulu kwa ajili ya kufanyiwa kazi, hasa ikizingatiwa kwamba wao ni wateule wa rais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno yake mwenyewe Pinda alisema: ‘‘Kutokana na nafasi yake kikatiba, mamlaka yake ya nidhamu ni Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;‘‘Kwa hiyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye alikuwa miongoni mwa watendaji wakuu watatu waliokuwa wanaishauri serikali, suala lake la kuhusishwa kwake katika mchakato mzima wa mkataba huo, linashughulikiwa na Ofisi ya Rais, Ikulu.” Mwisho wa kunukuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pinda hakuishia hapo, bali alikwenda mbele na kusema azimio namba saba la Bunge lililokuwa likitaka watumishi walioshiriki katika kamati ya serikali ya majadiliano wawajibishwe, lilikuwa limeangaliwa kwa namna ya kuwapa nafasi watuhumiwa kujitetea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miongoni mwa watu ambao Pinda alisema walikuwa wameandikiwa barua ya kujitetea ni pamoja na Hoseah ambaye alikuwa ameandikiwa na Katibu Mkuu Kiongozi ili aeleze namna alivyoshiriki katika mchakato huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Ili kutekeleza azimio hili, Mkurugenzi TAKUKURU amepelekewa barua ya kutakiwa kujieleza na mamlaka yake ya nidhamu ambaye ni Katibu Mkuu Kiongozi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Vilevile, wasaidizi walio chini yake walioshiriki katika zoezi la uchunguzi, nao wametakiwa kutoa maelezo yao kwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU ambaye ndiye mamlaka yao ya nidhamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;‘‘Hii ni kwa kuzingatia misingi ile ile ya kanuni asilia ya haki ya kusikilizwa kwanza,” alisema Pinda akitoa kauli ambayo inafanana kimantiki na ile aliyotoa Lowassa bungeni siku alipotangaza kujiuzulu wadhifa wake wa uwaziri mkuu, Februari mwaka jana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, katika kuonyesha namna serikali ilivyokuwa imedhamiria kuchukua tahadhari katika suala hili zima, Pinda alisema halitakuwa jambo rahisi kwa Rais Jakaya Kikwete, kuwastaafisha au kuwafukuza kazi watuhumiwa hao bila kufuata taratibu zinazotakiwa, kwani akifanya hivyo, kuna hatari kwa serikali kuwalipa fedha nyingi iwapo watakwenda mahakamani na kushinda kesi zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa haraka haraka, maneno hayo ya Pinda aliyotoa mwaka jana na hitimisho lililotolewa na serikali bungeni mwishoni mwa wiki iliyopita, ni ushahidi wa wazi wa namna serikali ilivyokuwa imeamua kwa dhati kuitupa kwa heshima ripoti ya Kamati Teule ya Bunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huku ikijua kile ilichokuwa ikikifanya, serikali kwa namna ya kuweza kulifunga mdomo Bunge kwa kutumia kanuni zake lenyewe, ikaamua kutekeleza baadhi ya maazimio ya Bunge ambayo hayakuwa na athari za moja kwa moja kwa watu wazito.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza, ikaanzisha utaratibu wa kufuta usajili wa Kampuni ya Richmond kutoka katika vitabu vya Wakala wa Usajili wa Makampuni (Brela) na kabla ya kumfikisha kortini mmoja wa wakurugenzi wa kampuni hiyo ambayo hakuna shaka usajili wake ulikuwa na utata na mashaka makubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hiyo haitoshi, huku ikijua hisia za kishabiki za baadhi ya wabunge, hususan wale waliojitoa mhanga kupambana na ‘mafisadi’ kisiasa, serikali ikaenda mbele na kuliagiza Shirika la Ugavi wa Umeme nchini (TANESCO) kuvunja mkataba wake na Kampuni ya Dowans Tanzania Ltd ambayo ilikuwa imeununua mkataba wenye utata kutoka Richmond.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya serikali kuvunja mkataba na Dowans kwa sababu tu ya kujaribu kupoza hasira za wazalendo wa Kitanzania wanaotoka katika makundi mbalimbali ya kijamii, waliojitwisha ufahari wa uanazuoni katika masuala yanayohusu nishati ya umeme, yalikuwa makali zaidi pale serikali hiyo hiyo ilipojaribu kuinunua mitambo hiyo yenye uwezo wa kuzalisha megawati 100 na ushei za umeme kwa mlango wa nyuma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati mzozo kuhusu ama kununua au kutonunua mitambo hiyo ya Dowans ukiendelea kulitikisa taifa, Rais Kikwete ambaye ndiye aliyepaswa kutoa mwongozo wa nini kifanyike kwa maslahi ya taifa, naye akaingia katika mtego rahisi wa kukiogopa kile ambacho yeye mwenyewe alikiita ‘alama za nyakati’.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukio hili la Rais Kikwete kuwatosa wateule wake wawili, Waziri wa Nishati na Madini, Ngeleja na Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Dk. Idris Rashid kwa lugha nyepesi isiyopaswa kutumiwa na kiongozi mkuu wa nchi ya ‘kusoma alama za nyakati’ ndiyo ambayo leo hii imelifikisha taifa hapa tulipo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukitafakari kwa makini sakata zima la Richmond kwa kuangalia mlolongo mzima wa matukio, hasa yale ya baada ya kusomwa kwa taarifa ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Mwakyembe na ambayo yamehitimishwa na tamko la serikali la majuzi, unaweza ukajikuta ukilazimika kuurejea ujumbe uliopuuzwa uliotolewa bungeni na Lowassa siku alipotangaza kujiuzulu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pengine kabla sijahitimisha hoja yangu nichote sehemu tu ya maneno aliyosema mwanasiasa huyu siku hiyo ambayo kwa bahati mbaya yaliachwa yakapita pasipo kujadiliwa mbali ya kujibiwa kwa maneno makali na Mwakyembe mwenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru sana kwa kunifanya msemaji wa kwanza katika hoja hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini la pili, nimpongeze Dk. Harrison Mwakyembe, Mwenyekiti wa Kamati Teule kwa kuwasilisha kwa mbwembwe nyingi sana taarifa yake, mbwembwe zilikuwa nzuri kweli. (Makofi).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kazi nzuri kwa maoni yao, wamewasilisha vizuri. Lakini nimesimama kuweka kwenye kumbukumbu kutoridhika kwangu na jinsi kazi hiyo ilivyofanywa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Dk. Harrison Mwakyembe ni mwanasheria, tena daktari, alikuwa anafundisha wanafunzi chuo kikuu. Moja ya vitu alivyokuwa anafundisha ni “Natural Justice”.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, wewe pia ni mwanasheria unafahamu suala la “Natural Justice”. Kwamba Kamati Teule imesikiliza watu wengine wote pamoja na wanaoita minong’ono ya mitaani, wamesafiri mpaka Marekani kutafuta mashahidi, lakini mimi ambaye ni mmoja katika watuhumiwa mle hawakunihoji hata siku moja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, nimesimama kueleza masikitiko yangu. Ofisi ya Bunge mpaka ofisini kwangu (Dar es Salaam) hata wangeniita ningekwenda kwa miguu kama hamna gari na nilikuwa tayari kufanya hivyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hawa ni watu makini sana siwezi kuamini kwamba wanaweza wakafanya ‘oversight’ kama hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu katika kila hoja walizojenga wamesema Waziri Mkuu ilikuwa hivi. Kulikuwa na shida gani kuja kuniuliza Waziri Mkuu wanasema ulitoa dokezo hili ni sawa sawa ni kweli? Kulikuwa na shida gani kwa mfano kufuata utaratibu wa Westmister kuthibitisha hapo unaposema mwenye Richmond ni fulani uka – lay on the table records na ushahidi kuwa ni fulani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, taifa letu ni taifa changa, lakini chombo hiki ndiyo mahali pa demokrasia pakubwa katika nchi pote, hapa ndipo penyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama katika chombo hiki hakitaonekana kutendeka haki nchi yetu haitakwenda vizuri. Hapa ndipo tunategemea tuwaonyeshe umakini wetu, umahiri wetu katika mambo ya demokrasia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, nilichofanyiwa napenda kuweka kumbukumbu sawa kwamba, naona si sahihi, nimefadhaika sana, nimedhalilishwa sana, nimeonewa sana katika hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maana zimechukuliwa tuhuma zikaja zikaelezwa hapa kwamba hivi ndivyo ilivyo. Mimi sijaulizwa. Kulikuwa na shida gani ya kuniuliza, kwa nini muamini minong’ono ya mitaani kuliko maelezo yangu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sisi wote hapa ni wanasiasa, tukianza kuamini minong’ono ya mitaani niambieni mwanasiasa atakayesimama. Hatuwezi, tume imepewa muda wa kutosha lakini inashindwa kumuona mtu ambaye wanamtuhumu na wanamsema kwa kirefu sana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, lakini hata pale uliponinong’oneza ukaniambia una ushahidi wowote? Nilikuwa ushahidi huo wa maandishi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika taarifa yao hakuna hata moja ya ushahidi ambao umetoka Waziri Mkuu. Kile kitabu cha majedwali kimejaa majedwali mengi pamoja na magazeti mpaka ya udaku lakini maelezo ya Waziri Mkuu hakuna hata moja. (Makofi).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, naamini ingekuwa ni heshima wangeiweka halafu wakasema tunakataa kitambulisho hiki kwa sababu hii na hii na hii, hiyo ndiyo imejengwa hoja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini kujenga hoja na kuja hapa bungeni tunahutubia nchi nzima na kusema Waziri Mkuu amefanya hiki, amefanya hiki bila ya kumsikiliza nachelea kuuliza hivi mtu wa chini itakuwaje?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, lakini nimetafakari kwa makini sana jambo hili nikajiuliza hivi hasa kulikoni mpaka watu wazima wenye uwezo wao, watu maarufu wenye heshima zao, mpaka wafike mahali waache jambo la msingi kama hilo kulikoni?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mimi nadhani there is a wish which I am going to grant, ni Uwaziri Mkuu. Nadhani tatizo ni Uwaziri Mkuu. Kwamba ionekane Waziri Mkuu ndio amefanya haya, tumuondolee heshima au tumwajibishe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, nimetafakari sana kwa niaba ya chama changu, kwa niaba ya serikali yangu nimeamua kumwandikia rais barua ya kumwomba niachie ngazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nafanya hivyo kwa moyo mweupe kabisa ili kuonyesha dhana ya uwajibikaji lakini na kutokukubaliana na utaratibu uliotumika kusema uongo ndani ya Bunge wa kumsingizia mtu.” Mwisho wa kunukuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, Bunge lililojaa watu makini na wachambuzi hodari wa mambo, kwa sababu tu ya kuelemewa na ushawishi wa kishabiki na woga uliojengwa katika misingi ile ile ya Kikwete ya kuzihofia alama za nyakati, lilishindwa kuzijadili kwa kina hoja za Lowassa ambaye kwa wengi habari, makala za kichambuzi tulielekeza mashambulizi kwake (Tuendako ikiwamo), na tahariri mbalimbali za magazetini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii ukitafakari kwa utulivu, unaweza kushangaa ni kwa nini Lowassa, yule mwanasiasa jeuri aingie katika mtego ule ule rahisi wa kutishwa na kishindo cha alama za nyakati hata kuamua ‘kuachia ngazi’ badala ya kuliomba Bunge liipe serikali muda wa kutosha kujibu hoja za Kamati ya Mwakyembe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiliacha hilo, ni jambo la ajabu sana kwamba, katika hali ile, wabunge wale wale ambao leo ni hodari kusimama kwa kujiamini wakitaka muongozo wa Spika, walishindwa kumwomba Spika, amtake Lowassa athibitishe matamshi yake mazito dhidi ya kamati teule kwamba ilisema uongo ndani ya Bunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika, leo hii serikali inapotoa taarifa ya kuwasafisha viongozi takriban wote waliotuhumiwa katika Kamati Teule ya Mwakyembe, huku jina la Lowassa likiachwa pasipo kuguswa, ni rahisi kabisa watu kuamini na kuaminishwa kwamba kumbe kweli tatizo lilikuwa ni uwaziri mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hiyo haitoshi, tunapomsikia Waziri Mkuu Pinda akisema serikali ilikuwa imewapa muda maofisa wake wote waliotuhumiwa na Bunge kutoa utetezi wao kwa mamlaka zilizowatetea, uamuzi huo, moja kwa moja unayafanya maneno ya Lowassa aliyelalamika ndani ya Bunge kuwa hakutendewa haki kwa kutopewa nafasi ya kujitetea kuwa na nguvu kubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunapofikishana hapa tulipo leo, kama taifa tunao wajibu wa kujitafakari upya na kukiri ukweli mchungu kwamba, ukianza na Rais Kikwete, Lowassa, Kamati ya Mwakyembe, wabunge, wanahabari na wananchi kwa ujumla, tulilishughulikia ndivyo sivyo suala zima lililohusu kashfa hii ya Richmond, kwa namna ya sote kubebwa na kile tulichokitengeneza sisi wenyewe na kukipa jina zito; ‘alama za nyakati.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama wasemavyo wana historia, kila mara tunao wajibu wa kujifunza kutokana na makosa tuliyotenda nyuma, ili kujenga mustakabali mwema leo hii, tayari kwa kujiandalia mazingira bora huko TUENDAKO.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwisho&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-3611693037753652964?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/3611693037753652964/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=3611693037753652964&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/3611693037753652964'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/3611693037753652964'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2011/10/richmond-laana-ya-alama-za-nyakati.html' title='Richmond: Laana ya alama za nyakati'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-6687470162765899410</id><published>2011-10-27T02:23:00.000-07:00</published><updated>2011-10-27T02:25:50.794-07:00</updated><title type='text'>Kikwete mchovu, Pinda dhaifu</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;VIONGOZI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake wanaoongozwa na Rais Jakaya Kikwete wanapata jeuri ya kimamlaka na kuendelea kujiona mabwana wakubwa waliopewa dhamana ya kuendelea kuitawala nchi si kwa sababu ya ubora wao au weledi wao wa kazi na kiuongozi, bali misingi imara iliyowekwa na waasisi wa taifa hili.&lt;br /&gt;Ni misingi hiyo imara ya uongozi iliyojengwa na viongozi waasisi wa taifa hili ndiyo inayowapa kiburi akina Kikwete, Mizengo Pinda na wenzao wengine kufaidi matunda ya madaraka wakati ushahidi ulio wazi umekuwa ukithibitisha pasipo shaka kwamba katika umoja wao wanaunda jeshi maarufu la viongozi wavivu wa kufikiri, wachovu wa kutenda, dhaifu katika kuona na wasanii katika maamuzi.&lt;br /&gt;Matokeo ya uchovu na udhaifu walionao viongozi wa zama hizi za Kikwete wanaofikiri kwa ndimi zao na kuamua mambo mazito ya kitaifa kwa kuangalia mustakabali mwema wa matumbo yao na yale ya familia zao ndiyo ambao umetufikisha hapo tulipo leo.&lt;br /&gt;Hauhitaji kuwa na akili nyingi kubaini kwamba, matukio ya siku za hivi karibuni kama yale ya sakata la Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, la mgomo wa wauza mafuta ya petroli, kushamiri kwa baa la njaa, mgawo wa umeme na hata kukwama kwa bajeti za wizara ndani ya Bunge ni matokeo ya mparanganyiko mkubwa ambao haujapata kutokea katika nchi hii katika kiini cha uongozi wa kitaifa.&lt;br /&gt;Ni jambo lisiloingia akilini hata kidogo kuiona serikali iliyosheheni viongozi ambao wamekuwapo madarakani kwa miaka mingi na wenye uzoefu mkubwa ikiyumbishwa bungeni kwa kiwango cha kupoteza mwelekeo wa wabunge wachache vijana wanaotokana na vyama vichanga vya upinzani.&lt;br /&gt;Ni jambo linalosikitisha kumuona Waziri Mkuu akilazimika kusimama katika nyakati zisizo zake na kwa dharura mara kwa mara ndani ya Bunge na kutoa hoja zisizo na mashiko za kujaribu kupooza hasira za wabunge na kuomba huruma zao ili kuifanya bajeti ya wizara fulani iweze kupita ilhali ikiwa na mafindofindo yaliyo bayana.&lt;br /&gt;Lakini pengine ni kielelezo cha wazi cha udhaifu uliovuka mipaka unapomsikia waziri mkuu huyo huyo, akizungumza kwa kujiamini ndani ya Bunge wakati akijua kuwa anachokizungumzia hana mamlaka juu yake na tena anakisema kwa msisitizo hata kabla hajawasiliana na mkuu wake aliye na dhamana katika kile anachokisemea.&lt;br /&gt;Nayaandika haya nikirejea kituko cha Pinda ndani ya Bunge aliposimama kuwakubalia wabunge wito wao wa kuikataa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini na akawaahidi kuzifanyia kazi tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka zilizokuwa zikimkabili Jairo ambaye alibainika kuandika barua kwenda katika taasisi kadhaa zilizo chini ya wizara hiyo akiomba michango ya shilingi milioni 50 kwa ajili ya kufanikisha kile alichokiita, uwasilishaji wa hotuba ya bajeti ya wizara. &lt;br /&gt;Akizungumza kwa kujiamini huku akionyesha kukerwa na kitendo hicho cha Jairo, Waziri Mkuu Pinda ambaye kitaaluma ni mwanasheria, alisema iwapo angekuwa na mamlaka (ambayo alipaswa ajue hata kabla hajashauriwa kuwa hana) angekuwa ameshachukua maamuzi dhidi ya katibu mkuu huyo.&lt;br /&gt;Katika kuthibitisha kwamba, Pinda alitoa matamshi hayo kwa kukurupuka na pengine kwa lengo la kupoza ki-propaganda hasira walizokuwa nazo wabunge dhidi ya Wizara ya Nishati na Madini, alikuwa ni mtu wa kwanza yeye mwenyewe kukiri siku moja tu baadaye kwamba alikuwa ameshapokea maelekezo tofauti kutoka kwa Rais Kikwete.&lt;br /&gt;Wabunge na Watanzania walipaswa wawe wa kwanza kutambua kwamba, maelekezo ya rais yaliyokuwa tofauti kiutashi na mwelekeo wa awali wa Pinda kilikuwa ni kielelezo cha kwanza kwamba, kauli ya waziri mkuu ama ilikuwa ni danganya toto au ilikuwa ina walakini. Ni bahati mbaya sana kwamba hakuna alilipa uzito jambo hili wakati huo.&lt;br /&gt;Kile ambacho Pinda alikiita maelekezo tofauti ya Rais Kikwete hakikuwa kingine bali uchunguzi ambao ulifanywa na Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa maelekezo ya Katibu Mkuu Kiongozi ambao ulikisafisha kitendo cha Jairo kuchangisha fedha kutoka katika taasisi zilizo chini ya wizara anayoiongoza.&lt;br /&gt;Katika mazingira ya kawaida, ripoti ya CAG iliyotolewa sambamba na tamko la Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo ya kumsafisha Jairo ikiwa ni pamoja na kuamuru aripoti ofisini kwake siku iliyofuata ilipaswa kufuatiwa na matukio makubwa mawili.&lt;br /&gt;Kwa serikali yenye viongozi wanaojiheshimu na wanatambua maana ya uwajibikaji wa pamoja, Katibu Mkuu Kiongozi na CAG walipaswa kurejea mchakato mzima wa suala la Jairo na kubaini kwamba, katikati alikuwapo Waziri Mkuu Pinda ambaye kwa bahati mbaya alishatoa kauli ya kipropaganda na isiyo na mashiko.&lt;br /&gt;Wangekuwa ni viongozi wastaarabu, wanaotambua maana ya kuheshimiana wao kwa wao, hata kama si katika hali halisi, basi hata hadharani, Luhanjo na CAG Ludovick Utouh wangeshauriana na Waziri Mkuu Pinda kwanza na pengine wangemuachia yeye wajibu wa kulihitimisha sakata hilo la Jairo akilitolea kauli ndani ya Bunge kama livyofanya siku alipoteleza kujitwisha uchungu wa kudhamiria kumtimua. Kwa bahati mbaya hilo halikufanyika.&lt;br /&gt;Ni wazi kwamba, tungekuwa na serikali makini na ambayo inatambua maana halisi ya kusoma alama za nyakati (si zile za Kikwete za kuiogopa mitambo ya Dowans) Luhanjo na Utouh wangesubiri kwanza Mkutano wa 10 wa Bunge umalizike ndipo watangaze kile walichokuwa wamekusudia. Hili nalo halikufanyika.&lt;br /&gt;Kwa kuwa haya yote mawili hayakufanyika basi, tulitarajia kulisikia jambo la tatu likitokea, nalo halikuwa jingine bali ni lile la kumsikia Waziri Mkuu Pinda akilitangazia Bunge uamuzi wa kujiuzulu wadhifa wake kwa hiari yake kwa kutoa sababu zifuatazo.&lt;br /&gt;Kwanza; alipaswa kuachia ngazi kama hatua ya kutambua kwake na kukiri kwamba alikuwa amelipotosha Bunge kwa kusema jambo ambalo halikuwa kweli pale aliposema kwamba Jairo alikuwa amekosea kwa kufanya jambo ambalo linaacha maswali mengi, kinyume kabisa na matokeo ya uchunguzi wa CAG Utouh yaliyothibitisha kwamba ulikuwa uamuzi sahihi na wa kawaida.&lt;br /&gt;Pili; alitakiwa atangaze kuachia ngazi kwa kuwa tamko la Luhanjo na Utouh lilikuwa ni ushahidi uliokuwa ukimchongea kwa wananchi na kwa Kikwete kwamba alimshauri rais vibaya kwa tamko lake la ndani ya Bunge, akifanya kosa lile lile lililopata kumgharimu Waziri Mkuu wa zamani, John Samuel Malecela zama za Serikali ya Awamu ya Pili.&lt;br /&gt;Ili aweze kulielewa vyema kosa lake hili la pili, Pinda anapaswa kukitafuta na kukisoma tena (nina hakika alishapata kukisoma) kijitabu cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kisemacho; ‘Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania’ ambacho ndicho kinachoaminika kumsukuma Rais Ali Hassan Mwinyi kubatilisha kama si kumfukuza kazi Mzee Malecela mwanzoni mwa miaka ya 1990.&lt;br /&gt;Tatu, kama tungekuwa tukiishi katika nchi zinazoheshimu mgawanyo wa madaraka ya mamlaka za dola (yaani Bunge, Serikali, Mahakama, Vyombo vya Habari) tamko la Katibu Mkuu Kiongozi na lile la Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ambao ni viongozi wazito serikalini, lililopingana waziwazi na mtazamo wa Waziri Mkuu anayetokana na serikali hiyo hiyo lilikuwa ni sababu inayojitosheleza ya Bunge kupiga kura ya kutokuwa na imani na Pinda. Ajabu hili nalo halikufanyika.&lt;br /&gt;Hatari ya kutokea kwa hili la tatu la kumpigia Waziri Mkuu Pinda kura ya kutokuwa na imani naye lilionekana dhahiri likikaribia kabisa kutokea ndani ya Bunge na kama si hoja aliyoibua Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe akitaka Bunge lijadili tamko la CAG na Katibu Mkuu Kiongozi, huenda leo tungekuwa tukizungumza lugha tofauti.&lt;br /&gt;Ingawa ukiliangalia kwa haraka haraka unaweza ukaingia katika mtego rahisi wa kulishangilia Bunge kwa namna lilivyoonekana kukerwa na tamko la Utouh na Luhanjo, upande wa pili wa hatua hiyo ilikuwa ni kuokoka kwa Pinda katika tundu la sindano kwa namna ambavyo kama si ujasusi ulifanyika basi kilichotokea ni ukachero.&lt;br /&gt;Ni wazi kwamba, Rais Kikwete, Waziri Mkuu Pinda na viongozi wengine wa serikali wanapaswa kuwashukuru kwa dhati Zitto, Spika wa Bunge, Anne Makinda, Naibu Spika Job Ndugai, Christopher ole Sendeka na wabunge wengine ambao walifanikiwa kwa kujua au kutojua kulifinyanga suala hili na hatimaye likamalizika kwa kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge.&lt;br /&gt;Kwa namna mambo yanavyokwenda, kama ilivyokuwa katika misukosuko mingine iliyopata kutokea siku zilizopita, hatua ya Bunge kutaharuki kwa namna ilivyotokea, iliyokwenda sambamba na kile kinachoitwa uamuzi wa Rais Kikwete kumrejesha tena likizoni Jairo, akipisha kile kinachoitwa uchunguzi wa Bunge itamalizika ikimuacha rais, waziri mkuu wake na serikali yake salama.&lt;br /&gt;Mambo ya namna hii ya kumuacha rais anayefanya kazi ofisi moja na kwa ukaribu mkubwa wa kimaamuzi na Katibu Mkuu Kiongozi akiwa salama na pengine kuonekana shujaa hata katika jambo ambalo mikono yake inaonekana dhahiri kuchafuka yanawezekana katika nchi kama zetu tu.&lt;br /&gt;Sakata la Jairo ambalo yumkini limeshaanza kuchukua mwelekeo wa kutafuta mtu au watu wengine wa kuwatoa kafara kama ilivyo ada katika mishipa ya fahamu ya viongozi wa CCM na serikali yake litahitimishwa kwa ripoti ya kamati teule ambayo itaandaliwa mahususi kwa malengo ya kuficha uchovu wa Rais Kikwete katika kuongoza, kutenda na kuchukua maamuzi sahihi.&lt;br /&gt;Kama hiyo haitoshi, hadidu rejea tano zilizotangazwa na Spika Makinda kwa Kamati Teule zimethibitisha hata kabla kazi haijaanza kwamba, zitamnusuru Pinda na kuficha udhaifu wake mkubwa wa kutokuwa makini wakati anapofikia hatua ya kutoa matamshi mazito yanayogusa masuala ambayo yumkini yanahitaji utulivu na ukomavu wa kiuongozi.&lt;br /&gt;Nayaandika haya kwa sababu kubwa moja tu kwamba, baadhi yetu tumejifunza kutokana na misukosuko ya kimadaraka iliyopata kulikumba taifa letu kama ile ya EPA, Richmond, Dowans na mengine mengi ambayo hitimisho lake lilithibitisha kwamba viongozi na waongozwa tumekuwa mabingwa wa kufikiri kwa mioyo badala ya bongo zetu.&lt;br /&gt;Sina hakika ni lini hasa wanasiasa wetu walio serikalini au bungeni watakuja kutambua na kuisimamia kwa vitendo dhana iliyozoeleka vichwani mwao inayowataka watambue kuwa, uongozi walionao ni dhamana kwa taifa na si neema ya kujisitiri na kulindana kwa malengo ya kujitwisha sifa bandia za ushupavu na ujasiri wasiostahili au ya kuwatoa kafara wachache ili kulinda mustakabali wa nyadhifa walizonazo. Tujisahihishe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Agosti 31, 2011&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-6687470162765899410?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/6687470162765899410/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=6687470162765899410&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6687470162765899410'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6687470162765899410'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2011/10/kikwete-mchovu-pinda-dhaifu.html' title='Kikwete mchovu, Pinda dhaifu'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-6018472247580422911</id><published>2008-12-10T02:01:00.000-08:00</published><updated>2008-12-10T02:02:33.996-08:00</updated><title type='text'>Tunaongozwa na kizazi cha watu wala watu</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;NCHI hii haiishi vituko.  Kila siku inayokwenda kuna jambo jipya linaloibuka katika nchi hii na kufunika lile lililotangulia au lililotokea siku, wiki, miezi au miaka kadhaa iliyopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika siku za hivi karibuni, Watanzania tumeshuhudia kuibuka kwa mambo kadha wa kadha mazito yanayogusa mwenendo wa mambo kitaifa na pengine kuathiri kwa namna njema au mbaya mustakabali wetu kama nchi leo hii na katika siku zijazo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jambo la kwanza ambalo nimekuwa nikilitazamia katika hayo yote ninayofikiria ni lile linalogusa kesi zinazowakabili baadhi ya watuhumiwa wa wizi wa mabilioni ya fedha kutoka katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) iliyokuwa ndani ya Benki Kuu ya Tanzania katika kipindi cha mwaka 2005. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufikishwa mahakamani kwa watuhumiwa 20, wote wakijimuishwa katika tuhuma mbalimbali ndani ya mtungi mmoja huo huo wa EPA wakiwamo wafanyabiashara wenye majina makubwa wa kiwango wa ‘Jeetu Patel’ kulifungua ukurasa mpya katika mapambano dhidi ya ufisadi, tatizo ambalo hakuna shaka limekuwa kitovu cha ulaji usiostahili kwa miaka mingi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matukio ya kufikishwa mahakamani kwa watuhumiwa hawa yaliyozingira hisia na mwenendo wa mambo nchini kwa takriban wiki mbili, kulianza kuonekana kuwa ni mwanzo wa kikweli kweli wa mafanikio ya vita dhidi ya ufisadi iliyoanzishwa katika kipindi cha karibu mwaka mmoja na ushee uliopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo kama ilivyo ada, tukio hili la kufikishwa mahakamani kwa watuhumiwa hao, lilionekana kuligawa taifa katika makundi mengi kwa kiwango cha kusababisha kila kundi kuibua hoja zinazokinzana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kundi moja la wanaharakati wenye msimamo mkali kuhusu ufisadi, lilikataa na kimsingi limeendelea kukataa kukiona kitendo cha kufikishwa mahakamani kwa watuhumiwa hao 20 wa EPA kuwa hatua ya kwanza ya mafanikio ya serikali, Rais Jakaya Kikwete, wao wenyewe na vyombo vya habari ambavyo kwa pamoja vimekuwa vikipambana na vitendo vya ufisadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa waumini wa kundi hili, mafanikio ya kweli kweli katika sakata hili la EPA yangeonekana iwapo tu, serikali na hususan Rais Jakaya Kikwete wangefumba macho na kuyafikisha mahakamani makampuni yote ambayo kwa namna mmoja au nyingine yalishiriki katika uchotaji wa shilingi bilioni 90 na ushee kati ya zile bilioni 133 zilizoibwa kutoka akaunti nzima ya EPA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo basi, wanaharakati wa kundi hili walikuwa wakiamini kwamba, Rais Kikwete na serikali yake walikuwa hawana sababu hata moja ya kuwatenga wezi wa EPA katika makundi mawili ya wale waliorudisha fedha na wale ambao hawakurudisha na badala yake wote walikuwa wakipaswa kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria na kuiacha korti iamue hatima yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa watu wa kundi hili, hatua ya serikali kutangaza msimamo wa kuwasamehe wale wote waliorejesha fedha, ilikuwa ina maana moja tu kwao; ‘usaliti katika mapambano dhidi ya ufisadi.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wafuatiliaji wasiopendelea upande wowote katika mapambano haya ya ufisadi ni mashahidi wazuri kwamba, uamuzi huu wa serikali kuwasamehe wale wote waliolipa fedha hizo ulizidi kuonekana usiofaa hasa baada ya taarifa kuanza kuvuja kwamba kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd ilikuwa miongoni mwa makampuni yaliyokuwa yamefanikiwa kurejesha fedha zote kiasi cha shilingi bilioni 40 ilichochota EPA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taarifa kwamba Kagoda ilikuwa imefanikiwa kukwepa kitanzi na hatari ya kufikishwa kortini, ilikuwa ni habari mbaya kwa wanaharakati ambao kwao, kampuni hiyo ndiyo iliyokuwa ikistahili kubebeshwa mzigo takriban wote wa EPA pengine kabla ya mtuhumiwa mwingine wowote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Joto la mtazamo wa wanahaerakati hao na mashabiki zao ndiyo ambayo imesababisha baadhi yao hadi leo hii kuendelea kuziona kesi zilizofunguliwa dhidi ya watuhumiwa wa EPA kuwa ni kiini macho na mchezo wa kuigizwa usio na lengo la kuikomboa nchi hii katika tatizo sugu la ufisadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, wanaharakati wa kundi hili wanaitaka serikali, Rais Kikwete na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) kuchukua hatua za kuifikisha Kagoda mahakamani huku wakisahau ukweli wa wazi kabisa kwamba, kampuni hiyo ambayo usajili, mahali ilipo, wamiliki wake na namna ilivyochota fedha ni mambo yenye utata mkubwa inaonekana kuwa na uhusiano wa moja kwa moja wa siri na wa wazi na watu wenye mamlaka au waliopata kushika madaraka makubwa kabisa kidola.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, wanaharakati hawa wa ufisadi ambao kimsingi nayaunga mkono mapambano waliyoyaanzisha, wanasahau kabisa kile ambacho mwanazuoni wa siku nyingi na mwanasheria aliyebobea, Profesa Issa Shivji alipata kukisema kuhusu uhalali wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuendelea kuongoza nchi kikiwa katika taswira yake ya sasa ya chama dola.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nasema hivi kwa sababu utafiti wangu binafsi kama mwanahabari na mtu ambaye katika kipindi cha miaka takriban 10 ya kazi yangu hii nimepata kukutana na kuzungumza na watu kadha wa kadha wakiwamo wale wanaohusishwa na Kagoda umenithibitishia pasipo shaka kwamba kampuni hii inayotajwa, ilianzishwa kwa utaratibu haramu ulioratibiwa na dola na kusimamiwa na baadhi ya viongozi wa juu serikalini na makada wenye nguvu ndani ya CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kwa sababu hiyo basi, ushahidi wa mazingira unaonyesha pasipo shaka kwamba, Kagoda ni jinamizi ambalo mizizi yake ilijengwa na uharamu uliokipa chama tawala uhalali wa kuendelea kuongoza nchi hii, kikiwa na sura yake ile ile ya CCM iliyostawi katika mizingira ya  kidikteta yaliyorithiwa na vyama vya kisoshalisti na kikomunisti duniani zama za vita baridi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna shaka kwamba, Kagoda katika maelezo ya kisomi, ni mfano wa taasisi za kifisadi, iliyojengwa ikihusisha dola na chama tawala ambavyo uhalali wa ubia wao uliwashirikisha wafanyabiashara marafiki na makada wakubwa wa CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mahusiano haya ndiyo ambayo kwa kiwango kikubwa yalisababisha serikali kushikwa na kigugumizi mapema kabisa sakata hili la EPA lilipoanza hata kufanya jitihada za kununua muda kwa kuhalalisha makampuni makubwa mawili ya kimataifa ya ukaguzi wa mahesabu, kwanza Delloite &amp;amp; Touche na kisha Ernst &amp;amp; Young kuyapitia mahesabu ya BoT na EPA na kisha kuwasilisha taarifa zake serikalini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la ajabu kwamba, hata baada ya Delloite &amp;amp; Touche kupitia mahesabu na kubaini wizi uliofanywa na Kagoda na makampuni mengine na serikali kuamua kuipa kampuni nyingine kazi ile ile, wanaharakati hawa wenye msimamo mkali walihadaika na kuipa dola nafasi nyingine ya kujipanga na kutafuta majibu ya namna ya kujinusuru.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la ajabu kwamba, wanaharakati hawa hawa, walikaa kimya na wakashindwa kutambua nini maana ya yote hayo ilhhali katika kumbukumbu zao wakiwa na barua mbili zenye kupingana zilizoandikwa katika kipindi kisichozidi wiki moja na aliyekuwa Waziri wa Fedha na Uchumi, Zakia Meghji kuhusu sakata hilo hilo la EPA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ukweli rahisi kabisa kwamba, iwapo wanaharakati wangekuwa wakiunganishwa na chombo chenye sauti moja kuhusu jambo hili, wangebaini mapema kabisa kwamba, Meghji aliingizwa katika mtego wa barua mbili zinazokinzana si kwa sababu ya udhaifu wake, bali kutokana na shinikizo la kidola ambalo lilikuwa likimtaka yeye kama Waziri wa Fedha kufanya lolote lililokuwa likiwezekana kuinusuru serikali, chama chake na baadhi ya watu wenye mamlaka ambao kwa namna moja au nyingine walitumia madaraka yao vibaya kuihalalishia CCM ushindi mwaka 2005. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii wanapoibuka kwa ujasiri mkubwa, akina Reginald Mengi, Dk. Willibrod Slaa, Zitto Kabwe, M.M Mwanakijiji, Mpayukaji, wanaharakati na wanasiasa wengine wengi makini wakitaka siri ya Kagoda ifichuke, kwa hakika hoja zao zinazidi kuongeza mtihani kwa serikali ambayo imenunua muda mwingi na kutumia kila aina ya mbinu kuinusuru kampuni hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Unapoziangalia juhudi zote hizi za serikali za kuinusuru Kagoda, kwani wakifanya siri taarifa zote za ukaguzi wa mahesabu ya BoT, hata baada ya nyingine kuonekana zimevuja, pili wakitumia kamati ya Mwanyika ambayo hadi leo hii matokeo yake ni kitendawili na tatu wakijaribu kujificha nyuma ya madaraka makubwa ya kisheria ya DPP, ndipo siri na nini hasa kinachofichwa kinapojulikana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika leo hii angetokea Mengi, Slaa, Mwanakijiji na Mpayukaji wakaniuliza ni jambo gani bora unalodhani linatupasa Watanzania tulifanye ili kujua kwa uhakika siri iliyojificha ndani ya Kagoda, sintapita na kuanza kutaja orodha ya wamiliki wa kampuni hiyo tata bali jicho langu na akili yangu nitaielekeza CCM moja kwa moja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nasema hivi kwa sababu naamini tena kwa dhati kabisa kwamba, Kagoda ni mchezo mchafu wa CCM ambao ulitumika kukirejesha madarakani isivyo halali chama hicho tawala mwaka 2005 kikinunua mioyo ya watu kwa fedha haramu hata kuwapa udiwani, ubunge na urais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo basi, kwangu mimi Kagoda si mtu mmoja, wawili watatu au wanne, bali ni mkakati wa miaka mingi, wa CCM na serikali yake wa kufuja matrilioni ya fedha ambazo malengo yake ya msingi ni kuwahudumia wananchi wanaoishi maisha yaliyozongwa na tabu ambazo kimsingi hawastahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo basi, jibu langu kwa Mengi lingekuwa mdudu Kagoda anayetafuta jibu lake ni tunda la uasi lililostawishwa kikatiba na kuipa CCM mamlaka ya dola ambayo yamkini mafisadi wachache wanaopewa baraka na dola wamekuwa wakiyatumia kufuja na kuimaliza nchi hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika staili iliyotumiwa na CCM na serikali yake kuhalalisha wizi BoT mwaka 2005 ndiyo ambayo ilitumika wakati serikali ilipoliingiza taifa katika mradi tata wa Richmond ambao uligharimu madaraka ya watu wachache sana serikalini ambao mpaka kesho naendelea kuamini walitolewa kafara ili kukinusuru chama hicho na fedhaha ya kuanguka kizima kizima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania tunapaswa kutambua kwamba, staili hii ya CCM ya kujivua gamba nusunusu na kuwatoa kafara wachache miongoni mwa mafisadi wengi walio ndani ya chama na serikali yake, ndiyo ambayo imekuwa ikikijengea uhalali wa kuendelea kuwahadaa wananchi wenye mapenzi ya kweli na taifa lao.  &lt;br /&gt;Ni kwa sababu ya kuifahamu CCM kwa jicho hilo ndiyo maana hadi leo hii nimekuwa ni mtu wa mwisho kushangilia kuanza kusikilizwa kwa kesi za EPA, kufikishwa mahakamani kwa Basil Mramba na Daniel Yona mahakamani na kabla ya hapo kulazimishwa kujiuzulu kwa Edward Lowassa, Nazir Karamagi, Andrew Chenge na.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwangu mimi mafanikio ya kweli ya vita dhidi ya ufisadi yataanza wakati Watanzania watakaposimama na kuacha kushangilia siasa za msimu na kuzika madhambi za wana CCM kulana wenyewe kwa wenyewe (Political Cannibalism) ama kwa kulazimishana kujiuzulu, kusutana, kunyosheana vidole, kutishana na kuburuzana mahakamani ilhali chama kinachotoa baraka za wizi huo kuendelea kikiendelea kubakia madarakani kikiwa na sura za watu wale wale wanaohamishana kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Huko ndiko tunakopaswa kwenda.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-6018472247580422911?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/6018472247580422911/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=6018472247580422911&amp;isPopup=true' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6018472247580422911'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6018472247580422911'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2008/12/tunaongozwa-na-kizazi-cha-watu-wala.html' title='Tunaongozwa na kizazi cha watu wala watu'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-7447718049843857274</id><published>2008-11-17T10:41:00.000-08:00</published><updated>2008-11-17T10:46:22.522-08:00</updated><title type='text'></title><content type='html'>&lt;a href="http://4.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSG7q_ilwEI/AAAAAAAAABQ/kvW1mMJfb9w/s1600-h/DSC_0247.JPG"&gt;&lt;img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5269699386285604930" style="DISPLAY: block; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 320px; CURSOR: hand; HEIGHT: 212px; TEXT-ALIGN: center" alt="" src="http://4.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSG7q_ilwEI/AAAAAAAAABQ/kvW1mMJfb9w/s320/DSC_0247.JPG" border="0" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;div&gt;Nikiwa Mwenyekiti wa Kongamano la Ukosefu wa Uongozi Tanzania, nikitoa maelezo mafupi kabla ya kongamano hilo kufunguliwa rasmi na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (katikati). Aliyeketi kulia ni Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad &lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-7447718049843857274?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/7447718049843857274/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=7447718049843857274&amp;isPopup=true' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/7447718049843857274'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/7447718049843857274'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2008/11/nikiwa-mwenyekiti-wa-kongamano-la.html' title=''/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://4.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSG7q_ilwEI/AAAAAAAAABQ/kvW1mMJfb9w/s72-c/DSC_0247.JPG' height='72' width='72'/><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-8223819308905329394</id><published>2008-11-17T10:33:00.000-08:00</published><updated>2008-11-17T10:41:01.461-08:00</updated><title type='text'></title><content type='html'>&lt;a href="http://3.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSG52D7XUGI/AAAAAAAAABI/6Hk9hKr72Yo/s1600-h/DSC_0231.JPG"&gt;&lt;img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5269697377418563682" style="DISPLAY: block; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 320px; CURSOR: hand; HEIGHT: 212px; TEXT-ALIGN: center" alt="" src="http://3.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSG52D7XUGI/AAAAAAAAABI/6Hk9hKr72Yo/s320/DSC_0231.JPG" border="0" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;div&gt;&lt;/div&gt;&lt;br /&gt;Hapa nikimpa mkono wa pongezi Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba mara baada ya kutoa hutuba wakati wa kongamano la Ukosefu wa Uongozi Tanzania (The Vacuum of Leadership in Tanzania) lililofanyika Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kulia ni Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad. Mimi ndiye niliyekuwa mwenyekiti wa kongamano hilo la kihistoria.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-8223819308905329394?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/8223819308905329394/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=8223819308905329394&amp;isPopup=true' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/8223819308905329394'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/8223819308905329394'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2008/11/hapa-nikimpa-mkono-wa-pongezi.html' title=''/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://3.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSG52D7XUGI/AAAAAAAAABI/6Hk9hKr72Yo/s72-c/DSC_0231.JPG' height='72' width='72'/><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-6486433690464740671</id><published>2008-11-17T07:07:00.000-08:00</published><updated>2008-11-17T07:17:39.363-08:00</updated><title type='text'></title><content type='html'>&lt;a href="http://1.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGKkQNc8HI/AAAAAAAAABA/PxCudL-VEbg/s1600-h/DSC_0410.JPG"&gt;&lt;img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5269645394431504498" style="DISPLAY: block; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 320px; CURSOR: hand; HEIGHT: 213px; TEXT-ALIGN: center" alt="" src="http://1.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGKkQNc8HI/AAAAAAAAABA/PxCudL-VEbg/s320/DSC_0410.JPG" border="0" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;Hapa nikiwaonyesha wanafunzi wa chuo kimoja cha uandishi wa habari gazeti letu la michezo na burudani la Sayari ambalo huchapwa kila siku ya Jumatatu na Ijumaa&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;div&gt;&lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-6486433690464740671?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/6486433690464740671/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=6486433690464740671&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6486433690464740671'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6486433690464740671'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2008/11/hapa-nikiwaonyesha-wanafunzi-wa-chuo.html' title=''/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGKkQNc8HI/AAAAAAAAABA/PxCudL-VEbg/s72-c/DSC_0410.JPG' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-6483891892798663491</id><published>2008-11-17T05:25:00.000-08:00</published><updated>2008-11-17T05:37:42.216-08:00</updated><title type='text'>Reginald Mengi na wahariri</title><content type='html'>&lt;a href="http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSFzAL7O3gI/AAAAAAAAAAU/_0G8t5UAzzk/s1600-h/DSC03369.JPG"&gt;&lt;img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5269619486038613506" style="WIDTH: 320px; CURSOR: hand; HEIGHT: 240px" alt="" src="http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSFzAL7O3gI/AAAAAAAAAAU/_0G8t5UAzzk/s320/DSC03369.JPG" border="0" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-6483891892798663491?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/6483891892798663491/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=6483891892798663491&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6483891892798663491'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6483891892798663491'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2008/11/reginald-mengi-na-wahariri.html' title='Reginald Mengi na wahariri'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSFzAL7O3gI/AAAAAAAAAAU/_0G8t5UAzzk/s72-c/DSC03369.JPG' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-5315600579694339576</id><published>2008-11-17T05:13:00.000-08:00</published><updated>2008-11-17T05:14:56.851-08:00</updated><title type='text'>Tarime: Ushahidi wa kupoteza mwelekeo</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;MAMBO yanayotokea Tarime hivi sasa na yale ambayo yamekuwa yakitokea katika miezi ya hivi karibuni yamesababisha nitafakari upya na nirejee kile ambacho nimepata kukiandika siku zilizopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimepata kusema na leo ninasema tena kwamba, nimekuwa miongoni mwa Watanzania ambao nimekuwa nikivutiwa na kuguswa na namna Chama Cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake kilivyosheheni watu wenye upeo mkubwa wa kuona mambo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na hali hiyo kwa kiwango kikubwa ndiyo ambayo imekuwa ikikifanya chama hicho tawala ambacho sala zangu kila siku zimekuwa zikitaka kukiona kikimeguka kiendelee kubakia hai hata katika mazingira ambayo aghalab kingepaswa kusambaratika kama ilivyo hali leo hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna asiyejua kwamba, kwa miaka mingi, hata baada ya kupoteza dira kwa maana ya kuwa na falsafa moja inayokiunganisha, chama hicho kimebakiza jeuri moja kubwa ya kuwa na makada wasomi wazuri wa kariba ya maprofesa na madaktari wa falsafa ambao ama kwa shuruti au kwa mapenzi yao ni wabunge au mawaziri katika serikali ya CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya hao chama hicho pia kwa kutumia nguvu kubwa za kiserikali kimejijengea uhalali unaokipa mamlaka ya kuwafanya wafanyabiashara wakubwa takriban wote walio na majina makubwa kuwa ama wafadhili au makada wa kuheshimika kama si kuogopwa ndani ya chama hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo ni ukweli ulio wazi kwamba, kundi la kwanza la wasomi wanaounda timu muhimu ya ushindi kwa chama hicho, wengi wao wamekuwa wakijiunga au kukiunga mkono chama hicho si kwa sababu ya kuvutiwa na changamoto za kifikra au mwelekeo sahihi wa kifalsafa bali, tamaa ya kupata madaraka na kuwa karibu na watawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ukweli ulio wazi kwamba, wengi miongoni mwa wasomi hao ambao chimbuko lao ni taasisi za elimu ya juu nchini, na ambao kuingia kwao katika siasa limekuwa ni moja ya mambo yanayoibua maswali mengi miongoni mwa wanazuoni wenzao, wamejiunga katika chama hicho tawala si kwa mapenzi yao ya kiitikadi, kimkakati na kivisheni ya chama hicho tawala, bali kiu yao ya kupata fursa ya kuteuliwa kuwa mawaziri na wakati mwingine kupata fursa ya kuwafikia wakubwa walio na madaraka makubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimepata kulisema hilo huko nyuma na likaungwa mkono na wadau wengine wengi kwamba, idadi kubwa ya wasomi wanaoingia katika siasa katika Tanzania wamechochewa zaidi na kushamiri kwa aina ya kipekee ya rushwa inayostawishwa na madaraka ya kidola (state sponsered corruption) inayoshika nafasi kubwa pengine kuliko aina nyingine yoyote ya ufisadi katika zama hizi.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushahidi wa hili haupatikani mbali, kwani unaweza kujionyesha waziwazi unapoangalia aina ya maisha wanayoishi leo hii wasomi wetu hao, walioingia katika siasa na ‘wakabahatika’ kuvuna madaraka ya kiuteuzi yawe ndani ya Kamati za Bunge au ukatibu mkuu, ubalozi na hata katika Baraza la Mawaziri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ufahari na utamu wa maisha ya kimadaraka wanayokutana nayo wanazuoni hao waliogeuka kuwa wasomi, ni mambo yaliyosababisha wafikie hatua ya kupoteza hulka za kawaida za kisomi za kujenga fikra kinzani (critical thinking), kuibua mijadala, kuanzisha mada na wakati mwingine, kuainisha na kutumia njia za kisomi kutatua matatizo ya kisiasa, kiuchumi, kitekinolojia na hata kijamii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kwa sababu hiyo basi ndiyo maana hata leo hii, wakati taiofa likipita katika tanuri la moto mkali wa siasa za kupakana matope, kuzushiana na kuchafuliana majina, kundi la wasomi walio katika siasa na pengine hata wale walio nje, nalo limejikuta likipoteza mwelekeo wa kimsingi wa zama zile za umarxist na uleninist wa miaka ya 1970 na 1980.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kupoteza huko kwa mwelekeo kwa wasomi wetu ndiko ambako kumesababisha leo hii, ndani ya CCM kwa mfano kuibuka na kushamiri kwa majibu ya kishabiki na yasiyo na tija kila linapotokea tatizo la msingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii kwa mfano Watanzania wamejikuta wakiendelea kulishwa upumbavu wa kishirikina na kipuuzi unaozingira mazingira ya ajali iliyopoteza maisha ya aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Chacha Zakayo Wangwe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mazingira ya ajali hii ambayo hadi sasa hakuna taasisi yoyote ya dola au ya kisomi imeonekana kufanya kazi yake sawasawa na kutoa majibu yanayoridhisha, yamesababisha kuibuka kwa nadharia za kizushi ambazo katika taifa linalotafuta siri ya maendeleo ni mwelekeo hatari na wa kimaskini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya wasomi wetu, mmoja mmoja au kupitia katika taasisi zao za kitaaluma kuingilia kati na pengine kulifuatilia suala hilo ili kulinusuru taifa kuingia katika mtego wa hoja za kupikwa na za kufikirika za wanafamilia wa Wangwe, makada wa CCM na akina Mtikila zimesababisha taifa zima kuingia kidogo kidogo kulishwa uongo na kuanza kupoteza imani na watu au taasisi ambazo zinahusishwa na suala hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii ikiwa ni miezi miwili kamili tangu kifo hicho kitokee, jeshi la polisi lililo na wanataaluma makini wa kuchunguza ajali, limekalia matokeo ya uchunguzi wake, ilihali likijua kwamba, mazingira ya kifo cha mbunge huyo yalikuwa yameshaanza kuibua maswali mengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hiyo haitoshi, vyuo vya elimu ya juu nchini ambavyo navyo vinao watalaam katika fani mbalimbali wanaoweza kufuatilia ajali hiyo na kuja na maelezo yao ya kitaalam navyo vimewafungia masandukuni wanazuoni wake na kusababisha nao waingie katika kundi lile lile la kulishwa hadithi za kufikirika za akina Mtikila.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Udhaifu huu wa kitaasisi umesababisha kuibuka kwa mambo mengi na ya kutisha kuhusu ajali hiyo na katika siku za hivi karibuni, wanasiasa wa aina ya Mtikila wamesikika wakitoa ‘taarifa zao za uchunguzi’ ambazo ukizisikiliza unaweza ukajikuta ukishawishika kuamini kwamba, huenda msimuliaji alikuwa eneo la tukio au alikuwa shuhuda katika mpango mzima kabla ya mauti kumkuta Wangwe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la ajabu kwamba, hata baada ya vyombo vya habari kuandika kila aina ya porojo kuhusu mazingira ya kifo hicho vikiwanukuu wabunifu wa hoja na mashabiki wa CCM wanaokihusisha Chadema na kifo hicho, hadi leo hii Jeshi la Polisi na taasisi nyingine za dola nazo kwa namna moja au nyingine zimeingia katika mchezo huo huo wa siasa za kufumbia macho matokeo mabaya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kuthibitisha namna taasisi za dola katika nchi hii zilivyoingizwa katika mtego huu wa kupuuzi na kusababisha vishindwe kujua nini cha kufanya ili kuwaokoa Watanzania na hatari ya kuendelea kujazwa uongo katika bongo zao na kulishwa hadithi za alinacha hadi leo hii, si Freeman Mbowe, Dk. Willibrod Slaa, Zitto Kabwe au Christopher Mtikila waliohojiwa kuhusu kauli suala hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pengine kibaya zaidi ni kwamba, taasisi hizo za dola na hususan polisi, katika mazingira yanayoonyesha kusahau wajibu wao na kutojua athari za uzushi wa namna hii, limeshindwa kuchukua hatua zozote za maana na za wazi dhidi ya wazushi ambao kwa kutoshughulikiwa kwao na kuachwa waendelee kusema uongo kunasababisha watu wengi kuanza kukiamini kile wanachokisema.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuzorota huko kwa mambo kumebabisha kuendelea kwa hoja hizo za kufikirika na juzi katika kampeni za ubunge na udiwani huko Tarime, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe naye akaibua hoja mpya yenye mwelekeo ule ule unaoibua maswali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mazingira ambayo hayafai kupuuzwa hata kidogo, Zitto, mmoja wa wanasiasa wenye ushawishi mkubwa katika zama hizi, akaeleza kusikitishwa kwake na matamshi yanayotolewa na makada wa CCM, Mtikila na yale yaliyosemwa na mmoja wa wake wa marehemu Wangwe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kujua au kutokujua, Zitto akafikia hatua ya kutaka mzizi wa fitina ukatwe kwa Spika wa Bunge kuunda tume huru kuchunguza mazingira ya kifo cha Wangwe na akaeleza kushangazwa na wale ambao wanaweza wakawa na mkono katika ajali hiyo kuwageuzia wengine madhambi yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa staili ile ile ya kawaida ya polisi, kauli hii ya Zitto kama ilivyokuwa kwa kauli zile nyingine zilizotangulia nayo inaonekana kupuuzwa na kuachwa iwaingie Watanzania wengi na pengine kusababisha wachanganyikiwe kwa kiwango cha kuanza kushindwa kujua ni nani anasema kweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pengine jambo baya zaidi ni kwamba, hulka hii ya uzushi unaozingira kifo cha Wangwe imesababisha wakazi wa jimbo hilo wanaojiandaa kumsaka mbunge wao kujikuta wakiwa majeruhi wa siasa chafu na zilizokosa mwelekeo za zama hizi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, wakazi hao wa Tarime ambao wanakabiliwa na matatizo mengi ya kijamii na kiuchumi wamejikuta wakiwa majeruhi wa siasa hizo za fitina badala ya kula uhondo wa hoja zitakazoeleza mipango ya wagombea ya kuwaondoa katika hatari ya mapigano ya mara kwa mara ya koo, umaskini na kilimo cha bangi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hiyo haitoshi, kampeni hizo za Tarime ambazo leo hii zimethibitisha kwamba vyama viwili vya CCM na Chadema ndivyo vilivyo na ushindani mkuwa zimeweka kando kabisa namna ya kuiwezesha wilaya hiyo kuweza kutumia vyema na kwa manufaa yake fursa yake ya kupakana na Kenya kwa maslahi ya wana Tarime na Watanzania kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siasa hizi chafu zinazotungwa zikizingira jina la Wangwe zimesababisha wananchi wa Tarime wanyimwe fursa ya kuvisikia vyama na wagombea ubunge na udiwani wakieleza ni nini watakifanya kumaliza uhasama wa miaka mingi kati yao wakazi wa eneo hilo na kampuni ya uchimbaji madini ya North Mara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika udhaifu huu wa mambo wa kuweka mbele siasa za majungu, uzushi, kufitiniana, kuchafuana na kupakana matope ndizo ambazo leo hii zimebabisha Tanzania kama taifa kupoteza mwelekeo na kujikuta tukishindwa kuendana na mabadiliko ya kiuchumi na kiteknolojia yanayoikabili dunia ya leo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siasa zenye mwelekeo huu ambazo kwa bahati mbaya zimekuwa zikishabikiwa kwa njia ya siri na ya wazi na viongozi wenye dhamana kubwa kabisa nchini, ndizo zilizozingira masuala makubwa makubwa takriban yote ya siku za hivi karibuni. Tunapaswa kutoka huko iwapo tunataka kupona.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-5315600579694339576?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/5315600579694339576/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=5315600579694339576&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/5315600579694339576'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/5315600579694339576'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2008/11/tarime-ushahidi-wa-kupoteza-mwelekeo.html' title='Tarime: Ushahidi wa kupoteza mwelekeo'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-8821556044264639796</id><published>2008-11-17T05:09:00.000-08:00</published><updated>2008-11-17T05:10:37.220-08:00</updated><title type='text'>Hii ni lala salama ya Kikwete</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;HALI ya hewa kisiasa imebadilika na inaendelea kubadilika kila kukicha hapa nchini kiasi cha kuifanya serikali na vyama vya siasa kuanza kukaa mguu sawa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mabadiliko hayo ya upepo wa kisiasa yamesababisha harakati za kuelekea katika hekaheka za uchaguzi mkuu miaka miwili baadaye kuanza mapema, pengine kwa namna na kwa njia tofauti na ambavyo imezoeleka kwa miaka mingi huko nyuma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dalili za wazi za kuanza kwa harakati hizo za kisiasa zimeanza kujionyesha na hivi sasa wanasiasa katika makundi na mitazamo tofauti wanaonekana kuanza kujijengea mazingira ya kujihalalishia ushindi wakati wa uchaguzi wa mkuu wa mwaka 2010.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matamshi yanayotolewa na wanasiasa hivi sasa yameanza kuchukua sura za wazi inayoonyesha kuanza kujipanga sambamba na kujaribu kuangalia mustakabali wao kwa siku zijazo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiyapima na kuyaangalia katika mizani sawia ya kisiasa matukio ya siku za hivi karibuni, unaweza ukashangazwa na namna wanasiasa wetu wanaopaswa kutambua uteke wa nchi hii kiuchumi wanavyopigana vikumbo kwa namna na kwa njia mbalimbali kujahalalishia ushindi wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matumizi makubwa ya fedha yaliyoshuhudiwa na wadau mbalimbali wa masuala ya siasa wakati wa uchaguzi mdogo wa ubunge wa Tarime ambako tulishuhudia wapigakura ‘wakinunuliwa’ kwa gharama kubwa, ni moja ya mifano hai ya namna mwaka 2010 unavyopewa mtazamo wa aina yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi ya wafuatiliaji wa siasa za ndani ya nchi wanaweza kukubaliana nami nikisema kwamba, juhudi kubwa zilizokuwa zikifanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tarime zililenga zaidi mwaka 2010 na si kuziba pengo la Chacha Wangwe aliyefariki dunia kwa ajali ya gari mwishoni mwa Julai mwaka huu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Makada wa CCM wakiongozwa na Katibu Mkuu wao, Yussuf Makamba walikuwa wamepania kwa nguvu zote kufanya kile walichokifanya katika jimbo la Kiteto miezi kadhaa iliyopita, dhidi ya wapinzani ambao katika miezi ya hivi karibuni wamejipambanua kuwa majemedari wa ufisadi, vita ambayo hakuna shaka sumu yake imeanza kuwaingia kwa kasi kubwa wananchi wa maeneo mbalimbali nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Makamanda wa propaganda wa CCM, chama ambacho kimefanikiwa kupenya hadi katika mishipa ya watendaji wakuu wa vyombo vya dola, vikiwamo vile vya ulinzi na usalama kama jeshi la polisi, walilazimika kufanya kila linalowezekana kulitwa jimbo la Tarime wakijua kwamba kufanya hivyo kulikuwa na maana moja kubwa; kushindwa kwa vita wanayoiharamisha kwa nguvu zote ya ufisadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni bahati njema kwamba, upepo wa mambo haukwenda kama ilivyotarajiwa kwa CCM (walioungana na vyama vingine vichache mamluki) na ndiyo maana kwa namna ambayo si rahisi kuieleza, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kikafanikiwa kupenya ukuta mgumu kabisa na kulirejesha jimbo hilo mikononi mwake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika ushindi wa Chadema Tarime kwa namna ya kipekee ukabadili upepo na kuchukua sura tofauti ukiungwa mkono na watumishi wa taasisi za umma, watendaji wakuu serikalini, mawaziri na mwisho wa yote makada maarufu wengi wa CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kishindo hiki cha ushindi wa Chadema kwa kiwango kikubwa kikabadili kabisa ndoto za CCM za kukizorotesha chama hicho na kukifuta katika mioyo ya watu ambazo zilianza mapema tangu aliyekuwa mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe akiwa hai.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika muanguko huo wa CCM ukawa pigo na funzo kubwa, dhidi ya hoja za kizushi na kuchuliana zilizoasisiwa na mabingwa wa fitina wa chama hicho tawala dhidi ya Chadema na hususan viongozi wake wakuu, Freeman Mbowe, Dk. Willibrod Slaa na Zitto Kabwe waliohusishwa katika ‘kutengeneza’ ajali na hatimaye umauti wa Wangwe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa siasa hizo za kufitiana, zilizoanzishwa wakati Benjamin Mkapa akiwa rais, kwanza zikiwalenga wana CCM wa kariba ya akina, Hassy Kitine, Profesa Philemon Mbilinyi, Frederick Sumaye, Abdallah Kigoda, Wilson Masilingi, John Magufuli, Mark Mwandosya, Dk. Salim Ahmed Salim na wengine wengi zikagonga mwamba. Tarime ikaandika historia mpya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa watu wanaofuatilia mwenendo wa mambo ya kisiasa ndani ya CCM na pengine serikalini ni mashahidi kwamba, ushindi wa Chadema katika jimbo la Tarime, ukawa kielelezo kingine bayana kwamba, lile kundi la ‘mtandao masalia’ linalojaribu kujitutumua likilenga kuhujumu harakati za kuisafisha nchi likajikuta likiangushwa kwa kishindo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matukio haya ya kustaajabisha kisiasa yaliyoanza kuthibitika (na si kutokea) hapa nchini Februari mwaka huu, wakati Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe iliposoma hotuba yake bungeni yamepokewa kwa hisia tofauti na wafuatiliaji mbalimbali wa masuala ya siasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwangu mimi mambo haya yanathibitisha jambo moja la wazi kabisa kwamba, ardhi ya Tanzania na raslimali zake zote imefikia hatua ya kusema hapana na sasa imeanza kudai mabadiliko makubwa kabisa ya kisiasa, kijamii na kiuchumi yanayolenga kulinufaisha taifa zima na si kikundi kidogo cha wanyang’anyi waliofikia hatua ya kutaka kuibinafsisha CCM, kuiteka nyara serikali na kuiuza nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, kikundi hiki cha watu wachache, wenye uwezo mkubwa kifedha na kiuchumi na ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakitumia nguvu zao hizo kuendesha mambo, bado hawajakata tamaa na sasa wanafanya kila linalowezekana kuhakikisha wanabadili upepo wa kisiasa na kurejea tena katika ulingo wa kisiasa mwaka 2010.&lt;br /&gt;        &lt;br /&gt;Hata hivyo, kwa namna ya kushangaza kikundi hicho cha wanasiasa wenye nguvu kabisa na ambao wakati fulani walijitambulisha kama watu wasioshindwa na mtu yeyote katika lolote watakaloamua wamejikuta wakiendelea kubakia kuwa majeruhi wa siasa za zama hizi, wakichafuka hatua kwa hatua kiasi cha kuanza kuhatarisha uhuru wao katika kipindi kifupi tu kijacho, iwapo hawatakubali kushindwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfa maji haachi kutapatapa, kifo hiki cha kisiasa cha kikundi hiki kidogo cha watu ambao kwa muda mrefu wamekuwa na ushawishi mkubwa, kimeamua kurejea katika mstari wake wa awali na sasa kimeamua kuchukua hatua mbadala, kikiamini kwa kufanya hivyo kitakuwa kimewafunga midomo watu wa aina ya akina Mbowe, Slaa, Zitto, Mnyika na wengine ambao upepo wa kisiasa wa siku za hivi karibuni unapunga upande wao.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu hawa kwa namna ya ajabu wameamua kupambana na vyombo vya habari binafsi ambavyo kwa mtazamo wao, wanaviona kuwa vimekuwa mstari wa mbele kuwaangusha, kuwaumbua na wakati mwingine wakisema vimekuwa vikiwazushia uongo mwingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kufanikisha hilo, kikundi hiki cha wanasiasa kimeamua kuyarejesha mitaani baadhi ya magazeti ambayo kimekuwa kikiyatumia kupika propaganda zao za kizushi na kifitini kama njia ya kueneza sumu za kisiasa, lengo likiwa ni kuwahadaa Watanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sambamba na hilo, kwa malengo hay ohayo ya kujipanga upya, kikundi hiki cha wanamtandao masalia kimefikia hatua ya kuwarejesha katika ulingo wa habari baadhi ya wana habari wanaowaamini kwamba wanao uwezo mkubwa wa  kutengeneza hoja nzito wakitumia kalamu zao kutengeneza habari kwa malengo ya kipropaganda (spinning) .&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, wanasiasa wa kundi hili wanafanya hivyo leo wakisahau kwamba, baadhi ya wanahabari hao, tayari wameshaanza kutambua mchele ni upi na pumba ni zipi na hivyo kurejea kwao katika kipindi kifupi kijacho kunaweza kuwa tukio litakalowaumiza wao wenye zaidi kuliko kuwasaidia. Tusubiri tuone haya yakitokea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wataalam hao wa fitina wakijipanga kuchukua hatua hizo wananchi waliosambaa katika maeneo mbalimbali nchini, nao wanaonekana kuguswa na upepo mkali wa mabadiliko na hivyo nao kujikuta wakiwa na kiu ya kufanya kile ambacho kimefanywa na wenzao wa Tarime.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Upepo huu wa mambo ambao sina shaka hata kidogo kuamini kwamba una nguvu kubwa zaidi kuliko ilivyo kwa mikakati ya kujipanga ya kundi hili jipya la mtandao masalia, unayo nafasi kubwa ya kutujengea taifa jipya, lenye matumaini mapya mara baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kujulikana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Unabii wa kisiasa ninaouona katika hili ni kwamba, katika kipindi kifupi au kirefu huko tuendako, kabla ya mwaka 2010, Rais Kikwete ambaye hadi hivi sasa ameendelea kujaribu kutofungamana na kundi lolote kwa uwazi ndani ya CCM na serikalini atalazimika kuachana na hulka yake hii ya kutofungamana na upande wowote na kuungana na wananchi kwa maelfu wanaolilia mabadiliko na neema aliyowaahidi mwaka 2005.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kwamba kabla hajafikwa na maono hayo mapya, Kikwete atalazimika kuyakubali mabadiliko kwa kuanza kuitakasa ofisi yake ili ichukue sura halisi ya utakatifu wa ikulu uliopaswa kuwapo pale.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-8821556044264639796?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/8821556044264639796/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=8821556044264639796&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/8821556044264639796'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/8821556044264639796'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2008/11/hii-ni-lala-salama-ya-kikwete.html' title='Hii ni lala salama ya Kikwete'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-6342542819378977607</id><published>2008-11-17T05:03:00.001-08:00</published><updated>2008-11-17T05:03:41.749-08:00</updated><title type='text'>Tumefika pabaya, neema yaja</title><content type='html'>Tumefika pabaya, neema yaja&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;NAANDIKA makala hii leo hii wakati taifa likipita katika kipindi cha kukata tamaa kwa upande mmoja na wakati huo huo kukiwa na kufufuka kwa hali ya matumaini kwa upande mwingine hususan kwa makundi kadhaa ya watu wanaoamini wameanza kuzika ufu wa kitaifa uliolikabili taifa hili kwa zaidi ya miaka 40 sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matukio ya hivi karibuni kabisa, ya migomo ya walimu, kufungiwa kwa miezi mitatu kwa gazeti la kila wiki la MwanaHALISI, serikali kukimbilia mahakamani kuwazuia walimu kugoma, ya wananchi wa Chunya kuurushia mawe msafara wa Rais Jakaya Kikwete na ushindi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mdogo wa ubunge wa Tarime ni mambo ambayo ama yanaeleza namna watu walivyokata tamaa au waliovyoanza kufufua matumaini yaliyoanza kutoweka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika yote hayo jambo moja ni dhahiri nalo ni kwamba, tupende tusipende, tukubali au tukatae, ahadi na mbwembwe nyingi za viongozi wetu ambao wamekuwa wakitembea kifua mbele wakitamba kwamba, wamelifanyia mema mengi taifa hili, hata kustahili kuenziwa kwa maneno, kalamu na kura ni mambo ambayo yanafurahisha genge zaidi kuliko kujenga misingi ya kuondokana na umaskini ulioota mizizi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushahidi wa hayo ni rahisi kabisa. Miaka 45 na ushee baada ya uhuru majigambo ya viongozi wetu kutamba kujenga kilomita nyingi tu za barabara za lami na za kokoto, kuongeza idadi ya wanafunzi wanaojiunga na elimu ya msingi, sekondari na vyuo vikuu na sifa nyingi nyingine zinazofanana na hizo ni mambo ambayo yameshindwa kulinusuru taifa hili na fedheha ya ufukara uliokithiri, maradhi yasiyokoma na ujinga usiomithilika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mambo makuu matatu ambayo Serikali ya Kwanza ya Tanzania (1961-1985) iliyaainisha kuwa maadui wakuu watatu wa maendeleo; ujinga, maradhi na umaskini yameendelea kubakia vidonda ndugu kwa taifa hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii ninalazimika kuyakumbuka na kuyarejea mahojiano aliyofanya Rais Kikwete na jarida la NewAfrican (soma toleo la Juni mwaka jana) kuhusu dhamira ya serikali yake kufanikisha mpango wa Elimu ya Msingi kwa Wote (UPE) baada ya kubaini kuporomoka kwa maelezo yanayoonyesha kuwa suala hilo ni jipya sana hapa nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati Kikwete akisema UPE ya zama zake imeingiza masomoni asilimia 96 ya watoto wote wanaopaswa kuwa darasani, ukweli ni kwamba kiwango kama hicho au zaidi yake kilipata kufikiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere mwishoni mwa miaka ya 1970.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiuweka kando ujinga, adui mwingine maradhi naye pia amekuwa tatizo kubwa kabisa linalokuwa. Ukiuweka kando ukimwi, maradhi kama kifua kikuu, malaria na kipindupindu ambayo leo hii yanaundiwa mikakati mipya na ya kila jina kukabiliana nayo, yamekuwa katika kuta za maandishi maeneo mbalimbali kwa zaidi ya miaka 35 sasa pasipo kupatiwa ufumbuzi. Nani halijui hilo!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati ukimwi ukiwa sababu mojawapo ya kurejea kwa kasi kwa kifua kikuu, ukweli wa kitakwimu unaonyesha kwamba, ugonjwa huo kama yalivyo hayo mengine (malaria na kipindupindu) yameendelea kuwa sugu yakichagizwa na umaskini mkubwa unaolikabili taifa hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo wakati viongozi wetu wakipiga mbinje kujivunia matunda ya utawala wao, kwa miaka hiyo yote baada ya kuambiwa kuwa tuko vitani tukikabiliana na umaskini, Watanzania tunaendelea kuwa miongoni mwa mataifa sita maskini zaidi duniani. Kwa maelezo yoyote yale hii ni aibu na fedheha.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya sana, wakati baadhi yetu tukitambua kuwa Watanzania, kuanzia kwa viongozi wao hadi kwetu wananchi wa kawaida, tunao wajibu wa kutafuta ufumbuzi wa matatizo haya, baadhi ya wenzetu, kwa sababu wanazozijua wao wameamua kudhihaki juhudi hizo na sasa wanavinyoshea vyombo vya habari kidole eti vinaendekeza ufisadi kama vile hakuna masuala mengine ya muhimu. Kwao vita dhidi ya ufisadi ni wivu, majungu, chuki na hadaa, hawa ndiyo wale ambao wamefikia hatua ya kuipa rushwa jina zuri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uamuzi wa baadhi yetu kuwakosoa viongozi fulani wasio waadilifu, kufichua baadhi ya maovu yao hata kama hayana harufu nzuri katika pua zetu na sura nzuri macho yetu, kuwakumbusha wajibu wao, na kukemea inapobidi kwa lengo la kuimarisha misingi ya utawala bora tukitumia kalamu zetu, unaonekana kuwa ni wa kipuuzi na usiolitakia mema taifa hili. Siku hizi wanasema tunataka nchi hii isitawalike.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Viongozi wa serikali wanaokosolewa kwa makali na uzito unaolingana na ukubwa wa makosa yao, wameanza kugeuka mbogo. Wanashambulia kila mmoja anayeonekana kujaribu kuhatarisha madaraka yao ambayo, badala ya kuyaona kuwa dhamana na wajibu wa kuwatumikia wananchi wameyageuza kuwa mtaji wa ulaji wa aina ile ambayo Augustine Mrema alipata kuuita ‘ya kula bila kunawa.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kile ambacho, mchambuzi mmoja maarufu wa masuala ya kisiasa alipata kukiandika akiwataja baadhi ya watu kuwa ni mamluki wa viongozi wa dola, ndicho kinachoonekana kutokea hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maelfu ya Watanzania wanaosoma safu hii, wanapaswa kutambua kuwa, huko tuendako, kalamu kali dhidi ya ukiukwaji wa uongozi bora unaofanywa na baadhi ya watu wenye madaraka ndani ya CCM na katika serikali zake zinaweza kukabiliana na dhoruba kutoka kwa mamluki wanaojulikana na ambao wameamua ama kujibebesha au kubebeshwa ukibaraka wa kifikra. Tayari baadhi ya mamluki hao wameshaanza kujitutumia ingawa ni bahati mbaya sana kwamba Mungu amewapa kisogo. Wasome alama za nyakati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pia, viongozi hao hao kwa kadri inavyoonekana, wameshaanza kujipanga tayari kukabiliana na jambo lolote lile linaloelekea kufanana na wimbi la upinzani kutoka kwa wazalendo wa kweli wa nchi hii na tukio la kufungiwa kwa MwanaHALISI ni moja ya mikakati ya namna hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya uchaguzi mdogo wa ubunge wa Tarime yaliyokipa ushindi Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) dhidi ya ubia haramu uliokishirikisha CCM na vyama vingine viwili vya upinzani ni kielelezo cha namna Watanzania wanavyoanza kuonyesha waziwazi kuchoshwa na hadaa za kisiasa za watawala wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la kheri kwamba, hayo yaliyotokea Tarime yamekuja wakati huu, tena katika kipindi ambacho viongozi wetu watatu wakuu wa kitaifa, Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wakifanya ziara za kupishana ama angani au ardhini wakizunguka kutoka kona moja ya nchi kwenda nyingine huku mara kadhaa wakibebebeana majukumu ya kuwakilishana katika mikutano au ziara za kimataifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waswahili husema, mwenye macho haambiwi tazama, leo hii ninapoandika makala hii, viongozi hao watatu kila mmoja yuko nje ya ofisi yake wakizunguka mikoani kufanya kile wanachojaribu kukifanya kionekane kuwa ni kuhamasisha shughuli za maendeleo ilihali wakijua fika kwamba, kwa uzito wa nafasi zao za kidola, ziara zao ni kitovu kikuu cha matumizi makubwa ya fedha yasiyo ya lazima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika kabisa, ninaweza nikasema pasipo kutafuna maneno kwamba, mizunguko ya Rais Kikwete, Ali Mohammed Shein na Mizengo Pinda mikoani hivi sasa imesababisha viongozi wa ngazi za mikoa na wilaya wapoteze maana halisi ya kuwapo kwao.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kweli ni jambo la bahati mbaya kwamba, pamoja na mbwembwe nyingi za ving’ora vya wakuu hao, kauli mbiu ya Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya imegeuka historia na sasa si yeye rais au wasaidi wake hao wawili wanaoonekana kuwa na ubavu wa kuipigania. Kwa wananchi kama ilivyotokea majuzi mkoani Mbeya, lugha imebakia moja tu; ufisadi, ufisadi ufisadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kile ambacho Jenerali Ulimwengu amepata kukielezea na nikakikariri mara kadhaa kuhusu ‘urafiki wa hatari na uliovuka mipaka kati ya wanahabari na wanasiasa’ ndicho ambacho leo hii tusipokuwa macho, kinaweza kikaivuruga taaluma ya habari yenye wajibu wa kuongoza njia, iwapo tutabebwa na mkumbo wa mambo&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilipata kuandika kwamba, Kwame Nkrumah angeamka leo hii kutoka kaburini na kufanya tathmini ya kile kinachoonekana kuwa mafanikio ya sera za soko huria na mfumo wa vyama vingi ninao uhakika jina la kitabu chake lisingelikuwa tena; ‘New Colonialism The Highest Stage of Imperialism’ (Ukoloni mambo leo ni hatua ya mwisho ya ubeberu).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Badala yake mwanasiasa na mwanazuoni huyo kwa namna yeyote ile Neo Colonialism ingebadilika na kuwa Neo Liberalism kwa maana ya Udikteta mambo leo ambao watawala wanaoshinda uchaguzi chini ya mfumo haramu wa vyama vingi uliojaa mizengwe iliyokithiri wanavyojaribu kutumia ushindi wao huo kuminya uhuru wa habari, uhuru wa vyama vingi, uhuru wa kufikiri na dhana nyingine za namna hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sikuishia hapo nilikwenda mbali zaidi nikasema; Nkrumah angeshangaa kubaini kuwa ubeberu umebadilika. Angestaajabu kuona watawala wa wa Kiafrika wakiwa wamejenga mtandao wa mahusiano ya ajabu kabisa na mabeberu walioupa jina la utandawazi. Mahusiano haya ndiyo yaliyowapa jeuri watawala wetu hata kuwa na jeuri ya kutumia udikteta mambo leo.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika udikteta mambo leo wa watawala wengi wa Kiafrika, umefanikiwa kuihadaa dunia kuwa demokrasia ya vyama vingi, uhuru wa habari, soko huria la kishindani ni mambo yanayofanya kazi pasipo shida yoyote, ilhali hali ikiwa tofauti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siyo jambo la siri kwa Watanzania wachambuzi wa mambo kutambua kuwa, udikteta mambo leo wa watawala wetu wanaojivunia ushindi wa kishindo ni matokeo ya wazi ya kazi kubwa iliyofanywa ya kuwanyonga wapinzani kwa fitina za uzushi, sheria ngumu na kandamizi zikiwamo zile 40 ambazo Tume ya Jaji Nyalali ilipata kupendekeza zifutwe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ukweli unaojulikana wazi kwamba, ushindi wa asilimia 80 ni matokeo ya kazi batili itakayobakia kuwa historia ya nchi hii ambayo ilivigeuza vyombo vyetu vya habari na na baadhi ya sisi wanahabari (Watanzania watusamehe) kuwa taasisi mahususi za uenezi za CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la ajabu kabisa kwamba, leo hii, ushindi huo wa kishindo wa asilimia 80 ambao badala ya kuwa mzigo na dhamana isiyobebeka ya wajibu wa kuwatumikia wapigakura umegeuka na kuwa jeuri ya kuwasakama na kuwazulia mambo wakosoaji wengi ninaoamini wanafanya hivyo kwa nia njema kabisa.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujinga wa sisi Watanzania tulio wengi kuendelea kuuona mfumo wa vyama vingi kuwa eti msingi wa kusambaratika kwa umoja wetu, na dalili mbaya za kutoweka kwa amani na utulivu, tukitahadharishwa kuwa makini tusije tukafikwa na yale yaliyowahi kuwafika wenzetu wa Rwanda, Burundi, Kongo, Sierra Leone na kwingineko una sehemu kubwa katika ushindi huo wa asilimia 80.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi Watanzania tumesahau kwamba, asilimia 80 ya watu ambao walipiga kura ya maoni wakitaka mfumo wa chama kimoja uendelee mbele ya Tume ya Jaji Nyalali  ya mwaka 1991 na 1992 ndiyo matunda ya ushindi wa CCM leo hii ambayo viongozi wake wanapita kifua mbele wakiwakebehi wachambuzi wa mambo wanaoikosoa serikali leo hii kwa kuwapa majina mabaya na hata kuwatenga na mema mengine yote wanayostahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika viongozi wetu hao wanapaswa kutambua na kujilazimisha kukubalia ukweli mchungu kwamba, filimbi iliyolia Tarime hivi majuzi na matukio mengine ya fadhaa wanayokabiliana nayo mitaani ni ushahidi wa wazi wa ujio wa Tanzania yenye neema ambayo inaweza ikajengwa na wale ambao leo wanaonekana wasaliti, wapiga domo na watu wasio na maana. Huko ndiko tuendako.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-6342542819378977607?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/6342542819378977607/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=6342542819378977607&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6342542819378977607'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6342542819378977607'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2008/11/tumefika-pabaya-neema-yaja_17.html' title='Tumefika pabaya, neema yaja'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-2201681741777554697</id><published>2008-10-13T08:35:00.000-07:00</published><updated>2008-10-13T08:39:45.826-07:00</updated><title type='text'>Tuna chembechembe za udikteta wa Mugabe</title><content type='html'>jpkhxTunazo chembechembe&lt;br /&gt;za udikteta wa Mugabe&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;NIMEGUSWA na mambo makubwa mawili au matatu hivi yaliyotokea katika siku za karibuni ndani na nje ya mipaka yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukio la kwanza ni kauli rasmi ya serikali iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ambayo aliielekeza kwa Rais wa Zimbabwe Robart Mugabe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika tamko hilo, serikali ilieleza kuhusu kuwa kwake na mashaka juu ya hali ya kisiasa nchini Zimbabwe wakati nchi hiyo ikijiandaa kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Membe katika tamko hilo la serikali alisema Tanzania ilikuwa ina wasiwasi mkubwa iwapo uchaguzi huo ungekuwa ni huru na wa haki, kutokana na matukio na vitendo vya ghasia vinavyoendelea pamoja na matamshi ya viongozi mbalimbali wa serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika tamko hilo la serikali, Membe alimkariri Rais Jakaya Kikwete akisema kuwa, pamoja na urafiki wa kihistoria uliopo baina ya Tanzania na Zimbabwe, Tanzania imeshtushwa na yanayoendelea katika taifa hilo la kusini mwa Afrika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Rais Kikwete amesema Tanzania ni rafiki mkubwa wa Zimbabwe kihistoria. Na mwaka 1980 walipoanzisha mapambano ya kudai ardhi, tulisimama nao pamoja na dunia nzima inajua. Hivyo inapofika katika suala la ardhi Tanzania ipo pamoja nao, lakini inapofikia kwenye suala la uongozi inaleta shida,” alisema Membe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aliongeza kuwa, pamoja na urafiki huo, Tanzania imeshtushwa na ghasia zinazoendelea nchini Zimbabwe, hivyo Kamati ya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), iliamua kila nchi ililizungumze suala hilo kwa nchi yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Membe alisema kutokana na hali hiyo, Kikao cha Ushirikiano wa Maendeleo wa Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), kilikutana Juni 17 mwaka huu, nchini Malawi na kuamua kupeleka waangalizi 380 wa uchaguzi nchini humo, ili kufuatilia uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Juni 28.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maelezo ya Waziri Membe, taarifa kuhusu mgogoro huo wa Zimbabwe walizipokea kutoka kwa Katibu Mtendaji wa SADC, Dk. Tomaz Salomao, ambaye alitembelea nchi hiyo na kuelezea hali tete ya kisiasa, uchumi na usalama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tamko hilo la Membe lilifuatiwa na kuondoka kwa balozi wa Zimbabwe hapa nchini ambalo tayari limesababisha kuibuka kwa minong’ono ambayo juzi ilimfanya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe aielezee hatua hiyo kuwa ni kuibuka kwa mgogoro wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Zimbabwe. Hilo ndilo tukio la kwanza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siku chache tu baada ya kutokea kwa hali hiyo, nchini Zimbabwe, mgombea urais kwa tiketi ya chama cha Movement for Democratic Change (MDC), Morgan Tsvangirai alitangaza kujitoa katika kinyang’anyiro cha urais akisema anafanya hivyo kutokana na kujiridhisha pasipo shaka kuwa, hali ya kisiasa nchini Zimbabwe ilikuwa mbaya kisiasa na kulikuwa hakuna uwezekano wowote wa kufanyika kwa uchaguzi huru na wa haki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uamuzi huo wa Tsvangirai mbali ya kuthibitisha wasiwasi uliokwishaelezwa na Tanzania umedhihirisha na kuweka bayana udikteta wa wazi wa Robert Mugabe ambaye kwa miaka mingi amekuwa akichukuliwa kuwa mwanapinduzi na mzalendo wa kweli wa nchi yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mara ya kwanza, mwenendo wa mambo ndani ya Zimbabwe katika kipindi cha mwaka huu, kimesababisha Mugabe ambaye alikuwa akiungwa mkono na mataifa kadhaa ya Kiafrika ikiwamo Tanzania kwa miaka mingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi yetu tungali tukikumbuka mahojiano aliyofanya Rais Jakaya Kikwete na gazeti la Financial Times la Uingereza na yakachapwa Oktoba 5 mwaka huo huo wa jana wakati akiwa katika jiji la Paris, nchini Ufaransa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mahojiano hayo, Kikwete alieleza bayana kumuunga mkono Rais Mugabe na akayataka mataifa makubwa duniani kuacha kumnyoshea kidole akisema kwamba, Tanzania ilikuwa ikiamini kwamba Wazimbabwe wenyewe ndiyo watakaokuwa na jukumu la kuamua kidemokrasia hatima ya taifa lao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno yake mwenyewe Kikwete wa mwaka jana alisikika akisema kwa kimombo; "Tanzania is standing by the people of Zimbabwe, including President Mugabe…We subscribe to the idea of working with them to get a solution, because if you end up condemning and insulting [Mugabe] he will not listen to you. Mugabe is there. He is president; he has been elected. If Tanzania said, 'You are hopeless! A murderer! A violator of basic human rights!' does that remove Mugabe from office? It doesn't."&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa tafsiri rahisi Kikwete alikuwa akisema; "Tanzania iko pamoja na wananchi wa Zimbabwe, akiwamo Rais Mugabe. Tunaunga mkono jitihada za kufanya nao kazi ili kupata suluhisho kwani iwapo mtaishia kumlaumu na kumdhihaki Mugabe hataweza kuwasikiliza. Mugabe yupo pale.Ndiye rais aliyechaguliwa. Kama Tanzania itamwita mtu aliyepotea njia, muuaji, na mkiukaji wa haki za msingi za binadamu sidhani kwamba maneno hayo yataweza kumuondoa madarakani.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimsingi msimamo huo wa Kikwete juu ya Mugabe ndiyo ule ule ambao ulikuwa ukichukuliwa kwa miaka yote na Benjamin Mkapa wakati huo akiwa Rais wa Tanzania katika kipindi chote cha miaka 10.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkapa anakumbukwa kama kiongozi mmoja wa Afrika aliyesimama bega kwa bega na Mugabe akimtetea kwa nguvu kubwa ndani ya Jumuiya ya Madola, katika makongamano ya kisiasa na kiuchumi ya kimataifa na hata alipokuwa akizungumza na wanahabari ndani na nje ya nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si hivyo tu, Mkapa alipata kuandika makala nzito akimuelezea Mugabe na kutoa msimamo kuhusu Tanzania kumuunga mkono Mugabe dhidi ya kile kilichokuwa kikionekana kuwa ni ubeberu wa mataifa makubwa ya magharibi dhidi ya ustaarabu wa Kiafrika na wa watu wa Zimbabwe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa Mkapa, kama ilivyokuwa kwa Mugabe, wapinzani wa MDC walikuwa si lolote bali vibaraka wa mataifa ya magharibi ambao wametumwa si kwa lengo jingine bali kuwarejesha wakoloni wa Kingereza katika ardhi ya Zimbabwe kupitia mlango wa nyuma. Msimamo huo ndiyo unaotumika leo kuhalalisha udikteta wa Mugabe dhidi ya upinzani nchini mwake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika sehemu kadhaa za makala yake kwa kuhusu Mugabe na Zimbabwe Mkapa aliandika yafuatayo: kwanza aliyaonya mataifa makubwa kuhusu hatari ya wao kuwachagulia Waafrika marafiki na akasema pasipo kusita kwamba, Mugabe hakuwa tu rafiki wa Tanzania bali komredi yaani mwenzi katika harakati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuishia hapo alikwenda mbele zaidi na asema, Tanzania itaendelea kusimama pamoja na Mugabe akisisitiza kuwa, kama rafiki Watanzania watashikamana na Wazimbabwe wakati wa amani na wakati wa shida pia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii maneno hayo ya Mkapa yanazidi kupoteza maana yake halisi. Mugabe anazidi kuwa dikteta kwa gharama kubwa za maisha ya wananchi wa taifa lake ambao hivi sasa wanakabiliwa na vitanzi vingi vya hali ngumu ya kiuchumi, kijamii na kiusalama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kwamba Watanzania wengi ambao miaka mitatu au mine hivi walikuwa wakimuona Mugabe kuwa mwanamapinduzi wa kuigwa wa Afrika na mzalendo wa kweli wameanza kubadili mtazamo wao na kwa hakika Mkapa angepewa fursa ya kuandika makala leo hii kuhusu Zimbabwe huenda asingerejea yale aliyoyaandika wakati huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwenendo huo wa mambo ndiyo ambao sasa umezaa ajenda mpya na ya aina yake ndani ya Bunge la Zimbabwe, ikianzishwa na Zitto na kupewa baraka zake na Spika wa Bunge, Samuel Sitta.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hoja yake, Zitto anaeleza bayana kuguswa na hali ya mambo nchini Zimbabwe na hata kuitaka Tanzania ifikie mahali itoe tamko lake kuhusu mustakabali wa hali ya mambo nchini humo chini ya uongozi wa Mugabe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo wakati Watanzania ambao wakati fulani tulipata kumuunga mkono na kumuona Mugabe kuwa shujaa wetu na mfano wa viongozi makini wa Afrika, leo hii tunapogeuka nyuma tunalazimika kabla ya kumnyoshea kidole mwenzetu kujiangalia wenyewe na kujipima iwapo kweli tunao ubavu wa kuwakemea wenzetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ninapotafuta jibu la swali hili, ndipo ninapojikuta nikirejea kuliangalia tukio jingine lililotokea juzi jioni bungeni mjini Dodoma wakati Waziri Mkuu kivuli wa kambi ya upinzani bungeni, Dk. Willibrod Slaa alipokuwa akisoma hotuba yake kujibu hotuba ya bajeti iliyosomwa asubuhi ya siku hiyo hiyo na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hali isiyotarajiwa na ambayo ni kielelezo cha udikteta wa kimya kimya wenye malengo yanayofanana na yale ya Mugabe ya kuendelea kubakia madarakani kwa gharama zozote zile, Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) liliamua kutorusha moja kwa moja hotuba hiyo ya Dk. Slaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukio hilo la aibu kwa serikali na TBC limekuja wakati huu wakati shirika hilo likiongozwa na Mkurugenzi mwenye uzoefu wa kimataifa, Tido Mhando ambaye uteuzi wake unahusishwa moja kwa moja na uswahiba wake na Rais Jakaya Kikwete, rais aliyeingia madarakani akitajwa na kupambwa kuwa kipenzi cha vyombo vya habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kwamba, serikali na TBC viliogopa kishindo cha hoja za Slaa ambaye hotuba yake iligusa eneo nyeti la ufisadi katika maeneo takriban yote serikalini ambayo Februari mwaka huu ilimuondoa madarakani Waziri Mkuu, Edward Lowassa na mawaziri wengine kadhaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Udikteta wa juzi wa kuwanyima fursa Watanzania kumsikia Slaa akisoma hotuba yake ni kielelezo cha hofu ya Pinda kuelemewa na uzito wa hoja za wapinzani, ni kipimo cha kupwaya kwa serikali, ni dalili za Pinda kuogopa kuporomoka na kimsingi ni dalili za wazi za serikali hii inayojidai kumnyoshea kidole Mugabe leo kuwa na chembechembe zile zile za ukandamizaji, uonevu, unyanyasaji dhidi ya haki za msingi za raia kupata habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukio la juzi dhidi ya wapinzani linapaswa kuwa darasa muhimu kwa vyombo huru vya habari kuanza kujipanga upya kwa ajili ya kukabiliana na udikteta unaofanana na ule wa leo hii nchini Zimbabwe unaotumiwa na Mugabe kukandamiza uhuru wa habari nchini mwake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika huko tuendako, akina Pinda na wenzao serikali watapaswa kukaa mguu sawa wakijiandaa kukabiliana na uamuzi wa pamoja wa wamiliki wa vyombo huru vya habari ambao siku moja isiyo na jina watakataa kuchapisha magazetini au kuripoti katika redio na televisheni matamko, maamuzi au hotuba rasmi zao rasmi. Mgomo huu uko njiani unakuja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;mwisho&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-2201681741777554697?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/2201681741777554697/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=2201681741777554697&amp;isPopup=true' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/2201681741777554697'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/2201681741777554697'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2008/10/tuna-chembechembe-za-udikteta-wa-mugabe.html' title='Tuna chembechembe za udikteta wa Mugabe'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-3625445978595894750</id><published>2008-10-13T08:12:00.000-07:00</published><updated>2008-10-13T08:15:51.507-07:00</updated><title type='text'>CCM imeiteka vita ya ufisadi</title><content type='html'>CCM imeiteka vita ya ufisadi&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na. Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;UJUMBE wangu naouandika leo hii unakwenda kwa Watanzania wenzangu, hususan wale ambao ni waadilifu si kwa matendo yao tu bali hata fikra zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili ninaloliandika leo, linalenga kuwaeleza wananchi wenzangu namna ninavyowaangalia viongozi wanaotutawala leo hii ambao kwa bahati kabisa wamefanmikiwa kushika madaraka makubwa kabisa ya kidola ama kupitia katika serikali, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilicho madarakani au Bunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimsingi uamuzi wa kuandika makala hii leo nimeufikia kwa tabu sana, kwani kwa mara ya kwanza imenifanya nikijuke nilikalizimika kujenga hoja yangu kwa kuwaangalia watu kama msingi wa kujenga hoja ili kufikisha ujumbe niliokusudia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siku zote pamoja na ukweli kwamba watu na hususan viongozi wamekuwa wakionekana kuchukua msingi wa hoja ninazojenga, ni dhahiri kwamba wao wamekuwa ni vyombo tu kama si madaraja ya kufikisha kile ninachokusudia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo pamoja na kupata shida kubwa kufikia uamuzi huo, nimejikuta nikilazimika kuendelea na makala yangu, hasa baada ya kujiridhisha kwamba, watu hawa ninaotaka kuwajadili ni wazito katika taifa letu na kimsingi ni watu ambao kauli zao, uongozi wao na maamuzi wanayofikia yana nafasi kubwa ya kubadilisha mwenendo wa mambo kitaifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kikubwa kilichosababisha nifikie uamuzi huo ni jeuri inayoanza kuonyeshwa na baadhi ya viongozi wa dola dhidi ya watu wengine kwa sababu tu ya kulewa sifa ambazo wakati mwingine huzibeba hata wasipostahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii, vita dhidi ya ufisadi ambayo imeshamirishwa kwa njia ya maandishi ya wanahabari hasa wa magazeti na wale wanaotumia mitandao ya intaneti, huku ikichombezwa na kuungwa mkono na wabunge wachache wa upinzani, imegeuka na kuwapa thawabu wasizostahili viongozi ama wa serikali, CCM na hata Bunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miongoni mwa viongozi wanaobeba sifa hata wao kuanza kuonekana kuwa ndiyo mashujaa dhidi ya vita hivi vya ufisadi ni pamoja na Jakaya Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mwenyekiti wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Amiri Jeshi Mkuu na Mkuu wa nchi..&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wa pili katika orodha yangu hiyo yuko, Samuel John Tegeza Sitta ambaye ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, watu hawa wawili kwa nafasi zao za kimadaraka ndiyo ambao kwa namna moja au nyingine leo hii wameaanza na wanaendelea kuonekana kuwa vinara wa kweli wa vita hii takatifu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini mbali ya hilo, ni jambo la hatari kwamba, mmoja kati ya viongozi hao wawili, huku akijua kuwa anaungwa mkono na baadhi ya majemedari wa kweli wa vita dhidi ya ufisadi, ameanza kwa sababu tu ya hulka yake ya kibinafsi kuibinafsisha vita hii na kujibebesha sifa nyingi ambazo aghalab nyingine hastahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutoka nje ya mstari kwa kiongozi mmoja kati ya hawa wawili ndiko ambako leo hii kumesababisha nijikute nikilazimika kuwakumbusha Watanzania wenzangu, wazalendo wa kweli kuanza kukaa macho na kuufuatilia utekaji nyara huu wa ajenda kwa jicho la karibu na la tahadhari zaidi. Nitaanza na Sitta.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Samuel John Tegeza Sitta&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huyu ni mwanasiasa machachari ambaye kitaaluma ni mwanasheria na mtu ambaye ninaweza kusema pasipo kusitasita kuwa, ameandika historia pekee tangu akiwa kiongozi wa juu wa Bunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ukweli usiopingika kwamba, katika kipindi cha miaka miwili na nusu tangu awe Spika, Sitta amefanikiwa kulijengea heshima ya pekee Bunge kutokana na namna alivyoweza kusimamia kwa umakini mkubwa baadhi ya masuala mazito.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza Sitta anaweza akatajwa kuwa ni spika aliyesaidia sana kuliongezea meno na nguvu Bunge akiliweka katika mstari sahihi wa kimaamuzi na kulijengea taswira ambayo haikupata kuwapo siku zilizopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uzito wa maamuzi kama lile la kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza utata katika mkataba wa Richmond ni ushahidi mmoja wa tu wa mafanikio ya uspika wa Sitta ambayo kwa kiwango kikubwa yalimjengea heshima ya pekee ndani na nje ya Bunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya Kamati hiyo teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe ambayo ni pamoja na kulazimishwa kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa na mawaziri wengine wawili, Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha yamemfanya Sitta aonekane shujaa wa kipekee ndani ya Bunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Richmond kwa upande mwingine imemfanya Sitta aonekane na achukue sura ya kuwa mpambanaji dhidi ya vitendo vya kifisadi ndani ya chama chake na pengine serikalini. Huu ni ukweli unaopaswa kuheshimiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, ushujaa huu wa Samuel Sitta umefikia hatua ya kumvimbisha kichwa hata kumfanya aanze kutembea kifua mbele na kujiona kuwa ni mtu asiyetaka kuguswa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii ni kosa kubwa na baya kabisa kumgusa au kumkosoa Sitta. Ushahidi wa maandishi unaonyesha bayana kabisa kuwa, wanahabari waliopata kumgusa mwanasiasa huyo tangu alipojitwalia ushujaa katika Kashfa ya Richmond wamejikuta wakipewa majina mabaya kabisa na wakati mwingine wakihusishwa na kundi la mafisadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi karibuni, mwandishi mmoja wa habari wa Tanzania Daima Jumapili; Charles Mullinda alifanya ‘kosa’ kwa kujua au kutojua, kwa makusudi au kwa bahati mbaya akamgusa Sitta sehemu mbaya kwa kuandika makala moja dhidi yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna ya ajabu kabisa, ukosoaji huo dhidi ya Sitta umechukua sura ya pekee. Wabunge na waandishi kadhaa wa habari wamesikika wakieleza namna Sitta alivyoshtushwa na makala hiyo hata kuiunganisha na kile alichopata kukielezea kuwa ni ‘siasa za majitaka’.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna ile ile alivyopata kufanya wakati zilipoandikwa taarifa kuhusu tuhuma za kutumia isivyofaa fedha na mali nyingine za Bunge, Sitta amesikika safari hii chini chini akihusisha upinzani huo wa hoja dhidi yake na ajenda ya mafisadi kumchafua. Huu ni upuuzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii Sitta kwa sababu ya kile kinachoweza kuonekana kuwa ni jeuri inayotokana na matokeo ya vita dhidi ya ufisadi amegeuka na kuwa mtu anayeweza kusema lolote baya dhidi ya watu wengine na akaaminika na hata kuonekana kuwa ni msema kweli. Hali hii lazima ifikie mwisho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi sasa kwa sababu ya jeuri hii, maofisa wa Bunge wanaomuona Sitta kuwa shujaa wao wa vita dhidi ya ufisadi ambayo Tanzania Daima ina kila sababu ya kutembea kifua mbele cha kupambana na tatizo hili kabla spika huyo hajatiwa ‘wakfu wa ushujaa zama za Kamati ya Mwakyembe’ wamefikia hatua ya kuwaogopesha wanahabari kutomgusa mkuu wao wa kazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jakaya Mrisho Kikwete&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huyu ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama na Mkuu wa Nchi. Ana madaraka makubwa kabisa ya kimaamuzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yeye ndiye kiongozi ambaye kwa kujiamini alimteua Edward Lowassa kuwa Waziri Mkuu wakati akiingia madarakani mwishoni mwa mwaka 2005 na kirahisi akakubali kung’oka akihusishwa na sakata la Richmond ambalo kitendawili chake Kikwete ameshindwa kukitegua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna shaka kwamba, Richmond, mama wa tuhuma za ufisadi wa Serikali ya Awamu ya Nne kama ikiangaliwa kwa umakini inaweza ikazaa jibu la swali la miaka mingi la ni ubora gani akina Sitta, Lowassa, Rostam Aziz, Nazir Karamagi, Emmanuel Nchimbi na wengine wengi walikuwa wakitusadikisha juu ya Kikwete ambaye hakuna shaka alishindwa kuimudu sakata hii, miezi mingi kabla ya kuliyumbisha na kulitia hasara taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maneno ya majuto aliyoyatoa siku alipozungumza na wazee wa Dar es Salaam akikiri kwa kinywa chake mwenyewe kwamba kulikuwa na uzembe wa kutochukuliwa kwa hatua za haraka kudhibiti mambo ni ushahidi kwamba, matokeo ya ufisadi wa Richmond yalimkuta akiwa usingizini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukimya wa JK wakati majemedari wa mtandao wakiparurana wenyewe kwa wenyewe kulikoanza baada ya Lowassa kuangushwa ni ushahidi mwingine unaopaswa kutufanya wanahabari kwa upande mmoja na wanasiasa wa kambi ya upinzani kwa upande mwingine kutambua kuwa, vita dhidi ya ufisadi haijapata kuwa ajenda ya dhati ndani ya CCM na serikali yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uamuzi huu wa Kikwete kuwa shabiki au mtazamaji katika vita dhidi ya ufisadi umesababisha wanamtandao wenzake waliosambaratrika kila mmoja kwa mtazamo na njia yake kuchukua mkondo anaoona unafaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hulka hii ya JK kuacha maji yachukue mkondo wake, imemjengea heshima katika jumuiya ya kimataifa na miongoni mwa Watanzania wengine ambao wanakiona kitendo chake cha kukubali kuwaacha maswahiba wake akina Lowassa, Rostam, Karamagi, Msabaha, Andrew Chenge, Zakia Meghji wabebe wenyewe mizigo ya tuhuma mbalimbali za kimaamuzi, kifisadi au kiutendaji kuwa ni uungwana na ya kuheshimu matakwa ya kijamii ya wakati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha maamuzi yake kama yale ya kutengua uteuzi wa aliyekuwa Gavana wa BoT, hayati Daudi Ballali, kuunda Kamati ya kufuatiliwa kashfa ya EPA, kuwatema katika Baraza la Mawaziri watu kama Meghji, Ngasongwa na wengine ni kipimo cha uwezo wake wa kuongoza katika misingi ya uadilifu na kutoyumba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hiyo haitoshi, uamuzi wake wa kuunda Kamati ya Kuchunguza Malalamiko ya Wananchi kuhusu Mikataba ya Madini wakati taifa likiwa katika kilele cha malalamiko tena akimjumuisha mwanasiasa wa upinzani Zitto Kabwe aliyeitikisa serikali kwa hoja ya Mkataba wa Buzwagi mwaka jana, ni sehemu nyingine iliyomjengea JK uhalali wa kuruka vikwazo vya ufisadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sambamba na hilo, kauli nzito alizopata kuzitoa siku zilizopita kama zile za; ‘urais wangu hauna ubia’ na ile ya ‘kutenganisha biashara na siasa’ ni sehemu tu ya mambo ambayo yamepata kumjengea taswira ya kiongozi asiyekuwa tayari kufanya kazi katika dimbwi la uchafu hata kama uchafu huo unaofanywa na swahiba au ndugu yake wa karibu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiweka kando hayo, uamuzi wake au wa serikali anayoiongoza wa kuwaruhusu wapelelezi wa kimataifa wa SFO kutoka nchini Uingereza kuingia nchini na kuwahoji ikiwa ni pamoja na kuwachunguza baadhi ya viongozi ndani ya serikali yake, ni sehemu ya mambo ambayo imeifanya jumuiya ya kimataifa kumuona Kikwete kuwa askari nambari moja wa vita dhidi ya ufisadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno rahisi kabisa, maamuzi, kauli na baadhi ya matendo ya kimyakimya na ya wazi ya Kikwete ni mambo yaliyomfanya aweze kujihalalishia ujemedari katika vita dhidi ya ufisadi ambayo kimsingi haikuanzishwa moja kwa moja na serikali yake au yeye mwenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, kushindwa kwake kujenga nidhamu ya kiwajibikaji ndani ya serikali, ikiwa ni pamoja na kutochukua kwake hatua za wazi dhidi ya watuhumiwa wa kweli wa ufisadi ni sehemu ya mambo ambayo kimsingi yanaanza kutoa ushahidi kwamba, vita dhidi ya ufisadi ilimkuta kwa bahati mbaya akiwa ofisini na yeye akaihalalisha kwa kufuata upepo wa wakati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya hayo yote, kukaa kwake kimya pasipo kueleza ukweli kuhusu kile anachokifahamu kwa undani juu ya Richmond, EPA, kauli za kitatanishi na viongozi kama Sitta na wengine ndani ya chama na serikali anayoiongoza ni sehemu ya mambo ambayo inawafanya Watanzania nikiwamo mimi kutilia shaka umadhubuti wake, kama Mwenyekiti wa CCM. Rais na Amiri Jeshi Mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanahabari ambao katika hili tunapaswa kutembea kifua mbele tunapaswa kutambua kuwa Kikwete akiwa rais mwenye mamlaka makubwa na jemedari mkuu ndani ya CCM ameshindwa kuonyesha kwa vitendo ni kifanyike na hatua gani za wazi zichuliliwe katika kuimarisha vita hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo basi, huko tuendako sisi wanahabari tutapaswa kuachana na siasa za majitaka za akina Sitta, Rostam, Lowassa, Kikwete na wengine za kila mmoja kujiona bora kuliko mwingine, wakati huu taifa linapopita katika kipindi kigumu kisiasa, kiuchumi na kijamii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimsingi katika hili tunazo sababu za wazi za kutambua kuwa, vita hii dhidi ya mafisadi, ikiachwa ikaendeshwa na akina Kikwete na Sitta watu wenye malengo yao ya kimadaraka, basi itafanywa katika mtindo wa kutafutana ubaya kwa malengo ya kisiasa na wala si kwa nia ya kulinusuru taifa hili siku zijazo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo basi, sisi wanahabari tunapaswa kutambua kwa dhati kabisa kuwa, neno ufisadi ndani ya CCM lina maana tofauti kabisa na ufisadi ambao Profesa Issa Shivji, Profesa Mwesiga Baregu, hayati Profesa Seth Chachege na wanazuoni wengine wanauzungumzia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii wanasiasa wakongwe na maskini ndani ya CCM ambao kwa miaka nenda miaka rudi wamekuwa mabingwa wa kufuja fedha za umma kwa ulevi wa kupindukia, starehe za kukufuru, na kwa kuwahonga vimada wanaowatunza katika maeneo takriban yote nchini ndiyo ambao leo hii kwa sababu tu ya kuchanganyikiwa kiakili (frustration) wanakuwa mstari wa mbele kuwanyoshea vidole wenzao wa umri wao ndani ya chama hicho tawala waliotumia muda wao mwingi kujiimarisha kimapato na wakitumia vyema kila shilingi wanayopata kihalali au isivyo halali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hili, ukichunguza kwa makini utabaini kwamba ndani ya CCM wale wanaowanyoshea wenzao vidole vya ufisadi wanafanya hivyo si kwa sababu ya uadilifu wao bali kutokana na ufukara wao na wakati mwingine kwa sababu za magomvi binafsi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la fedheha kwamba, wakati baadhi yetu tukiuona ufisadi kuwa vitendo vinavyohusisha matumizi mabaya ya madaraka, kufuja fedha na mali ya umma, rushwa za kisiasa na kimadaraka, wizi na ubadhirifu, kwa wana CCM wa leo, kitendo cha mtu kula ofisini kwake hata kama ni kwa rushwa, ni jambo halali na yeyote anayepingana na hilo ana wivu wa kijinga na roho ya kimaskini. Huko ndiko wanakotaka tuende.&lt;br /&gt;Mwisho&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-3625445978595894750?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/3625445978595894750/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=3625445978595894750&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/3625445978595894750'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/3625445978595894750'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2008/10/ccm-imeiteka-vita-ya-ufisadi.html' title='CCM imeiteka vita ya ufisadi'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-2253281677250542602</id><published>2008-10-13T07:59:00.000-07:00</published><updated>2008-10-13T08:11:34.968-07:00</updated><title type='text'>CCM inahitaji ujasiri wa ANC</title><content type='html'>CCM inahitaji ujasiri wa&lt;br /&gt;ANC kumweka sawa JK&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;WIKI iliyopita ilimalizika kwa matukio makubwa mawili ya kisiasa ambayo yote yalimgusa Rais wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki ambaye kesho anahitimisha kipindi chake cha urais kilichokatishwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukio la kwanza lililomgusa kiongozi huyo wa moja ya mataifa makubwa ya Afrika likiwa na nguvu kubwa ya kiuchumi, ni lile la kuhitimishwa kwa mazungumzo magumu ya kutafuta suluhu ya kisiasa katika nchi ya Zimbabwe ambayo aliyasimamia na kuyaongoza katika mazingira ambayo kimsingi yalikuwa magumu na yenye mabonde na milima mingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu wanaofuatilia siasa za Zimbabwe ni mashahidi wazuri wa namna Mbeki alivyoweza kuhimili vishindo vya upinzani mkali ama kutoka kwa Rais Robert Mugabe au mpinzani wake Morgan Tsvangirai kwa nyakati tofauti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya kupata changamoto hizo kutoka kwa viongozi hao wawili, kwa kiwango kikubwa, Mbeki aliweza kuhimili vishindo vigumu kutoka kwa mataifa makubwa mawili duniani ya Uingereza na Marekani ambayo yalikuwa yakifuatilia kwa karibu mustakabali wa mambo ya ndani ya Zimbabwe wakati wote wa kipindi cha mazungumzo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimsingi katika sura ya siasa za kimataifa na hususan za ukanda wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), Mbeki aliweza kujipambanua kuwa kiongozi madhubuti na mtu aliyeweza kumaliza mgogoro ambao kwa kiwango kikubwa na kwa muda mrefu uliwagawa viongozi wengi wa Kiafrika wakiwamo marais wawili wa Tanzania, Benjamin Mkapa na baada yake Jakaya Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni bahati mbaya sana kwamba, hata kabla wino wa furaha yake ya kufanikisha muafaka wa kisiasa wa Zimbabwe haujakauka, Mbeki akajikuta akiwa katika mazingira magumu ya kisiasa ndani ya nchi yake na hususan katika chama tawala anachokiongoza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna ambayo haikutarajiwa, Mbeki akajikuta akikamatwa na kile ambacho Baba wa Taifa Mwalimu Julus alipata kukisema wakati alipoamua kujiuzulu uenyekiti wa taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuyakabidhi madaraka hayo kwa aliyekuwa rais wa wakati huo, Ali Hassan Mwinyi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hotuba yake aliyoitoa wakati huo, mwaka 1990, Nyerere alisema ni jambo la hatari kwa nafasi za urais wa nchi na ile ya Mwenyekiti wa Taifa wa chama tawala kushikiliwa na watu wawili tofauti na mambo yakaenda sawasawa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno yake mwenyewe, Baba wa Taifa alisema ili mambo yasiharibike katika mahusiano ya namna hii ni; ‘kuomba watu hao wawili wapatane.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alichokisema Mwalimu ndicho hasa kilichomkuta Mbeki Afrika Kusini hasa kutokana na ukweli kwamba, akiwa rais wa nchi, madaraka ya juu ya urais wa chama tawala cha African National Congress (ANC) yako mikononi mwa hasimu wake mkubwa wa kisiasa, Jacob Zuma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maelezo mengine na kwa kuzingatia utabiri wa kisiasa wa Mwalimu, kuanguka kwa Mbeki mwishoni mwa wiki iliyopita kulianza siku ile ile wanachama wa ANC walipomchagua kwa kura nyingi Zuma kuwa rais wa chama hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kulikuwa ni dalili za mwanzo za kuanguka kwa Mbeki hasa kutokana na ukweli kwamba, hadi wakati wakiingia katika mchuano huo wa madaraka ya juu ndani ya chama hicho tawala cha ukombozi nchini Afrika Kusini, wanasiasa hao tayari walishakuwa ni mahasimu wakubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika kuanguka kwa Mbeki akilazimishwa kujiuzulu na chama chake mwishoni mwa wiki iliyopita kwa kiwango kikubwa ni tukio la pili linalompeleka mwanasiasa huyo katika muanguko wake katika siasa za nchi yake baada ya kushindwa katika mchuano wa urais wa ANC.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya kwa Mbeki kwamba, chama ambacho kilimpa tiketi ya kwenda ikulu kimekataa kuyatambua na kuyaenzi mafanikio aliyoyapata katika medani za diplomasia ya kimataifa, siku chache tu kabla ya tukio hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uamuzi wa ANC, chama ambacho kimekuwa kikijipambanua kama chama rafiki na CCM kwa miaka mingi tayari umeacha maswali na vigingi miongoni mwa makada wake kutokana na hali hiyo ya Mbeki kulazimishwa kujiuzulu na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho, (NEC).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na mgogoro huo mpya ndani ya ANC ambayo baadhi ya wadadisi wa mambo wanaanza kuingiwa na hofu ya kutokea kwa mmegeko wa ndani kwa mfano wa ule uliotokea miaka ya 1960 na kuzaa chama cha PAC, bado ni ukweli kwamba, hali hiyo ya mambo imefungua ukurasa mpya wa siasa za kistaarabu ndani ya ANC yenyewe na nchini Afrika Kusini kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ustaarabu tunaouona hapa ambao wana CCM wanao wajibu wa kujifunza na kuukubali ni ukweli kwamba, hakuna mto yeyote ndani ya nchi, akiwamo rais aliye na mamlaka yanayozidi nguvu za chama chake na matakwa ya msingi ya watu walio wengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sisi ambao siku zote na hususan kipindi hiki tumejikuta tukiwa mashabiki wa hoja inayohimiza kumeguka kwa CCM, tukio la mwishoni mwa wiki nchini Afrika Kusini ni kielelezo cha utayari wa viongozi wa chama tawala wa pande zinazopingana kuwa tayari kukabiliana na changamoto za kisiasa kwa kuweka mbele maslahi ya kitaifa kwanza badala ya kuyaangalia na kuyang’ang’ania yale ya kimataifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii kitendo cha wanachama na viongozi wa ANC kusimama kidete na kuyaweka kando mafanikio ya Mbeki katika diplomasia ya kimataifa yaliyomwezesha kuwaketisha chini Mugabe na Tsvangirai kwa sababu tu ya kuangalia kwanza mustakabali wa nchi yao, kinapaswa kuwa somo zuri kwa wana CCM ambao siku zote wamekuwa vinara wa kuyatumuia masuala ya kimataifa kama kinga yao ya msingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ile hulka ya wanachama wa CCM, kumlinda Mkapa kwa hoja kwamba ameliletea sifa kubwa taifa letu katika masuala ya diplomasia ya kimataifa katika nyanja za kiuchumi, biashara na siasa haina budi kupewa uzito iwapo tu mafanikio hayo yanakwenda sambamba na uhalali wake katika masuala yanayogusa maslahi ya moja ya ndani ya nchi kwanza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wana CCM wanao wajibu wa kujifunza hilo pia hata kwa Rais Kikwete ambaye katika siku za hivi karibuni ametokea kutumia mafanikio yake katika masuala ya diplomasia ya kimataifa kama kivuli cha kuficha udhaifu wa kimaamuzi na kiutendaji ama wake binafsi na wakati mwingine serikali yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tabia iliyojengeka ndani ya CCM ya kumpima Kikwete kwa kigezo cha namna alivyoweza kujenga ushawishi wa kumleta nchini na kumfanya aikubali Tanzania, Rais wa Marekani, George Bush haina budi kukomeshwa na tukio la hivi karibui la wana ANC, ambao wamekuwa wakijitambulisha kuwa marafiki wa karibu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kwamba, wana CCM wa karne ya 21 wameendelea kuwa ni wale wale wa TANU na ASP wa kusifia na kushangalia hata masuala yanayojieleza waziwazi kuwa kielelezo cha udhaifu wa Rais  Kikwete binafsi kwa namna ya kujenga propaganda za kusafisha kila aina ya uchafu wakitumia mafanikio Bandia ya diplomasia ya kimataifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ajabu kwamba, wajumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM ambao wanaona waziwazi namna mwenyekiti wao na rais anavyoshindwa kukabiliana na changamoto mbalimbali za kitaifa katika masuala mbalimbali muhimu kama yale yanayohusu mustakabali wa wafanyakazi, wanafunzi, wanasiasa wenzake ndani ya CCM na serikalini bado wao hao hao ndiyo wanaokuwa watu wa mwanzo kuandaa propaganda za kumsifu na kumpamba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii wana CCM hao hao na tena si wale wa mitaani bali wajumbe wa CC na NEC za chama hicho tawala wamekuwa mabingwa wa kulalama chini kwa chini wakieleza kusikitishwa na kufadhaishwa na rais wao na serikali yao, ilhali ndani ya vikao vyao vya ndani wamekuwa mabingwa wa kufunga midomo na kutozungumza lolote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbukumbu za hivi karibuni zinaonyesha kwamba, baadhi ya wana CCM tunaowaona kuwa ni mabingwa wa kujenga hoja kali dhidi ya serikali ndani ya Bunge na wakati mwingine wanapozungumza na wanahabari kwa siri au kwa uwazi hao hao ndiyo wamekuwa wa kwanza kufunga midomo yao wakati wa vikao ama vya CC au NEC.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushahidi wa hili ni rahisi kabisa, na ulionekana waziwazi wakati wa kikao cha pamoja kati ya wabunge wa CCM na wajumbe wa NEC kilichofanyika Dodoma hivi karibuni chini ya uenyekiti wa Kikwete ikiwa ni miezi michache kabisa baada ya matukio ya bungeni ya Februari yaliyomuondosha madarakani aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wa kikao hicho, kile ambacho baadhi yetu tulikitarajia kukisikia kutoka kwa akina Samuel Sitta, Anne Kilango-Malecela, Christopher ole Sendeka na wabunge wengine ambao ndani ya Bunge wamejipambanua kuwa majemedari wa vita dhidi ya ufisadi hakikusikika wala kuonekana kumtikisa Kikwete aliyekuwa mwenyekiti wa kikao hicho.&lt;br /&gt;Kama hiyo haitoshi, jeuri kama hiyo hiyo ya uwazi na ukweli ilishindwa kusikika kutoka kwa watu wa kariba ya Benjamin Mkapa, Edward Lowassa, Rostam Aziz na wana CCM wengine ambao ama wao wenyewe au watu wanaowaunga mkono wamekuwa wakisikika wakilalamika kuchezewa rafu kusingiziwa na kuzushiwa mambo ambayo wamekuwa wakipita kutuaminisha kuwa hayawahusu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha kati hali hiyo hiyo, hakuna mwanasiasa mmoja kutoka katika kundi lolote kati ya hayo ambayo hakuna shaka kwamba yako katika mvutano mkubwa aliyeweza kusimama na kutaka kusikia kwa uwazi kauli ya Kikwete mwenyewe ambaye kila siku minong’ono inayosikika kutoka kwa wapambe na wanasiasa wa makundi hayo imekuwa ikimuweka ama upande wa watuhumiwa wa ufisadi au ule mwingine wa majemedari wa vita dhidi ya uchafu huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika wana CCM na hususan viongozi wa kitaifa walikuwa na wajibu wa kuhakikisha wanaujua kwa uhakika kabisa msimamo wa rais kwa ufasaha kuhusu masuala yote makubwa yanayogusa mustakabali wa taifa kama yale ya Richmond, EPA, tuhuma dhidi ya Mkapa, Andrew Chenge na wengine wengi ambao aghalab ni makada muhimu wa kihistoria ndani ya chama hicho tawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Badala yake wana CCM wa leo tena wanaotokana na makundi tofauti kabisa kimtazamo ndiyo hao hao ambao wamekuwa tayari kwa gharama kubwa kuficha aibu zozote zile za serikali kwa njia ya kuandaa maandamano ya kupongezana hata katika masuala ambayo ushahidi unaonyesha waziwazi kupwaya kwa uongozi wa kitaifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya hali hii ndiyo ambayo yanamfanya Rais Kikwete leo hii atembee kifua mbele akiwa hana hofu yoyote ya kulazimishwa kujiuzulu kabla ya muhula wake, hata baada ya kuwapo kwa ushahidi kwamba, mtazamo wake kuhusu kile alichokiita mpasuko wa kisiasa wa Zanzibar unapingana na ule wa wajumbe walio wengi wa NEC na pengine CC anayoiongoza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo hayo ya unafiki wa kisiasa wa viongozi ndani ya CCM ndiyo ambao umewafanya wana mtandao wenzake ambao tunaambiwa wanakerwa na jinsi alivyoshughulikia suala kama lile la Richmond lililomlazimisha Lowassa na mawaziri wengine wawili kujiuzulu kubakia wakipiga majungu ya chini chini na kumnyoshea jemedari wao vidole pasipo kuchukua hatua zozote za msingi na za wazi za kumsuta. Ni nani atawaamini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya udhaifu huu wa kuishi katika propaganda ndiyo ambao kwa miaka mingi umeendelea kukifanya chama hicho tawala kifikie hatua ya kuwaaminisha Watanzania kwamba, rais aliyepo madarakani anapaswa kuendelea kutawala kwa miaka mitano ya kwanza na kisha akapewa miaka mingine mitano ya pili hata kama kiongozi huyo ameonyesha udhaifu na usanii wa aina ile unaoonekana nchini hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya ujinga huu wa viongozi wa ndani ya CCM wenye dhamana ya kuamua kwa niaba ya wananchi, ndiyo ambao unawapa jeuri rais na mawaziri wake kusafiri na kushinda nje ya nchi wakijua kwamba, diplomasia ya kimataifa inayoliweka taifa hili katika ufukara wa kuishi kwa kuombaomba misaada, ndiyo kinga ya kimsingi ya kustawi na kudumu kwao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya upofu huu ndiyo ambao leo hii unawapa jeuri wapambe na wasaidizi kadha wa kadha wa rais waliopo ikulu kuvitumia vyombo vya habari na wanahabari mamluki kumjengea rais heshima hata katika maeneo ambayo yeye mwenyewe amekuwa msingi wa kunyoshewa vidole na kukosolewa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya ududumizi huu ndiyo ambao leo hii umewahalalishia viongozi wa CCM na wapambe wao kuwageukia akina Profesa Ibrahim Lipumba, Freeman Mbowe, Maalim Seif Sharif Hamad, Dk. Willibrod Slaa na wengine wengi na kuwaona kuwa ni tatizo dhidi ya ulaji wao kwa gharama za kuweka kando, kupuuzia na kujifanya hauoni udhaifu unaoonyeshwa na mamlaka kuu ya nchi iliyopewa dhamana ya kukaa ikulu bure.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya wana CCM kulemaa kwao na kuendelea kuamini kwamba ‘Kikwete ni Mwenzetu na ‘Zidumu Fikra Sahihi za Mwenyekiti’ hata katika masuala ya msingi ndiyo ambayo leo hii yamesababisha chama hicho kupoteza sura yake ya msingi ya chama cha wakulima na wafanyakazi. Kwa hakika huko tuendako CCM itapaswa kujifunza kutoka ANC.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwisho&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-2253281677250542602?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/2253281677250542602/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=2253281677250542602&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/2253281677250542602'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/2253281677250542602'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2008/10/ccm-inahitaji-ujasiri-wa-anc.html' title='CCM inahitaji ujasiri wa ANC'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-9035469556141379961</id><published>2008-01-11T09:49:00.000-08:00</published><updated>2008-01-11T09:59:47.457-08:00</updated><title type='text'></title><content type='html'>Kenya leo, Tanzania kesho&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JUMATANO ya Desemba 19 mwaka jana, wiki tatu zilizopita, safu hii ilikuwa na makala iliyobeba kichwa cha habari kisemacho; ‘Ipo Siku Tutakesha’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maneno hayo yalitokana na tafakuri ya kikaragosi cha msanii maarufu nchini, Masoud Kipanya ambaye aliyatumia kutoa tahadhari dhidi ya viongozi wanaopuuzia malalamiko ya wananchi hata katika masuala ya msingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, utabiri wa kikaragosi na makala hiyo ya ‘Ipo Siku Tutakesha’ umetimia katika nchi jirani ya Kenya kupitia katika matokeo ya uchaguzi uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wananchi wa Kenya ambao miaka yote tangu uhuru wamekuwa wakiwapa ushindi marais walio madarakani, mwaka huu walikataa kasumba hiyo na kama si dhambi ya kupigania madaraka kwa gharama ya uhai wa watu, Mwai Kibaki angeandika historia mpya ya kisiasa nchini humo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu anazozijua yeye na wale wanaomuunga mkono, Kibaki aliamua kutumia aina mpya ya udikteta, akaendesha mapinduzi ya chinichini na ya kumwaga damu za Wakenya ambao idadi yao ingali haijajulikana sawasawa akajitangaza kuwa Rais wa Kenya kwa kipindi kingine cha pili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huku akidhani kuwa kutumia madaraka yake ya urais kuapishwa haraka haraka kunaweza kukamnusuru, Kibaki akaamuru Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwasilisha haraka hati ya ushindi wake ambao haukuhakikiwa na kabla ya hapo akawa amemwita ikulu Jaji Mkuu na akajipa fursa ya kuapishwa, ili kujipatia uhalali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, juhudi hizo za Kibaki za kujihalalisha kidikteta kuwa rais halali wa Kenya, akitumia vibaya mamlaka ya kikatiba hadi hivi sasa zinaonekana kuendelea kugonga mwamba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wananchi wengi wa Kenya ambao sasa wanaonekana dhahiri kuchoshwa na urithi mbaya wa ukabila na ulevi wa kuwakumbatia viongozi wezi wa kura, wameyakataa mapinduzi haya haramu ya Kibaki na wenzake kwa namna mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huku wakiungwa mkono na jumuiya ya kimataifa, wananchi hao wa Kenya kwa sauti moja, wamefanikiwa kuiinua dunia ya wapenda haki ndani ya nchi hiyo, barani Afrika na kwingineko duniani kuukataa ushindi haramu wa Kibaki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nguvu ya umma iliyoshindwa kumnusuru Maalim Seif Sharif Hamad wa CUF katika uchaguzi wa urais za Zanzibar mwaka 1995, 2000 na 2005 imejidhirisha nchini Kenya na kufanya kazi kuanzia huko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya nguvu hiyo ya umma ya Wakenya, Kibaki amejikuta kila kukicha akilazimika kuchukua hatua moja mbele kusalimu amri na kutafuta kila aina ya njia ya kukubali yaishe kabla hayajamfika yale yaliyopata kuwafika madikteta wengine wengi Afrika wa kabla yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika, iwapo itathibitika kuwa Kibaki na kundi la wenzake wengine lilishiriki katika wizi wa kura ili kujihalalishia ushindi, basi kiongozi huyo na genge lake watakuwa na kila sababu ya kufikishwa katika kizimba cha aina ile ile ya akina Charles Taylor aliyekuwa Rais wa Liberia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zipo dalili zinazoonyesha kuwa, Kibaki ameanza kutambua kuwa yuko hatarini kufikishwa mahali pabaya kabisa kutokana na maamuzi yake au ya watu wake wa karibu kuzichezea kura ambazo matokeo yake yamemtia wasiwasi hata mwenyekiti wa tume ya uchaguzi aliyemtangaza yeye kuwa mshindi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kibaki analazimika kulikubali hilo kwani idadi ya wabunge wa chama chake cha PNU isiyofikia hata nusu ya wale wa chama cha mpinzani wake mkuu, Raila Odinga ni ushahidi na msingi mkuu wa urais bandia aliovishwa na kuhalalishwa na uapishwaji batili kuwa hatua itakayomfanya ashindwe kuitawala nchi hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati njema kwetu (kwa maana ya kujifunza) kwamba, leo hii Wakenya kutoka makundi yote mawili yanayopingana wameamua kuja Tanzania na kumuomba Rais Jakaya Kikwete asaidie kuwasuluhisha wezi wanaoongozwa na Kibaki na wahujumiwa wanaomuunga mkono Raila.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati Kikwete akiombwa kuwa msuluhishi, kazi iliyokwishaanza kufanywa kabla yake na akina Desmond Tutu na John Kuffor, yeye mwenyewe bado angali akikabiliwa na kishindo kingine cha namna hiyo hiyo cha hapa nyumbani, kilichoanzia Pemba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa si rahisi kusema moja kwa moja ni kitu gani hasa kilichowaamsha Wakenya wa pande tofauti hata sasa waanze kumuona Kikwete (kiongozi waliyekuwa wakimpuuza awali) kuwa msuluhishi bora, ukweli ni kwamba uamuzi wake binafsi wa kukaa kimya na kutotangaza kumtambua Kibaki unamweka katika nafasi ya juu, kuliko ilivyo kwa rais mwingine wa Afrika Mashariki, Yoweri Museveni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwangu mimi, usuluhishi wa Kikwete ninauona kuwa ni moja ya mambo ya msingi si kwa Wakenya bali kwetu Watanzania ambao katika mihula mitatu tofauti tumefanya uchaguzi mkuu wa vyama vingi kwa namna ile ile ya hao jirani zetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ninaamini tena kwa dhati kabisa kwamba, Kikwete anaingia katika usuluhishi huo huku akijua kuwa, hata hapa nchini, kilio cha wizi wa kura kimekuwa kikipigwa na wapinzani na kupuuzwa na chama tawala kila kinapopigwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiiweka kando Zanzibar ambako kwa viwango vya Wakenya shinikizo limekuwa ni hafifu, katika uchaguzi wa madiwani, wabunge na hata urais, matokeo ya kura yamekuwa yakitoa mwelekeo ule ule wa ushindi wa Kibaki katika maeneo mengi, hata kama si yote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tofauti pekee iliyopo ni kwamba, Wakenya wa mwaka 2007, tofauti na ilivyo kwa Watanzania, wameyakataa makosa yao ya 2002 yaliyowafanya wamwamini Kibaki kuwa mtu wa mabadiliko, aliyeaminika kuridhia kwa dhati makubaliano aliyofikiwa na wenzake akina Raila, Kalonzo Musyoka na wengine kabla ya kuundwa kwa NARC.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais wetu na sisi wananchi wake tunapaswa kujifunza kuwa, wenzetu Wakenya wa leo, wameukataa ukondoo wetu wa ‘hewala bwana yaishe’ kwa kutoheshimu tangazo la Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi na kutokubali kutishwa na uapishwaji wa haraka haraka wa Jaji Mkuu uliokuwa ukilenga kuzima jitihada zozote za ushindi wa wizi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kikwete anapaswa kutambua kuwa, wakati tangazo la Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar na uapishwaji wa haraka haraka wa Rais Amani Abeid Karume ulionekana kumaliza kila kitu mwaka 2005 na kabla ya hapo mwaka 2000, mbinu hizo zimeshindwa kufanya kazi Kenya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika yote hayo, moja ya mambo ambayo Watanzania tuna kila sababu ya kujifunza kutoka Kenya ni kwamba, serikali inayoshindwa kutimiza ahadi zake kwa wananchi kwa mfano wa Kibaki, haina budi kung’olewa kwa nguvu ya kura halali na linaposhindikana hilo kwa njia ya wizi, basi nguvu ya umma haina budi kutumika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya hilo, Watanzania wanapaswa kujifunza kuwa, nguvu ya kweli ya upinzani haina budi kutiwa nguvu na wanasiasa wenye nia ya dhati ya kuwatetea watu wa aina ya Raila walio tayari hata kupoteza madaraka yao ndani ya serikali iliyoshindwa, iliyo madarakani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hili Wakenya wamekuwa watu wa kwanza kutii unabii wa kisiasa wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere aliyetabiri kuwa upinzani wa kweli ungetokana na kumeguka kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akina Raila, Musyoka na wenzao wamekuwa wana CCM wa kwanza wa Kenya kukiacha chama kilicho madarakani kilichokiuka ilani yake ya uchaguzi kikaitelekeza na kushindwa kuitekeleza kama kilivyoahidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii ndani ya CCM yetu, tunawaona na kuwafahamu kwa majina wanasiasa wakiwamo wale wanaounda Baraza la Mawaziri la Kikwete ambao haikubali visheni yake, wasiokubaliana na mwelekeo wa chama na serikali yao, wanaomkataa na kumpinga chinichini Waziri Mkuu Edward Lowassa ingawa bado wako ndani ya chama hicho hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wana CCM wa namna hii ambao wanaounda kundi kubwa lenye wanasiasa wakongwe wastaafu na walio madarakani kama wangekubali kukiasi chama hicho ambacho kimsingi kimepoteza mwelekeo wake wa msingi, wangewajengea wananchi matumaini makubwa ya ushindi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanasiasa wa namna hii ndiyo ambao leo hii wanasababisha tushindwe kuwa na akina Raila, Musyoka, Charity Ngilu, Musalia Mudavadi, William Ruto, Profesa Peter Anyang’ Nyong’o na wengine wengi wa aina yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Unafiki wa wanasiasa kadhaa ndani ya CCM wenye tofauti za kimsingi za kiitikadi na kimwelekeo na chama hicho tawala, wengi wao wakiwa ni wale wa Tanzania Bara, ndiyo ambao leo hii unaigharimu demokrasia yetu na kuifanya isiyo ya ushindi kwa mfano ule wa Kenya tunayoshinda tukipiga soga kuishangilia na kujifunza kishabiki na si kimatendo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hili, mafanikio kidogo yamepatikana Zanzibar ambako mwaka 1988 baadhi ya waliokuwa wana CCM waliopata kushika nafasi za juu kabisa ndani ya chama hicho na serikalini, wakiongozwa na aliyekuwa Waziri Kiongozi, Maalim Seif Sharif Hamad walitoa shinikizo zito lililoilazimisha CCM liwafukuze uanachama na kuwavua nyadhifa zao zote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kosa hilo la CCM kwa upande wa visiwani ambalo lilirudiwa na Kibaki miaka michache tu iliyopita, ndilo ambalo leo hii linazaa matunda tunayoyaona Zanzibar na haya tunayoyashabikia Kenya ambayo yote na kwa nyakati tofauti jukumu la usuluhishi wake analo Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania kwa ujumla wetu tunapaswa kutambua na kukubali japo kwa uchungu kuwa, hali ya siasa ya leo hii nchini Kenya, ndiyo mtukio ya kesho hapa Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ubabe na udikteta wa siri siri wa baadhi ya viongozi wa juu ndani ya serikali ya CCM ambao umejengewa historia ya kufumbiwa macho ndiyo ambao kimsingi unatujengea mazingira bora yatakayotutengenezea akina Maalim Seif wengine na akina Raila wapya siku miaka michache ijayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hulka za kulindana hata katika masuala yanayogusa maslahi na raslimali za taifa kwa namna ile aliyofanya Kibaki nchini Kenya leo hii, akifikiri kuwa ndiyo ustaarabu wa kisiasa, ndiyo ambazo zitaigharimu CCM hii ya Kikwete au ya mrithi wake miaka kadhaa ijayo. Huko ndiko tuendako.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Mwisho&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-9035469556141379961?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/9035469556141379961/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=9035469556141379961&amp;isPopup=true' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/9035469556141379961'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/9035469556141379961'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2008/01/kenya-leo-tanzania-kesho-jumatano-ya.html' title=''/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-6986973599607678445</id><published>2007-11-29T09:27:00.000-08:00</published><updated>2007-11-29T09:33:22.337-08:00</updated><title type='text'>Tumuenzi Kanyama Chiume</title><content type='html'>&lt;a href="http://3.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/R073jaBlPhI/AAAAAAAAAAM/rz7pkIYBlAE/s1600-h/Kanyama+Chiume.jpg"&gt;&lt;img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5138316412529753618" style="FLOAT: right; MARGIN: 0px 0px 10px 10px; CURSOR: hand" alt="" src="http://3.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/R073jaBlPhI/AAAAAAAAAAM/rz7pkIYBlAE/s320/Kanyama+Chiume.jpg" border="0" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;div&gt;Tanzia kwa Mwana wa Afrika&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tujifunze kutoka kwa Kanyama Chiume&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;NI wiki moja kamili sasa tangu Afrika impoteze mmoja wa majemedari wake wa mwisho na mwasisi wa mapambano ya uhuru na umoja wa kweli wa Afrika, Mzee Kanyama Chiume akijulikana kabla ya hapo kama, Murray William Kanyama Chiume (78).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mzee Chiume alifariki dunia Jumatano iliyopita akiwa New York Marekani, ambako alikuwa akiishi kwa miaka kadhaa na baadhi ya watoto wake walio huko kikazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika kifo cha shujaa huyu wa Malawi, Tanzania na Afrika nzima kinalifanya bara hili kuendelea kupoteza baba mmoja baada ya mwingine wa vita vya ukombozi na waasisi wa mapambano ya umoja wa Afrika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kabla ya kifo chake cha wiki iliyopita, Afrika ilikuwa imebakiwa na yeye na Rais wa zamani wa Zambia, Kenneth Kaunda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bila ya kutafuna maneno, viatu vya Chiume vilikuwa vikiwatosha wanasiasa wa kariba yake; akina Kwame Nkrumah, Julius Nyerere, Jomo Kenyatta, Sekou Toure na wachache wengine ambao idadi yao haizidi wanafunzi 12 wa Yesu Kristo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati Baba wa Taifa alipokuwa ndiye kiongozi wa harakati za mapambano ya uhuru wa Tanganyika miaka ya mwanzoni mwa 1950, Chiume ndiye aliyekuwa kinara nchini Malawi, akiwa ndiye mwakilishi wa chama cha Nyasaland Congress Party kilichokuja kujulikana baadaye kama Malawi Congress Party.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kupitia katika chama chake hiki, yeye ndiye aliyekiwakilisha katika mikutano ya kimataifa kule London, Accra Ghana na Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alishiriki kikamilifu katika uanzishwaji wa vuguvugu la kudai uhuru kwa pamoja kwa mataifa ya Kiafrika akiwa mjumbe wa Malawi katika mkutano uliozaa lile la nchi zilizo Afrika ya Mashariki na Kati (Pafmeca) kule Mwanza na baadaye Pafmecsa ukijumuisha na nchi za kusini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alikuwa miongoni mwa viongozi wa Kiafrika waliokutana mara kadhaa kwa ajili ya kuanzisha uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Kiafrika (OAU) na mwaka 1964 katika mkutano uliofanyika Cairo Misri, hotuba kali ya kimapinduzi ndiyo iliyomkera rais wake Kamuzu Banda na kumjenga uhasama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilipokutana naye kwa mara ya kwanza, Mzee Chiume alipata kunisimulia kuhusu mzozo mkali wa maneno uliozuka kati ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na Rais wa Kwanza wa Ghana, Kwame Nkrumah ambao ulitishia uhai wa OAU.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii miaka takriban 10 tangu anieleze kuhusu tukio hilo alilolielezea kuwa ni baya kuliko yote katika uhai wa OAU, bado naweza nikakumbuka kwa ufasaha maneno aliyonieleza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Bado naikumbuka siku hiyo vyema kabisa. Ilikuwa ni siku ngumu kwetu. Viongozi wetu wawili, tuliokuwa tukiwaheshimu na kuwasikiliza, walizozana kweli kweli. Mwalimu alikuwa akipinga mtazamo. Sijapata kumuona Mwalimu akiwa amekasirika kama siku hiyo. Ugomvi ule ungeweza kuimega OAU,” alinieleza Chiume aliyekuwa akizungumza Kiswahili kwa ufasaha kabisa huku akivuta tukio moja baada ya jingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mazungumzo yake siku zote, Chiume alikuwa akiiona Afrika kuwa moja na mipaka ya kikoloni haikuwa kikwazo cha kuwafanya Waafrika kupigana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ninapokumbuka maneno mengi mazito niliyoyasikia kutoka kwa Chiume miaka 1o iliyopita na kupekua pekuwa makabrasha ya historia ya bara hili, kwa mfano wa maneno ya Yohana Mbatizaji, napata shida kuwafunga kidamu za mzee huyo viongozi wa zama hizi wa Bara la Afrika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watoto wadogo na Watanzania wasioijua vyema historia ya mapambano ya uhuru wa Malawi na ile ya Afrika ya kati ya miaka ya 1950 hadi 1960 wanaweza wakashangaa, jina la mwanasiasa huyu likitajwa na kuwekwa katika mizania ya wanasiasa wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chiume na wenzake wengine kadhaa akiwamo rafiki yake mkubwa Henry Chipembere na Orton Chirwa wanaweza wakatajwa kuwa ndiyo viongozi waasisi wa mapambano ya uhuru wa Malawi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chiume ambaye miaka ya mwanzoni mwa 1950 alikuwa na umri usiodizi miaka 25 na wenzake zama hizo wakijulikana kwa jina kwa jina la Kiingereza ‘The Young Turks’ (Vijana wasiodhibitika).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilipokutana naye katika kipindi cha kati ya mwaka 1996 wakati huo akija hapa nchini mara kadhaa baada ya kurejea Malawi miaka miwili iliyotangulia, nilipata fursa ya kujifunza mambo mengi kuhusu maisha ya mwanasiasa huyu na namna alivyoshirikiana na wenzake wengine katika vita ya mapambano ya ukombozi wa Afrika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mzee Chiume alinipa fursa ya kuijua historia ya Malawi, Tanzania na Afrika, nje ya ile tunayosoma katika vitabu na maandiko mabalimbali ya kihistoria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndani ya akili yake, mzee huyo ambaye wakati huo alikuwa na umri wa miaka 66, alikuwa na kumbukumbu sahihi ya matukio mbalimbali yaliyokuwa yakitokea zama za harakati za kudai uhuru wa nchi yake na ule wa Afrika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika nikiwa mwanafunzi wa historia zama hizo, mzee huyu aliongeza ufahamu wangu kuhusu historia iliyopotoshwa ya harakati za ukombozi wa bara la Afrika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kupitia kwake nilimfahamu Kamuzu Banda, Rais wa kwanza wa Malawi ambaye miaka 30 ya utawala wake wa kiimla, aliiondoa nchi yake kuwa miongoni mwa mataifa ya mwanzo kabisa kudai na kupigania uhuru si wa taifa moja moja la Afrika bali la Afrika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno yake mwenyewe Mzee Chiume aliniambia kuwa alikuwa akijutia uamuzi wake yeye na mwenzake Chipembere wa kusikia ushauri wa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Ghana, Kwame Nkrumah wa kuwataka wao wamkubali Banda kuwa kiongozi wa harakati zao za ukombozi wa Malawi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakiwa wadogo kiumri, Chiume na Chipembere waliheshimu maoni hayo ya Nkrumah wakihadaika na ushiriki wa Banda katika harakati za mwanzoni kabisa za mshikamano wa Waafrika (Pan African Movement).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama ilivyokuwa kwa Nkrumah na kwa vijana hao ambao walikuwa wameshaasisi mapambano ya uhuru wa nchi yao, Banda wa zama hizo, miaka ya 1940 na 1950 alibeba taswira ya kweli ya mwana wa Afrika, mpigania uhuru mwenye uchungu na nchi yake na bara lake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la bahati mbaya kwamba, uamuzi wa Banda kuhudhuria mkutano wa kwanza wa Mwamko wa Afrika (PanAfrican Congress) mwaka 1945 kule Manchester, Uingereza akiwa na Kenyatta na Nkrumah ulimfanya aonekane kuwa mmoja wa wanamapinduzi hodari na wa kuaminika wa Kiafrika. Ukweli haukuwa huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mzee Chiume alinieleza namna Banda alivyoweza kutoka ndani ya gamba alilojificha kwa zaidi ya miaka 10, kwnai miezi isiyozidi mitatu tangu Malawi ipate uhuru wake mwaka 1964, ghafla alibadilika na akawa mpinzani mkubwa wa misingi ya ukombozi wa taifa lake na ule wa bara lake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akina Chiume walipigwa na butwaa kumuona Banda akitangaza kuutambua utawala wa kibaguzi wa makaburu wa Afrika Kusini ambao ulikuwa umetengwa na jumuiya ya kimataifa na miaka michache baadaye akaingia katika mzozo na Tanzania akigombea sehemu ya ardhi yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chiume, wakati huo akiwa Waziri wa Mambo ya Nje akiungwa mkono na mawaziri wenzake wengine watano, walikataa kumtii Banda, na matokeo yake wakafukuzwa kutoka serikalini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hii haikuishia hapo, Banda ambaye alishawatangaza kuwa ni wasaliti, akafanya jaribio la kuwakamata na kuwaua, tukio ambalo liliwanasa watu kadhaa na kumkosa Chiume ambaye kwa msaada wa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere alifanikiwa kutorokea Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama ilivyokuwa kwa wana mapinduzi wengine kadhaa wa Kiafrika Chiume akarejea Tanzania ambako alisomea na kukulia na akaishi katika kipindi chake chote cha miaka 30 akiwa mkimbizi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilipozungumza naye kuhusu matukio hayo, Chiume alikiri kufanya kosa kubwa la kumruhusu Banda kuziteka nyara harakati zao za mapambano ya uhuru wa Malawi nay ale ya Afrika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika, kama si hulka yake ya kutopenda madaraka na kuwa tayari kusikiliza ushauri wa wanamapinduzi wenzake, Chiume alikuwa na nafasi kubwa ya kuwa Rais wa kwanza wa Malawi huru na mmoja wa viongozi ambao kifo chake kingewekwa katika daraja moja na akina Nyerere na Nkrumah hata na wale ambao hawakupata kumfahamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati nikizungumza naye miaka 10 iliyopita, kulikuwa na maneno ya chinichini yalikuwa yakidai kuwa, Banda halisi aliyechukuliwa na Waingereza na kupelekwa Afrika Kusini na baadaye Uingereza hakuwa yule yule aliyerudi Malawi na kuwa Rais wa Kwanza wa Taifa hilo dogo lililo Kusini Mashariki mwa Afrika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilipozungumza naye kuhusu tetesi hizo, Mzee Chiume alinihakikishia kuwa alikuwa ameshaanza kulifanyia uchunguzi suala hilo na kimsingi alitaka kuandika kitabu juu ya kile kilichotokea Malawi na hadaa ya Banda iliyomwezesha kuupata urais wa Malawi. Sikupata kujua iwapo alitimiza lengo lake hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Amefariki akiwa na mapenzi makubwa kwa taifa lake na kwa Bara lake na ndiyo maana aliporejea nchini mwaka 1994, alianzisha chama cha upinzani akikiita Congress for Second Republic (CSR), akiamini kuwa taifa hili lilikuwa likihitaji uhuru wa kweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tangu wakati huo akawa mstari wa mbele kupigania uimara ya mfumo wa vyama vingi na akatumia muda wake mwingi kuwaasa Wamalawi wenzake kutokubali tena kuirejesha nchi yake katika udikteta wa chama kimoja. Utawala wa mkono wa chumba wa Banda ukampa fundisho kubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tanzania&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chiume hawezi kutenganishwa na Tanzania. Historia yake ya maisha yake binafsi, kifamilia na kisiasa yanaungana moja kwa moja na taifa hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwandishi mwenzangu Maggid Mjengwa katika blogu yake ameonyesha kwa ufasaha namna Mzee huyu alivyo na uhusiano na taifa hili. Maggid anaanza kwa kusema;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huyu mzee alisoma katika shule mbalimbali hapa nchini kuanzia elimu yake ya msingi hadi ile ya Sekondari kabla ya kwenda Chuo Kikuu cha Makerere alikosomea ualimu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha hata alipokuja kuishi ukimbizini, alioa mke wa Kitanzania akazaa watoto wake akina Nathan na ndugu zake wengine Tanzania. Wamesoma Tanzania na kimsingi wana Utanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akiwa ukimbizi hapa nchini, Chiume alikuwa akifanya kazi ya uandishia na makala zake za kimapinduzi zilikuwa zikichapwa katika magazeti mbalimbali kuanzia The Nationalist (baadaye Uhuru na Mzalendo) na katika gazeti la serikali la Daily News.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si hayo tu, hata kabla ya uhuru wa Malawi, Chiume akiwa mjumbe wa Vuguvugu la Kudai Uhuru eneo la Afrika ya Mashariki na Kati (Pafmeca) alitumwa Zanzibar kujaribu kuvusuluhisha vyama vya ZNP na ASP vilivyokuwa katika mgogoro.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sura ya mgogoro huo wa vyama viwili vya siasa vya Zanzibar ambavyo Chiume alitumwa kuja kuusuluhisha mwaka 1958, una sura inayofanana na ile ambayo leo hii inawaweka katika meza moja viongozi wa vyama vikuu viwili vya siasa CCM na CUF kwa tatizo la Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwanademokrasia wa Kweli&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati vuguvugu la kudai mfumo wa vyama vingi lilipopamba moto nchini mwake, akifanya kazi kutoka hapa nchini, Chiume hakulala hadi alipounda chama chake na hatimaye kurejea nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aliporejea nchini mwake kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1994, vyombo vya habari vya huko vilikuwa vikimtaja kuwa Mmalawi maarufu kuliko wengine wote waliopata kuishi uhamishoni na mpinzani mkubwa kabisa wa Rais wa wakati huo wa Banda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama chake cha upinzani alichokianzisha cha Congress for Second Republic na jitihada zake za kuviunganisha vyama kadhaa vidogo nchini huko mwaka 1996 ili kukabiliana na utawala wa aliyekuwa Rais wa Pili wa Malawi, Bakili Muluzi ni sehemu ya mambo yanayoonyesha namna alivyoheshimu misingi ya kidemokrasia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania tunayo mengi ya kujifunza kutoka kwa mzee wetu huyu ambaye kuondoka kwake kwa hakika kunaendelea kuwamaliza waasisi wa ukombozi wa mataifa yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii serikali ya Rais Mbingu wa Mutharika wa Malawi inapokubali kumpa heshima zote za kitaifa Chiume katika mazishi yake, angalau pazia linaonekana kuanza kufunguka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali ya matumaini inarejea na kwa kweli tunayo mengi ya kujifunza kutoka kwa viongozi wa aina ya Chiume ambao hawakupata kulewa madaraka, ambao kwao Afrika ni taifa moja na ambao kwao uzalendo maana yake moja, kuwapigania, kuwatetea na kuwalinda watu wako.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania wanaoishi leo hii ni mashahidi wa namna viongozi wetu wengi wanavyofikiria zaidi matumbo yao na yale ya familia zao kuliko watu wanaowaongoza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika tunapoyaangalia maisha binafsi na ya kisiasa ya wanasiasa wa kariba ya Chiume, tunapaswa kuyafanya kuwa masomo bora ya namna viongozi wetu wanavyopaswa kuishi leo na kesho ili huko tuendako waweke alama za uongozi uliotukuka na wa kuigwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa Chiume amefariki dunia, tunaamini kilio anacholiliwa, na Watanzania, Wamalawi, Waafrika wazalendo na ulimwengu mzima wa wapigania haki ni ushahidi kuwa mema aliyoyatenda yameacha alama ya aina yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika kifo chake kimethibitisha Chiume hapaswi kuliliwa kwa kusononeka na kwa kwikwi tu, bali tuna wajibu wa kulia kilio cha kumpoteza shujaa, mwana adhimu wa Afrika, mtetezi wa wanyonge, mpenda haki na shahidi wa mapambano yetu. &lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-6986973599607678445?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/6986973599607678445/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=6986973599607678445&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6986973599607678445'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6986973599607678445'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2007/11/tumuenzi-kanyama-chiume.html' title='Tumuenzi Kanyama Chiume'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://3.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/R073jaBlPhI/AAAAAAAAAAM/rz7pkIYBlAE/s72-c/Kanyama+Chiume.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-7415659921301683589</id><published>2007-07-05T23:14:00.000-07:00</published><updated>2007-07-05T23:18:37.151-07:00</updated><title type='text'>JK, Makamba watuandalia matanga</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;NATAMANI Watanzania wenye mitazamo inayokinzana pamoja na mitazamo tofauti ya kiitikadi na kifalsafa wangekaa katika meza moja na kukubali kuwa mfumo madhubuti wa vyama vingi vya siasa, vyenye hazina ya wanasiasa wenye upeo, visheni, programu, kauli mbiu na hoja yakinifu, ndiyo siri kubwa kabisa ya kuondokana na wingu la kihistoria la udumavu wa kiakili na kimwelekeo unaolikabili taifa hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya kulikubali hilo, Watanzania hao wangeamua kila mmoja kwa wakati wake, kufanya juhudi za dhati na za makusudi kuhakikisha kuwa, mfumo huo mchanga kabisa hapa nchini wenye umri utakaokuwa na umri wa miaka 15 kamili Julai mwaka huu unalindwa na kuimarishwa kwa nguvu zote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Majukumu hayo matatu ya lazima ya kukubali, kulindwa na kuimarishwa kwa dhati kabisa yanapaswa kuwa ndiyo msingi, dhana na dira ya utawala bora ambao leo hii imebakia kuwa nadharia isiyofanyiwa kazi kivitendo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwanasayansi ya Siasa ajulikanaye kwa jina la Anna Grzymaa-Busse anayendika katika jarida la kitaaluma la East European Politics and Societies la mwanzoni mwa mwaka huu anaandika kwa Kiingereza; Political party competition is critical to fostering good governance and preventing corruption. However, several aspects of competition—the number of parties, their vote share, or their specific ideology—have no demonstrable impact on corruption. In contrast, the robustness of competition is critical in constraining governments and monitoring policy.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno rahisi, msomi huyo anasema; “Ushindani ni jambo muhimu katika kuendeleza utawala bora na kuzuia ufisadi. Hata hivyo ili hilo liwezekane yapo mambo muhimu yanayopaswa kuwapo ili kukidhi ushindani huo- idadi ya vyama, mgawanyo wa kura zao au iwapo itikadi zao, hazina nguvu dhidi ya ufisadi. Kinyume chake, umadhubuti katika ushindani, ni jambo la msingi katika kuichunga serikali na kuzipima sera zake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maneno yenye maana hiyo na mchanganuo ulio na mwelekeo huo ndiyo msingi mkuu wa kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi katika nchi zote duniani na ushahidi unaonyesha kitakwimu, namna nchi zilizo na mifumo imara ya vyama vingi isiyoingiliwa na nguvu nyingine za nje kama za kijeshi au za kidikteta zilivyofanikiwa kupiga hatua kubwa kabisa kimaendeleo kuliko zile za kiimla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hiyo haitoshi, mataifa mengi ambayo yameukubali mfumo huo kwa mikono miwili na kustawi kisiasa, kiutawala, kiuchumi na kijamii yameweza kufikia hatua hiyo chini ya mwavuli wa soko huria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwenendo wa mambo katika kipindi cha miaka 15 hadi 20 iliyopita unaonyesha kwamba, hivi sasa chini ya mwavuli huo wa soko huria ndiyo silaha ambayo leo hii mataifa kama China, Korea Kaskazini na Urusi kwa mfano yaliyojiendesha kwa kufuata itikadi ya kidikteta ya kikomunisti yanaonyesha kupiga hatua za haraka kimaendeleo kuliko hata ilivyokuwa kipindi cha vita baridi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande mwingine, mataifa kama Italia, Ufaransa, Uingereza na Marekani ambayo kwa miaka nenda, miaka rudi yamekuwa yakiendeshwa kwa mfumo wa vyama vingi, leo hii yanaendelea kuwa mfano bora wa maendeleo ya katika kila nyanja kijamii, kiuchumi na hata kisayansi na kiteknolojia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati tukiutambua ukweli huo, Watanzania tukiongozwa na Rais wetu, Jakaya Kikwete tunakubali hata kufikia hatua ya kushangilia wakati taifa hili likipigwa ‘gia ya reverse’ ili tuzidi kuelekea kule walikotokea wenzetu hao miaka zaidi ya 100 na ushee iliyopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna ya ajabu kabisa, huku tukijua kuwa, kudhoofisha mfumo wa vyama vingi ni jambo la hatari kabisa kwa ustawi wa taifa hili, viongozi wetu, wakitumia ufahamu mdogo wa mambo wa wananchi wanakubali kuhutubia mikutano ya hadhara na kutamba kuwarejesha katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanachama wanaokaribia 1,000 wa upinzani huko Dodoma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jambo hili la fedheha kabisa kwa bahati mbaya linafanywa na kusimamiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye saa chache tu baada ya kutangazwa kushinda uchaguzi mkuu Desemba mwaka jana alikiri kwamba, wengi wa waliompigia kura walikuwa wananchi wasio wanachama wa chama hicho tawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna ya ajabu na isiyoelezeka kwa akili za kawaida, Rais, eti akitumia kofia yake ya uenyekiti wa taifa wa CCM, anasimama na kuwahutubia wananchi wa Kigoma katika moja ya majimbo machache kabisa ya upinzani na kukiponda hadharani chama hicho na mbunge wake kijana kwa lugha rahisi kabisa ya kukidhalilisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya, chama cha siasa kinachopondwa ni CHADEMA, na mwanasiasa anayejengewa hoja mbaya za kumalizwa tena na Rais kwa mfano wa tembo akimkanyaga sisimizi, ni Zitto Kabwe, mmoja wa wanasiasa wachache vijana wanaoweza kusimama hadharani wakajenga hoja za msingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dhambi pekee ya CHADEMA ni ile jeuri yake ya kuifanya Kigoma kuwa ngome yake kuu, jambo ambalo kwa CCM na Serikali ya Kikwete na wale waliowatangulia kabla yao ni udhia usiopaswa kuvumilika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hiki anachokifanya leo hii Rais Kikwete akisaidiwa na akina Yussufu Makamba ndicho kilichofanywa na akina Benjamin Mkapa, Frederick Sumaye na wana CCM wengine ambao nao kwa staili hiyo hiyo waliwahi kuua baadhi ya ngome za upinzani kama mkoa wa Kilimanjaro.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati njema, wakati ufa ukionekana kustawi kwa upande wa Tanzania Bara ambako makumi ya wanasiasa waliokuwa upande wa upinzani wameweka matumbo yao mbele na kujiunga na CCM, kule Zanzibar hali ni tofauti kabisa, kwani majemedari wa CUF wanao ubavu wa kutembea kifua mbele dhidi ya chama hicho tawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Fitna za kisiasa za akina Dk. Salmin Amour, marehemu Dk. Omar Ali Juma, Dk. Gharib Bilal, na baadaye Karume na wasaidizi wake wengine zimeshindwa kuubomoa mtandao imara wa CUF unaoongozwa na vinara wa siasa za upinzani visiwani akina Maalim Seif Sharif Hamad, Hamad Rashid Mohammed, Aboubakar Khamis, Haji Duni, Ismael Jussa na wengine wengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika msimamo usitetereka wa viongozi hao wa CUF na wafuasi wao ndiyo ambao leo hii umewafanya CCM tena wakiongozwa na Kikwete huyo huyo walazimike kukaa meza moja na wapinzani hao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna mambo yalivyo, huu moto wa viongozi wa serikali na CCM kuendeleza hulka ya kuvunja ngome za wapinzani, wakifanikiwa Bara na kukwama Zanzibar unaoneka kuchochewa na hulka ya chama hicho tawala kutopenda kukalishwa kwa shuruti katika meza moja na wapinzani kama wanavyofanyiwa sasa na CUF.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii matunda mabaya kabisa ya moto wa makada hao wa CCM ni kuiua hata kufikia hatua ya kukaribia kuizika ile jeuri ya akina Augustine Mrema, Mabere Marando, James Mbatia na wengine wengi ambao kipindi cha kati ya mwaka 1995 na 1997 walikuwa wanasiasa wanaoheshimika kwa kukitikisa vilivyo chama tawala na serikali yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunaweza tukasema kwa uhakika kuwa, iwapo majemedari wa CCM wa wakati huo wasingecheza faulo dhidi ya imara ya upinzani iliyoanza kujengwa wakati huo, leo hii kashfa za aina ya ANBEM, ununuzi wa rada na ndege za kifahari na sasa Richmond na mambo mengine yanayofanana na hayo yasingekuwa miongoni mwa matatizo yanayotutesa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hilo ndilo ambalo Watanzania tunapaswa kutambua kwamba wakati wakisherehekea kuvishwa skafu za kijani na njano na kupokea kwa mbwembwe kadi za uanachama wa CCM kwa ahahdi za uongozi ndani ya chama hicho tawala au serikalini nyuma ya pazia wanaruhusu kukithiri kwa vitendo vya rushwa na kuifanya serikali iendelee kuwa legelege na hata kupoteza mwelekeo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati fulani miaka kadhaa iliyopita, nilikuwa miongoni mwa watu niliokuwa nikikiona kitendo hiki cha wana CCM kufanya juhudi za kumaliza upinzani kuwa mchezo wa kawaida tu wa kisiasa ambao ulipaswa kufanywa pia na vyama vya upinzani dhidi ya chama hicho tawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii najiona mwenye bahati kulitambua hilo na kufahamu namna majemedari hawa wa CCM walivyo tayari kucheza rafu za kila aina kuwanyonga wapinzani wao wa kisiasa wanaotoka ndani ya vyama au wakati mwingine wakitokea katika asasi za kitaaluma kama HakiElimu na katika vyombo vya habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, ni nani aliyetuloga sisi Watanzania hata kuwa kama walivyokuwa Wagalatia ambao pamoja na ‘Mwana wa Mtu’kutupa kila ishara kuwa mfumo wa vyama vingi ndiyo msingi wa utawala bora na mkombozi wa kweli wa taifa hili, sisi bado tunapiga mbio kurudi kule kule tulikotoka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi ni kwa nini tunashindwa kukaa chini na kujiuliza, ni kwa sababu gani, viongozi wetu walio mabingwa wa kudai kwamba wataenzi falsafa zote za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere waamue kwa makusudi kuukana wito wake wa siku za mwisho za kutaka kuona upinzani wenye nguvu ukijengwa hapa nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Acha historia inihukumu. Jitihada za viongozi wetu, akina Kikwete, Edward Lowassa, Makamba, Tambwe Hizza na makada wengine wa CCM kujaribu kuua upinzani au hata kuudhoofisha kwa kisingizio chochote ni mwelekeo wenye nia mbaya unaolenga kulihujumu taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi yetu pamoja na ukweli kwamba si makada wala wanachama wa chama chochote kile cha siasa, tunaungana na wanazuoni wa aina ya akina Issa Shivji na wale wenye mawazo kama yake kufanya kila linalowezekana kuukubali, kuulinda, kuuimarisha na mfumo huu wa vyama vingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunafanya hivyo tukijua na tukiamini kwa dhati kabisa kuwa, tunazo sababu za msingi za kufanya hivyo, tuna nia ya dhati ya kulipigania hilo na mwisho tumeshaanza kujijengea uwezo kukabiliana na hulka mbaya ya majemedari wa vita wa CCM na serikali yake.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-7415659921301683589?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/7415659921301683589/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=7415659921301683589&amp;isPopup=true' title='3 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/7415659921301683589'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/7415659921301683589'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2007/07/jk-makamba-watuandalia-matanga.html' title='JK, Makamba watuandalia matanga'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>3</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-8942655499989749047</id><published>2007-07-05T23:11:00.000-07:00</published><updated>2007-07-05T23:13:58.555-07:00</updated><title type='text'>Huyu si Kikwete tuliyesimuliwa</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;MAJIRA kama haya, miaka miwili tu iliyopita taifa hili lilikuwa katika mchakato wa kumtafuta Rais wa Nne wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa mchakato ulikuwa umeanza, machoni mwa wachambuzi wa mambo wa ndani ya nchi na hata wale wa nje, Kikwete ndiye aliyekuwa akionekana dhahiri kuwa; ‘President in Waiting.’ (yaani Rais Mtarajiwa).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa katika uchaguzi huo, wagombea wengine wawili wa urais, Profesa Ibrahim Lipumba (CUF) na Freeman Mbowe (Chadema) walionekana kuamsha hisia mpya za kuungwa mkono na makundi kadha wa kadha, bado ukweli ulikuwa ukionekana kuwa walikuwa washindani wa kutoa changamoto na si wa kuchukua jahazi la uongozi, japo kwa wakati ule.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zama hizo, vyombo mbalimbali vya habari, hususan magazeti takriban yote ya kila siku yalikuwa yakiimba wimbo mmoja zaidi katika kampeni; Kikwete, Kikwete, Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vichwa vya habari kama vile vilivyokuwa vikiandika; Kikwete shujaa!, Hakuna kama Kikwete! Kikwete we acha tu! Kikwete aiteka… na vingine vingi ambavyo kimantiki vilikuwa vikifanana na hivyo, vilipamba kurasa za habari na makala katika magazeti mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waandishi na wahariri waliokuwa na jeuri ya kuandika kwa kina habari na makala za wagombea wengine wa urais na kufikia hatua ya kuwapamba kwa namna ile ya Kikwete walikuwa wakihesabika na idadi yao ilikuwa ikipungua kadri siku za uchaguzi zilivyokuwa zikikaribia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kile ambacho Kikwete mwenyewe hivi karibuni alipata kukiita maandalizi yake ya miaka 10 ya kuwa Rais wa Tanzania yalijipambanua kwa uwazi kabisa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kati ya mwezi Machi na Mei mwaka 2005 wakati CCM ikiwa katika mchakato wa kutafuta mgombea urais, wakiwa wamejitokeza wanasiasa 10 kusaka kiti hicho, niliandika safi za makala za kuwachambua wagombea hao wote nikieleza nguvu na udhaifu wa kila mmojawapo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu ya mwelekeo wa makala yangu ya leo nitanukuu moja ya sehemu muhimu inayoendana na makala yangu ya leo inayomuelezea Kikwete niliyemuweka katika mizania ya wagombea wengine washindani wake. Niliandika hivi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni  jambo la wazi kwamba, watu ambao wamekuwa wakimuunga mkono Kikwete, tangu mwaka 1995 wamekuwa wakimuona kama mgombea anayewakilisha mawazo ya kizazi kipya cha Watanzania na mtu anayeweza akawa daraja la mahusiano kati ya wazee wastaafu na vijana wenye uchu wa kutaka kupewa nafasi ya kuongoza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na ukweli kwamba, Kikwete anapogombea hivi sasa ana umri wa miaka 55, vijana na wana CCM wanaoungana na falsafa ya Baba wa Taifa ya kuwataka wazee wang'atuke madarakani wanamuona kuwa ndiye chaguo lao sahihi kabisa la 'wakati huu' pamoja na ukweli kwamba, watu wa rika lake kama vile Frederick Sumaye (55) na Mark Mwandosya (57) wanaonekana kuwa ni wa kizazi kingine na tena waliochomoza kwa bahati mbaya tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;…Swali moja hadi hivi sasa linaonekana kutojibiwa sawasawa: Ni kwa nini basi miaka 10 baada ya kugombea urais kwa mara ya kwanza mwaka 1995, Kikwete bado anaonekana ndiye mwakilishi wa Watanzania wa kizazi hiki na mtu anayeonekana kufaa zaidi kuongoza taifa katika karne ya 21 zaidi kuliko ilivyo kwa wengine kama hao akina Sumaye, Mwandosya kwa upande mmoja na hata akina Malecela, Salim, Iddi Simba kwa upande mwingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je ni hulka yake ya kujichanganya na watu wa rika tofauti? Ni haiba yake ya ujana aliyodumu nayo kwa miaka yote 10 tangu mwaka 1995? Ni upofu wa mashabiki zake? Ni upeo wake mkubwa wa kuona mambo? Ni hoja zake za kisasa? Ni uzalendo wake? Ni mapungufu waliyonayo washindani wake? Ni kitu gani hasa? Watanzania wanapaswa kuliangalia hilo na kulitafutia majibu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hicho nilichokiandika Aprili mwaka 2005 ndicho ambacho kweli kilitokea ndani ya CCM. Benjamin Mkapa, akiwa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM huku akiungwa mkono kwa siri siri na majemedari kama Kingunge Ngombale Mwiru, Ali Hassan Mwinyi na Rashid Kawawa (kwa kuwataja wachache) walitumia ajenda za namna hiyo hiyo kumpa ushindi Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siku ilipotoka makala yangu hiyo, rafiki mkubwa wa Kikwete, Rostam Aziz ambaye sasa ni Mweka Hazina wa CCM Taifa alinipigia simu na akaeleza kushangazwa kwake na hoja zangu hususan katika aya hiyo ya mwisho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno yake mwenyewe; Rostam aliniuliza; “Hivi mdogo wangu Kibanda unaishi katika dunia gani? Kweli hujui ni kwa nini Kikwete ni mgombea maarufu na anayekubalika kuliko mwingine yeyote?.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya kwangu, hata Rostam mwenyewe hakunieleza ni kitu gani hasa kilichokuwa kikimfanya Kikwete atokee kuwa kipenzi cha Watanzania hata kufikia hatua ya baadhi ya wadadisi wa mambo kama akina Prince Bagenda kumuita Tumaini Lililorejea.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, mwitikio mkubwa na wa kipekee wa wapiga kura na matokeo ya ushindi wa asilimia 80, yaliyopewa majina anuai, ushindi wa kishindo, kimbunga, el-nino na mengi mengine yaliendelea kumpamba, Kikwete aliyeonekana kuwa mtu wa watu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mmoja wa wasaidizi wakubwa wakati wa kampeni za urais wa CCM niliyezungumza naye wakati akiwa katika msafara wa Kikwete mkoani Ruvuma aliniambia kwamba, wengi wanaomuunga mkono Kikwete katika harakati zake, wanamuona kuwa ndiye kiongozi pekee atakayeleta mabadiliko makubwa ndani ya CCM na katika mfumo wa kiutawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msaidizi huyo wa Kikwete huku akiwa amezingirwa na wapambe watu wengine kadhaa waliokuwa ndani ya timu ya ushindi wa mwanasiasa huyo alinieleza, nitamnukuu, ili nisipotoshe maana; “Kikwete ni mpinzani ndani ya CCM, wenzake wengi wanalijua hilo na ndiyo maana baadhi ya watu wanamuogopa wakijua akiingia madarakani atafanya mabadiliko makubwa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii ninaweza nikawaeleza Watanzania wenzangu kuwa, kwa kiwango fulani nilianza kushawishika kuwa JK alikuwa mtu wa mabadiliko na kiongozi ambaye angeweza kuleta mapinduzi makubwa kabisa ya kifikra katika mfumo wa kiutawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni bahati mbaya sana kwamba, miezi 18 sasa tangu aingie madarakani, matarajio makubwa waliyokuwa nayo watu wengi juu yake yanaonekana ama kutoweka au kutokwenda kama ilivyodhaniwa awali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ahadi zake kwamba ari, kasi na nguvu mpya vitakuwa chachu dhidi ya rushwa, uwajibikaji serikalini na hata katika mahusiano ya kisiasa na kijamii na vyama vingine vya siasa na nchi jirani ni mambo yanayoonekana kutokuwapo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunapowauliza vijana wasio na ajira waliojitoa mhanga kumuunga mkono kwa kishindo, wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu waliofikia hatua hata ya kumuona mtu aliyekuwa akifuata nyayo za Baba wa Taifa, wadadisi huru wa mambo na wasomi wa kada mbalimbali, jibu utakalopata ni rahisi kabisa; ‘tumeanza kukata tamaa’ ndivyo wanavyosema.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si rahisi hivi sasa kusema kwa uhakika kabisa iwapo kasi, ari na nguvu inaonekana katika utendaji wa wizara moja moja au hata idara zake, hata baada ya kufanyika kwa milolongo ya semina elekezi na JK mwenyewe kutembelea wizara hizo na idara kadhaa nyeti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kile ambacho Waziri Mkuu, Edward Lowassa alipata kukielezea kuwa mwisho wa ‘business as usual’ serikali ndicho kinachoonekana kuendelea kubakia kikistawi serikalini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiacha tu kwamba, hivi sasa Rais ni Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu ni Edward Lowassa, kasi ya mambo serikalini inabakia ile ile ya zama za Benjamin Mkapa na Frederick Sumaye.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jambo baya zaidi ni kwamba, kabla ya Mkapa hajaanza kusukwasukwa na jinamizi la maamuzi yake ya kibiashara akihusishwa na mikopo ya benki na kampuni ya ANBEM, midomo ya Watanzania ilishaanza kusema mara kwa mara; ‘ni afadhali serikali iliyopita.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa ni kweli kwamba, Kikwete anaweza akatembea kifua mbele akijivunia mafanikio yake na Lowassa katika kuchochea ujenzi wa shule nyingi za msingi na ongezeko la wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari katika kipindi chao kifupi madarakani bado sekta nyingine muhimu kama afya, miundombinu, maji, kilimo hazina mifano hai ya kuisemea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi sasa Watanzania hawawajui mawaziri na naibu mawaziri wa Kikwete kwa majina na kwa kazi za wazi za uwajibikaji wanazozifanya kwa namna tuliyopata kuiona zama akina John Magufuli, Augustine Mrema, Lowassa mwenyewe, Meghji (wa zama zile).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hii ya mambo imetufanya baadhi yetu tuanze kujiuliza je huyu ndiye Kikwete yule yule aliyeungwa mkono kwa kishindo kwa hoja za ushawishi kwamba ataanzia pale alipoishia Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi yetu ambao tuliaminishwa tukubali kuwa Kikwete ni mpinzani wa kweli ndani ya CCM na ‘nabii’ aliyekuja kurejesha heshima iliyopotea ya chama hicho tawala na kuirejeshea msingi wake wa ‘mapinduzi’ leo hii tumeanza kuona ndivyo sivyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati tukiona namna Kikwete anavyolemewa na mambo, tumeanza kujiuliza ni kitu gani hasa  kinamzuia Kikwete kuchukua hatua dhidi ya mawaziri wake wengi wasindikizaji, wakuu wa mikoa wavivu na wakuu wa wilaya waliolala?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi ni jambo gani hasa linalomfanya ashindwe kuwawajibisha makatibu wakuu na wakurugenzi wa taasisi na idara za serikali aliowateua walioshindwa kusimamia vyema maeneo yao ya kazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa mashahidi na manabii wa uongo wamekuwa wakijaribu kujenga hoja za kumlinda Kikwete na serikali yake kwa sababu wanazozijua wao, ukweli unabaki pale pale kwamba, matarajio makubwa waliyotujengea, yameanza kufifia na tuombe Mungu yasije yakatoweka kabisa.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-8942655499989749047?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/8942655499989749047/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=8942655499989749047&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/8942655499989749047'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/8942655499989749047'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2007/07/huyu-si-kikwete-tuliyesimuliwa.html' title='Huyu si Kikwete tuliyesimuliwa'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-4501222737999344373</id><published>2007-07-05T23:10:00.000-07:00</published><updated>2007-07-05T23:11:41.432-07:00</updated><title type='text'>Serikali ikubali lawama kujiepusha na fedheha</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;WATANZANIA tunaumwa magonjwa mengi ya kifikra na kisaikolojia ambayo kwa bahati mbaya, matokeo ya kuendelea kuugua huko kusikoisha yamekuwa ni mambo mengi mabaya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kufanya mambo mengi ya msingi na yasiyo ya msingi, zaidi ya miaka 45 tangu tupate uhuru wetu, Tanzania bado imeendelea kubakia moja ya mataifa masikini kabisa duniani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Juhudi za viongozi wetu kujaribu wakuu wanne kujaribu kulinasua taifa hili kutoka katika hali mbaya kabisa ya ufukura bado zimeendelea kugonga mwamba, pamoja na kuwapo kwa mafanikio ya hapa na pale.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii wakati Watanzania tukiwekwa katika majaribu ya kutakiwa kuingizwa kwa kasi zaidi (fast tracking) katika Shirikisho la Afrika Mashariki, sauti kubwa kutoka kwa watu walio wengi ni ile ya kupinga hatua hiyo, tukiwa na hofu ya wazi na kimsingi ya kweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wale wanaopinga kuingia katika shirikisho kwa kasi, wanasema bayana namna wanavyohofia kile kinachoonekana kuwa ni hatari ya Tanzania kugeuzwa koloni la kiuchumi, kisiasa na kijamii la mataifa jirani, hususan Kenya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya hilo, wapinzani wa hoja hiyo hawaishii hapo, wanakwenda mbali zaidi na kueleza bayana kwamba, kuzorota kwa hali ya amani na usalama katika nchi majirani kama vile, Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda nchi ambazo ndizo zilizo chini ya wigo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo siku moja itazaa shirikisho kunaweza kukailetea nchi yetu matatizo makubwa siku zijazo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watetezi wa hoja hiyo ambao kimsingi sipingani nao, wanasema bayana namna Watanzania tunavyopaswa kujivunia amani na utulivu tuliyojijengea kwa miaka yote tangu mwaka 1961 tulipopata uhuru wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tangu zama za uongozi wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere (1961-1985) na baadaye Ali Hassan Mwinyi (1985-1995), Benjamin Mkapa (1995-2005) na sasa Jakaya Kikwete, amani na utulivu vimekuwa ni ajenda ya kujivunia na kimsingi ya kuilinda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mara kadhaa viongozi wetu wakuu wanapozungumza katika majukwaa ya kisiasa wamekuwa wakiwataka Watanzania kutambua kuwa amani (na utulivu) tunayojivunia leo hii tumeijenga kwa kutumia nguvu kubwa na kwa sababu hiyo basi tunao wajibu wa kuilinda kwa juhudi zote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati fulani wakati wa midahalo mikali ya hoja katika ukumbi maarufu wa Nkrumah mwanzoni mwa miaka ya 1990, msamiati huu, mara kadhaa ulipatwa kutundikwa msalabani hasa baada ya kundi moja la wanazuoni kuamua kuubatiza jina na kuutita ukondoo uliovishwa joho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii wakati tafiti zikiwa zimeshathibitisha kuwa vijinchi kimoja kimoja kama ilivyo Tanzania (haya ni maneno ya Mwalimu Nyerere si yangu) bila ya kuungana na nyingine kichumi haziwezi zikasonga mbele au zikapiga hatua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uzoefu wa peke yetu wa miaka zaidi ya 40 ya kusimamia falsafa ya Ujamaa na Kujitegemea tukijaribu kujenga viwanda vingi kabla ya kujihakikishia malighafi bora na ya kutosha na pasipo kuwa na masoko ya uhakika ya kuuzia mazao yetu na pengine kutokuwa na uwezo wa kuviboresha viwanda hivyo, umetufikisha hapa tulip oleo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ile jeuri tuliyokuwa nayo miaka ya kati ya 1961 na 1980 ya kutumia Tan Bond yetu, maziwa na nyama zetu wenyewe za kusindika, viwanda vyetu vya nguo na vitu vingi vingine vya namna hiyo vya kwetu wenyewe, hata kuweza kuonyesha jeuri dhidi ya nchi jirani kama Kenya ambayo tulikuwa tukiiona kuwa taifa kibaraka la mabepari (leo wawekezaji) wa kigeni imepotea na kutugeuka sisi wenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati tukiwahofia Wakenya hao kuwa watakuja kuumeza uchumi wetu, ukitembea katika maduka yanayouza bidhaa mbalimbali za kutumia majumbani kwetu utashangaa kuona kwamba asilimia zaidi ya 70 ya vitu vinavyouzwa na kuuzika, vinatoka katika nchi hiyo jirani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Blue Band ambayo miaka ya 1970 haikufua dafu kwa Tan Bond, leo hii imeshika chati na kuuzwa kila duka hata kule ambako kwa lugha ya mitaani leo hii tunakuita uswazi (yaani uswahilini).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vyakula vya majumbani kuanzia maziwa ya unga kama Nido, vyakula vya watoto kama Celerac, na bidhaa nyingine nyingi zinazopamba maduka mengi zinatoka kati nchi hiyo ya Kenya huku zile zilizobakia zikitokea Afrika Kusini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya Tanzania kugeuka kuwa soko la bidhaa za nchi hizo mbili, kwa kiwango kikubwa kikubwa yamesababisha Kenya kuishangaa Tanzania na kuiangalia kwa jicho la kutoiamini sana huku wasomi wake wengi wakionyesha waziwazi kuipinga sera ya serikali yetu kuikumbatia Afrika Kusini kwa kutumia mgongo wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mfano ule ule ambao mabepari walilazimika kuigombea Afrika hata kulazimika kuigawa vipande vipande ili kila mmoja apate koloni lake, ndivyo ilivyo sasa kwetu ambako mataifa hayo mawili kila moja kwa namna yake, yanaligombea soko Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mataifa hayo mawili yote mawili kwa namna na njia zinazofanana yamefikia hata hatua ya kufungua mabenki yao hapa nchini, Afrika Kusini ikijivunia kuongoza kwa kuwa nayo mengi kama Stanbic Bank, Barclays Bank na NBC huku Wakenya wao wakiwa na Kenya Commercial Bank.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wachumi wa nchi hii bado tunawasubiri watupe majibu sahihi wakitufafanulia kwa kina ni wapi tulipoteza mwelekeo hata kufikia hatua ya leo hii kulazimika kukikubali kile ambacho wakati fulani zama za vuguvugu la vita baridi, walimu wa siasa wa zama hizo kama akina Kingunge Ngombale Mwiru walijenga desturi ya kukiita ukoloni mambo-leo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati tukiendelea kusubiri majibu ya kitaalam kutoka kwa wachumi wetu, bado tunayo nafasi ya kukiri kwamba, viongozi wetu ambao wamejenga hulka ya kutembea kifua mbele wakisema amani na utulivu ni tunda la juhudi zao, wanao wajibu wa kusimama na kuigeuza shilingi upande mwingine na kutamka kwamba, kuporomoka kwa mwelekeo wa mambo ni matunda ya kuweka mbele mustakabali wetu wa kisiasa na kusahau maeneo mengine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, ni haki kwa viongozi wetu leo hii kutuita sisi tunaokosoa sera na falsafa zao kadha wa kadha kuwa ni wapinzani tusio na hoja na ambao hatulitakii mema taifa letu hili ambalo eti lina viongozi wanaofanya kazi usiku na mchana pasipo kuchoka?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna yoyote ile, viongozi wa taifa hili, wakiwamo akina Kingunge ambao kwa nyakati tofauti walipata kutuambia kuwa tulikuwa tukipita katika kipindi cha mpito hata wakatuletea mikakati mingi yenye majina lukuki yaliyojaa misamiati yenye mbwembwe nyingi wanao wajibu wa kutueleza ni wapi tulipojikwaa hata tukaendelea kuanguka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo wakati tukilazimika kugeuka nyuma na kuwanyoshea kidole viongozi wetu, sisi Watanzania pia tunao wajibu wa kujibebesha lawama wenyewe kwa kukubali kwetu kimsukule kuaminishwa kila tulichoambiwa na viongozi hao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya hilo, wakati tukilazimika kukiri kwamba, tulikuwa tumepotea njia hata kama mwelekeo ulikuwa ni sahihi, kila Mtanzania anao wajibu basi wa kuanza kutimiza wajibu wake ipasavyo kwa ajili ya manufaa ya taifa hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa ni kweli kwamba, tunayo mambo mengi ya kufanya, moja ya mambo ya mwanzo kabisa ni kukubali kuacha ile hulka yetu ya miaka nenda miaka rudi ya kushangilia kila msamiati unaoonekana kusikika masikioni mwetu unaotolewa na viongozi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Viongozi wetu wa sasa, wanapokuja na lugha za “Kwa Kasi Mpya, Ari Mpya na Nguvu Mpya, Tanzania yenye Neema Tena Inawezekana! Tunao wajibu wa kuipima kauli hiyo kwa kuangalia hali halisi iwapo inaendana na maneno hayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya, leo hii wanapoibuka wachambuzi wa mambo na kuwauliza akina Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais Dk. Ali Mohammed Shein na Waziri Mkuu Edward Lowassa kuhusu utekezwaji wa kauli mbio za namna hiyo wanaanza kuonekana wasaliti na wapinzani wa dhamira njema ya viongozi wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi ya watu katika nchi hii wanataka kutulazimisha tuache kuwakosoa viongozi wetu, wanataka tufikiri kwa namna na mwelekeo wanaoutaka wao na kimsingi wanataka kuendelea kuifanya nchi hii kuwa soko-koloni la mataifa rafiki na jirani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huku wakijua kwa hakika kabisa kwamba, viongozi wa CCM na kabla ya hapo wale wa Tanu wamekuwa ni mabingwa wa kutunga kauli mbiu ambazo zimeshindwa kuzaa matunda yaliyokusudiwa, bado wanakubali kuendelea kuukumbatia ujinga wa kushindwa kufikiri kwa kiwango cha ajabu kabisa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hulka yetu ya kushabikia kila tamathali za semi, tabia yetu ya kulewa ahadi zenye ladha tamu akililini na desturi zetu za kuwafanya viongozi wetu waungu watu, wasiokubali kukosolewa ilihali wakijua kuwa wamebeba dhamana kubwa ya kuliongoza taifa hili ni mambo yaliyopitwa na wakati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kutambua hilo, napenda kuweka bayana kwamba, tutaendelea kuhesabu na kuzichambua kauli nzito zinazotolewa na viongozi wetu wakuu na kama hiyo haitoshi, tunaziweka katika mizania ya hoja, kauli mbiu zao na falsafa wanazotumia huku tukiamini kuwa, kwa kuwa kwao madarakani, wao ni watumishi wa wananchi.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Viongozi wetu wakuu ambao walikuwa wanyenyekevu kweli kweli wakati wakiomba kura ama za ubunge, urais au zile za kuidhinisha uteuzi wao wanapaswa kutambua kuwa, wale ambao wanawakosoa kwa dhati leo hii wanawaepusha kukumbwa na fedheha siku watakapostaafu au kumaliza mihula yao ya uongozi ama kikatiba au kwa kulazimika. Heri lawama kuliko fedheha.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-4501222737999344373?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/4501222737999344373/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=4501222737999344373&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/4501222737999344373'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/4501222737999344373'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2007/07/serikali-ikubali-lawama-kujiepusha-na.html' title='Serikali ikubali lawama kujiepusha na fedheha'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-696496146652567108</id><published>2007-07-05T23:03:00.000-07:00</published><updated>2007-07-05T23:09:48.330-07:00</updated><title type='text'>Lowassa; Kiepuke kikombe hiki</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;WAZIRI Mkuu, Edward Lowassa amekalia kaa la moto. Ameshika moja ya nafasi za juu za kimadaraka katika nchi hiyo ambayo inabeba lawama nyingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna mambo yanavyokwenda Lowassa sasa anaonekana ama ameanza kulitambua hilo kwani kiwango chake cha uvumilivu kwa tuhuma zinazoelekezwa kwake, kwa uwazi na wakati mwingine kwa siri, kinaonekana kuongezeka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande mwingine hicho kinachoonekana kuwa ni uvumilivu kinaweza kikawa pia aina ya ushauri anaopewa Waziri Mkuu unaofanana na ule waliowahi kupewa watangulizi wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Iwapo hali hii ya sasa inatokana na Lowassa kutambua ukweli kwamba kazi yake ni ya lawama kiasi kwamba anapaswa kwanza kutafakari kabla ya kufurukuta kwa kasi na kuanza kuchukua hatua, basi, hilo ni jambo jema na kimsingi linapaswa kupongezwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikiwa ukimya wa sasa wa Lowassa unatokana na ushauri wa wasaidizi wake wanaomtaka akae kimya na kuuacha upepo upulize hadi utakapochoka wenyewe, basi atakuwa anafanya makosa makubwa ambayo atakapoamua kuchukua hatua huenda akajikuta akiwa amechelewa sana na hivyo kukwama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo wakati Lowassa akitafakari hayo anapaswa kutambua jambo moja la wazi kuwa, uwaziri mkuu, wadhifa alioubeba sasa, una historia ngumu kwa wateule wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akiwa Waziri Mkuu wa tisa tangu uhuru na wa nane baada ya Tanganyika kuwa Jamhuri, Lowassa anapaswa kwenda katika rekodi na kuangalia mustakabali wa kikazi wa watangulizi wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kati ya mawaziri wanane waliomtangulia kabla yake, ni watatu tu, Julius Kambarage Nyerere (1961-1962), Edward Moringe Sokoine na Dk. Salim Ahmed Salim ambao waliondoka serikalini wakiwa majina safi masikioni na machoni mwa wananchi wa kawaida.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengine wote waliobaki, Rashid Kawawa, Cleopa Msuya, Joseph Warioba, John Malecela na Frederick Sumaye, wote kwa vipindi tofauti wakiwa mawaziri wakuu walipita katika hatua ngumu kabisa kiutendaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lowassa akiwa wa mwisho katika mlolongo huo anapaswa kutambua na kimsingi naamini ameshaanza kuliona hilo kuwa, kiti alichokishika kina makali kila upande.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akiwa mmoja wa wanasiasa ambao uchapakazi wao hautiliwi shaka hata kidogo, Lowassa anatakiwa kutambua kwamba, kina cha maji anachoogelea ni kirefu kuliko ujasiri wake binafsi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si hilo tu Lowassa anapaswa pia kutambua kuwa, ingawa yeye ni mteule wa Rais, utendaji wake wa kazi unapimwa si na rais tu, bali mawaziri, makatibu wakuu, wabunge, wasomi wa kada mbalimbali, waandishi wa habari na wananchi wa kawaida.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lowassa anapaswa kutambua pia kwamba, majibu yatakayotokana na mizani itakayowekwa na makundi mbalimbali yanayoangalia utendaji wake ndiyo yatakayokuwa taswira halisi ya utendaji si wake tu bali pia wa serikali kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hiyo haitoshi, Lowassa anao wajibu wa kutambua kuwa, iwapo serikali ya Kikwete itaanguka katika maamuzi na katika utekelezaji wa programu zake, ndani ya serikali yenyewe na nje, basi lawama za kwanza zitaelekezwa kwake yeye hata kabla ya kufikishwa kwa Rais na mawaziri wengine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kwa sababu hiyo basi ndiyo maana hata hivi sasa, baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa wa ndani ya nje ya nchi, wakati wanapounyoshea kidole utendaji wa serikali ya awamu ya nne, jina la Lowassa ndilo linaloonekana kurushiwa mawe mengine na makali zaidi wakati mwingine kuliko hata yale anayorushiwa Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii ukipita katika mitaa mbalimbali na ukakutana na wasomi, maafisa wa juu wa serikali, wabunge, wafanyabiashara wakubwa na watu wengi wengine ni jambo la kawaida kusikia jina la Lowassa likitajwa si kwa mema bali kwa lawama ambazo wakati mwingine ukizipima unaziona zisizo za msingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la ajabu na la kujiuliza hivi ni kwa nini basi kila maamuzi yenye utatanishi hivi sasa yaliyochukuliwa na serikali, yote tunaelezwa kuwa nyuma yake yuko Lowassa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama ilivyopata kuwa zama za Sumaye, Msuya, Malecela na hata Warioba mwaka mmoja sasa tangu ashike kiti hicho muhimu kabisa, Lowassa ndiye anayebebeshwa mzigo wa lawama kwa kila baya linalotokea hapa nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii, Lowassa ndiye anayehusishwa na kuchelewa kupatikana kwa mwekezaji anayefaa wa kuchimba chuma Liganga na kuendeleza makaa ya mawe ya Mchuchuma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata Rais Jakaya Kikwete alipofanya mabadiliko ya kumuondoa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Taifa, NDC, taasisi ya umma iliyokuwa ikishughulikia miradi hiyo miwili ya chuma na makaa yam awe, Lowassa ndiye aliyenyoshewa kidole na baadhi ya watu kuwa mtu aliyekuwa nyuma ya mabadiliko hayo ambayo baadhi hayakuwafurahisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni Lowassa huyo huyo ambaye hivi sasa anahusishwa pia na kuwapo kwa jitihada zenye walakini za kubomolewa kwa baadhi ya majengo yaliyo katikati ya jiji la Dar es Salaam ambayo awali yalikuwa yametengwa kwa sababu za kihistoria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naamini baadhi ya watu wanakumbuka vyema namna Mbunge wa Moshi, Philemon Ndesamburo alivyomhusisha Lowassa katika sakata la mgogoro kati ya Mbunge wa Mkuranga, Adam Malima (CCM) na Reginald Mengi, ugomvi ambao sasa umechukua sura tofauti kabisa kiasi cha kulifanya suala hilo lichukue sura ya kitaifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiunganisha na hilo, ni Lowassa huyo huyo ambaye baadhi ya wabunge wanamtaja kuwa nyuma ya Malima aliyeamua kulihamisha suala lake kutoka katika mtiririko wa masuala ya Bunge na kulipeleka CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu wanaomhusisha Lowassa na hilo wanasema mahusiano yake mabaya ya kikazi na Spika wa Bunge, Samwel Sitta ndiyo sababu kuu ya yeye kuamua kuungana na Malima katika jitihada za kumshughulikia mbaya wake. Falsafa rahisi. ‘Adui wa adui yako ni rafiki.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunapowauliza baadhi ya wanasiasa, mawaziri, wabunge wanasiasa ndani na nje ya CCM na wanamtandao wengine, sababu hasa za Lowassa na Sitta kuhitilafiana nje ya genge lao lililomuandalia ushindi Kikwete majibu tunayoelezwa ni ya ajabu kweli kweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini kikubwa kinachotajwa kuwa kiini cha mzozo huo ambao hakuna yeyote kati yao wawili amewahi kuuweka bayana ni kile kinachoelezwa kuwa ni ‘Urais baada ya Kikwete.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu hili wakati mwingine haliniingii akilini, ingawa kwa bahati mbaya huwa nakataa kulipinga, hasa ninapoangalia historia ya utendaji wa kazi wa wanasiasa hao wawili ambao wote kwa miaka 10 iliyopita walipitia hatua mbalimbali za kumuandaa Kikwete kuwa Rais wa Nne wa Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimsingi jibu hili ndilo ambalo limewahi kumfanya hivi karibuni kabisa mwandishi mwenzangu wa habari, Deodatus Balile kuhoji, iweje nchi hii watu washindwe kufanya kazi kwa sababu ya kuogopa kuhusishwa na ‘urais baada ya Kikwete.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hayo ni sehemu tu ya mambo ambayo baadhi ya watu wanayahusisha na Lowassa. Kwa bahati mbaya mengi miongoni mwake ni yaliyo na harufu mbaya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimepata kuyazungumza haya na marafiki zangu na wakati fulani nilipata kuandika makala nikihoji ni siri gani mbaya iliyojificha nyuma ya uwaziri mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lowassa anapaswa kulitambua hilo na kimsingi anao wajibu wa kukisafisha kiti hicho alichokalia kwa kukataa kuhusishwa na kila aina ya takataka. Anapaswa kufanya hivyo akitambua kuwa uongo akisemwa sana hugeuka ukweli.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-696496146652567108?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/696496146652567108/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=696496146652567108&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/696496146652567108'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/696496146652567108'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2007/07/lowassa-kiepuke-kikombe-hiki.html' title='Lowassa; Kiepuke kikombe hiki'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-8176085225085443154</id><published>2007-07-05T23:01:00.000-07:00</published><updated>2007-07-05T23:03:28.325-07:00</updated><title type='text'>Majungu; Falsafa ya ushindi CCM!</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;HUU ni mwaka wa Uchaguzi Mkuu ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kimsingi huu ni msimu wa kuibuka kwa mambo mengi makubwa na madogo yasiyo na kichwa wala miguu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waswahili wanao msemo mzuri kabisa unaokwenda sambamba na majira au nyakati. Msemo huu si mwingine bali ule usemao; ‘dalili za mvua ni mawingu.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa CCM ya zama hizi, limekuwa ni jambo la kawaida kila ukaribiapo msimu kama huu kuanza kusikika na kuonekana kwa matukio ya ajabu ajabu yanayoambatana na vituko vya hapa na pale miongoni mwa wanasiasa wa kada mbalimbali ndani ya nchi hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika dalili za msimu mbaya kabisa za ‘wanasiasa kuanza kuvuna kile walichopanda na kupanda kile wanachotarajia kukivuna zimeanza kuonekana waziwazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno rahisi kabisa, kupitia katika vyombo vya habari, huu sasa ni wakati ambapo CCM hujipambanua kuwa chama ambacho wanasiasa wake, wakiwamo wale wanaoonekana kuwa hodari kabisa kuanza kushikana mashati, kushambuliana, kukashifiana na kupeana sifa nzuri na mbaya. Kimsingi hapo ndipo tulipo sasa, tukijiandaa kufika tuendako.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa lugha rahisi kabisa, chama tawala kinaingia katika kipindi kigumu kingine kigumu kabisa kinachotawaliwa na majungu mepesi na mazito ya kisiasa ambayo yanaendelea kuyathibitisha maneno ya Profesa Issa Shivji ya hulka ya siku zote ya wanasiasa kupenda madaraka, kuliko kuipenda siasa yenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii tunaposoma habari zinazomhusu Amina Chifupa, baadhi yetu tunaishia kuangalia pale alipoangukia mwanasiasa huyo, huku tukisahau kabisa kutupa macho yetu kule alikojikwaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika Amina anapita katika tanuri lenye moto mkali kabisa, lililopata kuwakaanga wanasiasa wengi wakongwe katika nchi hii kama akina John Samuel Malecela, Dk. Salim Ahmed Salim, Dk. Abdallah Kigoda, John Pombe Magufuli, Frederick Sumaye, Prof. Mark Mwandosya na wengine wengi wengine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Amina Chifupa mwanasiasa mwepesi kiumri na mtu anayeonekana kukosa uangalifu katika mambo yake mengi binafsi, pamoja na kutambua kuwa amekuwa ‘target’ safari ametumbukia ndani ya maji ya kina kirefu yaliyopata kuwazoa na kuwamaliza kisiasa kila mmoja kwa kiboko chake wanasiasa hao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna shaka kabisa kwamba, watu anaokabiliana nao, wameamua kwa dhati kabisa kumvua joho la ufahari wake kisiasa na kimsingi makosa yake binafsi yanaweza yakagharimu kwa kiwango kikubwa nafasi yake ya kisiasa iwapo hatakuwa makini kukabiliana nao sawasawa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Amina na wanasiasa wengine wachanga ndani ya CCM wanaojiandaa kwa ajili ya nafasi nyeti za kiuongozi wanapaswa kulifahamu hilo na kutambua kuwa, jitihada za kuwakata miguu ili kuwazuia wapoteze nguvu za kusimama mchuano wakati utakapowadia, ndiyo azma kuu ya wapishi wa fitna hizo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa mbele ya macho yetu tunamuona Amina Chifupa, ukweli ni kwamba, katika suala lake la sasa, yeye ni kivuli tu cha mwenendo wa mambo machafu, siasa za kuvutana mashati na falsafa kuu kuu ya majungu na yenye mafanikio makubwa kabisa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;‘Fitna’ mbaya kabisa kisiasa anayojaribu kukabiliana nayo leo na ambayo sasa imempotezea mume huku ikijaribu kusonga mbele na kumpokonya ubunge wake na baadaye kumnyima matunda mengine ya kisiasa inaweza ikamfanya abakie kuwa majeruhi kwa kipindi kingine kirefu kijacho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna yoyote ile magwiji wa mtandao wanaokabiliana na Chifupa wanaoungwa mkono kisirisiri na genge kubwa la maadui wa mwanasiasa huyo wanaomtuhumu yeye kwa kuwahusisha na biashara za dawa za kulevya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya sana, miongoni mwa wale ambao wanapinga harakati za kujijenga za mwanasiasa huyo ni wabunge wenzake na wengine ni wanachama wenye madaraka ndani ya CCM wakiwa ama wabunge au wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho tawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kile ambacho kimekuwa kikionekana kuwa ni jitihada za Amina kujijengea jina na kujipatia umaarufu mkubwa hata kuwashangaza baadhi ya watu waliokuwa wakimdharau wakati alipoingia bungeni kwa ‘mlango wa nyuma’ akizishinda jitihada za viongozi wake kadhaa ndani ya Umoja wa Vijana wa CCM, sasa kinageuka haraka haraka na kuonekana kuwa uchafu usiopaswa kutetewa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jitihada za kumjengea taswira chafu mwanasiasa huyo, inafanana na kile kilichoitwa uziro wa Sumaye, uarabu wa Salim Ahmed Salim, ukabila wa Mwandosya, ukarani wa Mangula, ubadhirifu wa Kigoda na uzee wa Malecela.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwetu sisi, watawaliwa, walipakodi, wananchi wa kawaida na umma wa Watanzania tatizo tunalopaswa kuliangalia sasa, si kile kinachoweza kuonekana leo kuwa ni ufuska wa Amina Chifupa unaoweza ukafananishwa na sifa mbaya wanazojaribu kubebeshana wana CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimsingi tatizo ni CCM. Mfumo wake wa uongozi na staili ya viongozi wa zama hizi wa chama hicho kukubali kuliongoza taifa hili kwa njia haramu kabisa ya kupikiana majungu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Iwapo Amina Chifupa anastahili kuvuna kile alichopanda kwa sababu ya kukosa kwake uaminifu katika ndoa yake au hata katika chama chake, bado hilo halitoshi kulifanya taifa hili liwe la watu wanaosubiri mabaya ya wengine kama kigezo cha kuanza kuchafuana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenzetu Wamarekani ambao tumenyofoa mambo kadhaa muhimu katika mfumo wa vyama vingi vya siasa wamefikia hatua ya kuwapima viongozi wao kwa kuangalia rekodi zao za utendaji wa kazi za kisiasa kabla hawajaingia katika nafasi ya uongozi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa mfumo wetu wa siasa ya vyama vingi bado ni mchanga kabisa, binafsi naamini kwa dhati kabisa kwamba, CCM, chama kikongwe kuliko vyote, kilipaswa kujijengea mfumo madhubuti wa kuwapata viongozi wake, ambao ungekuwa na uwezo wa kuwaandaa makada, wasomi katika ngazi mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii tabia ya chama hicho tawala kujijengea desturi ya kukusanya wanachama kwa mfano wa kokoro linalovua samaki, pasipo kuangalia rekodi za siku za nyuma kisiasa, kijamii na hata kiuchumi za wanachama wake eti tu kwa sababu ya kuwaonyesha jeuri wapinzani, ni moja ya chachu kuu za kujengeka na kushamiri kwa hulka mbaya za majungu yasiyokoma ndani ya chama hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kile chama chenye heshima ambacho Baba wa Taifa alijaribu kukijenga chini ya mwavuli wa kauli mbiu ya ‘huyu ni mwenzetu’ iliyokuja kubadili maana yake halisi ya awali na kuwa kitovu cha kuwakataa baadhi ya watu makini, leo hii inakitafuna polepole chama hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taifa linalojaribu kujitoa katika tatizo lililoota mizizi la ufisadi, kamwe haliwezi kupata nafasi ya kujinasua katika jinamizi hilo, iwapo nyufa za namna hii zitaendelea kustawi na kuboreshwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii unaposikia taarifa kwamba, viongozi wa juu kabisa wa kiserikali, wakijiingiza katika mitandao ya kuwabomoa baadhi ya wanasiasa na wafanyabiashara kwa sababu zisizo na maslahi ya kitaifa, unapata picha halisi ya mahali tulipo Watanzania na pengine mwelekeo wetu wa siku za usoni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si rahisi kujua ni vikao vingapi vya CCM au Bunge vitakaa na kulijadili suala hili la Chifupa ambalo kwa namna ambayo si rahisi kabisa kuielezea, limepenyezwa kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa njia ya barua ambayo nakala yake anayo Katibu Mkuu wa CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi kweli, viongozi wetu wakuu, wanazo sababu za msingi za kukubali kuingizwa katika mtandao wa majungu ambayo wakati mwingine huwa tunaambiwa huwa yana baraka za viongozi ambao ukiambiwa majina yao na kuangalia nyadhifa tulizowapa unapigwa na butwaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je; baada ya sakata la Reginald Mengi na Mbunge Adam Malima ambalo chimbuko na hitimisho lake ni majungu lililogharimu takriban shilingi bilioni 100 bado Bunge hilo hilo na chama kile kile tawala vina sababu ya kuendelea kujiingiza katika masuala ya kijinga yasiyo na tija?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi kweli tunamtendea haki spika wetu ambaye hivi sasa yuko katika kipindi kigumu cha kulijengea Bunge heshima kwa kuwa na meno ya kujadili mambo yenye tija kitaifa, kuendelea kumuingiza katika masuala ya ufuska ya wabunge wake?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, ni sahihi kwa Yussuf Makamba, kumuingiza katika mjadala mwingine wa ugomvi wa Amina Chifupa na mumewe na akaacha kukiandaa chama chake kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa ndani baadaye mwaka huu, au hata akaweka kando mazungumzo muhimu anayoyaongoza kati ya chama hicho na kile cha CUF.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, ni haki kwa Watanzania wote kujiingiza katika mtego mwingine wa kuwa washangiliaji wa ugomvi wa Mpakanjia na Amina au ufuska wa Mheshimiwa Kabwe na Amina hata kusahau masuala mengine mazito na ya msingi tunayokabiliana nayo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna yeyote ile, Watanzania tunapaswa kuachana na hulka ya kuendekeza majungu kama kweli tunataka kujenga mustakabali mwema wa taifa hili wa siku zijazo. CCM inapaswa sasa kurejea masomo ya maadili kwa viongozi wake ambayo hatimaye yatawarudisha katika mstari wa kusudio la kuasisiwa kwake. Wanahabari tunao wajibu wa kukwepa kuingia katika mtego wa habari za kashfa za ngono kila kukicha wakati nchi hii ikiwa na masuala mengi mengine ya kijamii ya kuyaandikia.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-8176085225085443154?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/8176085225085443154/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=8176085225085443154&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/8176085225085443154'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/8176085225085443154'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2007/07/majungu-falsafa-ya-ushindi-ccm.html' title='Majungu; Falsafa ya ushindi CCM!'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-7710341430557524875</id><published>2007-07-05T22:59:00.000-07:00</published><updated>2007-07-05T23:00:52.730-07:00</updated><title type='text'>Tuna njaa na kiu ya migomo ya kifikra</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;LAITI kama Rais Jakaya Kikwete angelijua, asingekwenda katu kuonana na wanafunzi wa vyuo vikuu Diomond Jubilee mwanzoni mwa mwaka huu kwa lengo la kuwapooza na kuwapa ahadi ya matumaini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokwenda kwake kungetoa fursa kwa wanafunzi hao waliokuwa wamegoma, uongozi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Wizara ya Sayansi, Tekinolojia na Elimu ya Juu na Bodi ya Mikopo kutafakari upya madai ya wanafunzi hao na kuyatafutia majibu yakinifu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kuthubutu kwake kwenda, Kikwete alionyesha ujasiri ambao uliwashinda watangulizi wake kadhaa miaka kadhaa iliyopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo mkutano wake huo na wanafunzi kwa upande mwingine ulibadili kabisa sura ya mzozo kutoka kuwa wa  kitaaluma na kuchukua taswira ya kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimsingi mkutano wa Kikwete na wanafunzi hao, ambao awali ulionekana kuwapa matumaini makubwa wanafunzi hao, sasa umegeuka na kuchukua sura fadhaa kwa wasomi hao na serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zaidi ya miezi miwili sasa tangu Kikwete atoe ahadi kwamba serikali yake isingekuwa tayari kuona mwanafunzi yeyote akifukuzwa shule kwa sababu ya umaskini wa wazazi wake, hakuna kilichoonekana kufanyika bayana katika macho ya wanafunzi hao ambao kwa maneno yao wenyewe wanasema aliwaeleza kuwa jibu lao lingekuwa tayari katika kipindi cha mwezi mmoja tangu hiyo Februari 3 alipozungumza nao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kushindwa huko kwa serikali kutoa jibu la mapema kwa wanafunzi limetoa matokeo mabaya kabisa, kwani subira ya vijana hao wasomi imekoma na badala ya kuelekeza lawama zao dhidi ya sera mbaya ya mikopo, wamejikuta wakirukia hoja mpya kabisa za uendeshaji wa serikali na hata kuingiza siasa za vyama katika malalamiko yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mabango waliyoyabeba siku moja kabla ya kusimamishwa masomo yao, yote yakidhihaki uundwaji wa serikali, utendaji wake wa kazi na hata kufikia hatua ya kuomba msaada kutoka kwa viongozi wa upinzani, yalikuwa ni matokeo ya mkutano ulioshindwa kuzaa matunda kati yao na Rais Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mabango hayo yamezua maoni tofauti miongoni mwa watu mbalimbali. Wako wanaowaona wanafunzi hao kuwa ni watovu wa nidhamu kutokana na kitendo chao hicho cha kuwakebehi viongozi wakuu wa kitaifa na serikali yake na wako wengine wanaowaona wanafunzi hao kama wasemaji wa kweli wa sura halisi ya serikali yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watangazaji wawili wa kituo maarufu cha utangazaji cha Clouds FM, Fina Mango na Masoud Kipanya wao wamekuwa wakikielezea kitendo hicho cha wasomi kuwa kinachoonyesha dharau na kinachotoa sura mbaya kabisa kwa viongozi wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo walichokifanya wanafunzi hao hakikuwa kipya. Wamefanya kile ambacho kinafanywa na vyuo vikuu vyote duniani hadi hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiangalia katika rekodi mbalimbali, wanafunzi wa vyuo vikuu wanatatizwa na ugonjwa unaotokana na msongamano wa kifikra unajengwa na masomo anuai wanayosoma, ukianzia na falsafa, historia, haki za binadamu na mengi mengine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mchanganyiko huo huzaa tafakuri kwa kila kinachopita mbele yake. Hufungua milango ya kupima kila jambo, kulalamikia kila aina ya maumivu, yawe ni madogo au makubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa wanafunzi wa vyuo vikuu duniani. Uvumilivu dhidi ya hujuma ya aina yoyote ni ukondoo na hata subira dhidi ya unyanyasaji wa aina yoyote ni ujinga na kimsingi ni mambo yanayokwenda kinyume kabisa na hadidu za rejea zinazotokana na usomi wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukifungua katika mitandao ya kompyuta leo, utashangaa utakapoona migomo ya chuo kikuu ikiwa imesambaa katika mataifa mbalimbali duniani ukianzia na yale ambayo ni maskini hadi nchi tajiri kupindukia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wingi wa migomo inayotokea katika vyuo vikuu mbalimbali duniani inakwenda sambamba na wingi wa hoja zinazosababisha migomo hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo basi serikali inapaswa kutambua jambo moja kwamba, wanafunzi wa vyuo vikuu hawezi kamwe kukosa sababu ya kugoma katika kipindi chochote wakiwa masomoni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naamini kwa dhati kabisa kwamba, serikali inapaswa kushukuru kwamba, hivi sasa wanafunzi katika vyuo vikuu vyetu wanasumbuliwa na njaa katika matumbo yao, wanakabiliwa na ukata katika mifuko yao na kimsingi wanaishi maisha magumu kabisa wakiwa vyuoni kuliko walivyopata kuishi ndugu, jamaa na Watanzania wenzao waliowatangulia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ufukara wa kimaisha unaowakabili wanafunzi wa vyuo vyetu vikuu, uliochangiwa kwa kiwango kikubwa na sera batili ya uchangiaji wa elimu ya juu, ndiyo msingi mkuu wa malalamiko ya sasa ya wasomi wetu hao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini jambo baya kabisa ni kwamba, hivi sasa wanafunzi hao wanalalamikia kiu na njaa za matumbo yao, tofauti na ilivyokuwa zama zile ambazo kiu ya fikra ndiyo iliyokuwa chagizo kuu la migomo ya wanafunzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wanafunzi wakijenga desturi ya kugoma wakidai posho zao au kuongezewa fedha katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni, wenzao wa zama zile walikuwa wakigoma kupinga sera za uchumi na kijamii za &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushahidi wa hili ni rahisi kabisa. Mwaka 1978/79 wanafunzi wa Chuo Kikuu walipogomea masomo walikuwa wakipinga uamuzi wa wabunge kujiongezea mishahara wakati taifa likiwa ndiyo kwanza limetoka kukabiliana na vita iliyogharimu uchumi wa nchi hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Miaka ya mwanzo ya 1990, wanafunzi wa chuo hicho hicho, tena wakiungwa mkono na maprofesa wao, waligoma kupinga maamuzi ya serikali ya kutaka kuwahamisha wahadhiri kadhaa waliokuwa wakionekana kuwa chachu kuu ya migogoro katika chuo kikuu hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Walichokuwa wakikigomea wanafunzi hao ni kiu yao ya kitaaluma na ‘kiitikadi’ ya kukataa kuondokewa na wahadhiri wao wanamapinduzi akiwa Profesa Mwesiga Baregu, Issa Shivji na Chachage S Chachage.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii ni nadra sana kuikuta migomo ya namna hii ikifanyika katika vyuo vikuu vyetu. Njaa ya matumbo imebadili kabisa ile kiu ya kifikra ambayo kimsingi ndiyo iliyozaa viongozi makini wa migomo wa zama zile, akina Samuel Sitta, Andrew Chenge, na marehemu Wlifred Mwabulambo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Migomo ya kifikra ya namna hiyo hiyo ndiyo ambayo baadaye ilizaa wasomi wa aina ya Zitto Kabwe, John Mnyika na wengine wengi ambao unaweza ukawatofautisha na wagomaji waliokuwa wakiangalia mustakabali wa matumbo yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii wanafunzi kwa makosa yasiyo yao, wanaishia kugomea chakula duni na ukata wa mifukoni, ilhali nchi hii ikiwa imebeba orodha ya majinamizi ya ubadhirifu ambayo kelele zake zinapigwa na vyombo vya habari na viongozi wachache wa vyama vya kisiasa na kijamii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanafunzi wa vyuo vikuu ambao leo hii wamegomea haki yao ya msingi kabisa, tunawaasa kugeuka upande mwingine kwa kuangalia mienendo isiyoridhisha ya maamuzi mabovu kabisa ya kiserikali na kuandaa maandamano kwa ajili yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati huu tunapokaa na kutafakari, tunajikuta tukilazimika kujiuliza hivi wanafunzi wa vyuo vikuu, wamewahi kufikiria kuongoza maandamano ya nchi nzima kupinga kashfa kama zile za rada, matumizi yaliyokithiri serikalini, mikataba yenye utata kama ile ya madini na Richmond?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huko ndiko ambako wanafunzi wanapaswa kuelekea. Wanapaswa kutambua kuwa wao wakiwa vijana wanaopaswa kuwa tanuri la kifikra wanao wajibu pia wa kuhakikisha kuwa wanaliongoza taifa katika kuimarisha maamuzi ya kisera na kisheria ambayo hatimaye yataliondoa taifa hili katika umaskini uliokosa dawa.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-7710341430557524875?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/7710341430557524875/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=7710341430557524875&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/7710341430557524875'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/7710341430557524875'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2007/07/tuna-njaa-na-kiu-ya-migomo-ya-kifikra.html' title='Tuna njaa na kiu ya migomo ya kifikra'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-2864608014079456536</id><published>2007-07-05T22:57:00.000-07:00</published><updated>2007-07-05T22:59:03.816-07:00</updated><title type='text'>Huu ni mwanzo wa mwisho wa matumaini</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;‘Sema unachomaanisha, maanisha unachosema;’ huu ni moja ya misemo maarufu kabisa na iliyozoeleka na wengi. Msemo huu umetafsiriwa neno kwa neno kutoka katika msemo wa Kiingereza; ‘Say what you mean, mean what you say’.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa si rahisi kusema kwa hakika ni nani aliubuni msemo huu au ni kitu gani hasa kilisababisha ukaibuka, ni ukweli wa wazi kabisa kwamba, hivi sasa umegeuka kuwa moja ya semi maarufu inayoandikiwa vitabu, inayofundishwa mashuleni na kufanyiwa tafiti na wasomi wa fani mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mataifa yaliyoendelea na hususan katika medani ya siasa, msemo huu umekuwa mwiba mchungu kwa wanasiasa wengi wanaosaka nafasi za kuchaguliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli wanaozotoa katika majukwaa ya kisiasa aghalab zimekuwa kipimo kikubwa cha kupima utekelezwaji wao mara tu wanapoingia madarakani na wakati mwingine wanapomaliza mihula yao wau wanapotafuta fursa za kugombea uongozi kwa mara nyingine tena.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hiyo ni tofauti kubwa kwa nchi maskini za Kiafrika kama zetu ambazo wanasiasa husema maneno mengi, wakijua hakuna anayeweza akaja siku moja akawapima kwa kuyaangalia maneno yao kwa dhati kabisa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya hulka hii, ndiyo hasa iliyosababisha baadhi ya watu kuwakejeli wanasiasa na hata kufikia hatua wa kuiponda dhana nzima ya (uana) siasa hata ikaonekana kuwa ni sawa na mchezo wa kuigiza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la kawaida hivi sasa kwa wananchi wa kawaida kuwaelezea wanasiasa kuwa watu wa mzaha, waongo na mabingwa wa kusema kile wasichomaanisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya hali hii yamekuwa ni ya kukatisha tamaa kabisa, kwani maana halisi ya siasa katika nchi maskini kama Tanzania imebadilika na kuwa ‘si-hasa’ (not real) badala ya siasa ambayo katika nchi za wenzetu ni dhana inayotumika kutoa changamoto muhimu kabisa za kimaendeleo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hii ya kusikitisha imesababisha basi, wanasiasa wetu kuitumia siasa kama mwanya na daraja la kutafutia madaraka ya kuongoza, wakitambua kuwa kwao wao, uongozi ni ulaji na si utumishi wa watu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwenendo huo wa mambo ndiyo ambao wakati fulani ulimfanya Profesa Issa Shivji atamke maneno ambayo leo hii huenda yana maana kubwa kuliko ilivyopata kuwa miaka michache tu iliyopita pale aliposema; ‘Wasomi wanapenda siasa. Wanasiasa hawapendi siasa, wanapenda madaraka’.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiyatafakari maneno ya msomi huyu, jibu utakalopata ni rahisi kabisa kwamba. Wanasiasa wetu wameamua kuweka kando maana halisi ya siasa kuwa dhana ya uongozi inayompa wajibu mtu kuwaongoza wenzake kisheria na kisera na kuwa dira na kioo cha mwelekeo wa kikundi, taasisi, nchi au jumuiya ya kimataifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hicho alichokisema Shivji kimechukua maana halisi leo hii, wakati serikali ya awamu ya nne, inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete ikiwa ndiyo kwanza iko madarakani kwa miezi 16.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maneno hayo ya Shivji na mwenendo wa mambo hapa nchini unatoa jibu moja rahisi kwamba, maneno matamu tuliyoyasikia kwa viongozi wa awamu hii tangu wakati wa kampeni yameanza kuchukua mwelekeo ule ule wa kusemwa kwa kile kisichomaanishwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la fedheha na kukatisha tamaa kwamba, hadi hivi leo, viongozi wetu wakuu wangali wakitumia misamiati ya ‘wakati ujao’ ya tuta..fanya, tuta..tekeleza, tuta..timiza, tutaendeleza wakati kipindi cha kufanya hivyo kilikwishapita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo lisiloingia akilini hata kidogo leo hii kwa Rais Kikwete na Waziri Mkuu wake, Edward Lowassa kuamua kuitisha kile kinachoitwa kikao cha watendaji serikalini na kuwapa maelekezo ya nini cha kufanya siku zijazo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno mengine ni kichekesho kuwaona viongozi hao wakiwaita kwa mara nyingine tena wakuu wa mikoa na wilaya wakiwa na makatibu tawala wao kwenda Dodoma eti kujadili Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali ambayo imeonyesha hulka ya kudumu ya serikali ya CCM ya kutumia fedha isivyopaswa kila mwaka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ninasema ni kichekesho na hata kuufananisha na mchezo wa kuigiza kwa sababu Kikwete anafanya hivyo leo wakati akijua fika kuwa mwanzoni mwa mwaka jana alitoa tamko zito wakati alipotembelea Wizara ya fedha pale aliposema wale wote ambao watabainika kutumia fedha isivyo watawajibika kwa kupelekwa mbele ya vyombo vya habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwaka mmoja baada ya kutoa tamko hilo, Kikwete huyo huyo tena eti anaitisha kikao cha watendaji cha kuijadili ripoti nyingine ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu na halafu anaahidi kitu kingine kwa ajili ya siku zijazo. Jina la kitendo hiki sinalo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maamuzi ya namna hii yanafanana kabisa na yale yaliyolalamikiwa katika Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu na kimsingi yanaongeza gharama ambazo zingeweza kuepukwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huku akijua kwamba ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu inahusu matumizi yaliyokwishapita, kwa makusudi kabisa Rais Kikwete anajaribu eti kutoa tahadhari ya nini kinapaswa kufanywa kuanzia sasa ili kuepuka makosa yaliyopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi iwapo Rais Kikwete angeamua kusambaza waraka maalum kwa watendaji nchi nzima akitoa maelekezo ya nini kifanywe kuhusu ripoti hiyo ni fedha kiasi gani zingeweza kuokolewa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Iweje leo hii siku chache tu baada ya Bunge kuelezwa kuwa mikutano ya siku moja moja ya Waziri Mkuu na watendaji wa mikoa 10 ya mwanzoni mwa mwaka huu kujadili namna ya kuboresha elimu, ilitumia kiasi cha shilingi milioi 160, serikali iamue kuwakutanisha watendaji wakuu wa mikoa yote nchini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi ni lini serikali yetu hii ambayo daima imejenga hulka ya kudai kuwa gharama kubwa za mikutano kama hiyo ni ndogo kuliko faida ya mikutano yenyewe itaacha kutudanganya Watanzania kwa maneno ambayo hayawezi kupimwa kwa vigezo vya kitakwimu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi Rais Kikwete na Waziri Mkuu Lowassa wanataka kutuambia kwamba, hoja kuhusu matumizi bora serikalini haikuwa sehemu ya mada wakati wa semina elekezi za mapema mwaka jana za watendaji wa mikoa na wilaya ambazo gharama zake bado hazijawekwa bayana?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika huku si kuziba ufa nyumbani, bali ni staili rahisi ya viongozi wetu wakuu kuendelea kutupa matumaini Watanzania kila kunapokucha ili tuaamini kuwa serikalini yetu inakerwa na mabaya yanayotokea na kwamba huo ni mwanzo wa kuelekea kule walikokuita; ‘Maisha Bora kwa Kila Mtanzania’.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati mwingine ninapoziangalia mbwembwe hizi za viongozi wetu huwa nashindwa kutuelewa Watanzania namna tulivyoshindwa kuwawajibisha hawa viongozi wetu ambao kwa miaka zaidi ya 45 wameendelea kuyaahirisha matatizo yetu hata kuufanya umaskini ndiyo uzishinde zile zinazoitwa sera za kuukabili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii Watanzania ambao mara kadhaa Baba wa Taifa alipata kutusifu kwa kusema si wajinga, katika kutambua kile tunachokitaka, tumegeuka na wajinga kwelikweli ambao tumeendelea kusahaulishwa matatizo yetu wakati wa kampeni kabla ya kuanza kunungunika baada ya sura mpya ndani ya CCM ile ile kuingia madarakani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii ukiwasikiliza wale waliokuwa mashabiki wa falsafa za kuahirisha matatizo za Kikwete wakati wa kampeni na baadaye siku za mwanzo za utawala wake unaweza ukawashangaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wao ndiyo wamekuwa watu wa kwanza kulalamika. Wao ndiyo ambao leo wanasema hakuna kinachokwenda mbele, wao ndiyo ambao wameanza kuikebehi serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni juzi tu wasomi wa chuo kikuu ambao waliendesha kampeni za wazi za kumshabikia Kikwete, walibeba mabango ya kudhihaki matumizi yasiyomithilika ya serikali hii tofauti kabisa na ilipokuwa wakati wa kampeni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukisikiliza michango ya waziwazi ya wabunge wa CCM wenye uchungu wa kweli kweli wa nchi yao, katikati ya mistari ya hoja zao utasikia namna walivyo na wasiwasi na namna nchi hii inavyoendeshwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu la mwenendo huu wa mambo ni rahisi kabisa. Matumaini makubwa ambayo Kikwete aliwajengea Watanzania tangu siku alipotangaza kugombea urais kule Kibaha yameanza kupungua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waraka wa Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohammed Shein wa kudhibiti uharibifu wa mazingira kwa kuchukua hatua za mara moja, nao unaonekana kubakia katika makabrasha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ile ahadi ya Lowassa aliyotoa siku alipopitishwa na Bunge kwa kusema atawapa Watanzania utumishi mahiri na makini inaanza kuonekana kuwa ni simulizi ya kufikirika, hasa kiongozi huyo anapowekwa katika mizania na watangulizi wake kadhaa waliowahi kushika wadhifa huo.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Lakini kikubwa ambacho kimeanza kuwafikisha Watanzania huko wanakokwenda sasa, ni hii hulka ya viongozi wetu hao, kuanza kuonekana kuwa ni watu wanaopenda kusema yale wasiyomaanisha na kuziweka viporo ahadi lukuki walizopata kuzitoa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika Serikali ya Kikwete inaonekana dhahiri kuendeleza yale yale yanayoitwa mema ya serikali zilizotangulia za CCM, ambazo kwa bahati mbaya, rekodi ya kipekee inayowatembeza kifua mbele ni amani na utulivu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii Kikwete ambaye baadhi ya wapambe wake wa zama za kampeni walipata kumuita mpinzani aliye ndani ya CCM anaonekana wazi kuanza kuwaangusha wasomi wa vyuo vikuu, wawekezaji wazalendo wanaogombea miradi na wawekezaji wa nje na wakashindwa, wabunge wa CCM, waandishi wa habari na makundi mengine aliyoyapa matumaini mengi yasiyomithilika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika baadhi yetu sasa tumeanza kuamini kwa dhati kabisa kuwa, tabasamu lisilokwisha la Kikwete si suala la maumbile tu kama alivyopata kusema yeye mwenyewe, bali ni kielelezo halisi ya undani wake, upole wake na pengine kushindwa kwake kuchukua maamuzi magumu pale inapobidi.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-2864608014079456536?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/2864608014079456536/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=2864608014079456536&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/2864608014079456536'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/2864608014079456536'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2007/07/huu-ni-mwanzo-wa-mwisho-wa-matumaini.html' title='Huu ni mwanzo wa mwisho wa matumaini'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-1976658908417478214</id><published>2007-07-05T22:56:00.000-07:00</published><updated>2007-07-05T22:57:48.485-07:00</updated><title type='text'>Tuko zama za udikteta mamboleo</title><content type='html'>LEO nawaandikia Watanzania wenzangu, wenye mtazamo kama wangu, ujumbe unaokusudia kutufungua macho kutoka katika usingizi wa pono tuliolazwa na viongozi wetu na sisi wenyewe tukajifunika mablanketi mazito tukiridhia ubembelezwaji haramu wa ‘mtoto lala’.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujumbe wa leo ni rahisi kabisa na ambao kimsingi unaiendeleza hoja yangu ya wiki iliyopita ambayo ilikuwa ikilenga kuamsha hisia na fikra zitakazotuwezesha kutambua kuwa, mfumo unaofungua milango kwa ajili ya soko huria- kiuchumi, demokrasia ya vyama vingi- kisiasa na utawala bora- kijamii ndiyo njia pekee sahihi ambayo hatimaye itatuondoa hapa tulipo leo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania, tupende tusipende, tukubali au tukatae, ahadi na mbwembwe nyingi za viongozi wetu wanaotembea kifua mbele wakitamba kwamba, wamelifanyia mema mengi taifa hili, hata kustahili kuenziwa kwa maneno, kalamu na kura ni mambo ambayo yanafurahisha genge zaidi kuliko kujenga misingi ya kuondokana na umaskini ulioota mizizi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushahidi wa hayo ni rahisi kabisa. Miaka 45 na ushee baada ya uhuru majigambo ya viongozi wetu kutamba kujenga kilomita nyingi tu za barabara za lami na za kokoto, kuongeza idadi ya wanafunzi wanaojiunga na elimu ya msingi, sekondari na vyuo vikuu na sifa nyingi nyingine zinazofanana na hizo ni mambo ambayo yameshindwa kulinusuru taifa hili na fedheha ya ufukara uliokithiri, maradhi yasiyokoma na ujinga usiomithilika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mambo makuu matatu ambayo Serikali ya Kwanza ya Tanzania (1961-1985) iliyaainisha kuwa maadui wakuu watatu wa maendeleo; ujinga, maradhi na umaskini yameendelea kubakia vidonda ndugu kwa taifa hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii Kikwete anapolieleza jarida la NewAfrican (soma toleo la Juni mwaka huu) kuhusu dhamira ya serikali yake kufanikisha mpango wa Elimu ya Msingi kwa Wote (UPE) baada ya kubaini kuporomoka kwa maelezo yanayoonyesha kuwa suala hilo ni jipya sana hapa nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu makini wanafahamu kuwa, wakati Kikwete akisema chini ya UPE ya zama zake hizi imeingiza masomoni asilimia 96 ya watoto wote wanaopaswa kuwa darasani, ukweli ni kwamba kiwango kama hicho au zaidi yake kilipata kufikiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere mwishoni mwa miaka ya 1970.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiuweka kando ujinga, adui mwingine maradhi naye pia amekuwa tatizo kubwa kabisa linalokuwa. Ukiuweka kando ukimwi, maradhi kama kifua kikuu, malaria na kipindupindu ambayo leo hii yanaundiwa mikakati mipya na ya kila jina kukabiliana nayo, yamekuwa katika kuta za maandishi maeneo mbalimbali kwa zaidi ya miaka 35 sasa pasipo kupatiwa ufumbuzi. Nani halijui hilo!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati ukimwi ukiwa sababu mojawapo ya kurejea kwa kasi kwa kifua kikuu, ukweli wa kitakwimu unaonyesha kwamba, ugonjwa huo kama yalivyo hayo mengine (malaria na kipindupindu) yameendelea kuwa sugu yakichagizwa na umaskini mkubwa unaolikabili taifa hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo wakati viongozi wetu wakipiga mbinje kujivunia matunda ya utawala wao, kwa miaka hiyo yote baada ya kuambiwa kuwa tuko vitani tukikabiliana na umaskini, Watanzania tunaendelea kuwa miongoni mwa mataifa sita maskini zaidi duniani. Kwa maelezo yoyote yale hii ni aibu na fedheha.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya sana, wakati baadhi yetu tukitambua kuwa Watanzania, kuanzia kwa viongozi wao hadi kwetu wananchi wa kawaida, tunao wajibu wa kutafuta ufumbuzi wa matatizo haya, baadhi ya wenzetu, kwa sababu wanazozijua wao wameamua kutudhihaki hata kutupiga mkwara tena wa kimaandishi wakitaka eti tuache kuwafuatafuata, vigogo serikalini. Tunasubiri tuone nani atamuacha mwenzake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uamuzi wetu wa kuwakosoa viongozi, kuwakumbusha wajibu wao, na kukemea inapobidi kwa lengo la kuimarisha misingi ya utawala bora tukitumia kalamu zetu, unaonekana kuwa ni wa kisaliti na unaofananishwa na ukibaraka tunaotumwa na wale wanaowaita ‘mabwana’ zetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Viongozi wa serikali wanaokosolewa kwa makali na uzito unaolingana na ukubwa wa makosa yao, wameanza kugeuka mbogo. Wanashambulia kila mmoja anayeonekana kujaribu kuhatarisha madaraka yao ambayo, badala ya kuyaona kuwa dhamana na wajibu wa kuwatumikia wananchi wameyageuza kuwa mtaji wa ulaji wa aina ile ambayo Augustine Mrema alipata kuuita ‘ya kula bila kunawa.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kile ambacho, mchambuzi wa habari, Ansbert Ngurumo alipata kukiandika akiwataja baadhi ya wanahabari wenzake kuwa ni mamluki wa viongozi wa dola, ndicho kinachoonekana kutokea hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukimsoma Ngurumo, ndani ya makala yake utawabaini mbwa wanaowaita watu, mbwa. Wasaliti wanaojivika joho la ushujaa na kuwaita wapambanani vibaraka. Hii ni jeuri ya ajabu kabisa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi ya viongozi walio katika serikali hii ya Rais Kikwete hivi sasa wameanza kuhusishwa na magenge ya ‘kimafia’ yanayoundwa na baadhi ya watu tukiwamo wanahabari ambao pengine kwa ahadi za kupata nafasi za kiuongozi au kimaslahi wanayoyajua wao, wameamua kuanza kutumia vyombo vya habari kuwalinda majemedari wao hao kwa gharama zozote zile.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maelfu ya Watanzania wanaosoma safu hii, wanapaswa kutambua kuwa, huko tuendako, kalamu kali dhidi ya ukiukwaji wa uongozi bora unaofanywa na baadhi ya watu wenye madaraka ndani ya CCM na katika serikali zake zinaweza kukabiliana na dhoruba kutoka kwa wanahabari mamluki wanaojulikana na ambao wameamua ama kujibebesha au kubebeshwa ukibaraka wa kifikra.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pia, viongozi hao hao kwa kadri inavyoonekana, wameshaanza kujipanga tayari kukabiliana na jambo lolote lile linaloelekea kufanana na wimbi la upinzani kutoka miongoni mwa wafanyabiashara na wanasiasa makini kutoka kambi ya upinzani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hiki ambacho wapinzani wa vyama vinne vya siasa, NCCR-mageuzi, TLP, Chadema na CUF wanataka kukiita ushirikiano unaotarajia kuzaa umoja wenye nguvu wa vyama hivyo, tayari umeshaanza kuonyesha dalili za kukisumbua chama tawala na serikali yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukisoma katikati ya mistari, baadhi ya tahariri, ukasadifu viponzo kadha wa kadha na ukazitafakari makala nyingi tu za kichambuzi ndani ya magazeti utayaona mashambulizi makali dhidi ya muungano huo wa upinzani na namna ulivyoshindwa kabla ya wakati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kweli ni jambo la bahati mbaya kwamba, kauli mbiu za Kikwete za Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya zimegeuka na kuwa falsafa na muongozo wa kazi za wanataaluma wa kada mbalimbali wakiwamo wana habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jukumu la wanahabari limegeuka kabisa kutoka katika kundi la wachokozi wa mada, wakosoaji kupitia katika tahariri na makala za kiuchambuzi na kuwa washangiliaji na walinzi wa status quo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kile ambacho Jenerali Ulimwengu amekuwa akikielezea kuwa ni ‘urafiki wa hatari na uliovuka mipaka kati ya wanahabari na wanasiasa’ ndicho ambacho leo hii tusipokuwa macho, kinaweza kikaivuruga taaluma ya habari yenye wajibu wa kuongoza njia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii, Kwame Nkrumah angeamka kutoka kaburini na kufanya tathmini ya kile kinachoonekana kuwa mafanikio ya sera za soko huria na mfumo wa vyama vingi ninao uhakika jina la kitabu chake lisingelikuwa tena; ‘New Colonialism The Highest Stage of Imperialism’ (Ukoloni mambo leo ni hatua ya mwisho ya ubeberu).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Badala yake mwanasiasa na mwanazuoni huyo kwa namna yeyote ile Neo Colonialism ingebadilika na kuwa Neo Liberalism kwa maana ya Udikteta mambo leo ambao watawala wanaoshinda uchaguzi chini ya mfumo haramu wa vyama vingi uliojaa mizengwe iliyokithiri wanavyojaribu kutumia ushindi wao huo kuminya uhuru wa habari, uhuru wa vyama vingi, uhuru wa kufikiri na dhana nyingine za namna hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nkrumah angeshangaa kubaini kuwa ubeberu umebadilika. Angestaajabu kuona watawala wa wa Kiafrika wakiwa wamejenga mtandao wa mahusiano ya ajabu kabisa na mabeberu walioupa jina la utandawazi. Mahusiano haya ndiyo yaliyowapa jeuri watawala wetu hata kuwa na jeuri ya kutumia udikteta mambo leo.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika udikteta mambo leo wa watawala wengi wa Kiafrika, umefanikiwa kuihadaa dunia kuwa demokrasia ya vyama vingi, uhuru wa habari, soko huria la kishindani ni mambo yanayofanya kazi pasipo shida yoyote, ilhali hali ikiwa tofauti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siyo jambo la siri kwa Watanzania wachambuzi wa mambo kutambua kuwa, udikteta mambo leo wa watawala wetu wanaojivunia ushindi wa kishindo ni matokeo ya wazi ya kazi kubwa iliyofanywa ya kuwanyonga wapinzani kwa fitina za uzushi, sheria ngumu na kandamizi zikiwamo zile 40 ambazo Tume ya Jaji Nyalali ilipata kupendekeza zifutwe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ukweli unaojulikana wazi kwamba, ushindi wa asilimia 80 ni matokeo ya kazi batili itakayobakia kuwa historia ya nchi hii ambayo ilivigeuza vyombo vyetu vya habari na na baadhi ya sisi wanahabari (Watanzania watusamehe) kuwa taasisi mahususi za uenezi za CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni jambo la ajabu kabisa kwamba, leo hii, ushindi huo wa kishindo wa asilimia 80 ambao badala ya kuwa mzigo na dhamana isiyobebeka ya wajibu wa kuwatumikia wapigakura umegeuka na kuwa jeuri ya kuwasakama na kuwazulia mambo wakosoaji wengi ninaoamini wanafanya hivyo kwa nia njema kabisa.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujinga wa sisi Watanzania tulio wengi kuendelea kuuona mfumo wa vyama vingi kuwa eti msingi wa kusambaratika kwa umoja wetu, na dalili mbaya za kutoweka kwa amani na utulivu, tukitahadharishwa kuwa makini tusije tukafikwa na yale yaliyowahi kuwafika wenzetu wa Rwanda, Burundi, Kongo, Sierra Leone na kwingineko una sehemu kubwa katika ushindi huo wa asilimia 80.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi Watanzania tumesahau kwamba, asilimia 80 ya watu ambao walipiga kura ya maoni wakitaka mfumo wa chama kimoja uendelee mbele ya Tume ya Jaji Nyalali  ya mwaka 1991 na 1992 ndiyo matunda ya ushindi wa CCM leo hii ambayo viongozi wake wanapita kifua mbele wakiwakebehi wachambuzi wa mambo wanaoikosoa serikali leo hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwangu mimi, CCM na serikali yake wanafanya makosa kuutumia ujinga wetu wa kuvinyanyapaa vyama vya upinzani na kukishabikia chama hicho tawala kwa staili ya zimwi likujualo, kuwa ndiyo jambo la kuwatembeza kifua mbele.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ninasema ni makosa kwa sababu, viongozi hao na mashujaa wao wanaowatumia kuwadhihaki na kuwatukana wachambuzi wanaoikosoa serikali ikiwa ni pamoja na kuwashusha hadhi wanasiasa wa kambi ya upinzani hawajui wanafanya hivyo kwa sababu ya matumbo yao na wala si kwa maslahi na uzalendo wenye manufaa ya leo na kesho ya taifa hili. Hakika huu ni udikteta mambo leo. Tunaelekea kubaya.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-1976658908417478214?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/1976658908417478214/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=1976658908417478214&amp;isPopup=true' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/1976658908417478214'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/1976658908417478214'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2007/07/tuko-zama-za-udikteta-mamboleo.html' title='Tuko zama za udikteta mamboleo'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-7585076624994364845</id><published>2007-07-05T22:53:00.000-07:00</published><updated>2007-07-05T22:55:11.320-07:00</updated><title type='text'>Tumeangushwa na manabii wa uongo, tuanze upya</title><content type='html'>Tunakabiliwa na tatizo kubwa la kiuongozi katika nchi hii. Kimsingi tupo katika tanuru la uongozi uliolipotezea mwelekeo taifa, kiasi kwamba hivi sasa ni jambo gumu kwelikweli kutofautisha baina ya pumba na mchele.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii umaarufu wa kiongozi mmoja binafsi umechukua nafasi ile ile ya uwezo wa kiuongozi au hata kiutawala wa kiongozi huyo huyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ubora wa kiongozi hivi sasa unapimwa kwa maneno rahisi kabisa; ‘Je, akubalika!?’ Kukubalika kunakozungumzwa hapa ni kule kunakojengwa na uwezo wa ushawishi wa kiongozi mhusika ama wapambe wake au mawakala wake rasmi na wasio rasmi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukianzia na uongozi katika vyuo vya elimu ya juu, vyama vya michezo, klabu za kijamii, uongozi wa kidini na hata ule wa kisiasa, hoja kubwa imekuwa ni hiyo hiyo; anakubalika? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya sana, kukubalika huko hakujengwi na historia yeyote ile ya kutukuka ya kiongozi mhusika, mabadiliko aliyowahi kuyafanya huko nyuma au rekodi ya kipekee ya utendaji wake, bali haiba yake binafsi na namna alivyoweza kuwa karibu na watu wengi wanaomuunga mkono.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kile ambacho kwa kimombo kimekuwa kikijulikana kama ‘charisma’ ndicho hicho ambacho sasa kimekuwa kigezo kikuu na sifa ya uongozi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tumefikishwa hapa na historia yetu. Tumefikishwa hapa na urithi mbaya kabisa tulioachiwa na waasisi wa taifa hili. Tumefikishwa hapa na ulafi wa watu wachache ambao kwa makusudi kabisa wamefanikiwa kuipa rushwa jina jema, wale ambao wamebariki ufisadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya kufikishwa kwetu hapo ndiyo yaliyotufanya tuwaite ‘wajanja’, ‘mashujaa’, ‘wenye akili’, ‘wanaoona mbele’, maafisa wa serikali waliojenga makasri katika maeneo mbalimbali nchini kwa fedha ambazo haziwezi kulinganishwa hata kwa chembe ya haradali na mapato yao halali yanayojuolikana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatima ya kupelekwa hadi huko ndiyo ambayo leo hii imetufikisha hatua ya kuwacheka na kuwadharau viongozi waadilifu wa kweli kweli (ukiwaacha walevi, mafuska na wale wenye tabia zinazofanana na hizo) ambao wanastaafu serikalini wakiishi maisha ya kawaida yasiyo na makuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii, taifa hili limefikishwa mahali ambapo wajasiriamali wa kwelikweli wasiofungamana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) au serikali yake kimtazamo wanafinyangwa na kukamuliwa kwelikweli kimapato na serikali huku matapeli makada wa chama hicho tawala wanaofanya biashara kwa njia haramu zenye maswali mengi, wakilindwa na kuheshimiwa kwa kiwango cha kuabudiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hayo ndiyo matunda ya miaka 45 ya uongozi wa Chama Cha Mapinduzi kilichoingia madarakani madarakani mwaka 1961 kwa jina la Tanganyika African National Union (TANU) kwa Tanzania Bara na kuanzia mwaka 1964 kikijulikana kwa jina la Afro Shiraz Party (ASP) kule Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hayo ndiyo matokeo ya urithi mbaya tuliogawana wakati wa zama za vita baridi ambayo upepo wa mabadiliko yake umewakamata pabaya Watanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msingi wa mambo hayo ni maamuzi ya kimaono ya kiongozi mkuu wa kwanza wa chama hicho tawala, Julius Kambarage Nyerere, aliyeamua kulipeleka taifa hili maskini katika kundi la nchi zisizofungamana na upande wowote mwanzoni kabisa mwa miaka ya 1960 baada ya kutambua kuwa tulikuwa hatuna ubavu wa ama kushikamana na mataifa ya kibepari ya kimagharibi au kuungana na yale ya kisoshalisti ya mashariki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwalimu, akitumia maono yake binafsi na taaluma yake ya masomo ya historia akaona namna ilivyokuwa vigumu kwa kijinchi maskini kama hiki kujitwisha ubepari au ukomunisti na badala yake akaifanya kile walichofanya viongozi wenzake kadhaa wa Kiafrika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yeye na wenzake kadhaa ambao leo wanaitwa mashujaa wa Afrika wakaja na kile walichokiita Ujamaa wa Afrika (Africa Socialism), wakisema huo ndiyo mfumo unaotokana na mazingira ya kihistoria ya bara hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujamaa huo wa Afrika ulichukua sura tofauti katika nchi mbalimbali za Kiafrika. Kwame Nkrumah shujaa nambari wani, yeye akaunda wake, Milton Obote naye akaja na wake, hivyo hivyo Leopold Senghor wa Senegal, baadaye Muamara Gaddafi wa Libya na hata Jomo Kenyatta wa Kenya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwalimu yeye akaja na ujamaa. Akautaja kwa mara ya kwanza mwaka 1962 na miaka mitano baadaye akaja na Azimio la Arusha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huo ukawa mwanzo wa Tanzania kuanza kuzalisha orodha ndefu ya manabii wa kisiasa, wengi wao wakiwa ni wanafunzi waliopata masomo yao katika nchi za kisoshalisti duniani zikiongozwa na lililokuwa Shirikisho la Kisoshalisti la Kisovieti (USSR), iliyokuwa Ujerumani Mashariki, Cuba na kwingineko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii miaka mingi baadaye, mafundisho ya unabii huo, ambao kiongozi na mwasisi wake alikuwa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, Tanzania imezalisha viongozi mahodari wa kusema kile wasichoamini na kuamini kile ambacho hawakisemi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya sana, orodha ya viongozi wa namna hiyo imekuwa ikiongezeka kwa kasi ambayo inapaswa kudhibitiwa, kutoka kizazi kimoja kwenda kingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Karibu miaka 22 sasa tangu Mwalimu ang’atuke kutoka madarakani, Tanzania imepata jina jipya ikijulikana kama ‘Bongoland’ ambalo wakati fulani Mkapa alipata kuonyesha hisia ya kukerwa na maana yake ya sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wa zama za Mwalimu na baadaye enzi za Mzee Ali Hassan Mwinyi, neno Bongoland likimaanisha watu wanaoishi kiujanjaujanja, lilikuwa ni neno lililokuwa likiwagusa watu wa daraja la chini kabisa, waliokuwa hawana mbele au nyuma na waliokuwa wakiishi kwa utapeli, leo hii neno na tafsiri halisi ya neno hilo vimepanda daraja. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Upandaji wa daraja kwa maana na matumizi ya neno hilo yalikwenda sambamba na mabadiliko ya serikali tangu zama za Mwalimu, na baadaye Mwinyi kabla ya kujistawishi wakati wa uongozi wa Benjamin Mkapa na hatimaye kuchukua kabisa madaraka mwaka 2005.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kundi lililompa ushindi Rais Jakaya Kikwete lililojumuisha watu kama, Bernard Membe, Edward Lowassa, Mohammed Abdulaziz, Rostam Aziz, Ukiwaona Ditopile Mzuzuri na wengine ambalo miaka takriban 10 iliyopita lilipewa majina mengi ya utani yaliyokuwa yakiendana na haiba zao enzi hizo kama; ‘watoto wa mjini’, ‘Boyz 2 Men’ na mengine mengi leo hii limefanikiwa kushika madaraka ya juu kabisa ya nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanachama wa kundi hilo ambalo kabla ya kupanda ngazi hata kuingia katika viunga vya ikulu na wengine kukalia makazi ya waziri mkuu na kusindikizwa kwa mbwembwe za ving’ora lilikuwa likisifiwa kwa namna lilivyokuwa na uwezo wa kujichanganya na watu wa aina mbalimbali, leo hii ni nadra kuwaona katika hali kama ile tena.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Urithi wa kundi hili haukuanza nao, bali ulirudi nyuma zaidi zama za Mkapa mwenyewe ambaye naye zama zake za kabla ya ikulu alikuwa mtu wa kariba hiyo hiyo ya kujichanganya, japo yeye kundi lake lilihusisha wasomi vijana wa zama zao, miaka ile ile ya 1970, 1980 na 1990.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushahidi wa hili ni rahisi kabisa. Mtazame Mkapa, angalia mbwembwe za uvaaji wake, utanashati wake, mapenzi yake kwa vidani, pete kubwa kidoleni chain pana shingoni na salamu yake maarufu ya; ‘mambo!!!’ vyote vilikuwa vikionyesha jitihada zake za kujaribu kuwasiliana na vijana wenzake aliojichanganya nao zama akiwa hajagusa zulia jekundu la ikulu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukimwacha Mkapa warejee wadogo zake aliowarithisha ikulu, madaraka na mamlaka. Anza na Kikwete na baadaye wachunguze akina Lowassa, Membe, Nao utaona mambo mengi yanayowafanya wajaribu kila mara kuwasiliana japo kwa haiba na kundi lile waliloliacha. Hii inaweza ikawa falsafa ngumu kuielewa haraka. Itafakari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo haya ya malezi mchanganyiko ndiyo ambayo leo hii yanauweka uongozi wetu hivi sasa katika zama tofauti kabisa na zile za akina Mwinyi na Nyerere ambao malezi yao yaliwanyima fursa ya kuchamana na makundi yaliyo nje na haiba za kiuongozi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa ni kweli kwamba, viongozi wa zama za Mkapa na hawa wa Kikwete wanazo fursa fursa za kulijua vyema kundi lililowazunguka linalowakilishwa na vijana wa mitaani, au vijana wa zamani kama wanavyojulikana baadhi yao hivi sasa, bado wamerithi hulka mbaya ambazo wanapaswa kukabiliana nazo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa hulka hizo walizorithi ni nyingi, kubwa ambayo nitaanza kuizungumzia wiki hii na kuendelea nayo wiki ijayo ni hii ya unabii wa uongo wa viongozi wetu ulioanza tangu zama za Serikali ya Awamu ya Kwanza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania wenye umri wa zaidi ya miaka 40 sasa wanakumbuka namna taifa hili mwaka 1980 lilipoahidiwa kuanza kupata neema ya kukua kwa uchumi katika kipindi cha miezi 18 baada ya kumalizika kwa vita ya Uganda ambayo iligharimu mamilioni ya fedha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii miaka 27 baadaye hali ya uchumi bado haijatengemaa na unabii wa kwanza wa kuikomboa nchi hii kiuchumi umekwama hadi hivi leo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kukwama kwa unabii huo wa kiuchumi kulikuja miaka zaidi ya 10 baada ya kukwama kwa unabii wa Azimio la Arusha ambalo Baba wa Taifa alilisimamia na akalipigania kwa nguvu zake zote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huku akidhani kwamba, alikuwa amefanikiwa kurithisha ajenda yake kwa manabii wake, Mwalimu alipigwa na butwa baada ya kubaini kuwa takriban manabii wake wote walikuwa wamemsaliti. Walihubiri Ujamaa mchana na jioni wakakiuka misingi ya falsafa hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuzorota kwa Azimio la Arusha na baadaye kukwama kwa  programu ya miezi 18 ya kujinasua kiuchumu kulifuatiwa na kuzorota na baadaye kuendelea kushindwa kabisa kwa mipango mingine ya kiuchumi ya taifa hili iliyoasisiwa na serikali za awamu za pili na tatu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiuliza leo ni kwa nini unabii wa akina Nyerere, Rashid Kawawa uliorithishwa kwa akina Mwinyi na baadaye kwa Mkapa wa kukabiliana na maadui wakuu watatu, umaskini, ujinga na maradhi umeishia wapi? Hautapa jibu la moja kwa moja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii hotuba aliyowahi kutoa rais wa zamani wa Marekani, Ronald Reagan Novemba 2 mwaka 1988 kuhusu mapambano dhidi ya umaskini unaweza ukapata jibu rahisi kabisa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Reagan mmoja wa marais wa taifa hilo kubwa siku hiyo alisema bayana akiilenga nchi yake pale aliposema umaskini ndiyo ulioshinda vita ya kuukabili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna anayeweza akabisha kuwa hata hapa nchini, umaskini umeushinda nguvu unabii wa akina Nyerere, Mwinyi, Mkapa na sasa Kikwete naye akiwa na unabii ule ule uliopambwa kwa maneno totauti; “Maisha Bora kwa Kila Mtanzania” umeanza kuonyesha dalili zile zile za kukwama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii vita anavyoongoza Lowassa vya kuhamasisha ujenzi wa shule za msingi na sekondari nyingi zaidi katika kila kata inapiganwa kama vile nchi hii haijawahi kuwa na programu maarufu ya enzi za Mwalimu Nyerere ya Elimu kwa Wote (UPE) ambayo tafsiri yake ilibadika na kuwa Elimu Pasipo na Elimu (UPE).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Unabii wetu kuhusu maradhi ndiyo mbaya zaidi kuliko mwingine wowote kwani, kwa zaidi ya miaka 40 tangu tutangaze vita dhidi yake, tumeshindwa kuyamaliza baadhi ya magonjwa sugu huku mengine mapya yakiendelea kuibuka kila kukicha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii taifa linashindwa kukabiliana na maradhi kama kipindupindu, malaria, kifua kikuu, Homa ya Bonde la Ufa na mengine mengi kwa sababu unabii wake ulijengwa katika misingi mibaya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umefika wakati wa kugeuka Kaskazini na kuachana na unabii na manabii wa uongo. Tukiendelea kuwa mafundi wa kujidai tunaanzisha programu mpya za kumaliza matatizo yetu kila kukicha, taifa hili litaendelea kupiga maktaimu wakati wenzetu wakiruka na kutuacha tukiwa pale pale. Tunapaswa kuanza upya.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-7585076624994364845?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/7585076624994364845/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=7585076624994364845&amp;isPopup=true' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/7585076624994364845'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/7585076624994364845'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2007/07/tumeangushwa-na-manabii-wa-uongo-tuanze.html' title='Tumeangushwa na manabii wa uongo, tuanze upya'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-6343881135493105879</id><published>2007-07-05T22:48:00.000-07:00</published><updated>2007-07-05T22:53:29.322-07:00</updated><title type='text'>Je huu ndiyo ushupavu wa uongozi?</title><content type='html'>Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;AGOSTI 25 mwaka 2004, takriban mwaka mmoja na ushee kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu uliomwingiza Rais Jakaya Kikwete na wanamtandao wenzake madarakani, Benjamin Mkapa wakati huo akiwa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, alitoa moja ya hotuba ambazo kwangu itaendelea kubakia kuwa ya kihistoria.&lt;br /&gt;Mkapa alitoa hotoba hiyo iliyokuwa ikibeba ujumbe mzito wakati alipokuwa akiwahutubia wajumbe wa mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika Dodoma.&lt;br /&gt;Siku hiyo hiyo baada ya Mkapa kumaliza hotuba yake hiyo, aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Philip Mangula aliielezea hotuba hiyo kuwa ya kihistoria na akatamka kwamba ndiyo itakayotumika kama dira ya chama hicho kitakapokuwa kikielekea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.&lt;br /&gt;Kimsingi Mkapa aliibadilisha hotuba yake na ikachukua sura ya mada ya kisiasa na kwa maneno yake mwenyewe, akaipa kichwa cha habari kisemacho, ‘Ushupavu wa Uongozi’ au kwa Kiingereza, ‘The Courage of Leadership’.&lt;br /&gt;“Leo nimeamua kutoa hotuba, tena iliyoandikwa, maana jambo nitakalo kulizungumza ni zito na nimelitafakari kwa muda sasa. Napenda kuzungumza nanyi kuhusu ushupavu wa uongozi, kwa Kiingereza: “The Courage of Leadership.&lt;br /&gt;“Nafanya hivyo kwa vile tunaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu mwakani (2005).” Hayo yalikuwa ndiyo maneno ya utangulizi katika hotuba hiyo aliyokuwa akiitoa huku akisoma.&lt;br /&gt;Hakuishia hapo Ben; bali alikwenda mbele zaidi na akahoji kwa kujiamini kabisa akisema: “Napenda leo tujiulize swali la msingi kabisa. Sisi Chama Cha Mapinduzi tunataka uongozi; vema, lakini je, chama chetu kinao ushupavu wa uongozi unaohitajika katika mazingira ya karne ya 21? Wagombea wetu watarajiwa nao je?”&lt;br /&gt;Huo ulikuwa ni utangulizi wa maneno mazito. Kwa hakika ni dhahiri kwamba Mkapa alijenga hoja kwa kauli nzito.&lt;br /&gt;Nikiwa miongoni mwa waandishi wa habari waliokuwa wakifuatilia moja kwa moja hotuba hiyo, niliguswa na msingi wa ujumbe wake na leo hii miaka karibu mitatu baada ya kutoa hotuba yake hiyo, bado maneno hayo ya Mkapa yameendelea kubakia chachu ya tafakuri zangu kuhusu mwenendo wa siasa zetu na mustakabali wa taifa letu.&lt;br /&gt;Hotuba hiyo ya Mkapa ilibadili kwa kiwango kikubwa mwelekeo wa kifikra wa wanasiasa wengi, na kwa mara ya kwanza akawajengea Watanzania subira ya kuwapo kwa matumaini mema.&lt;br /&gt;Kwangu hiyo ilikuwa ni hotuba ya nne bora kabisa iliyowahi kutolewa na Mkapa. Iliingia katika kumbukumbu ya hotuba nyingine tatu alizopata kuzitoa awali.&lt;br /&gt;Kwanza alinikumbusha ujasiri na kujiamini aliotuonyesha Watanzania wakati wa mdahalo wa wagombea urais wa Tanzania mwaka 1995, alipowafunika wenzake akiwamo Augustine Mrema, ambaye alikuwa akionekana chaguo la wengi, nje ya CCM.&lt;br /&gt;Pili, alirejesha nyuma kumbukumbu zangu hadi Oktoba 10 mwaka 2001 alipotoa hotuba nzito siku vyama vya CCM na CUF vilipotia saini muafaka wa kisiasa uliopanga kumaliza mgogoro wa kisiasa wa Zanzibar.&lt;br /&gt;Tatu, alirejesha hisia zangu hadi Oktoba ya mwaka 1999, alipotoa hotuba nyingine nzito wakati wa mazishi ya Baba wa Taifa, hata baadhi ya watu kudiriki kusema, ‘mzimu’ wa Mwalimu Julius Nyerere ulikuwa umemgusa.&lt;br /&gt;Kwa maneno mengine yoyote yale, hotuba ile ya Mkapa ya ‘Ushupavu wa Uongozi’ ilipaswa na kimsingi inapaswa iendelee kuwa moja ya hotuba za kukumbukwa miaka mingi baadaye.&lt;br /&gt;Kama zingekuwa zikipangwa katika madaraja, basi hotuba hiyo ya Mkapa ingeweza kushika nafasi ya pili kwa kuwa na mawazo ya kimapinduzi baada ya ile aliyoitoa Rais Jakaya Kikwete bungeni, Desemba 31 mwaka 2005, siku chache tu baada ya kuingia Ikulu.&lt;br /&gt;Mkapa katika hotuba yake hiyo ndipo alipotangaza kwa mara ya kwanza, haja ya CCM kuwa na wagombea kuanzia wa urais, ubunge na hadi udiwani wenye uwezo wa kutenda pasipo kutegemea nguvu za chama.&lt;br /&gt;Ni katika hotuba hiyo, Mkapa alionyesha kutambua kuwapo kwa uwezekano wa chama hicho kuwa na kapu la viongozi aliowaita wa hovyo, ambao ushindi wao ungetegemea tu nguvu ya CCM.&lt;br /&gt; “Na zipo njia mbili kubwa za mtu kushinda uchaguzi. Moja ni kuhakikisha unakuwa mgombea wa chama chenye nguvu na mvuto, kama ilivyo CCM hivi sasa. Maana yake ni kuwa hata wewe mgombea ungekuwa hovyo kiasi gani, utabebwa na chama, na utachaguliwa kuwa diwani, mbunge au rais, kwa sababu tu ya chama. &lt;br /&gt;“Njia nyingine na ya pili, ni mgombea mwenyewe kuwa na sifa ambazo zinatosha kuvutia wananchi wampigie kura, sio chini ya kivuli cha chama chake.  Napenda leo tujikumbushe kuwa yote haya mawili ni muhimu: Chama imara, chenye ushupavu wa uongozi; na wagombea imara, wenye sifa, uwezo na ushupavu. Na kuhakikisha kabisa, yote mawili ni muhimu na ni vema yaambatane,” alisema Mkapa.&lt;br /&gt;Hicho alichokisema ndicho kinachoonekana leo. CCM imeendelea kama alivyopata kusema Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere kuwa dodoki au kokoro lililobeba uchafu wa kila namna ndani yake.&lt;br /&gt;Si jambo la siri kwamba wanasiasa kadhaa wa hovyo kabisa (kama alivyotanabaisha Mkapa) wameweza kupenya na kushinda ubunge na baadhi yao wameukwaa hata uwaziri kwa sababu tu ya dhamira ya rais kuwianisha uwakilishi wa kimikoa na kikanda.&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo basi, msingi mbaya uliojengwa na CCM umesababisha wanasiasa wa hovyo wafanikiwe kukitumia chama hicho kama maficho ya ama udhaifu wao wa kupindukia au madhambi yao mengi mengine.&lt;br /&gt;Matokeo ya hili ni ya wazi kabisa. Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu, wanalazimika kufanya kazi za  mawaziri, naibu mawaziri, wabunge na hata madiwani.&lt;br /&gt;Ushahidi wa hili ni rahisi kabisa. Kikwete ndiye anayeongoza hamasa katika michezo, ndiye anayetoa muongozo katika sekta ya ardhi na ndiye huyo huyo anayekwenda kufungua shule na kuagiza TANESCO waipelekee umeme. Unajiuliza mawaziri, makatibu wakuu, watendaji mbalimbali wako wapi?&lt;br /&gt;Edward Lowassa, ndiye anayelazimika kurudiarudia harakati za rais wake kuchochea ari ya ujenzi wa madarasa katika mikoa, hata kufikia hatua ya kuwaita watendaji wa mikoa kwa zamu wakati nchi hii ikiwa na wizara mbili zinazoshughulikia maendeleo ya elimu.&lt;br /&gt;Ni Lowassa huyo huyo anayeratibu mapambano dhidi ya homa ya bonde la ufa na kipindupindu ilhali kuna mawaziri, watendaji na mawaziri katika wizara za afya, kilimo, mifugo na taasisi nyingine za kitaalam zikiwamo.&lt;br /&gt;Mbaya zaidi ni kwamba, Waziri Mkuu anakwenda nje ya nchi, kama alivyokuwa New Zealand hivi karibuni, na anajikuta akilazimika kufanya ziara ya kutembelea mashamba ya kabeji na kujionea ukulima wa kisasa, akiwa ameongozana na viongozi wengine kadhaa isipokuwa Waziri wa Kilimo. Hili nalo ni jambo la kushangaza.  &lt;br /&gt;Kwa maneno rahisi kabisa, matendo haya yanayofanywa na viongozi wetu wakuu hayatokani na ushupavu wao kiuongozi, bali ni udhaifu mkubwa wa kiutawala unaotokana na CCM kuruhusu kuwa na jeshi kubwa la viongozi wasio na uwezo.&lt;br /&gt;Haya ndiyo matokeo ya kuendeleza kasumba inayodai kuwa, nafasi za uwaziri, ukuu wa mikoa na wilaya ni za kisiasa wakati tukijua kuwa matatizo yanayotokea katika maeneo wanayofanyia kazi yanatakiwa kupatiwa majibu ama ya kimenejimenti, kisaikolojia au hata kisayansi. Huku kwa hakika ni kucheza mchezo wa kujificha na mwenzi wetu umaskini.&lt;br /&gt;Kila mara ninapopata fursa ya kuzungumza na wasaidizi wa Rais Kikwete na Waziri Mkuu Lowassa, huwa napata jibu moja kutoka kwa watu hao, la kunitaka nitambue kuwa eti viongozi wetu hao wawili wanatumia muda wao mwingi kuhangaikia matatizo ya watu kwa maslahi ya taifa.&lt;br /&gt;Majibu hayo hugeuka kichekesho kikubwa kabisa kwangu, kwani wakati nikikubali kwa dhati kabisa kwamba viongozi wetu hao wawili hutumia muda mwingi kufanya kazi hizo, natambua vile vile kuwa wanafanya kazi ambazo si zao.&lt;br /&gt;Kikwete na Lowassa wanapaswa kutambua kuwa, wakati wakiwa na wajibu wa kufuatilia utendaji wa kazi kitaifa, wanao wajibu pia wa kuwaamini wasaidizi ambao wengi wao wameteuliwa na wao wenyewe.&lt;br /&gt;Hii tabia ya Rais na Waziri Mkuu kuzikimbia kabisa ofisi zao, mwaka mmoja na ushee sasa, eti wakitafuta kuonekana kuwa wao ni watu wa ‘field’, hata kufikia hatua za wao kugeuka na kuwa madiwani, wabunge, wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa, naibu mawaziri na hata mawaziri, inakinzana na misingi ya utawala bora.&lt;br /&gt;Kama wanabisha hebu wawaangalie viongozi wakuu wa mataifa yaliyoendelea kama Marekani, yenye uwezo mkubwa kifedha kuliko sisi, wenye miundombinu bora kabisa kama barabara kuliko sisi, na waangalie muda ambao rais na makamu wake wanatumia nje ya ofisi zao ndani ya nchi yao.&lt;br /&gt;Ni nadra na kimsingi hakuna kitu kinachoweza kikafanana na uzururaji kwa Rais wa Marekani, George Bush ndani ya Marekani na kila anaposikika akisafiri kutoka Washington yaliko makao yake makuu, kwenda katika jimbo jingine, basi ni ama anafanya hivyo yanapotokea maafa kama yale ya Katrina au anadhuria mkutano muhimu.&lt;br /&gt;Leo hii hapa nyumbani, kasi ya Rais Kikwete kushughulikia masuala madogo madogo ya ndani ya nchi au yale yanayohusu mahusiano ya kimataifa, inaonekana kuwa ni kubwa kuliko hata alipokuwa Mbunge wa Chalinze na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.&lt;br /&gt;Kikwete anakaribia kufanya makosa yale yale ya mtangulizi wake, ambaye hata alipokuwa Rais wa Jamhuri kwa miaka 10, bado alikataa kabisa kuiacha nafasi ya uwaziri wa mambo ya nje, akitumia kisingizio kile kile kinachotumika leo, kuwavuta wawekezaji na kurejesha imani ya mataifa makubwa.&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo basi, nikitumia maneno ya Mkapa; “The Courage of Leadership”, napenda kutumia fursa hii kuwaasa viongozi wangu wakuu wawili; Kikwete na Lowassa, kutafakari upya matumizi mabaya ya fursa waliyopewa na Watanzania, kwa kujenga mtandao imara wa wasaidizi kuanzia ngazi za chini kabisa ili kujipunguzia mzigo mzito wa madaraka wanayojaribu kujitwisha.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-6343881135493105879?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/6343881135493105879/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=6343881135493105879&amp;isPopup=true' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6343881135493105879'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/6343881135493105879'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2007/07/je-huu-ndiyo-ushupavu-wa-uongozi.html' title='Je huu ndiyo ushupavu wa uongozi?'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-2424436984951164992</id><published>2007-01-25T02:32:00.000-08:00</published><updated>2007-01-25T23:23:56.607-08:00</updated><category scheme='http://www.blogger.com/atom/ns#' term='Politics'/><title type='text'>Zanzibar inadai Mapinduzi mengine</title><content type='html'>Zanzibar inadai mapinduzi mengine!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na Absalom Kibanda&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vyama viwili vya siasa, vyenye ushawishi unaowiana&lt;br /&gt;Zanzibar, Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha&lt;br /&gt;Wananchi (CUF) vimewarejesha tena Watanzania na&lt;br /&gt;hususan Wazanzibari kule walikotoka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vyama hivyo vimeanzisha tena kile kinachoitwa&lt;br /&gt;mazungumzo ya kuponya jinamizi lililobadili jina la&lt;br /&gt;awali la ‘mgogoro’ na ambalo hivi sasa limebatizwa&lt;br /&gt;jina tofauti; ‘mpasuko.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jemedari mkuu anayeongoza mapambano ya kukabiliana na&lt;br /&gt;jinamizi mpasuko safari hii ni mpya, naye si mwingine&lt;br /&gt;bali Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Nne wa Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kikwete anaingia katika pambano hilo la Zanzibar&lt;br /&gt;akikabiliana na kinara wa siasa za visiwani kwa zaidi&lt;br /&gt;ya&lt;br /&gt;miongo miwili na ushee, Seif Sharif Hamad, al- maarufu&lt;br /&gt;‘Maalim’ miongoni mwa Wazanzibari na hususan watu&lt;br /&gt;wanaohusudu sera zake na za chama chake cha CUF.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa ajenda ya sasa ya kutafuta suluhu dhidi ya&lt;br /&gt;mpasuko wa Zanzibar ilijengwa na Kikwete siku chache&lt;br /&gt;tu baada ya kutwaa madaraka ya urais Desemba mwaka&lt;br /&gt;juzi, ukweli uko wazi kwamba hicho alichokisema&lt;br /&gt;kilikwisha kuwapo na kwa hakika alikuwa akilazimika&lt;br /&gt;kutafuta maneno yaliyokuwa na mwelekeo wa kutoa tiba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuanza tena kwa mazungumzo kati ya vyama hivyo vya CCM&lt;br /&gt;na CUF wiki iliyopita, vikiongozwa na Katibu Mkuu wa&lt;br /&gt;chama tawala, Yussuf Makamba kwa upande mmoja na&lt;br /&gt;Maalim Seif kwa upande mwingine, kumelirejesha taifa&lt;br /&gt;kule kule lilikoshinwa miaka kadhaa iliyopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa CCM katika kipindi chote tangu Uchaguzi Mkuu wa&lt;br /&gt;kwanza wa vyama vingi mwaka 1995 imekuwa ikibadilisha&lt;br /&gt;majemedari wakuu na wasaidizi wake wa kukabiliana na&lt;br /&gt;mzozo wa kisiasa wa Zanzibar, kutoka kwa Ali Hassan&lt;br /&gt;Mwinyi (1994-95), Dk. Salmin Amour Juma (1995-2000) na&lt;br /&gt;Benjamin Mkapa (1995-2005), CUF wao kwa miaka hiyo&lt;br /&gt;yote wamekuwa wakimuweka mbele Maalim Seif katika&lt;br /&gt;makabiliano hayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno mengine, mwenendo huu wa mambo ambao&lt;br /&gt;hauendi mbele zaidi ya kurudi nyuma na kuongeza hali&lt;br /&gt;ya wasiwasi, umemwacha Maalim Seif kuwa ndiye nguzo&lt;br /&gt;kuu ya kubadilika kwa mwelekeo wa mambo katika siasa&lt;br /&gt;za Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Japo mwenyewe Kikwete, hajatoa kauli yoyote&lt;br /&gt;akimwelekezea Maalim Seif, anaonekana kutambua ukweli&lt;br /&gt;wa mambo ulivyo huko Zanzibar ambao nyuma ya jinamizi&lt;br /&gt;mpasuko yuko huyo mwanasiasa huyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa CCM na CUF wameanzisha tena mazungumzo ya aina&lt;br /&gt;ile ile yaliyofanyika kwa mara ya kwanza mwaka 1998 na&lt;br /&gt;baadaye tena yakarejewa mwaka 2001, bado kuna&lt;br /&gt;uwezekano kuwa majibu ya mazungumzo ya sasa yakazaa&lt;br /&gt;mazungumzo mengine baada ya mwaka 2010.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vyama hivyo vinaingia katika mazungumzo, wakati hali&lt;br /&gt;ya kisiasa ya Zanzibar ikiwa iko bayana kabisa machoni&lt;br /&gt;mwa wadadisi wa masuala ya kisiasa na kiutawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Majibu ya tatizo la Zanzibar ni mengi na rahisi kwani&lt;br /&gt;katika kipindi cha miaka 15 kilichopita yamekuwa&lt;br /&gt;yakibainishwa na watu mashuhuri, yakafanyiwa utafiti&lt;br /&gt;na taasisi za kisomi na matokeo yakaonekana pia katika&lt;br /&gt;chaguzi tatu zilizopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hayati Abdulrahaman Babu mmoja wa Wazanzibari wasomi&lt;br /&gt;alipata kutafakari kuhusu namna bora kabisa ya&lt;br /&gt;kumaliza tatizo la Zanzibar ambalo wakati fulani huko&lt;br /&gt;nyuma liliwahi kushuhudia uhasama mkali kati ya&lt;br /&gt;wanachama wa vyama viwili vya CCM na CUF.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Profesa Babu, mmoja wa wanaharakati wa mwanzo wa siasa&lt;br /&gt;za Zanzibar alikufa akiamini kwamba suluhu ya kudumu&lt;br /&gt;visiwani humo itakapitakana iwapo tu itajengwa nguvu&lt;br /&gt;kubwa ya tatu, itakayovilazimisha vyama vikuu hivyo&lt;br /&gt;viwili vya CCM na CUF kupoteza ushawishi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya, si Babu mwenyewe wala waumini wa&lt;br /&gt;ajenda yake hiyo wakiwamo wanasiasa kama Sultan Sultan&lt;br /&gt;na Naila Jiddawi walifanikiwa kuiweka mezani na&lt;br /&gt;ikapata visheni ya mafanikio ambayo alikuwa&lt;br /&gt;akiyafikiria. Hilo likawa moja ya majibu ya kupatikana&lt;br /&gt;kwa suluhu ya kudumu Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwaka 1995 muda mfupi tu baada ya kupata taarifa&lt;br /&gt;kwamba, Dk. Salmin Amour Juma aliyekuwa mgombea urais&lt;br /&gt;wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM alikuwa ndiye mshindi&lt;br /&gt;kwa kupata asilimia 50.2 ya kura zote zilizopigwa,&lt;br /&gt;Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alitoa kauli&lt;br /&gt;ambayo chama alichokiasisi kimeendelea kuikataa na&lt;br /&gt;kuifumbia macho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwalimu ambaye wakati huo alikuwa Morogoro akimpigia&lt;br /&gt;kampeni Benjamin Mkapa aliyekuwa mgombea wa urais wa&lt;br /&gt;Tanzania, aliwataka wana CCM wa Zanzibar kukubali&lt;br /&gt;kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa ambayo&lt;br /&gt;ingekishirikisha chama cha CUF ambacho mgombea wake,&lt;br /&gt;Maalim Seif alipata asilimia 49.8 ya kura zote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu la CCM na la Salmin ambalo lilikuja kuungwa mkono&lt;br /&gt;na viongozi wenzake wote wa CCM (ukimwacha Mwalimu)&lt;br /&gt;zama hizo, akiwamo Mkapa aliyekuja kuwa Rais wa&lt;br /&gt;Tanzania, lilikuwa rahisi kabisa; “ushindi ni ushindi&lt;br /&gt;hata ukiwa ni wa kura moja.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu hili lilikwenda sambamba na uamuzi wa chama hicho&lt;br /&gt;tawala kuamua kuchukua kilichokuwa chake na ambacho&lt;br /&gt;hakikuwa chake, kikafanya ubabe kuwatawala hata wale&lt;br /&gt;waliokuwa wakikipinga dhahiri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CCM kimefanya hivyo wakati kikijua bayana kwamba,&lt;br /&gt;uhalali wake wa kuitawala Zanzibar yenye visiwa viwili&lt;br /&gt;ulikuwa ukikomea katika eneo moja tu la Unguja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jeuri ya CCM kukataa kukubali ukweli mchungu kwamba&lt;br /&gt;hakina uhalali Pemba, leo hii umelifikisha Taifa hili&lt;br /&gt;hapa lilipo na kimsingi imezaa kile ambacho mwenyekiti&lt;br /&gt;wake wa sasa, Kikwete amekiita mpasuko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jitihada za chama hicho tawala za miaka 12 iliyopita&lt;br /&gt;za kujaribu kugeuza mioyo ya Wapemba ikigeukie&lt;br /&gt;zimekwama na kimsingi zimeendelea kupoteza mwelekeo na&lt;br /&gt;kudharauliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapemba wa CCM wa aina ya marehemu, Dk Omar Ali Juma,&lt;br /&gt;Dk. Ali Mohammed Shein, Mohammed Aboud na wengine&lt;br /&gt;wachache wameendelea kuonekana kuwa ni wasaliti wa&lt;br /&gt;wenzao wa kwao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mpemba pekee anayebakia kipenzi cha watu wake na&lt;br /&gt;shujaa wa kisiwa hicho, ni Maalim Seif. Mwanasiasa&lt;br /&gt;huyo hivi sasa amepoteza uhuru wake binafsi ndani ya&lt;br /&gt;chama chake, amefanywa kuwa taasisi inayojitegemea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu wa kisiwa hicho anachotoka wamekataa kumsahau,&lt;br /&gt;tangu alipotimuliwa kutoka ndani ya CCM mwaka 1988,&lt;br /&gt;karibu miaka 20 iliyopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kile ambacho alikifanyia kisiwa hicho tangu akiwa&lt;br /&gt;ofisa wa juu serikalini kabla hajapanda na kuwa Waziri&lt;br /&gt;wa Elimu na baadaye Waziri Kiongozi kwa marais watatu,&lt;br /&gt;Aboud Jumbe Mwinyi, Dk Abdul Wakil Nombe na baadaye&lt;br /&gt;Ali Hassan Mwinyi hakijasahaulika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa CCM haipendi kuyasikia maneno haya, wala&lt;br /&gt;kuukubali ukweli huu, Maalim Seif bado anabakia kuwa&lt;br /&gt;kiongozi aliye ndani ya mioyo ya Wazanzibari&lt;br /&gt;wasiyoikubali CCM kihistoria na kisera huko visiwani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilipofanya mahojiano na Rais Jakaya Kikwete, mjini&lt;br /&gt;Dodoma siku chache tu kabla hajashinda urais, Desemba&lt;br /&gt;mwaka 2005, na kumuuliza iwapo CCM ilikuwa ikijutia&lt;br /&gt;uamuzi wake wa mwaka 1988 wa kumfukuza Maalim Seif na&lt;br /&gt;wenzake 17 ndani ya chama hicho tawala, hakuwa tayari&lt;br /&gt;kuukubali ukweli huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa Kikwete kama walivyo wana CCM wenzake wameamua&lt;br /&gt;kuukataa ukweli, historia itaendelea kubakia pale pale&lt;br /&gt;kwamba, dhambi ya chama hicho tawala ya kuwanyima&lt;br /&gt;Wapemba dhamana ya kuviongoza visiwa hivyo ndiyo&lt;br /&gt;inayowatafuna hadi leo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wazanzibari, hususan wale wenye asili ya Pemba,&lt;br /&gt;tofauti na Wabara wamejengwa katika kuheshimu na&lt;br /&gt;kuikubali historia ya visiwa hivyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CCM ipende isipende inapaswa kutambua kuwa, Wapemba&lt;br /&gt;wanakumbuka namna Mapinduzi ya mwaka 1964&lt;br /&gt;yalivyokisahau kisiwa hicho kutokana na udhaifu mkubwa&lt;br /&gt;wa kimuundo ambao chama cha Afro Shiraz Party (ASP)&lt;br /&gt;ilikuwa nao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inapaswa kufahamu pia kwamba, Maalim Seif ni miongoni&lt;br /&gt;mwa vijana wasomi wa mwanzo wa baada ya Mapinduzi hayo&lt;br /&gt;ambao kuingia kwao serikalini, mwanzoni mwa miaka ya&lt;br /&gt;1970, kulianza kufufua matumaini mapya ya Wapemba&lt;br /&gt;kutambulika na kukubalika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kikwete na wana CCM wenzake wa sasa wanapaswa kutambua&lt;br /&gt;na kukubali kuwa, kupanda haraka haraka kisiasa kwa&lt;br /&gt;watu kama Maalim Seif na vijana wenzake wa zama hizo,&lt;br /&gt;akina Hamad Rashid Mohammed halikuwa suala la bahati&lt;br /&gt;mbaya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, Kikwete, Rais Amani Abeid Karume na wahafidhina&lt;br /&gt;wengine wa CCM Zanzibar wanapaswa kutambua kuwa,&lt;br /&gt;mchango mkubwa wa Maalim Seif na uwezo wake binafsi wa&lt;br /&gt;kiuongozi tangu akiwa serikalini ndiyo sababu kuu&lt;br /&gt;iliyomjengea heshima na kukubalika hata kufikia&lt;br /&gt;kiwango cha kuabudiwa kisiasa na wale wanaomuenzi leo&lt;br /&gt;hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hiyo haitoshi; CCM inapaswa kutamka bayana ama&lt;br /&gt;ndani ya vikao vyake na ikibidi hadharani kwamba,&lt;br /&gt;uamuzi wa kibaguzi na wa kimizengwe uliompokonya&lt;br /&gt;Maalim Seif haki yake ya kukubalika ya kuwa Rais wa&lt;br /&gt;Zanzibar, baada ya Mzee Mwinyi kuwa Rais wa Tanzania,&lt;br /&gt;ni sehemu ya dhambi zinazoitafuna Zanzibar leo hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa CCM ilifanya hivyo ikimlenga Maalim Seif,&lt;br /&gt;matokeo ya uamuzi huo wa hovyo, yaligusa hisia za&lt;br /&gt;Wapemba na vijana wapenda maendeleo wa zama hizo wa&lt;br /&gt;aina ya akina Juma Duni Haji (Muunguja), Hamad Rashid&lt;br /&gt;Mohammed, Aboubakar Hamisi na wengine wengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushahidi wa hili ni rahisi kabisa. Vijana wengi&lt;br /&gt;machachari na wapenda mabadiliko waliamua kufungamana&lt;br /&gt;na Maalim, tangu wakati huo wakaunda mtandao wa&lt;br /&gt;kuihujumu CCM Zanzibar iliyoamua kwa makusudi&lt;br /&gt;kuendesha ubaguzi ule ule ambao ulizaa mapinduzi mwaka&lt;br /&gt;1964.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kikwete na wana CCM wenzake wanapaswa kutambua kwamba,&lt;br /&gt;Zanzibar inadai Mapinduzi mengine na kimsingi&lt;br /&gt;mapinduzi hayo yanakuja. Yatakuja kwa CCM kupenda au&lt;br /&gt;kutopenda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania, Wazanzibari na dunia ya wapenda mageuzi&lt;br /&gt;inatakiwa kulifahamu, kulikubali na kujiandaa kwa&lt;br /&gt;tukio hilo linaloweza kuja wakati wowote na kuundoa&lt;br /&gt;usultani wa ‘CCM Zanzibar kukubali kubeba dhamana ya&lt;br /&gt;makosa yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mapinduzi mengine Zanzibar yanakuja. Yatakuja wakati&lt;br /&gt;huu wakati akina Kikwete, Karume, Maalim Seif na&lt;br /&gt;wenzake wa CCM na CUF wakiwa hai au hata watakapokuwa&lt;br /&gt;wamekufa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zanzibar inahitaji mapinduzi yatakayoiondolea CCM&lt;br /&gt;ukiritimba na dhana ya mapinduzi daima. Zanzibar&lt;br /&gt;inadai mapinduzi yatakayoondoa udikteta wa CUF Pemba.&lt;br /&gt;Zanzibar inadai mapinduzi yatakayoondoa ubaguzi wa&lt;br /&gt;Wazanzibari dhidi ya Watanganyika, Wapemba dhidi ya&lt;br /&gt;Waunguja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zanzibar inadai mapinduzi ya fikra yatakayoondoa&lt;br /&gt;ubaguzi wa rangi wa sisi weusi, wale Waarabu, sisi&lt;br /&gt;Wangazija wale Wanyamwezi na kadhalika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zanzibar inadai mapinduzi yatakayomaliza urithi wa&lt;br /&gt;hovyo kabisa wa kibaguzi wa sisi ndiyo CCM- ASP wale&lt;br /&gt;ni wabuguzi wa Ki-Hizbu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zanzibar inadai mapinduzi yatakayoondoa uhalali wa&lt;br /&gt;Waaunguja kuendelea kuwatawala Wapemba. Mapinduzi ya&lt;br /&gt;kuondoa uhalali usio halali wa CCM kujipa dhamana ya&lt;br /&gt;kuvitawala visiwa hivyo kimabavu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Iwapo CCM Zanzibar inadhani kwamba, tatizo la Zanzibar&lt;br /&gt;ni Maalim Seif, itakuwa ikifanya makosa ya Marekani&lt;br /&gt;inayofanya katika dunia ya sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati fulani, Taifa hilo kubwa duniani lilidhani kuwa&lt;br /&gt;kifo cha kiongozi mkuu wa Korea Kaskazini, Kim Il Sun&lt;br /&gt;alipofariki dunia na ikadhaniwa kwamba huo ndiyo&lt;br /&gt;ungekuwa mwisho wa sera za kikomunisti za Juche.&lt;br /&gt;Ilikosea alikuwapo Kim Jong Ill.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kosa hilo hilo ambalo taifa hilo kubwa limekuwa&lt;br /&gt;likilifanya Irak leo, inakodhani kuuawa kwa watoto wa&lt;br /&gt;Saddam na baadaye baba yao na jamaa wengine wa&lt;br /&gt;kiongozi huyo wa zamani wa Irak kungemaliza mambo.&lt;br /&gt;Maafa yanayotokea Irak leo yanatisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si huko tu, hivi sasa taifa hilo kubwa linafuatilia&lt;br /&gt;kwa karibu hali ya afya ya Rais Fidel Castro wa Cuba&lt;br /&gt;ambaye ni mgonjwa, likidhani kuwa kifo chake&lt;br /&gt;kitamaliza sera za kikomunisti za nchi hiyo ya&lt;br /&gt;Marekani Kusini. Hata katika hilo inajidanganya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika CCM Zanzibar inapaswa kutambua kwamba,&lt;br /&gt;Maalim Seif ameshafika hatua ya kujijenga na kuwa&lt;br /&gt;taasisi na kwa bahati kwao alipata kuwa kada mwaminifu&lt;br /&gt;wa chama hicho tawala ambacho kimsingi kuondoka kwake&lt;br /&gt;kulikuwa ni kwa kulazimika kama si kwa kulazimishwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo basi, Maalim Seif ndiye mtu wanayeweza&lt;br /&gt;kukaa naye meza moja wakazungumza kutokana na kuwa&lt;br /&gt;kwake na chembe chembe za damu ya CCM, tofauti na&lt;br /&gt;ilivyo kwa vijana Wazanzibari wanaokiunga mkono CUF&lt;br /&gt;waliosambaa dunia nzima na ambao hawajahai kunusa&lt;br /&gt;harufu ya U-CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Viongozi wetu wa kisiasa na kiserikali wanapaswa&lt;br /&gt;kutambua kuwa, vijana hao walio ndani ya nje ya&lt;br /&gt;Zanzibar, ndani na nje ya Tanzania, wana hasira kubwa&lt;br /&gt;na CCM. Wao ndiyo waliopiga kura ambazo wanaamini&lt;br /&gt;ziliibwa mwaka 1995, 2000 na 2005.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watakapobaki wenyewe bila ya kuwapo kwa Maalim Seif,&lt;br /&gt;mwanasiasa mliberali, vijana hao ambao miongoni mwao&lt;br /&gt;wako wale waliochinja polisi mwaka 2001 na&lt;br /&gt;kuvishambulia kwa mawe vituo vya polisi wakijaribu&lt;br /&gt;kuzifikia silaha na wengine kukimbilia nje ya nchi&lt;br /&gt;wanaweza wakaamua kufanya lolote litakalofanana na&lt;br /&gt;Mapinduzi ya mwaka 1964.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa juhudi za sasa za CCM na mwenyekiti wake&lt;br /&gt;Kikwete zinaweza zikawa na lengo kama lile la akina&lt;br /&gt;Mkapa la kutaka kuwaridhisha wafadhili badala ya&lt;br /&gt;kuutazama mustakabali wa Zanzibar ki kweli kweli,&lt;br /&gt;mtazamo wa namna hiyo unaweza ukaja kuliweka taifa&lt;br /&gt;hili katika wakati mgumu ujao siku zijazo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwisho&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-2424436984951164992?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/2424436984951164992/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=2424436984951164992&amp;isPopup=true' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/2424436984951164992'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/2424436984951164992'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2007/01/zanzibar-inadai-mapinduzi-mengine.html' title='Zanzibar inadai Mapinduzi mengine'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114874970206052633</id><published>2006-05-27T10:04:00.000-07:00</published><updated>2006-05-29T09:14:06.180-07:00</updated><title type='text'>Msuya: Tatizo la Zanzibar ni chimbuko la uongozi wa CUF</title><content type='html'>&lt;a href="http://photos1.blogger.com/blogger/4909/992/1600/Kibanda.jpg"&gt;&lt;img style="float:right; margin:0 0 10px 10px;cursor:pointer; cursor:hand;" src="http://photos1.blogger.com/blogger/4909/992/320/Kibanda.jpg" border="0" alt="" /&gt;&lt;/a&gt; &lt;em&gt;Mwandishi wa makala hii Absalom Kibanda akimuaga Waziri Mkuu na Makamu wa Rais Mstaafu, Cleopa David Msuya nyumbani kwake Upanga hivi karibuni. &lt;/em&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwanzoni mwa wiki hii Waziri Mkuu na Makamu wa Rais Mstaafu, Cleopa David Msuya alifanya mahojiano na Mhariri wa Mwananchi Jumapili, ABSALOM KIBANDA nyumbani kwake Upanga jijini Dar es Salaam. Katika mahojiano hayo, Msuya alizungumzia masuala mbalimbali yanayohusu siasa, uchumi na maendeleo ya jumla ya taifa hili. Yafuatayo ni mahojiano kamili na kiongozi huyo mstaafu.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Ukiwa Kiongozi wa juu mstaafu wa serikali na sasa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) unauonaje mwelekeo wa sasa wa chama hicho ambacho ndicho chama tawala?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Mnapiniuliza mimi kuhusu mwelekeo wa CCM mnanifanya mimi nionekane ndiye spokesman (msemaji wa chama?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Hapana, tunasema tukijua kuwa wewe umekuwa kiongozi muda mrefu na sasa uko nje, mawazo yako yanaheshimika katika jamii kwa hiyo unao fursa nzuri ya kuona mambo yanavyokwenda pengine kwa uzuri zaidi, pamoja na kwamba hivi sasa ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Labda niseme kwa kifupi, kwa kuwa swali lenyewe ni pana sana, Uhalali wa chama chetu cha CCM ni dhana ya kuwa mtetezi wa wanyonge na watu wenye shida. Kwa hiyo chama hicho kikaibuka kuonyesha njia kwa kutumia umoja wetu kushika madaraka ya dola, tukajiinua hatua kwa hatua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tangu tupate uhuru mwaka 1961 sasa hivi ni miaka 45, tumepiga hatua  kiasi fulani, lakini bado kazi kubwa inahitaji kufanyika, hasa katika kuendeleza miundo mbinu, kuongeza kipato cha wananchi, kuongeza huduma za jamii, kupunguza umaskini na matatizo mengine kama ajira na kadhalika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo chama cha siasa kama cha kwetu ni kila wakati kujirekebisha na kuona kinawezaje kufanya kazi vizuri zaidi katika malengo hayo makubwa ya kitaifa. Mimi ni imani yangu ni kwamba, CCM imejaribu kufanya hivyo ukitazama tulikotoka tangu TANU hadi tulipoungana na Afro Shiraz na baadaye CCM mpaka sasa hivi, na hasa katika lengo la kushika dola.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Katika moja ya kauli zake Baba wa Taifa, Mwalimu (Julius) Nyerere aliwahi kuifananisha CCM na dodoki akimaanisha kwamba chama hicho kilikuwa ni mkusanyiko wa watu ambao wakati mwingine walikuwa hawana mtazamo unaofanana. Je unafikiri CCM ya sasa imebadilika au bado ina sura kama hiyo aliyoielezea Mwalimu.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Mambo mawili. Moja ni matokeo ya mfumo, unajua tangu tulipokuwa na Katiba inasema tuwe na chama kimoja, ni kwamba legally hatukuwa na chama kingine kwa hiyo watu wote waliotaka kushiriki katika kutoa mawazo ya maendeleo ya jamii ilibidi waingie CCM, kwa hiyo matokeo ambayo hayakutazamiwa wakati wa uanzishwaji wa mfumo wa chama kimoja yalikuwa ni kama dodoki ambalo lilivuta maji kila mtu mwenye hisia zake akaingia ndani ya CCM, Si kwa sababu anakubali hizo ideal bali kwa kuwa ndiyo iliyokuwa njia pekee.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa imani yetu ni kwamba baada ya kufungua milango kwamba mtu anaweza kuanzisha chama chake, watu wakitaka kubuni na kutetea sera mbalimbali za kuwaendeleza Watanzania wakaunda vyama vyao kwa hiyo tuko kwenye huo mchakato, mwanya umetolewa kikatiba sasa, kwamba watu wenye mitazamo yao wanaweza wakaendelea na wakati huo huo CCM nayo inajitafsiri, inaji-tune (inajiweka sawa) ili iweze kurudi kwenye malengo yake ya awali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Kwa muda mrefu kumekuwa na mgogoro katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) katika huko Mwanga na jina lako limekuwa likitajwa sana kuhusika katika mgogoro huo, kwa kiwango cha kukufanya utofautiane na aliyekuwa Katibu Mkuu wa KKKT, Amani Mwenegoha Unaweza ukatueleza hali ikoje hivi sasa baada ya kuwapo kwa jitihada za usuluhishi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Labda niseme mambo mawili (kicheko). ni kweli palikuwa na mgogoro ambao mpaka sasa upo, kuna kundi waumini wa Kilutheri wanaoishi wilaya ya Mwanga waliomba wapewe dayosisi ya peke yao. Kwa hiyo mgogoro upo na unaendelea, ninavyofahamu ni kwamba kanisa yaani KKKT imeunda Kamati ya Amani yenye wajumbe wa KKKT yenyewe na wa Mwanga kuchambua lile angalia inakuwaje. Ninavyoelewa tume bado inafanya kazi na haijafikia hatima yake. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;La pili kuna watu walijaribu kuhusisha jina langu na huo mgogoro, wengine walikwenda kusema mimi ndiye nina uchochea lakini nimesema mara nyingi kuwa mimi ni muumini, Mlutheri. Katika hili la kuomba dayosisi ningeulizwa kama Mlutheri ningesema nakubali, lakini siyo mimi nimeanzisha huo mgogoro, wenyewe wako huko na wanaendesha shughuli zao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hili ndiyo likaja lile suala la tukafika hadi tukagombana na ndugu Amani Mwenegoha kwa sababu alitoa matusi dhidi yangu katika vyombo vya habari katika dhana hiyo ya kufikiri kwamba mimi ndiye niliyesababisha huo mgogogoro. Katika hilo la ugomvi kati yangu na Mwenegoha, nataka kusema kwamba suala hili limemalizika, nadhani mliona kwenye magazeti siku za hivi karibuni, yeye mwenyewe amekuja kuomba msamaha nami nimekubali kumsamehe na madai yangu yale yaliyokuwa kwenye kesi tumekubaliana kuya sort-out (kuyatatua), hatuna ugomvi tena lakini hao wenye kudai dayosisi yao wanaendelea kudai.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Kumekuwa na madai kwamba ukiwa kiongozi, uliamua kutumia ramani ya Mpango wa Maendeleo wa Makao Makuu Dodoma (CDA) kwa ajili ya maendeleo ya Wilaya ya Mwanga. Madai haya yana ukweli wowote?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Huo ni uongo kabisa kabisa, Huwezi kuchukua mpango wa Dodoma ambao maumbile yake ni tofauti nikaupeleka Mwanga ambako ni tofauti. Kuna watu walikuwa wanaeneza hayo mambo lakini ni uongo. Kitu ambacho nakiri kimefanyika ni kwamba, Wilaya ya Mwanga ilianzishwa na Serikali Julai 1979 kwa hiyo wizara ya Ardhi ya Mipango Miji iliombwa iende Mwanga kutengeza plan (mpango), wakaja wakatoa mapendekezo ya jinsi ya kuanza, mapendekezo yale yalikuwa mafinyu sana, tukashauri kwamba viongozi wa Wilaya ya Mwanga na viongozi wa Wizara ya Ardhi na Mipango Miji waende CDA kuona kwamba kweli itafaa na walipofika watalaam kule wakaona kuna marekebisho mengi ya kuyafanya na wakayafanya. Kwa hiyo kutumia utaalam na ushauri wao ndiyo, lakini, kusema tulichukua mipango miji ya Dodoma kupeleka Mwanga ni uongo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Kuna madai mengine kwamba ukiwa Waziri Mkuu na Makamu wa  Rais ulitumia muda wako mwingi kuangalia maendeleo ya jimbo lako la uchaguzi na wilaya yako ya Mwanga zaidi kuliko hata ilivyokuwa kwa maeneo mengine ya nchi, jambo ambalo baadhi ya watu wanaliona kuwa ni matumizi mabaya ya madaraka&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Hilo nalo pia napenda niseme ni uongo. Yamezushwa mambo mengi, unajua kwenye hizi nafasi za uongozi kila mtu anaona ni jalala lake la anatupa uchafu. Nakumbuka kuna watu walikwenda wakaeleza kwamba, huyu mzee pamoja na mambo yote, ametia barabara zote za lami katika Wilaya ya Mwanga sasa safari moja niko nyumbani kule kwenye hizi sherehe za mbio za Mwenge, hawa vijana wa Mwenge wakashangaa mabarabara yetu mabovu kule milimani,  wakauliza yale mabarabara ambayo tunaambiwa Msuya kajenga yako wapi, wakaambiwa hayo ni maneno tu yanazongumzwa huko Dar es Salaam. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitu ambacho nakubali nimefanya, na si aibu nashauri hata wenzangu wabunge. Nilikuwa mbunge wa kuchaguliwa pale tangu mwaka 1980 mpaka 2000 nilipostaafu. Katika mwanzo wake, miaka ya 1980 kama mnavyofahamu hali ya uchumi ilikuwa mbaya sana, kwa hiyo kama mbunge kazi yangu ya kwanza ilikuwa ni kwenda kueleza wananchi kwamba wasije wakatazamia kwa sababu wamenichagua mimi kama mbunge wasifikiri kwamba watapata  vinono kutoka serikalini, kwa sababu hamna lakini kama wakitaka maendeleo ni lazima tuungane nao watu wajikusanye nguvu, wachange, na wanaoweza kufanya kazi kwa mikono wafanye. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kweli nilifanya kazi ya ku-mobilise opinion na wananchi kujishughulisha na kazi ndogondogo za maendeleo za kujenga zahanati, shule maji, barabara na kitu kimoja ambacho nilijivunia na nikashawishi wakakubali si sehemu moja katika kila pembe ya Wilaya tuwe tunashawishi chini ya kamati zao wawe na kitu cha kufanya na kazi za mbunge unakuwa unapita na unaona wanavyofanya na wakiwa wana matatizo unawasaidia, ukipata msaada unawapelekea, hivyo ndivyo tulivyofanya. Kwa uzoefu wenu kama vyombo vya habari ukichunguza wabunge waliopo pale bungeni wale wabunge ambao wako karibu sana na wapigakura wao na wanajishughulisha na hizi kazi ambazo wananchi wanafanya kuna vuguvugu la maendeleo. Ukikuta wale wabunge ambao wanakwenda siku moja, wakishachaguliwa hawarudi tena wanakaa mjini huku na kuuliza serikali itafanya nini hapa, utaona hakuna kitu kinachofanyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mimi niliungana na wale wenzangu ambao walikuwa wanamotisha wilaya zao, wako wengi utaona kama kule wilaya ya Njombe, Mufindi, Lushoto mahali kama Ruvuma sehemu kama Songea, mobilization imekuwa ni kubwa sana na watu wamefanya mambo mengi, mobilisation kama ya kilimo na kadhalika. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wale ambao wanajua historia, zamani Ruvuma haikuwa kitu lakini katika mobilisation ile Gama na nani wamemobilise watu sasa iko katika Big Four, wanazalisha mahindi, wanazalisha tumbaku, watu wamejenga nyumba nzuri. Kwa hiyo mobilisation inafanya kazi, wenzetu wa Rukwa wanafanya hivyo hivyo.  Kwa hiyo hicho ndicho nilichofanya, kwa hiyo hii shutuma inayokuja kuwa ooho ametumia nguvu zake..., mimi tena kila wakati nilikuwa nikiomba hao wenye shutuma hizo waende wakakague ni vitu gani hivyo? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Ukiwa Waziri Mkuu na pengine katika nyadhifa nyingine ulizoshika kama Waziri wa Fedha, Waziri wa Viwanda na Biashara, unafikiri ni maamuzi gani makubwa unayojivunia kama uliyachukua ambayo yanaendelea kubaki katika kumbukumbu zako kuwa yalizingatia ?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Jambo la kwanza unapokuwa Waziri Mkuu ni mara chache sana kufanya maamuzi peke yako wewe kama Waziri Mkuu kwa kuwa kama kuna jambo unalipeleka kwenye Baraza la Mawaziri, halafu linaamuliwa kama serikali imeamua. Moja wapo ambalo nilishiriki katika maamuzi hayo ni la kurekebisha uchumi. Mnakumbuka kati ya mwaka 1980 na 1985 hali yetu ilikuwa ni mbaya kweli kweli, Tulishiriki katika kujenga utaratibu wa kurekesbisha uchumi wa taifa letu na kurudisha uhusiano mazuri na hivi vyombo vya kimataifa kama Benki ya Dunia, IMF na wafadhili wengine, na ile ndiyo iliwezesha katika Awamu ya Pili marekebisho makubwa ya uchumi na kisiasa ambayo Mheshimiwa Mkapa amekuja mwaka 1995 mpaka 2005 kuyaimarisha na sasa ameyakabidhi kwa Mheshimiwa Kikwete. Kwa hiyo nilikuwa mmoja kati ya watu walioshiriki katika marekebisho hayo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Katika huu uamuzi mkubwa ulioshiriki kuufanya na kurejesha uhusiano na taasisi za kimataifa za fedha, moja ya masharti tuliyopewa ni ubinafsishaji. Sasa tumeona kuwapo kwa matatizo kama yale ya NETGroup Solution na City Water. Sasa unauzungumziaje ubinafsishaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza dhana ya ubinafsishaji, kimsingi ni kwa sababu tulikosa fedha za kutumbukiza kwenye makampuni ili yaweze kufanya kazi zaidi. Sasa unapokosa fedha za kuingiza kwenye chombo ulichonacho, unaweza kuacha kikafa au ukasema nikaribishe mbia aje tuendeshe pamoja, na hapo ndiyo ikaja hii dhana ya ubinafsishaji. Labda nitoe mfano mmoja ambao ninaufahamu kwa kuwa nilipata kuwa Waziri wa Viwanda (na Biashara), wakati ule bia ya Tanzania ilikuwa inatolewa na kiwanda chetu Dar es Salaam na Arusha, kilikuwa kinatoa nafikiri masanduku milioni 2.5 yalikuwa hayatoshelezi, watu wakawa wanaagiza bia nje kama Kenya, kama hakuna basi hizi ndogo tunazozalisha tugawane na kama tutakosa fedha za kulipia Kenya basi tufanye magendo. &lt;br /&gt;Kwa hiyo uamuzi mmoja ukawa kwamba tubinafsishe kiwanda kile cha bia, tukatangaza na tukapata watu, wakaja South African Breweries wakawekeza, sasa hivi kiwanda ni kikubwa, wakaimarisha kile cha Arusha, sasa ni kikubwa, wakajenga Mwanza, hiyo ndiyo faida ya ubinafsishaji, mmeungana, ameweka fedha, ameongeza na zile za kwenu, ameleta wataalam. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kazi ya ubinafsishaji ingefanyika vizuri yote yangekuwa hivyo. Lakini sasa katika utekelezaji ndiyo unapata matatizo kama hayo ya City Water. Akaja kumbe kazi haiwezi tukaona tuachane naye. Kule ambako kulifanyika juhudi za kutafuta wabia wazuri, na wakasimamia vizuri, maana usifikiri hawa watu ni miungu, ni malaika, ukiwaachia watachukua mapesa. Sasa mfano mmoja nakumbuka wakati ule nikiwa Waziri wa Fedha, Serikali ilikuwa na viwanda vitatu vya saruji, Dar es Salaam, Tanga na kingine Mbeya. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vikatushinda kuendesha, kwa hiyo tukatafuta wabia cha Tanga kimeleta wabia, kimeendelea kuingiza fedha kule ndani nadhani juzi mmesoma wanasema katika kukabiliana na kupanda kwa bei ya mafuta, wamejenga kinu cha kutumia makaa. Aliyechukua kiwanda cha Mbeya, kuna uuzaji wa nje wa saruji Zambia, Burundi na Kongo. Ubinafsishaji unatakiwa kupewa nguvu za nje na nguvu za ndani ili uweze kupata chenye faida, inataka usimamizi mzuri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Mheshimiwa Msuya kuna taarifa kwamba ukiwa serikalini ulikuwa hauna uhusiano mzuri wa kikazi na aliyewahi kuwa Waziri Mkuu kabla na baada yako, Edward Sokoine, Je habari hizi zina ukweli wowote?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Huo ni uongo mtupu sijui limetoka wapi. Maana mimi wakati nimechaguliwa Waziri Mkuu mwaka 1980, Mheshimiwa Sokoine alikwenda kusoma, mwaka 1983 nimetoka uwaziri mkuu ameteuliwa yeye kuwa Waziri Mkuu, mimi nikiwa Waziri wa Fedha nikafanya naye kazi vizuri sana tukawa tunashirikiana naye vizuri sana. Hii dhana ndiyo nimeisikia sasa kwa watu wawili watatu wanasema wewe ulikuwa hushirikiani naye. Nikasema siyo kweli. Tulikuwa tunapatana na tulishirikiana naye katika kazi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Kuna watu wanasema kwamba ilikuwa ni kazi ngumu sana kufanya kazi na Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere hasa kutokana na hulka yake ya kutokuwa tayari kupokea ushauri. Sijui wewe uliwezaje basi kufanya naye kazi kwa muda wote huo&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Mimi sijui hizo dhana mmezipata wapi. Sijui kama mnajua historia yangu. Mimi nilikuwa mtumishi wa umma wakati wa Uhuru, nilikuwa Katibu Mkuu mpaka mwaka 1972 Mwalimu aliponiteua kuwa mbunge na kunifanya kuwa Waziri wa Fedha, tangu wakati ule nimekuwa waziri mpaka nilipotoka mwaka 1985.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Napenda kusema kwa dhati kabisa siyo kwa sababu ya kujipendekeza wala nini katika watu niliwaona intellectually engaging mkiwa na hoja mkajadili kinagabaga bila kuwa na visa ni Mwalimu. Mimi alinisaidia sana katika nafasi yangu ya kujifunza uwaziri tangu 1972 hadi 1984. Alikuwa engaging mkiwa na matatizo mnakwenda pale, mnaweza kutumia muda mrefu mnabishana kweli kweli na akiona una pointi anakubali. Na mkiona ameshinda na ninyi mnabidi mkubali. Kule kwenye Cabinet (Baraza la Mawaziri) alikuwa anashawishi watu wengi kweli kuja ku-debate (kuleta mjadala) mambo siyo mambo yaje yakubalike na yapite hivi hivi tu, kwa hiyo, mimi nilmuona Mwalimu kuwa ni mtu anayependa kusikiliza mawazo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Ulikuwa Waziri Mkuu kwa marais wawili tofauti na katika kipindi viwili tofauti, ukianzia na Mwalimu na baadaye Ali Hassan Mwinyi. Unaweza kuvilinganishaje vipindi hivyo viwili vya kufanya kazi na marais hao kwa kuangalia tofauti zao&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Unataka niseme nini&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi: Tunataka utueleza tofauti uliyoiona ya kufanya kazi na Mwalimu na ile ya Mwinyi hasa ukizingatia kwamba awali umetueleza kwamba Mwalimu alikuwa engaging, sijui kwa Mwinyi ulijifunza nini&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Labda niseme mambo mawili kwamba kazi hizi za uongozi zinategemea na mazingira ambayo unafanyia kazi. Kipindi kile cha kwanza cha Mwalimu mwaka 1883 hali ya uchumi ilikuwa inaserereka, kwa hiyo preoccupation kubwa ilikuwa ni kuhakikisha hiyo hali na kugeuka. Wakati Mheshimiwa Mwinyi  ameniteua kuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais, mwaka 1994 na 95 zaidi yalikuwa na marekebisho ya uchumi ambayo yalishaanza wakati mimi nikiwa Waziri wa Fedha mwaka 1985-86 na kuendelea na kurekebisha mfumo wa serikali kutoka mfumo wa chama kimoja kwenda vyama vingi. Kwa hiyo mazingira yalikuwa tofauti. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kipindi hiki cha pili zaidi ilikuwa ni maelezo kwa nini tunafanya hivi kwa nini tunafanye vile. Ile ya kwanza yalikuwa ni mapambano halisi ya kutafuta maslahi ya kitaifa kwa sababu ya hali mbaya ya uchumi. Kwa hiyo hiyo ndiyo naweza kusema tofauti iliyokuwapo hasa kwa Mwinyi ambaye alikuwa mtu wa visiwani alikuwa hajazoea mambo ya huku Bara kwa hiyo mara kwa mara ilikuwapo haja ya kushauriana naye juu hali halisi ya huku bara, lakini kwa jumla naye tulifanya naye kazi vizuri. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Wakati wa Mwinyi inaonekana kwamba uliwahi kumshauri amfukuze uwaziri Augustine Mrema  kutokana na kukiuka misingi ya uwajibikaji wa pamoja. Je uliwahi kutoa ushauri kama huo kwa Mwalimu Nyerere?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya:  Ile ya Mrema nilimshauri hivyo na akakubali..&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Uliwahi kutoa ushauri wa namna hiyo wakati wa Mwalimu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Hapana&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Pengine twende kule Zanzibar, Umekuwa serikalini kwa muda mrefu. Kuna hili suala la Zanzibar ambalo linaonekana kuleta matatizo tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi. Nini kifanyike kumaliza hali ya uhasama wa kisiasa inayoonekana kuongezeka katika visiwa vya Unguja na Pemba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Katika siasa sidhani kuna njia ya mkato, isipokuwa mjadala. Katika suala hili la Pemba na Unguja lazima tukubali kwamba kwa kiasi fulani linatokana na aina ya viongozi ambao chama hicho cha CUF kimewachukua katika uongozi wake, hawa wamesimamia uongozi ambao hatima yake ni kugawanya watu. Hatima yake siyo maendeleo ya Wazanzibari wote, hatima yake ni kutetea Upemba. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande mmoja ilivyo sasa hivi tangu CUF ianze kule Zanzibar hawajashinda, kwa lugha nyingine unaweza kusema wananchi hawajakubali hizo siasa, ingawa sehemu kubwa ya wapigakura wa Pemba wamekubaliana na uongozi wa CUF. Lakini mimi naamini kwamba kilichopo mbele yetu sasa ni changamoto, moja ni kuanza mazungumzo ambayo Mheshimiwa Kikwete ameita mjadala wa kuzungumza lakini pia ni dynamics kwamba viongozi ambao wana madaraka ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar nao wasikilize utashi wa wananchi wa Pemba kwa sababu demokrasia inataka wakazi wa Pemba wasijione wamesahalika, na haya yakitendeka nadhani kutakuwa na mabadiliko katika uongozi, maana katika chaguzi tatu sasa hakuna mabadiliko, naamini wananchi wa Pemba wamechoka, dialogue ingetusaidia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Kumekuwa na maoni kwamba Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 ambayo kimsingi hayakuinufaisha Pemba ni moja ya sababu ya magawanyiko huu wa sasa. Una maoni gani katika hilo&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Sasa hili ni la kihistoria na la kijiografia. Ninachojua ni kwamba ni kweli kuwa inawezekana mapinduzi ya mwaka 1964 yaligusa zaidi Unguja kuliko Pemba, lakini mchakato wa hali ya sasa ya Pemba ni uongozi. Hatimaye inaanza na mtu. Sasa kuna dhana za Hizbu, kule ndiyo walikuwa wengi, lakini bado kuna Waafrika wengi wako Pemba. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mimi nadhani tatizo ni chimbuko la uongozi wa CUF, na tumaini tu kwamba katika matokeo ya chaguzi hizi tatu ambazo zote uongozi hauchukuliwi kutoka SMZ nadhani wananchi nao watakuwa wameshajifunza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Maneno yako yanaonyesha kwamba wewe haukubaliani na dhana ile kwamba Uchaguzi wa Zanzibar haukuwa huru na wa haki? Kwani kumekuwa na malalamiko sana katika chaguzi zote hizo tatu&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Sasa bwana, uchaguzi ulifanyika, itakuwa ni ajabu tu na hisia kwamba matokeo ni hayo halafu uchaguzi usiwe huru na haki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Hivi karibuni Mahakama Kuu imetoa maamuzi makubwa mawili. La kwanza ni kuhusu takrima na la pili la wagombea binafsi. Sijui wewe una maoni gani kuhusu maamuzi hayo mawili ambayo yanaonekana kubadilisha mwelekeo wetu wa sasa wa misingi ya kidemokrasia na utawala bora.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Hili la takrima si ajabu mimi ni tofauti kidogo. Nadhani tunachohitaji hapa Tanzania ni kuweka utaratibu unaokubali kwamba uchaguzi una gharama. Awe ni mtu au awe ni chama akiingia kwenye uchaguzi ataingia gharama fulani fulani sasa tunatakiwa tufanye yafuatayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Moja, ziwe gharama kiasi gani, tuweke limit (ukomo), hizo gharama zipatikane kutoka kwa nani, michango ya watu, chama chenyewe au kwa wafadhili. Zitumike kwa vitu gani, kutoa zawadi au kutoa misaada ya maendeleo au TV, au habari kwenye magazeti tungekuwa na sheria ambazo wenzetu mahali pengine duniani wameweka, wanakubali kwamba ni kweli kuna gharama, ijulikana mgombea anaweza kutumia kiasi hiki, ama yeye mwenyewe au chama chake, na atumie kwa vitu kama vipi ambavyo vinaruhusiwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukiwa na vitu kama hivi ambavyo vinaweza kufika mahali vikakaguliwa, na wakaguzi au mtu yeyote ambaye haridhiki, tungefika mahali ili suala lingeweza kudhibitiwa kwa upeo mkubwa zaidi kuliko kuishi kwenye takrima, maana takrima sijui unafanyaje. Kuna hili la kukaribisha watu, lakini katika art ya kampeni ni lazima watakutana watu, wakati mwingine marafiki zao watagharimia, sasa hiyo ni takrima au siyo mimi sijui. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Kuhusu hili la wagombea binafsi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya:  Nadhani hili panatakiwa pawe na mjadala wa kitaifa kidogo, utakumbuka katika uchaguzi uliopita wagombea zaidi ya 10 walikuwa wanagombea nafasi ya urais, wengine hawakuweza kuzunguka hata mikoa miwili au mitatu mizima kwa sababu hawakuwa na uwezo. sasa unavyozidi kufungua zaidi kwamba kila mmoja aje, utakuwa na watu wengi lakini kufanya ile kazi ya kujieleza kwa watu haitafanyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Unaweza ukasema umefungua milango ya demokrasia lakini kwa namna hiyo mimi sidhani kwamba ni demokrasia tuendeshe debate kidogo ni nini tunachotaka. Kama ni kuwapa uhuru watu kugombea uhuru upo sasa hivi kwani kila mtu ana uhuru wa kuunda chama chake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Kuna watu wanasema iwapo sheria ya wagombea binafsi itakuwa rasmi, basi tutashuhudia wagombea wa urais, ubunge na hata udiwani kutoka ndani ya CCM ambao hawataridhishwa na namna uteuzi wa wagombea ulivyopitishwa wakisimama kama wagombea binafsi. Kwa mujibu wa watu hao hicho ndicho kinachoiogopesha CCM kuruhusu sheria hii ikijua kile alichokisema Baba wa Taifa kwamba upinzani wa kweli utatoka ndani ya CCM kinaweza kutokea kwa namna hiyo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Ilani yake ataitoa wapi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Hapana anaweza akajitambulisha kama yeye bado ni mwana CCM na kwamba wewe umesema suala la ubunge kwa mfano ni uwezo binafsi wa mtu si wa chama tu, na ndiyo maana umesema kuna wabunge wako karibu na wapigakura wao na wengine wako mbali, ingawa wanalindwa na mwavuli wa chama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: CCM hawaogopi hilo, waogope kitu gani, kwa kuwa uhuru wa kwenda kwenye chama kingine upo. Mimi nasema kwa hili ushauri wangu kuwe na mjadala wa kitaifa.      &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Uliyapokea namna gani matokeo yaliyompitisha Benjamin Mkapa kuwa mgombea urais wa Tanzania mwaka 1995 yakiwaacha wewe na Kikwete mkishindwa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Sasa mambo haya unajua ni magumu kwanza kibinadamu ukigombea unakuwa ukijua utashinda, lakini kila mtu anayeingia anajua kuna watakaoshindwa. Asiyekubali kushindwa si mshindani. Tulikwenda tukaona wazi, Mkutano Mkuu haukunichagua kwa hiyo tukarudi. Kwa taratibu za chama chetu tukamuunga mkono Kikwete. Na baada ya muda kupita hatukuona kuna haja ya kuingia kwenye uchaguzi mwingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Majibu yako yametufikisha kwenye suala la kuwapo kwa mjadala au fukuto la chini chini kuhusu haja ya wazee kung'atuka madarakani na kuwaachia vijana kuongoza na wao wakabaki kwenye nafasi za ushauri zaidi. Wewe unalieleza vipi hili. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Mambo haya yanategemea kila mtu hali yake ilivyo. Wakati ule mimi nilipoamua kustaafu mwaka 2000 kwamba sintagombea tena, nilishakuwa ndani ya Bunge tangu mwaka 1972. Sasa mwenyewe nikajiona nimekuwa mbunge na serikalini hadi mwaka 1995 na nimekuwa back bencher tangu 1995 hadi 2000 hivi bado ningekuwa na msaada kuendelea kuwawakilisha watu wa Mwanga  na nikaendelea na debate pale ndani ya Bunge na nikapata hitimisho kwamba mimi nitoke na nimwachie mtu mwingine aendelee, kwa hiyo nikaamua kustep aside (kukaa pembeni) tukaanzisha process ya kumtafuta mtu mwingine, kwa bahati wakamchagua Profesa Maghembe kijana, kwa hiyo na yeye ataendelea kuzungumza hapo hadi atakapokuwa na miaka mingi kama sisi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa wilaya nyingine pengine si suala la mtu kuwa mzee tu au vile vile kuwasaidia. Kama wakiridhika kwamba mbunge wao anaweza kutoa matunda, kukimbia, akapanda milima akafanya hivi akafanya hivi sawa wamchague. Kama ni lengo la kusema kwa kuwa mimi ni mbunge nibaki pale, kwa sababu kura za maoni ni kipengele kimoja cha kujua kuwa watu wamekukataa. NImekuwa nikiwashauri marafiki zangu kwamba ni afadhali utoke kabla watu hawajachoka na wewe.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Kwa ufupi unauona vipi mwelekeo wa kisera wa Serikali ya Awamu ya Nne na hasa katika masuala ya utawala bora kama vile vita dhidi ya rushwa hasa zile kubwa kubwa na katika maeneo mengine pia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Kwa upande mmoja mimi nadhani tumshukuru na kumpongeza Rais kwa kuwa na msimamo huo. Rushwa,hasa zile kubwa kubwa ndiyo hasa zimelengwa zitafsiriwe vizuri, zitafitiwe vizuri, na kama wakipatikana watu hatua zichukuliwe, ni imani yetu kwamba tutafika sasa kwenye vitendo. Wanasema unapokuwa na mfumo huru wa kutambua watu gani walivyoshiriki kwenye rushwa na pakawa na hatua za kisheria ambazo zinachukuliwa dhidi yao, inajenga imani. Kama hazionekani taratibu za kisheria zimechukuliwa dhidi ya walarushwa wanaohisiwa serikali inaonekana haina maana.  Kwa hiyo tunampongeza Rais, tunaamini ataweza kusimamia kama alivyotamka.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi Jumapili: Swali la mwisho, pengine Watanzania wangependa kujua unaendelea kiafya&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuya: Ahha naendelea vizuri, Mungu ananisaidia. Ahsanteni tutawasiliana siku zijazo.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-114874970206052633?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/114874970206052633/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=114874970206052633&amp;isPopup=true' title='6 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114874970206052633'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114874970206052633'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2006/05/msuya-tatizo-la-zanzibar-ni-chimbuko.html' title='Msuya: Tatizo la Zanzibar ni chimbuko la uongozi wa CUF'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>6</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114656981773436919</id><published>2006-05-02T04:02:00.000-07:00</published><updated>2006-05-02T04:36:58.073-07:00</updated><title type='text'>Mahita ameliacha jeshi la polisi chafu. Uchambuzi huu ulioandikwa na Absalom Kibanda ulichapwa katika Mwananchi Jumapili Feb 26, 2006</title><content type='html'>MKUU wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Omar Iddi Mahita amemaliza muda wake wa kazi katika jeshi hilo alilolitumikia kwa muda wa miaka 38 akiliacha likiwa limepoteza imani yake kwa  wananchi na katika jamii ya kimataifa hususan watetezi wa haki za binadamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mahita ambaye alistaafu rasmi kazi akiwa na umri wa miaka 60, Machi 4, 2006 ameondoka katika wadhifa wake alioutumikia kwa muda wa miaka 10 akiliacha jeshi aliloliongoza likiwa na rekodi mbaya kabisa ya utendaji wa kazi na hususan katika eneo la ulinzi na kuheshimu haki za binadamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kipindi chake cha uongozi, jeshi la polisi limetiwa misukosuko na kulaumiwa kwa kukiuka misingi na miiko yake ya kazi na raia wa kawaida, wabunge, wanasiasa na hata mashirika ya kitaifa na kimataifa ya kutetea haki za binadamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akiwa mkuu wa jeshi hilo matukio makubwa matano yametokea kati ya mwaka 1996 (alipoteuliwa na Rais wa wakati huo Benjamin Mkapa) na sasa ambayo ama yalisababisha kuwapo kwa msukumo au shinikizo la kumtaka ajiuzulu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukio kubwa la kwanza 'lililomtia majaribuni' ni lile lililotokea miaka miwili tu baada ya uteuzi wake huo, mwanzoni mwa mwaka 1998, katika eneo la Mwembechai jijini Dar es Salaam lililosababisha vifo vya watu watatu waliopigwa risasi na polisi wakati wa maandamano yaliyokuwa yameandaliwa na wanaharakati wa Kiislamu huku wengine wengi wakijeruhiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitendo cha Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kukataa pendekezo la wabunge 23 waliotaka bunge kujadili tukio hilo la Mwembechai kwa madai kwamba ingeshughulikiwa na jeshi la polisi lenyewe limeendelea kubakia katika maandishi ya mashirika ya kimataifa ya utetezi wa haki za binadamu kama mfano mmoja mbaya wa utendaji wa jeshi hilo baada ya kutochukuliwa kwa hatua zozote  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuuawa kwa watu hao kulikoenda sambamba na kukamatwa kwa viongozi wa juu wa wanaharakati hao, kulisababisha manung'uniko makubwa  ndani  ya nchi na nje kiasi cha kuijengea taswira mbaya Tanzania machoni mwa jumuiya ya kimataifa hasa baada ya mashirika ya kimataifa ya utetezi wa haki za binadamu kulichukulia tukio hilo kwamba doa kubwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miezi michache tu baadaye, mwaka huo huo wa Mahita tena na asasi nyingine za usalama wa ndani ziliingizwa majaribuni tena baada ya magaidi wa kundi la al Qaeda kufanikiwa kupenya nchini pasipo kutambulika na hatimaye kupanga na kutekeleza shambulio katika jengo ulipokuwapo ubalozi wa Marekani Agosti mwaka 1998 na kusababisha vifo vya watu na wengine kadhaa wakiachwa majeruhi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka mitatu tu baada ya Mwembechai, Mahita aliingia tena katika msukosuko mkubwa kutokana na kitendo cha jeshi lake kupambana na risasi na wanachama wa Chama Cha Wananchi (CUF) waliokuwa wakiandamana Januari 26 na 27 mwaka 2001 huko Pemba ambako watu 22 waliuawa na kusababisha kelele nyingi kutoka ndani ya nchi na katika jumuiya ya kimataifa. Hata hivyo, shinikizo la kumtaka Mahita na viongozi wengine wa juu serikali kujiuzulu lilikwama.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka miwili tu baadaye wakati wa kikao cha Bunge, aliyekuwa Mbunge wa Shinyanga Mjini, Leonard Derefa (CCM) alimtia majaribuni tena Mahita pale alipotoa pendekezo la kufumuliwa na kuundwa upya kwa jeshi la polisi kutokana na kukithiri kwa uoza ndani ya jeshi hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli hiyo ya Derefa iliyoungwa mkono na wabunge kadhaa ilizusha mjadala mkali kati ya wabunge na Mahita ambaye aliwatuhumu wabunge kwa kujali maslahi yao na kusahau kwamba polisi walikuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu ya ukosefu wa vitendea kazi, malazi duni na mishahara ya chini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo kishindo hicho cha wabunge kilizimwa haraka na Mkapa ambaye miezi michache tu baadaye aliibuka na kuwataka watu waache kulisakama jeshi la polisi akisema lilikuwa likiyafanya mengi mazuri na yanayopaswa kuungwa mkono na wananchi na siyo kukebehiwa.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata baada ya mvutano huo kumalizika, jeshi la polisi liliendelea kubakia na sura ile ile machoni mwa jamii na mwaka jana Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ilitoa taarifa nyingine kali iliyokuwa ikiwashutumu polisi kwa ukiukaji wa maadili ya kazi, rushwa, kuwazushia watu kesi na tuhuma nyingine nyingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sura hiyo mbaya ya jeshi la polisi imeendelea kubakia hivyo machoni mwa wananchi hadi Januari mwaka huu wakati polisi walipowaua watu wanne katika maeneo ya Sinza wakiwatuhumu kuwa ni majambazi, hatua ambayo ilizusha utata mkubwa uliomlazimisha Rais Jakaya Kikwete kuunda Tume ya Jaji Kipenka kuchunguza chanzo, mazningira na sababu ya mauaji hayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya Tume ya Kipenka kuthibitisha kwamba waliouawa hakuwa majambazi, Mahita ambaye sasa amebakiza wiki moja kamili kustaafu amejikuta tena katika kaa la moto la kuwapo kwa shinikizo la kumtaka ajiuzulu ambalo limekuwa likitolewa na makundi mbalimbali ya watu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati kwake, shinikizo hilo linaonekana kutotekelezwa kutokana na ukweli kwamba mkuu huyo wa jeshi la polisi hana tena muda mrefu wa kuliongoza jeshi hilo baada ya kumaliza muda wake na hivyo kumnusuru kwa mara ya kwanza katika hatari ya wazi kabisa ya kuwajibika kutokana na makosa ya vijana wake. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbukumbu zinaonyesha kwamba Mahita alijiunga na jeshi hilo Oktoba mwaka 1968 baada ya kuhitimu mafunzo ya awali katika chuo cha polisi. Kwa mujibu wa kumbukumbu hizo, Mahita alipata mafunzo ya juu ya kipolisi katika chuo cha Polisi cha Ontario nchini Canada na pia katika chuo cha Bramshill cha Uingereza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kati ya mwaka 1978 na 1980 Mahita aliongoza kikosi cha polisi kilichokuwa nchini Uganda kwa ajili ya kulijenga upya jeshi la polisi la nchi hiyo. Tangu wakati huo ameshika nyadhifa mbalimbali katika jeshi hilo, ukiwamo ukamanda wa polisi wa mkoa kabla hajapanda na kuwa Mkuu wa jeshi hilo mwaka 1996.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akiwa kazini, Mahita aliwahi kutunukiwa nishani mbalimbali, zikiwamo mbili alizotunukiwa na Rais za Utumishi wa Muda Mrefu na ile ya Utumishi uliotukuka ambazo ni za juu za kitaifa na zenye hadhi kubwa. Mbali ya hizo, Mahita pia alitunukiwa nishani  ya Mashujaa wa Vita ya Kagera kutokana na mchango wake nchini Uganda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mahita amemaliza kipindi chake kigumu cha kazi cha ukuu wa polisi akiwa ameacha kumbukumbu ya matukio yaliyoliachia sura mbaya jeshi hilo.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-114656981773436919?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/114656981773436919/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=114656981773436919&amp;isPopup=true' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114656981773436919'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114656981773436919'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2006/05/mahita-ameliacha-jeshi-la-polisi-chafu.html' title='Mahita ameliacha jeshi la polisi chafu. Uchambuzi huu ulioandikwa na Absalom Kibanda ulichapwa katika Mwananchi Jumapili Feb 26, 2006'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114614225310966303</id><published>2006-04-27T05:47:00.000-07:00</published><updated>2006-04-27T06:25:27.416-07:00</updated><title type='text'>Hivi ni kweli Dk. Mwakyembe anawatakia mema waandishi?</title><content type='html'>KATIKA Kikao cha Bunge cha mwanzoni mwa mwaka huu, aliyewahi kuwa mwandishi wa habari na mwanasheria, Dk Harrison Mwakyembe alitoa hoja ambayo iliwagusa vilivyo waandishi wa habari akiwamo rafiki yake wa karibu ambaye pia ni rafiki yangu, Ansbert Ngurumo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hitimisho la hoja ya Mwakyembe lilikuwa ni kutaka serikali ihamasishwe ili iwasomeshe waandishi wa habari wa hapa nchini kutokana na kile ambacho alikielezea kuwa ni udhaifu mkubwa kitaaluma miongoni mwa waandishi wa habari wa hapa Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa manufaa ya wana Magazeti Tando, msingi wa hoja ya Mwakyembe ilikuwa ni kukerwa kwake na habari zilizokuwa zimeandikwa na magazeti mengi kuhusu madai ya wabunge kadhaa kutaka waongezewe posho na malipo yao mengine kwa maelezo kwamba kile walichokuwa wakilipwa kilikuwa hakitoshi kukidhi mahitaji halisi ya kazi zao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akitumia rekodi yake ya uandishi, Mwakyembe aliwalaumu waandishi wa habari kwa kuandika habari hiyo juu juu kiasi cha kujenga taswira kwamba, wabunge wote walikuwa wamejumuishwa katika madai hayo ambayo kwake yeye yalikuwa ni maoni ya wawakilishi wachache tu miongoni mwao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja hiyo ya Mwakyembe, kwanza ilithibitisha jambo moja tu kwamba, alikuwa hajachukua muda wa kutosha kuzisoma habari ambazo zilikuwa zimeandikwa kuhusu suala hilo la wabunge kutaka kupewa maslahi zaidi. Naweza nikasema kwamba alichofanya yeye kilikuwa ni kuishia kusoma vichwa vya habari pekee. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi ya vichwa vingi vya habari vilivyokuwa vikiandika habari hiyo vilikuwa vikisomeka; "Wabunge wataka posho zaidi..., "Wabunge sasa...." na vingi vingine vya namna hiyo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndani ya habari hizo yalitajwa majina ya wabunge waliotoa hoja za kutaka madai yao hayo. Wabunge waliotoa madai hayo walifanya hivyo wakati wa semina ya wabunge iliyofanyika jijini Dar es Salaam siku chache kabla ya kikao cha Bunge kufanyika, semina ambayo Mwakyembe alihudhuria.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wa kipindi hicho chote cha semina ya takriban wiki moja, si Mwakyembe wala mbunge mwingine yeyote aliyesimama na akapinga madai hayo ya wabunge waliokuwa wakidai posho zaidi, isipokuwa chama cha upinzani cha Chadema ambao siku chache baadaye kilitoa tamko lililosema wabunge wake walikuwa wakiipinga hoja hiyo ya wabunge wenzao ya kutaka kuongezewa posho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimantiki Mwakyembe alikerwa na namna 'vichwa vya habari' vilivyokuwa vikiwasema wabunge (Kwa kutoa mwelekeo wa kuwajumuisha). Pengine yeye alitaka iandikwe bayana kwamba ( "Baadhi ya wabunge..., au "Wabunge John, Mussa, Mustafa wataka ...." ) utaratibu ambao aghalab hautumiwi katika vyombo vya habari. Nadhani hata yeye anajua umuhimu uchache wa maneno katika vichwa vya habari (au word economy kama wanavyosema Waingereza).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikumbukwe kwamba baada ya hoja ya wabunge kutaka posho ziongezwe, Spika wao, Samuel Sitta (ambaye naye ni mwana CCM kama alivyo Mwakyembe) naye hata kabla ya semina kuisha, aliunga mkono suala hilo na akasema ni la muhimu kwani wabunge walikuwa na wajibu mzito wa kuwatumikia watu waliowachagua na hivyo walikuwa wakihitaji kulipwa vizuri na akatetea hoja ya kudai mafao zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapo ndipo inapokuja ile hoja ya Ndesanjo kama kweli viongozi wetu ni Watwawala ambao siku zote wanabuni mbinu za kujiongezea mapato zaidi na zaidi, bila ya kujali uwezo wa nchi kiuchumi au hali ya kimaisha ya watu wanaowawakilisha. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa taarifa ya akina Ndesanjo, Makene na wenzetu mlio nje ya nchi, hoja ya wabunge kutaka posho na mishahara minono zaidi ilionekana kumkera hata Rais wa Jamhuri, Jakaya Kikwete ambaye katika mkutano wake na wazee wa Dar es Salaam siku chache baadaye bila ya kuwataja kwa majina wabunge alieleza kushangazwa na watu wanaoanza kudai malipo zaidi ya posho hata kabla kazi haijafanyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya kwake, Mwakyembe alipoamua kuwamiminia waandishi wa habari lawama kuhusu aina ya uandishi wao alisahau yote hayo.  Yeye akaona tu kwamba, waandishi wa Tanzania wanapwaya kitaaluma. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jambo baya ni kwamba, baada ya Mwakyembe kutoa hoja hiyo na waandishi kuibuka na kumpinga, rafiki yake Ansbert aliibuka na kusimama kidete kumtetea akitumia kibaji kikubwa alichonacho katika kujenga hoja, kuficha msingi wa hoja ya Mwakyembe na akakimbilia kulijadili hitimisho la msomi huyo huku akiiweka pembeni hoja ya msingi ya Mwakyembe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ansbert akageuza kibao akamwita Mwakyembe mtetezi wa hoja ya kuwaendeleza kitaaluma waandishi wa habari, ilhali akijua fika kwamba mtu huyo alikuwa akitukebehi na kutuponda. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna anayepinga umuhimu wa waandishi wa habari kutafuta nafasi zaidi za elimu ya juu. Hakuna anayepinga kwamba taaluma ya uandishi wa habari kwa miaka mingi ilisahaulika. Hakuna anayepinga kwamba taaluma hii imevamiwa na mamluki na kundi kubwa la wababaishaji wanaodhani ni eneo la watu walioshindwa shule.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sisi tunaompinga Mwakyembe hatupingi hoja ya kutafuta elimu zaidi. Tunajua umuhimu wa elimu na ajenda ya kupigania elimu ya waandishi haikuanzishwa na Mwakyembe tumeianzisha sisi waandishi wa habari. Sisi ndiyo tumekuwa tukihoji kukosekana kwa elimu ya juu ya uandishi wa habari hapa Tanzania kabla ya kuanza kwake miaka ya karibuni. Jenerali Ulimwengu amekuwa akiandika kuhusu hilo miaka mingi tu iliyopita, kabla Mwakyembe au Anbsert hawajaja na ajenda yao iliyofichwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunajua kwamba Mwakyembe alipokuwa mwandishi, alikuwa na elimu ndogo tu ya sekondari na alipokwenda Chuo Kikuu akaukimbia kabisa uandishi. Mimi kwa mtazamo wangu, Ansbert umeupotosha mjadala. Mwakyembe ameidharau taaluma ya uandishi wa habari. Ameipuuza, na sasa anaitukana na kuikashifu kwa sababu tu, waandishi wamegusa maslahi ya wabunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania tunapaswa kuanza kuwahoji viongozi wetu na kupima kile wanachokisema na kubaini iwapo kweli kinatoka ndani ya mioyo yao na kinatokana na uzalendo wa kweli uliojengeka ndani mwao. Huyo Mwakyembe kwa mfano, hadi majuzi tu hapa alikuwa ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Magazeti ya Uhuru na Mzalendo yanayomilikiwa na CCM. Je  wakati akiwa huko alifanya jambo gani la maana kupigania elimu ya waandishi? Kwa kweli hakufanya jambo lolote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kinachonisikitisha na kusababisha nilazimike kuandika hili ni kuona kwamba Watanzania wenzangu wengi kwa bahati mbaya tumejikuta tukiingia katika mtego wa hoja ya Mwakyembe ambayo kwa ufundi mkubwa ilitengenezwa na mwenzetu Ansbert katika misingi ya 'kumhifadhi' rafiki yake mbunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waandishi tunapaswa kuishinikiza serikali kutafuta elimu zaidi. Waandishi tunapaswa kusoma kwa makini habari na makala magazetini na katika mitandao. Hulka kama ya Mwakyembe ya kuishia kusoma vichwa vya habari na kutamba kwamba umesoma gazeti si hulka ya usomi wa kuijenga nchi hii. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rekodi zipo zinazoonyesha kiwango cha umakini wa Mwakyembe, kama msomi, na mwanasiasa. Kila mmoja wetu afanye jitihada kuangalia alikotoka mwanasiasa huyo na anakoelekea. Changamoto yangu ni kuwaasa vijana wa Kitanzania wampime Mwakyembe kuanzia sasa na kuendelea. Bado tunayo nafasi ya kujua aina ya viongozi tulionao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naomba pia ielekewe kwamba, pamoja na kwamba nilimpuuza Mwakyembe katika misingi ya hoja, sikuona wala sioni kuwapo kwa busara kuamua kususia habari zake katika magazeti kwani kwa kufanya hivyo tungeweza kuwanyima fursa wapigakura wake kujua aina ya mbunge anayewawakilisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pia sioni sababu ya kukerwa na hoja ya Mwakyembe kwa kuwa, mimi kama mwandishi wa habari ninao wajibu wa kukubali lawama ziwe za haki au la, ingawa pia ninao wajibu wa kusahihisha pale ambapo nitaona kwamba lawama zinazotolewa dhidi ya waandishi zina walakini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ninahitimisha kwa kusema kwamba, mtazamo wa Mwakyembe ni wa kuwadharau waandishi kijumla jumla kwani pamoja na ukweli kwamba waandishi wengi ni 'makanjanja' na wasio na elimu inayojitosheleza kitaaluma, bado liko kundi la waandishi makini, waliosoma shule vizuri kabisa na ambao kila siku wanajiendeleza kitaaluma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja ya Mwakyembe kwa waandishi ilikuwa ni ya kinafiki na yenye kujiwekea ukuta wa kujilinda. Ni ukweli ulio wazi kwamba, wakati waandishi wa habari wakiwamo makanjanja wengi wao wana elimu ya kuanzia sekondari, sifa za wabunge wetu kitaaluma ni za kuwataka wawe na angalao elimu ya msingi na wajue kuandika na kusoma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunao ushahidi wa wazi kwamba, kuna waandishi wasomi kabisa kabisa, wenye shahada za uzamili (M.A) katika uandishi na katika fani nyingine au hata zaidi ambao wamekuwa wakiharibu sifa nzuri za taaluma hii kama ilivyo kwa wasomi wengi tu wa ngazi za hadi madaktari wa falsafa ambao hoja zao zimekuwa hazifanani na usomi wao.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-114614225310966303?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/114614225310966303/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=114614225310966303&amp;isPopup=true' title='6 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114614225310966303'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114614225310966303'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2006/04/hivi-ni-kweli-dk-mwakyembe-anawatakia.html' title='Hivi ni kweli Dk. Mwakyembe anawatakia mema waandishi?'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>6</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114604108184632706</id><published>2006-04-26T01:41:00.000-07:00</published><updated>2006-04-26T01:44:42.033-07:00</updated><title type='text'>This article was published in The Daily Nation (in March 19, 2003) few days before United States of America led the coalition to invade Iraq.</title><content type='html'>Tanzania is restless as Bush beats drums of war   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;By ABSALOM KIBANDA  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;This article was published in The Daily Nation (in March 19, 2003) few days before United States of America led the coalition to invade Iraq. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;According to US President George W. Bush, his Iraqi counterpart Saddam  Hussein has not understood the message: If he does not give up alleged  weapons of mass destruction, America will attack.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Thousands of kilometres away in Tanzania, however, policy makers, economists,  businesses and local people have heard President Bush loud and clear.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nearly everyone you talk to in Dar es Salaam will tell you that the use of force to  oust Saddam will change the Middle East situation, and indeed the world,  dramatically.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The only thing they don't agree on is whether it will be for better or worse.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Closing the 10th parliamentary session in Dodoma on January 14, Prime Minister  Frederick Sumaye told Tanzanians to brace themselves for a war in Iraq, adding  that it would have major effects on the country's economy.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mr Sumaye said the world was already experiencing the economic effects of a  possible war in Iraq.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;He said the fears had contributed to the rise of prices in petroleum products,  adding that the number of tourists worldwide and international trade were also  likely to be affected.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The Tanzanian Government's biggest concern, he said, was what would happen  to oil prices if the conflict erupted. Mr Sumaye predicted a shortage of petroleum  in the world since the largest quantity of crude oil comes from the Middle East  and if its supplies were disrupted, there would be no quick alternative stocks.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;He said: "Tanzanians are part of the international community. We can't run away  from the effects of oil price rises. The increase would greatly affect our economy.    "Transportation costs will definitely rise and industrial production expenses where  oil is extensively used will go high."   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mr Sumaye explained that the living standards of Tanzanians would, as a result,  go down.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;According to government statistics, transportation is the main consumer of  petroleum products. Presently, oil supply meets just about 70 per cent of the  demand for petroleum.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The prime minister's speech followed statements by the Governor of the Bank of  Tanzania, Mr Daudi Ballali, on the possible effects of a war in Iraq. Mr Ballali said  Tanzania should diversify its exports if it wanted to save the economy from  succumbing to the looming oil crisis.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;He said diversifying and increasing production for export would cushion the  country from the effects of the global fuel crisis. The oil crisis will not have as  much impact on our economy as was the case in the 1970s. There are now more  oil producers than before.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;"However, by merely producing more crops, Tanzania's gross domestic product  (GDP) will not go beyond 5 per cent," Mr Ballali said.   According to the governor, by December 31, 2002, the economy was performing  well.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt; "We have recorded 6 per cent GDP, our reserves are at $1.4 billion and the  inflation rate is at 4.4 per cent. With good rainfall, we will do just fine," he stated.   Facts bear Mr Ballali out.    Although prices of traditional exports in the world market keep falling,  diversification into the non-traditional export goods, especially minerals, has  saved the economy against what would otherwise have been devastating  effects.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;According to the Bank of Tanzania's Economic Review for last November, in  October earnings from non-traditional exports rose by 26.7 per cent to $66.9  million.    This was due to increases in exports of all major sub-categories: minerals,  manufactured goods, fish and fish products and horticultural goods among  others.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;However, these optimistic signs are still too few not to worry the government.  Fears of war struck early in Zanzibar, forcing the isle government to announce  new prices for petroleum products as from February 16, 2003.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The principal secretary in the Ministry of Finance and Planning, Mr Julian  Raphael, said the new prices were a response to the increases in international oil  prices sparked by the possibility of a war against Iraq.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;He described the increases as "a loss-rescue mechanism" without which the  government would have been required to subsidise petroleum.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The new prices per litre changed: Bunker oil Tsh580 (fromTsh470), diesel  Tsh650 (from Tsh550) and petrol Tsh660 (from Tsh580).   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt; In all probability, these will increase, even if only marginally, should a conflict  send global prices up significantly.   The result of the increases were predictable. A day after the announcement,  there was a rise in fares.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Where fares were previously Tsh100, they were increased to Tsh150 and those  who were charging Tsh150 increased to Tsh200.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Until the war jitters, Tanzania had enjoyed a long streak of good economic  fortunes compared to the past.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The annual inflation rate had edged down to a record 4.4 per cent, a rate only  associated with the liberal economic reforms that started in earnest a decade  ago.    By regional standards, and judged against its own past performance, Tanzania  has come a long way since it began carrying out economic and institutional  reforms.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Foreign Direct Investment (FDI) inflows, for example, have been steady and  impressive. Inflows have risen from $172.22 million in 1997 to $183.83 million in  1999, representing the highest figure in sub-Sahara Africa.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The Director for Investment Promotion at the Tanzania Investment Centre, Mr  Emmanuel ole Naiko, fears that those gains could be scuttled by a war in the  Gulf.    "The threat of war has already shaken the economy. There has been an abrupt  rise in the prices of goods. The situation will surely halt investors' plans to come  to countries like ours," Mr Naiko said.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; An expert with the Economic Research Bureau of the University of Dar es  Salaam, Dr Wilbald Maro, made similar observations, but was more pessimistic.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;He said the Tanzanian economy would "collapse or stagnate" if the United States  and her allies attacked Iraq.   He reasoned that the war would affect prices of agricultural products in the world  market, and thus lead to lower incomes for farmers.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dr Maro said a war in Iraq could also upset the African Growth and Opportunity  Act (AGOA), under which Tanzania has been listed among 36 sub-Saharan  African countries, eligible to export textiles to the vast US market without tariffs.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;If diplomacy fails to prevent the third Gulf war, Tanzanians only hope will be with  Oil Producing and Exporting Countries (Opec).    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leading members of Opec have promised to remove the oil cartel's output ceiling  in the event of a war with Iraq.   Observers say such a move would allow Saudi Arabia, the world's largest oil  exporter, to regain some of the market share it has lost to non-Opec producers,  particularly Russia.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;This article appeared in Daily Nation Newspaper (Kenya) and The Monitor Newpaper (Uganda) in March 2003. It can be viewed in website. The author is a journalist with Mwananchi Communications, Tanzania, a Nation Media  Group company.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-114604108184632706?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/114604108184632706/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=114604108184632706&amp;isPopup=true' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114604108184632706'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114604108184632706'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2006/04/this-article-was-published-in-daily.html' title='This article was published in The Daily Nation (in March 19, 2003) few days before United States of America led the coalition to invade Iraq.'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114603556612092966</id><published>2006-04-26T00:06:00.000-07:00</published><updated>2006-04-26T00:14:55.496-07:00</updated><title type='text'>Makala hii ya John Tendwa ilichapwa katika gazeti la Mwananchi mwaka 2005</title><content type='html'>KUNA mvinyo mkali unawalevya viongozi wetu wa serikali. Kwa miaka, miezi na siku nimekuwa nikijaribu kutafuta aina ya mvinyo huo na jibu la haraka haraka nimeshindwa kulipata. Pamoja na kukosa majibu ya swali langu hilo, bado nimeweza kubaini kwamba kipo kileo kibaya ambacho aghalab kinawalevya viongozi wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bado nina kumbukumbu zinazoonyesha kwamba, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere katika hotuba zake amewahi kutumia neno 'ulevi wa madaraka' akilenga kuwazungumzia watu tuliowapa dhamana ya mamlaka ya umma na ambao baada ya kupata thawabu hizo wamegeuka na kujifanya wafalme wasio na unyenyekevu kabisa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nje ya vyombo vya dola (mahakama na polisi kwa mfano) kuna njia nyingi za kumbaini mlevi aliyepata kileo chake kupita kiasi, kwa kiwango cha kushindwa kuitawala akili na mwili wake. Moja ya njia hizo ni kumbaini mtu huyo kwa namna anavyoshindwa kumudu fikra zake za upole, simile na tahadhari hususan anapoutumia mdomo wake kujenga hoja za ovyo ovyo na zisizochujwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Namna ya pili ya kumtambua mlevi ni kumwangalia jinsi anavyoshindwa kuuhimili mwili wake. Anapotembea aghalab mlevi huyo hupepesuka na iwapo kileo alichopata ni kingi zaidi basi mtu huyo hujikuta akienda hatua moja mbili mbele na kurudi moja nyuma na wakati mwingine kuanguka kwa sababu tu ya kupoteza 'balance' yake.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huo ndiyo ulevi unaotokana na kunywa pombe au mvinyo uliotiwa chachu. Huo ndiyo ulevi tunaokabiliana nao katika maisha yetu ya mitaani kila siku, ingawa huo si ule ulevi aliokuwa akiuzungumzia Mwalimu na kwa yakini huo si ulevi ninaotaka kuuzungumzia katika makala hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ulevi ninaouzungumzia leo ni ule wa kulewa mvinyo wa madaraka, ulevi wa rushwa, udikteta, ubazazi, vitisho na mambo mengine yote yanayofanana na hayo. Ulevi huo ndiyo ule ambao unatokana na mvinyo waliokunywa akina John Tendwa, Muhammad Seif Khatibh na Ramadhan Omar Mapuri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ulevi wa watu hao watatu, umethibitishwa hivi karibuni kabisa. Kauli walizozitoa katika siku za hivi karibuni kabisa zinashabihiana na zile anazozitoa mlevi halisi aliyekunywa pombe. Ukizitafakari na kuwaangalia usoni wakati wakitoa kauli zao, utabaini mara moja kwamba, kuna kasoro kubwa vichwani mwao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo tutamjadili John Tendwa, Msajili wa Vyama Vya Siasa. Huyu mtu ni mwanasheria na mtu aliyechukua madaraka yake kwa mbwembwe nyingi. Siku zake za mwanzo ofisini akaonekana ni mtu makini kweli kweli. Akathubutu hata kutunisha misuli yake dhidi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ningali ninazo kumbukumbu za kauli za kizalendo kabisa alizowahi kuzitoa wakati wa siku zake za mwanzo katika ofisi ile aliyoirithi kutoka kwa mwasisi wake George Liundi. Wakati fulani alikaririwa na vyombo vya habari akitishia kukifuta katika daftari lake CCM, iwapo kingeshindwa kutimiza masharti ya usajili wa vyama vya siasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuishia hapo, wakati fulani akanukuliwa akiitaka CCM kuwasilisha ripoti yake ya mapato na matumizi ofisini kwake, kama inavyotakiwa kisheria na akatishia akisema, iwapo chama hicho kingeshindwa kutekeleza agizo lake hilo basi angekinyima mgawo wake wa ruzuku wa kila mwezi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakukomea katika hilo tu, akaenda mbali zaidi na miaka si mingi akatoa kauli ambayo kwa hakika iliwashangaza 'wana CCM wenzake' wengi. Akakipongeza Chama cha Wananchi kama moja ya vyama makini kabisa vya siasa, kauli ambayo ilikwenda kinyume kabisa na ya viongozi wa chama hicho tawala ambao kwa miaka nenda, miaka rudi wamekuwa wakikipa jina baya chama hicho kikuu cha upinzani hapa nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama vile haitoshi, Tendwa akasonga mbele, akatetea wingi wa vyama vya siasa hapa nchini na akawaponda wale waliokuwa wakitaka serikali itunge sheria ya kuvibana ambayo hatimaye itaviua vyama dhaifu na hivyo kubakia na vile vyenye nguvu pekee.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Misimamo ya namna hiyo ikamfanya aonekana shujaa machoni mwa vyama vya siasa vya upinzani na kwa mara ya kwanza ikajengeka sura ya matumaini mapya katika ujenzi wa demokrasia ya vyama vingi ambayo ilikuwa imekosekana tangu mfumo huo ulipoanzishwa rasmi Julai mwaka 1992. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Viongozi vya vyama vya siasa, hususan wale wa kambi ya upinzani wakamuona Tendwa kuwa ndiye mkombozi wao, kwani kauli na matendo yake vilionekana dhahiri kuwa mwiba mkali dhidi ya uhafidhina wa CCM na sera zake za kibabe. Akasifiwa na akina Augustine Mrema na viongozi wengi wengine wa upinzani. wadadisi wa mambo wakasema; "Hatimaye Ofisi Imepata Mwenyewe."   &lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Huyo ndiye Tendwa aliyeingia ofisi ya msajili akiwa fikra pevu na akili tulivu. Ndiye Tendwa kwa kihistoria ambaye hakika si huyu wa leo ambaye kwa kauli na matendo ameanza kuonekana kulewa mvinyo waliokunywa aliowakuta na waliokuja baada yake serikalini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tendwa wa sasa ni huyu tuliyemsikia juzi akiziponda jitihada sahihi za uongozi wa Tanzania Labour Party (TLP) za kuitisha Mkutano Mkuu Maalum wa kuwapata viongozi wake wwa kitaifa ili kukinusuru chama hicho na uwezekano wa kufutwa kwa tishio lililotolewa na msajili mwenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya Mrema na wenzake kufanikiwa kuitisha mkutano huo, Tendwa anaonekana kukwama. Sasa anadai eti mkutano huo ni batili na hata maamuzi yake hayatakuwa na nguvu kisheria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huyu wa leo ndiye ambaye, amegeuka na kuanza kucheza ngoma za kishabiki na za kuvikandamiza vyama vya upinzani. Wengi watakumbuka namna alivyokibana Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wakati kilipotangaza kuunda kikosi chake cha ulinzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si hayo tu, Tendwa wa zama hizi ndiye aliyekiletea TLP matatizo mengi tu ya kiutendaji kwa kuamua kwa makusudi kabisa kukinyima chama hicho ruzuku yake, akitumia malalamiko  ya kimbeya aliyoletewa na watu waliokorofishana na Mrema kwa sababu wanazozijua wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata baada ya uchunguzi wa kitaalam kuthibitisha kwamba Mrema hakushiriki katika ulafi huo uliopikwa, bado msajili huyu anaonekana kuiendeleza ajenda yake ya kukimaliza TLP akitumia kila analoliweza ili mradi tu kuhakikisha kwamba anatimiza ajenda yake ya siri anayoijua yeye.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tuna kila sababu ya kuamini kwamba, anaona fedheha ya kushindwa na sasa anafanya yale ya mfa maji. Pamoja na kuutambua udhaifu mkubwa wa kiuongozi wa Mrema na genge lake, hatuko tayari kumuona Tendwa akijaribu kuinyonga demokrasia ambayo wengine tunafahamu vyema madhara ya kuipoteza. Hilo analolisema Tendwa leo haliiingia akilini.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-114603556612092966?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/114603556612092966/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=114603556612092966&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603556612092966'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603556612092966'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2006/04/makala-hii-ya-john-tendwa-ilichapwa.html' title='Makala hii ya John Tendwa ilichapwa katika gazeti la Mwananchi mwaka 2005'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114603471118331009</id><published>2006-04-25T23:54:00.000-07:00</published><updated>2006-04-25T23:58:31.256-07:00</updated><title type='text'>Kigoda; Simba mwendapole, anayejua mawindo yake</title><content type='html'>HII ni sehemu ya sita na ya mwisho ya makala za uchambuzi zinazowaangalia wana CCM 11 waliojitokeza kusaka nafasi moja ya kuteuliwa kuwa wagombea wa kiti cha urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya uchaguzi wa baadaye Oktoba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tumewachambua wagombea sita tayari japo kwa ufupi. Sasa tunalazimika kwa muhtasari kuwaangalia Abdallah Kigoda, Ali Karume, Patrick Chokala, Dk. William Shija na John Shibuda na kuziangalia nafasi zao za kuteuliwa na chama hicho. Miongoni mwao wote, Kigoda ndiye kada mzito zaidi kuliko wenzake, akifuatiwa kwa mbali mbali na Shija. Shibuda ndiye mwepesi kabisa miongoni mwa wagombea wote ambaye ni muujiza pekee utakaomwezesha kupenya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo si rahisi kuwachambua wagombea hao watano waliobaki pasipo kufanya ulinganifu na wenzao waliotangulia, akina Jakaya Kikwete, Salim Ahmed Salim, John Malecela, Mark Mwandosya, Frederick Sumaye na Iddi Simba. Kwa kuzingatia ukweli huo basi, tunalazimika kurejea na  kufanya tathmini linganifu, ili wasomaji na wana CCM watakaokuwa na jukumu la kuteua mgombea waone upande mwingine wa mtazamo kuhusu wanachama wenzao.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika makala zilizotangulia kwa mfano tuliwaangalia vilivyo wana CCM wawili, Iddi Simba na Mark Mwandosya si kwa sababu nyingine yoyote kubwa, bali kwa kuheshimu uwezo wa bongo zao katika kufanya kazi na kuyaangalia mambo kwa upeo wa juu kabisa, pengine kuliko wagombea wengine tuliowazungumzia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hawa wagombea wawili, mbali ya sifa hiyo kubwa, ndiyo pekee ambao nje ya uwanja wa kisiasa wamekuwa na uwezo angalau wa kusimama kwa miguu yao miwili na kutumia vyema kabisa ujuzi wao kitaaluma, kufanya mambo mengine katika taasisi za umma, kimataifa na wakati mwingine katika asasi binafsi. Nje ya siasa, wagombea hawa wawili ni wajasiriamali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika ubunge wa Ilala alionao Simba au ule wa Rungwe Mashariki wa Mark Mwandosya, pamoja na kuwa madaraja muhimu kwao, yaliyowaingiza bungeni hata kuwawezesha kuteuliwa kuwa mawaziri kwa mara ya kwanza katika serikali ya Rais Benjamin Mkapa, si mkate pekee wa maisha yao ya kila siku. Wanayo mambo mengine ya wazi, yawe ni ya kibiashara au kitaaluma wanayoyafanya na ambayo aghalab yanaakisi taswira zao barabara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dk. Salim Ahmed Salim ni mwanadiplomasia na mwanasiasa tu. Udaktari wake wa falsafa ameupata wakati akiwa ndani ya uanadiplomasia wake na kimsingi umekuwa ukimwimarisha kistaha kama mwanasiasa na mwanadiplomasia wa kimataifa, hana jingine alilowahi kulifanya nje ya hilo kitaaluma au hata kikazi. Nje ya siasa si rahisi kutabiri ni kitu gani anaweza akakifanya zaidi ya kustaafu kimya kimya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiiangalia historia yake kisiasa, huwezi ukapata shida hata kidogo kubaini ni kwa nini hasa ameamua kugombea urais wa Tanzania. Jibu ni rahisi, huo ndiyo mkate wake. Siasa ndiyo taaluma anayoifahamu vyema na siasa za nchi maskini, ni siasa za madaraka. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Angekuwa mwanasiasa msomi na mwanadiplomasia anayejali taaluma yake barabara, Salim kama walivyofanya akina Madeline Albright, Mchungaji Charles Stith ambao baada ya kuachana na shughuli za kisiasa sasa wanaendelea na masuala ya kitaaluma.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siasa pia ndiyo imekuwa sehemu muhimu ya kimaisha ya, kada nambari moja wa chama hicho, Jakaya Kikwete mtu anayeweza akatembea kifua mbele na kujivunia ukada huo kwa maana halisi ya ukada ndani ya Chama Cha Mapinduzi, pengine kuliko ilivyo kwa mgombea mwingine yeyote. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Malecela, kada mwingine wa CCM, ambaye rekodi yake ya uanasiasa uliopevuka, uanadiplomasia  uliotukuka na uongozi wa umma katika ngazi mbalimbali uliomfikisha hadi kuwa Waziri Mkuu na sasa Makamu wa Mwenyekiti wa CCM (Tanzania), ndiye mtu pekee ambaye anaweza akavaa kiatu cha saizi moja na Kikwete unapochanganya utumishi kwa maana na uzito wa majukumu, uzoefu na uwajibikaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mantiki hiyo kwa maana ya utumishi wa kisiasa, Salim, Kikwete na Malecela wanaweza wakawekwa katika mizania inayofanana na hivyo kuwafanya wawe katika daraja moja linalowawezesha hatimaye kuwa na sifa inayofanana unapokiangalia kigezo nambari moja cha sifa za kugombea urais miongoni mwa 13 vilivyowekwa na chama tawala, kinachosema; " (mgombea urais) awe na uzoefu wa kuongoza taifa kwa kuzingatia uzoefu wake katika uongozi wa shughuli za serikali, umma na taasisi."  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wagombea kama Dk. Abdallah Kigoda, Patrick Chokala, Mark Mwandosya, William Shija na hata Iddi Simba waliingia serikalini kitaaluma na kujikuta wakifanya kazi na wanasiasa na baadaye nao wakavutiwa na 'mchezo' wenyewe, hali ni tofauti kabisa kwa Kikwete kwa mfano ambaye tangu amalize Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam mwaka 1975, mbali ya kwenda jeshini amekuwa sehemu muhimu ndani ya TANU na baadaye CCM kwa miaka yake yote iliyofuata.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na kimsingi uzoefu wa kazi za kiutendaji serikalini na baadaye kuingia kwao katika siasa, ni moja ya silaha kubwa za kujiamini kwa Kigoda, Chokala, na Shija kwa mfano za kujiona kuwa watu wenye sifa za kuweza kupewa jukumu la kuliongoza taifa hili katika nafasi ya urais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, dhamira za kuingia kwa wanasiasa kama Shibuda, Chokala na Shija kwa mfano katika kinyang'anyiro hicho huenda hazitokani na sababu za kuamini kwa dhati kabisa kwamba urais unaweza ukapatikana kwa kubahatisha, hasa baada ya kufanya maandalizi ya kushtukiza kabla ya kuingia katika kinyang'anyiro chenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si rahisi kuamini kwamba Shibuda kwa mfano, mtu ambaye mbali ya kuwahi kuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ambamo sasa hayumo, kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Shinyanga na baadaye kujaribu kuupata mara mbili bila mafanikio uenyekiti wa taifa wa jumuiya hiyo ana dhamira ya kweli kweli ya kuutaka urais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika Shibuda anazielewa fika fitna za kisiasa ndani ya CCM, anafahamu vyema namna alivyo mdogo na mtu asiyepewa uzito mkubwa wa kuaminika miongoni mwa viongozi wa juu wa chama hicho. Anafahamu vyema kwamba, kwa kuwa kwake nje ya NEC na Kamati Kuu (CC) ya chama hicho, misukosuko ya kisiasa aliyowahi kuipitia na mingine mingi iliyowahi kumkumba kwa sehemu kubwa ni mambo yanayomfanya asiwe na nafasi yoyote, ndogo au kubwa ya kuteuliwa kuwa mgombea.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alipotangaza azma yake ya kuchukua fomu, mara moja Shibuda alionekana akijaribu kwa mara ya tatu kumtunishia misuli, mpinzani wake wa siku nyingi katika siasa za CCM, Iddi Simba ambaye ndiye aliyemwangusha kwenye kinyang'anyiro cha uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi mwaka 1999.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Historia kubwa na ya wazi ya Shibuda ni namna alivyoulalamikia kwa kishindo, ushindi wa kura saba alizozidiwa na Simba kwenye uchaguzi huo, akisema kulikuwa na kampeni chafu dhidi yake. Katika kuhalalisha malalamiko yake, akaandika taarifa ndefu kupinga ushindi huo wa Simba na akaipeleka katika asasi za juu za umma, akieleza namna mpinzani wake huyo alivyocheza rafu hadi akaibuka mshindi. Kwa bahati mbaya hakufanikiwa kubadili matokeo.       &lt;br /&gt;   &lt;br /&gt;Ni kwa mantiki hii pengine mtu anaweza akapata mawazo kwamba, uamuzi wa Shibuda mtu ambaye unapokutana naye mitaani amekuwa akijitambulisha kwa jina la ' Mimi mnyonge bwana' kuingia katika kinyang'anyiro hicho kwa kweli hautokani hata kidogo na dhamira yake ya kutaka kweli kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, bali sababu nyingine kabisa ya kujijengea wasifu wa kisiasa au pengine kuendeleza hulka yake ya kujipima ubavu na watu kama Simba.      &lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Hali iko hivyo pia kwa Chokala na Shija ambao aghalab kuingia kwao katika kupigania nafasi moja ya kuteuliwa kumekuja kwa njia ya kushtukiza sana. Miaka miwili mitatu hivi, kulikuwa na dalili za wazi za akina Malecela, Sumaye, Kikwete, Mwandosya, Simba na Kigoda kujipanga na kujiandaa kwa ajili ya nafasi hiyo ya juu kabisa kitaifa. Udadisi wa mara kwa mara wa vyombo vya habari kwa nyakati tofauti na kwa muda mrefu umekuwa ukiwataja wana CCM hao na azma zao za kuutaka urais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu ya kuzingatia ukweli huo wa kihistoria, unaweza ukaona dhahiri kwamba, maandalizi yaliyofanywa na Chokala, Shija,  na Shibuda kwa ajili ya urais ni hafifu sana na ambayo yanaweza yaeleza jambo moja la wazi kwamba, watu hawa wanayo ajenda nyingine nje ya nafasi hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ajenda gani basi? ni ubunge? ugombea wenza au ni kitu gani hasa wanakitaka? Majibu ya maswali haya tutayaona muda si mrefu kwani, watakaposhindwa kuteuliwa kwa ajili ya urais basi tutawasikia wakipigana vikumbo kwa ajili ya kuzipata nafasi nyingine za kisiasa au za kuteuliwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukimwacha Shibuda, hebu tumwangalie Dk Kigoda, ambaye pamoja na kwamba ni mtu ambaye katika makala hii ameingizwa katika kundi hili la mwisho, yeye ni mtu ambaye aghalab nafasi yake ya kuteuliwa na wana CCM wenzake ni kubwa kwa kiwango kinachoweza kulingana na hata pengine kuwazidi wagombea wenzake kama Malecela, Sumaye na pengine Salim Ahmed Salim.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tangu mwaka 1997, Kigoda daktari wa falsafa wa mchumi wa kilimo ambaye kati ya mwaka 1975 na 1995 alikuwa afisa-mchumi wa juu serikalini, akianzia katika ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Fedha, Mipango na Uchumi na baadaye akahamishiwa katika Tume ya Mipango, kabla hajaingia rasmi katika uringo wa siasa mwaka 1995.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aliingia bungeni mwaka 1995 akitokea jimbo la Handeni na miaka miwili baadaye akawa mjumbe wa Kamati Kuu, kikao chenye nguvu kubwa ndani ya chama hicho na akachaguliwa kuwa Mweka Hazina wa chama hicho. Mwaka 2002, akarejea tena katika Halmashauri Kuu ya Taifa na akaendelea kuwa mjumbe wa Kamati Kuu. Nje ya chama amekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara (1995-1997), Waziri wa Nishati na Madini (1997-2000) na baadaye akawa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mipango na Ubinafsishaji 2000-hadi hivi sasa).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nafasi zake hizo kwa hakika zimemfanya awe ni mmoja wa wana CCM anayeheshimika sana ndani ya vikao vya chama hicho na kimsingi si mgombea wa kumpuuza hata kidogo. Anaweza  akateuliwa na kuwa mgombea wa urais katika hali ambayo inaweza ikawashangaza Watanzania walio nje ya chama hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu waliosoma naye Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam wanasema, mchumi huyo anayo akili tulivu kweli kweli, ni mwepesi wa kuchanganua mambo na anajua kile anachokisema akitafakari kabla ya kutamka. Ni mwanasiasa asiye na mbwembwe wala makuu na yeye ni rafiki mkubwa wa watu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokana na hulka yake hiyo, yeye ni mmoja wa wagombea ambaye ana uhusiano mzuri takriban na wenzake wote waliogombea nafasi hiyo kupitia CCM. Anawafahamu vyema Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF aliyetangaza kugombea urais wa muungano pia kwa tiketi ya CUF na Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Shariff Hamad anayekusudia kugombea urais wa Zanzibar kwa sababu alisoma nao Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yeye ni mmoja wa wana CCM wenye msimamo mkali dhidi ya CUF, kwani kumbukumbu zinaonyesha kwamba amewahi kueleza katika mikutano kushangazwa kwake na Lipumba, msomi anayemfahamu kutokana na uamuzi wake wa kujiunga na CUF, chama ambacho yeye, Kigoda amewahi kukiita cha Wapemba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nafasi yake ya ujumbe wa CC ambayo pia wagombea wengine kama Kikwete, Malecela, Salim na Sumaye wanazo, zinamweka Kigoda katika nafasi zinazolingana na hao na kuwaacha akina Chokala, Shija na Shibuda kuwa na nafasi finyu kabisa ya kupita hata katika hatua ya awali ya mchujo ndani ya kikao hicho kitakachopeleka majina ya wagombea wasiozidi watano. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa majina yatakayopelekwa NEC yanaweza yakawa mawili, matatu au hata manne, bado kwa hakika Kigoda anaweza akapita hatua hiyo. Kama ni kupoteza basi anaweza kufikia hatua hiyo mwishoni. Kwa sababu hiyo basi, Kigoda anaweza akawa kundi moja na Mwandosya msomi mwenzake ambaye anaingia pia katika kinyang'anyiro hicho akiwa hana cha kupoteza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu hawa wawili kwa hakika ndiyo wanaoweza wakawaduwaza akina Kikwete, Salim na Malecela. Uwezo wao wa kuona mambo unawaweka hata juu ya Sumaye kwa mfano ambaye ni Waziri Mkuu. Iwapo kwa mfano mmoja kati ya hao wawili angekuwa katika nafasi ya uwaziri mkuu katika kipindi cha miaka 10 alichokaa Sumaye, basi kwa hakika hali ya hewa katika mchuano wa urais mwaka huu ungelikuwa ni kitu kingine kabisa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kuzingatia hilo basi, uamuzi wao wa kugombea urais unavifanya vikao vya CC, NEC na Mkutano Mkuu wa CCM kuwa tayari kumpitisha mmoja miongoni mwa akina Kikwete, Salim, Kigoda, Mwandosya, Malecela, na Sumaye (kwa mpangilio huo huo) kuwa mgombea wao wa urais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika, akina Simba, Shija, Shibuda na Chokala watalazimika kuukubali ukweli wa kushindwa kuteuliwa na kukubali kwamba, urais si lelemama, urais si ubunge wala ujumbe wa Kamati Kuu au Halmashauri Kuu. Urais ni thawabu ya pekee, ni nafasi ya mmoja aliye bora miongoni mwa wengi na kwamba lazima wasindikizaji ama waondoke wenyewe au wasubiri kuondolewa kwa kura. Wiki mbili tu za subira zimebaki.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-114603471118331009?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/114603471118331009/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=114603471118331009&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603471118331009'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603471118331009'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2006/04/kigoda-simba-mwendapole-anayejua.html' title='Kigoda; Simba mwendapole, anayejua mawindo yake'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114603438414077189</id><published>2006-04-25T23:48:00.000-07:00</published><updated>2006-04-25T23:53:07.533-07:00</updated><title type='text'>Ni kwa nini basi Iddi Simba anagombea?</title><content type='html'>TUNAENDELEA na uchambuzi wetu wa wagombea urais wa Muungano. Hii ikiwa ni sehemu ya tano ya uchambuzi huo, tunalazimika kuendelea na mgombea asiyetajwa sana kwa jina na mtu anayeonekana kusahaulika katika akili za Watanzania wanaowaniwa urais. Jina la mwanasiasa huyo masikioni mwa watu halitajwi sana linapolinganishwa na akina Jakaya Kikwete, Salim Ahmed Salim, John Malecela na Frederick Sumaye. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huyo si mwingine ni Iddi Simba ambaye tulimchambua kwa sehemu kubwa wiki mbili zilizopita. Yeye kwa upande wa umaarufu masikioni mwa watu anaonekana kuzidiwa hata na Profesa Mark Mwandosya mwanasiasa mgeni ambaye katika kipindi kifupi ameweza kusikika kweli kweli. Pengine Simba anawekwa katika mizani inayofanana na akina Dk. Abdallah Kigoda na Dk. William Shija.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kihadhi, anaonekana kuwazidi washindani wake wengine wasiopewa nafasi kubwa kama Patrick Chokala na mpinzani wake wa muda mrefu katika siasa hususan ndani ya Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi, John Magale Shibuda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na hilo, kuondoka kwake katika nafasi ya uwaziri wa Viwanda na Biashara kwa kujiuzulu kutokana na shinikizo la wabunge na vyombo vya habari kwa sababu ya sakata ya sukari Novemba mwaka 2001 kama tulivyoona katika makala ile ya kwanza, bado linabakia kuwa doa lake kubwa kisiasa ambalo linamfanya apewe nafasi ndogo ya kuteuliwa kuwa mgombea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alipoondolewa madarakani, kelele nyingi zilipigwa. Baadhi ya watu wakamtetea na wengine wakaeleza kusikitishwa wakisema, Simba alikuwa ametolewa kafara tu, kwani kulikuwa na makosa mengine mengi tu ambayo serikali ilikuwa imeyafanya pasipo wahusika kujiuzulu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza watetezi hao wa Simba wakasema bayana kwamba sakata ya sukari ilikuwa haifanani kwa namna yoyote, na kashfa kama zile za mradi wa umeme wa IPTL, uuzwaji wa Benki ya Taifa ya Biashara na mikataba mibovu ya madini ambayo hata hivyo hakuna waziri au kiongozi aliyejiuzulu kutokana na hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, wana CCM wenzake kadhaa ambao wamewahi kufanya naye kazi kama mbunge mwenzao, waziri, mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, mbunge wa Ilala, Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) wamekuwa wakimuona kuwa mwanasiasa mwenye jeuri ya kujiamini kupita kiasi, sifa ambayo anaonekana kuwa nayo kwa kiwango cha kumzidi hata Rais Benjamin Mkapa ambaye naye hiyo inaonekana kuwa kasoro yake kubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kuwa mmoja wa wana CCM wenye bongo zinazochememka barabara, mtu mwenye upeo mkubwa wa kuona mambo hususan, yale ya kiuchumi, kwa sehemu fulani hulka yake ya ujeuri ndiyo hasa ambayo mwaka 2004 ilisababisha ajikute akiipoteza nafasi aliyokuwa nayo ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, ambayo ilikuwa ikimpa fursa ya moja kwa moja ya kuingia katika vikao muhimu vya maamuzi vya CC na NEC za CCM.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nje ya kasoro hiyo ya 'jeuri', tangu akiwa waziri, Simba aliingia katika mzozo mwingine na wana CCM wenzake, mzozo ambao msingi wake pengine ni hulka yake hiyo hiyo ya kujiamini kupita kiasi. Huo si mgogoro mwingine bali ni falsafa ya uzawa aliyoanza kuijenga waziwazi mapema kabisa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza alianza kwa kuiingiza katika Makadirio na Matumizi ya Wizara ya Viwanda na Biashara kama ajenda muhimu kabisa ya kuwawezesha wazawa hao na baadaye akaendelea nayo hadi mwaka 2003 alipoamua kuandika kitabu alichokiita 'Dhana ya Uzawa'.     &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitabu hicho kilisababisha mtafaruku mkubwa ndani ya CCM kwenyewe na nje. Wako waliokiunga mkono na wengine wakakipinga. Lakini alikitoa kwa wakati kwani wakati huo kulikuwa na kelele nyingine kutoka kwa wananchi wa kawaida na wafanyabiashara wa Kitanzania waliokuwa wakilalamikia kutengwa kwao katika umiliki wa uchumi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimsingi kuna kila sababu ya kuamini kwamba Simba alililenga kundi hilo katika kujihakikishia kwamba anaungwa mkono na watu wengi waliokuwa wakipinga kile ambacho kilionekana kuwa ni wageni kushika uchumi wa taifa na kusahaulika kwa wazelendo hao weusi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya ndani ya CCM hoja hiyo ikapata upinzani wa kweli kweli, mbunge wa Dodoma Mjini Hashim Saggaf  akasimama ndani ya bunge na akaeleza kukerwa na dhana hiyo ya uzawa. Hakuishia hapo akaifananisha na ubaguzi uliofanywa na kiongozi wa zamani ya Uganda, Iddi Amin Dada ambaye kwa makusudi aliamua kuwaondoa Waingereza Uganda na kuwapa wazalendo wa nchi hiyo mamlaka ya kiuchumi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si Saggaf pekee aliyempinga Simba. Kundi kubwa la watu likaibuka kumpinga, moja ya hoja za upinzani zikidai kwamba alikuwa ni mtu ambaye msimamo wake haukuwa bayana kwani yeye ndiye aliyekuwa akilaumiwa kwa kuwapa wageni kazi za uwakala wa meli zilizosababisha kufa kifo cha kawaida cha Shirika la Kizalendo la Uwakala wa Meli (NASACO).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Upinzani huo mkali dhidi yake umekuwa ukiendelea hadi hivi sasa, wakati akiwa ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji katika Kampuni ya Watanzania ya Uwekezaji (NICO) ambayo imekuwa ikipita kuwahamasisha Watanzania wazalendo kununua hisa zake ili kuwajengea uwezo wa kumiliki uchumi wao wenyewe.. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Niko ikiwa mkoani Mbeya kwa mfano, wananchi wa huko wakiongozwa na viongozi wa juu wa mkoa huo walimtaka , Simba kujitoa katika kinyang'anyiro cha urais mwaka huu kama sharti la wao kuiunga mkono taasisi hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakizungumza kwa jazba wakati wa mkutano ulioitishwa na NICO ili kuzungumza na wananchi wa mkoa huo kuhusu uuzwaji wa hisa za kampuni hiyo, kwa nyakati tofauti wananchi haowalisema wana wasiwasi mkubwa kuwa anatumia nafasi hiyo kwa ajili ya kujipigia debe la urais. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mmoja wa watu waliotoa maoni yao siku hiyo ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Frank Uhahula, alisema kwa kuwa hiyo ni kasoro ya wazi katika NICO ni hiyo na hivyo iwapo watataka watu wawaelewe na wasionekane kuwa na lengo la kuwajenga baadhi ya watu kisiasa hawana budi kuiondoa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uhahula alinukuu kauli ya Mwenyekiti wa NICO, Felix Mosha, aliyewahi kusema kuwa, mmoja wa waasisi wa wazo la NICO, Waziri Mkuu staafu, Jaji Joseph Warioba, alikataa nafasi ya uenyekiti ili kukwepa kuonekana kampuni hiyo ni ya kisiasa, hivyo Simba hakupaswa kukubali uongozi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Busara alizotumia Mheshimiwa Warioba zinapaswa kuigwa, kwa kuwa kama tunataka kueleweka kuwa si wanasiasa lazima tuweke pembeni mambo yetu mengine, sasa kati yenu yupo mheshimiwa amekwishatangaza kugombea urais, ajitoe huku ili tuelewe kuwa anataka kipi,” alisema Uhahula.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alichosema Uhahula na wananchi wa Mbeya kilichangiwa kwa kiasi kikubwa na mambo mawili makubwa. Mosi watu wengi wamekuwa wakimuona Simba kama mtu anayejaribu kutumia nafasi zake kuu mbili za hivi sasa katika kujiimarisha. Ya kwanza ikiwa ni hiyo ya NICO na ya pili ya uenyekiti wa Taasisi ya Mikopo Nafuu ya Pride Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengi wanaomwangalia Simba katika mitazamo hiyo miwili wanasema kwamba, mwanasiasa huyo anajaribu kujijengea taswira ya mtu wa watu na pengine mzalendo ambaye wakati alipokuwa akitekeleza majukumu yake kama waziri, watu walikuwa hawamfahamu sawasawa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya sana kwake, wenzake wengi ndani ya CCM wanaonekana kutoyasahau maamuzi aliyoyasimamia, yawe ni yake au ya serikali wakati akiwa waziri. Wanamuona kuwa ni mtu anayesema hili wakati akiamini jingine. Amewapotezea imani wana CCM wenzake kadhaa ambao kimsingi ndiyo watakaompigia kura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na akili yake kuwa ni inayochemka sawasawa kwa kiwango cha watu kama Mwandosya au Kigoda kwa mfano, bado anawekwa katika kundi la kuwa mmoja wa wanachama wa chama hicho wenye nafasi ndogo sana ya kuteuliwa na kuwa mgombea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni rahisi kuthibitisha uwezo wa Iddi SImba kiakili kwani watu wanaofuatilia utendaji wake wa kazi wanaweza wakakumbuka kwamba pamoja na kufanya kazi ndani ya nchi amewahi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, akiishi London Uingereza kati ya mwaka 1978 na 1981 na kabla ya hapo alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki kati ya mwaka 1968 na 1978 makao makuu Uganda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kwa kuzingatia historia yake hiyo ndiyo maana hata alipojiuzulu uwaziri wake, Rais Benjamin Mkapa alimuopmba aahirishe uamuzi wak&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo uamuzi wake wa kugombea urais unaweza ukawa umemweka katika nafasi muhimu kabisa kisiasa. Inaweza ikamsaidia kujiimarisha kisiasa jimboni kwake Ilala aliyoishika kwa takriban miaka 10 sasa au nyingine ya kuteuliwa baada ya Uchaguzi Mkuu kuanzia Novemba mwaka huu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika uamuzi wake wa kugombea urais hakuufanya kwa kukurupuka, kwani kwa upeo wake wa kuona mambo anaitambua vyema nafasi ndogo aliyonayo ya kuteuliwa kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama chake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ameingia katika kinyang'anyiro hicho cha urais wakati wana CCM wenzake wakiikumbuka vyema kauli aliyoitoa siku chache tu baada ya kuupoteza wadhifa wake wa  uenyekiti wa taifa wa Jumuiya ya Wazazi mwishoni mwa mwaka jana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bila ya kutaja jina la mtu, alisema tukio hilo lilikuwa ni kampeni chafu zilizokuwa zikiendeshwa na kiongozi mmoja wa juu kabisa serikalini aliyekuwa na malengo ya urais wa mwaka huu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli hiyo kwa hakika ilimlenga mmoja wa watu ambao wamejitokeza kugombea urais. Si rahisi kusema bayana kwamba Simba amechukua fomu ili kumdhibiti kiongozi huyo ama la. Wana CCM na Watanzania watakuwa wakisubiri kuona kule anakoelekea.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-114603438414077189?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/114603438414077189/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=114603438414077189&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603438414077189'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603438414077189'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2006/04/ni-kwa-nini-basi-iddi-simba-anagombea.html' title='Ni kwa nini basi Iddi Simba anagombea?'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114603393866546528</id><published>2006-04-25T23:42:00.000-07:00</published><updated>2006-04-25T23:45:38.743-07:00</updated><title type='text'>Iddi Simba; Mchumi jeuri anayeutaka urais</title><content type='html'>Hii ni sehemu ya nne ya uchambuzi wetu, unaolenga kutanabaisha nafasi za ushindi wa wagombea wetu, tukizingatia uwezo wa wagombea hao kuhimili mikiki mikiki ya uongozi, hoja zao zinaowajengea haiba yao kisiasa na mitazamo yao ya jumla katika maendeleo ya taifa letu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ili kuweza kuwapima sawasawa wagombea hao, tumekuwa tukilazimika kuziangalia kwa mantiki ya kuzipembua historia zao za kiutendaji, kifalsafa na namna walivyo na nafasi ya kushinda urais wa Tanzania. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bado tunaendelea kuwaangalia wanasiasa ambao  hivi sasa wapo katika hatua ya kupigania nafasi ya kuteuliwa kubeba bendera ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM), idadi yao sasa imefikia 11, baada ya mwanachama mwingine matata wa chama hicho, John Magale Shibuda kuchukua fomu mwanzoni mwa wiki hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya kumwangalia kwa muhtasari, Profesa Mark Mwandosya, Jumapili iliyopita na kabla ya hapo kuwachambua, Salim Ahmed Salim, Jakaya Kikwete, John Malecela na Frederick Sumaye, sasa tunaendelea na Iddi Mohammed Simba, mwana CCM wa kwanza kabisa kuweka bayana azma yake ya kugombea urais wa Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siyo jambo gumu hata kidogo kutanabaisha sababu hasa zilizomsukuma Iddi Simba, mbunge wa Ilala kwa vipindi viwili sasa, mwanasiasa mwenye sifa adhimu kabisa ndani ya CCM na pengine mgombea pekee mwenye uwezo wa kusema bayana kile anachoamini hata kama kitu hicho kitaonekana kuwa ni kinyume na mtazamo wa chama chake au viongozi wenzake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukimwacha Jakaya Kikwete kwa mfano, Iddi Simba ndiye mwanasiasa pekee mwenye 'kifua' na mtu asiye na silika ya kutafunatafuna maneno, wakati anapokusudia kufikisha ujumbe anaoulenga iwe ni kwa waandishi wa habari, wabunge wenzake, wapinzani wake, wakubwa zake wa kazi au ye-yote yule anayekabiliana naye ana kwa ana. &lt;br /&gt;       &lt;br /&gt;Pamoja na kuwa na sifa hiyo kubwa inayomfanya afanane-fanane na mgombea mwenzake ndani ya chama hicho, (Kikwete) hususan katika kuweka bayana kile anachoamini, bado kuna tofauti kubwa kati ya watu wawili wakati wanapoamua kuweka bayana fikra zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hulka, Kikwete na Iddi Simba wote ni wanasiasa wasio na simile hasa wakati wanapokerwa na kuamua kutoa madukuduku yao. Hata hivyo watu hao wawili wanacho kitu kimoja kikubwa ndani yao kinachowatofautisha wakati wanapowasilisha ujumbe wanaoulenga. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati Iddi Simba huwasilisha hoja zake wa kutumia maneno makali, yaliyojaa nasaba za kijeuri kabisa, hoja za za kisomi na pasipo kujali iwapo walengwa wake wanaweza kuyastahimili na kuyakubali pasipo kukerwa nayo, Kikwete yeye ni mtu anayewasilisha kile alichokilenga, hata kama ni kichungu kwake kwa namna ambayo walengwa au hata wale wanaomsikiliza wanalazimika kuyasikia na kuyakubali kutokana na namna anavyojieleza kwa kutumia lugha laini, upole na wakati mwingine sura ya tabasamu hata katika mambo ambayo mzungumzaji anapaswa kuonyesha huzuni au hata kilio.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hulka yake hiyo (Iddi Simba) ndiyo hasa ambayo mara kadhaa imekuwa ikimuweka katika mazingira magumu kisiasa miongoni mwa wanasiasa wenzake na wakati mwingine hata kwa watu wa chini, ambao amekuwa akiwaongoza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukirejea historia yake, iliyomfikisha hatua ya kulazimishwa kujiuzulu kiti chake cha Waziri wa Viwanda na Biashara, Novemba mwaka 2001 na baadaye kupoteza uenyekiti wa Jumuiya (ya CCM) ya Wazazi mwaka jana, si uwezo mdogo alionao katika uongozi, au maamuzi mabovu aliyokuwa akiyatoa, bali ni jeuri yake (hususan ya kauli) ambayo wenzake ndani ya CCM na wakati mwingine bungeni, wamekuwa wakimtuhumu kuwa nayo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukizungumza na mtu yeyote anayemfahamu Iddi Simba vizuri kabisa, atakueleza bayana namna Simba alivyo na mitazamo pevu katika masuala mengi tu, mchapakazi wa kweli kweli na ambaye uwezo wake wa kufikiri kama msomi si wa kutiliwa shaka hata kidogo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno rahisi kabisa, Simba ni mmoja wa wanasiasa adhimu ambao uwezo wao wa kunyumbulisha mambo, hususan yale yanayohusu masuala na mienendo ya kiuchumi, fedha, biashara na hata yale mahusiano ya kijamii na mataifa ya nje ni mkubwa kabisa kuwazidi mawaziri wengi tu ambao bado wako katika serikali ya sasa ya Rais Benjamin Mkapa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati Rais Benjamin Mkapa alipokuwa na timu ya mawaziri wa kariba ya Iddi Simba na Profesa  Simon Mbilinyi ambao kwa nyakati tofauti walilazimika kujiuzulu kutokana na kuhusishwa na maamuzi mabovu katika wizara zao, hakuna shaka kwamba rais alikuwa na kila sababu ya  kujivunia ubora wa kikosi chake cha kazi ambacho aghalab kilikuwa na nguvu kubwa kuzidi hata zile alizokuwa nazo Waziri Mkuu, Frederick Sumaye ambaye amekuwa akivishwa joho la 'kiranja wa mawaziri' asilostahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna shaka kabisa kwamba, Simba, katika kipindi alichokuwa Waziri wa Viwanda na Biashara (1997-2001), akiingia serikalini kwa mara ya kwanza, alifanya mengi ya kukumbukwa na ambayo kimsingi yamechangia kabisa katika kubadilisha mustakabali wa taifa hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maamuzi aliyoshiriki katika kuyafanya au yale aliyoyaongoza, aghalab ndiyo yaliyokuwa chachu kuu ya kutambulika kwake kama kiongozi shupavu mwenye uwezo wa kupitisha maamuzi, hata kama ni mazito kwa namna gani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Simba aliingia serikalini, wakati ajenda kuu ya kitaifa katika mahusiano ya kimataifa ikiwa ni uchumi na biashara. Akiwa mchumi kitaaluma, mara moja alianza kuonyesha makucha ya uwezo wake kama kiongozi na waziri anayeongoza wizara sahihi kabisa kwake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka miwili tu baada ya kuingia serikalini, akishirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Iddi Simba alikuwa kinara katika ajenda ya kuiondoa Tanzania katika Soko Nafuu la Nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mara ya kwanza, Iddi Simba aliutangaza uamuzi huo wa Tanzania kujitoa COMESA Julai mwaka 1999 wakati alipowasilisha Makadirio na Matumizi ya Wizara ya Viwanda na Biashara ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akisema uamuzi huo ungeanza kutekelezwa katika kipindi cha mwaka mmoja baadaye yaani mwaka 2000.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uamuzi huo ambao ulipingwa kwa nguvu kubwa na baadhi ya taasisi za kibiashara za ndani na hata nchi wanachama wa COMESA kwa kiwango cha kuitaka Tanzania kubadilisha uamuzi wake, ulipingwa kwa nguvu kubwa na Iddi Simba mwenyewe na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Jakaya Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Septemba Mosi mwaka huo huo, aliyekuwa Balozi wa Tanzania, nchini Zambia, Shani Lweno aliwasilisha notisi ya mwaka mmoja ya nia ya kujitoa COMESA. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwaka mmoja baadaye aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari, Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Patrick Chokala, ambaye naye ni mmoja wa wana CCM waliochukua fomu kuomba kuteuliwa kugombea urais ndani ya chama hicho akaitisha mkutano wa waandishi wa habari na kueleza kujiondoa huko kwa Tanzania (COMESA).    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapinzani wa uamuzi huo walipojitokeza kwa makundi kuupinga uamuzi huo wa serikali, huku wengine wakimuonya Rais Mkapa kuwa makini na ushauri wa Simba kuhusu suala hilo, yeye mwenyewe alisimama kidete kuutetea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja za kumpinga zilipoongezeka, Simba alisimamana akasema kwa jeuri kabisa kwamba, huo ulikuwa ni uamuzi wa lazima kwa Tanzania, ambayo imekuwa mwanachama katika taasisi nyingi za kimataifa ambazo malengo yake ama yanafanana au yanakinzana na hivyo kuwa mzigo kiuchumi badala ya kuwa na manufaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akaeleza bayana kwamba, uamuzi wa kujitoa COMESA, usingeweza kuathiri uchumi wa taifa, kwani malengo mengi ya taasisi hiyo yakiwamo yale ya kuondolewa kabisa kwa ushuru wa bidhaa (zero tariff), kuendeleza amani na usalama na soko la pamoja, yanafanana na yale ya Jumuiya ya Ushirikiano wa Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) ambayo Tanzania ni mwanachama wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja zake hizo zikawashinda wapinzani wake, ingawa maneno yameendelea hadi leo hii na kwa muda sasa ajenda ya kuitaka Tanzania ifikirie upya uamuzi wake wa kujiondoa COMESA haijafa, ingawa vile vile hoja za Simba kuhusu suala hilo bado zinaungwa mkono na serikali hadi leo hii. Hiyo ndiyo silaha yake ya kwanza kabisa; Nguvu ya Hoja, ushawishi unaozingatia takwimu sahihi, na utayari wa kuchukua maamuzi magumu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati suala hilo la COMESA likifukuta, Simba akaingia tena katika msuguano mwingine wa kimaamuzi pia. Safari hii msuguano huo ambao mpaka hivi sasa unachukuliwa na baadhi ya watu kuwa kasoro yake kubwa, ukamfanya ajengewe jina baya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msuguano huo ulitokana na uamuzi wake wa kutoa leseni kwa kampuni za kigeni kuanza kufanya kazi za uwakala wa meli katika bandari ya Dar es Salaam, shughuli ambayo kwa miaka 26 hadi mwaka huo wa 1999 ilikuwa ikifanywa na Shirika la Taifa la Uwakala wa Meli (NASACO).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uamuzi huo wa Simba, ambao mara kadhaa yeye mwenyewe amekuwa akisema ulifikiwa na Baraza la Mawaziri, ukamwondolea sifa ya uzalendo miongoni mwa wapinzani wake na hususan wale waliokuwa wafanyakazi wa NASACO na familia zao.&lt;br /&gt;    &lt;br /&gt;Mzozo huo kimsingi haukuanza na Simba kama, Waziri wa Viwanda na Biashara, bali kwa kiwango kikubwa ulitokana na uamuzi wa kisera wa serikali wa kujiondoa katika shughuli za kibiashara na kuiachia sekta binafsi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya sana, wafanyakazi wa NASACO hawakujiandaa kwa hilo na pili serikali yenyewe ikaamua kutekeleza sera yake hiyo, na kusahau kabisa 'factor' ya wafanyakazi hao na shirika lao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimsingi, serikali ilibanwa na makampuni yaliyokuwa yakifanya biashara na NASACO. Agosti Mosi mwaka 1999 kwa mfano, makampuni manane ya meli yaliyokuwa yakifanya biashara na shirika hilo la umma yalitoa notisi ya siku 30 ya kuvunja rasmi mikataba ya kikazi na NASACO, kwa kuacha kuitumia kuwaingizia mizigo yao.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Makampuni hayo makubwa ambayo ni pamoja na Mediterranean Shipping Company (MSC);Belgian Conglomerate, Compagne Maritime Belge (CMB); Maersk; Zim Line; P&amp;O Nedlloyd; Laurel Navigation Line (LNL) na Messina Line.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uamuzi wa makampuni hayo makubwa ulikuja miezi minne tu baada ya serikali chini ya usimamizi wa moja kwa moja wa Simba, kuyasajili makampuni 15 binafsi kwa ajili ya kufanya kazi za uwakala wa meli, uamuzi ambao kimsingi ndiyo uliyoyachochea makampuni hayo makubwa kuachana na NASACO.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna yoyote ule uamuzi huo ulikuwa mchungu kwa NASACO na hususan wafanyakazi wake 600 ambao walikuwa katika hatari ya kupoteza ajira kutokana na shirika lao kupoteza biashara ya uwakala. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini serikali pia na hususan Iddi Simba mwenyewe alikuwa katika wakati mgumu kwani, iwapo ingeamua kuwapunguza wafanyakazi wafanyakazi kuwapunguza wafanyakazi hao, basi ilipaswa kutenga kiasi cha shilingi bilioni moja hivi, kufanikisha jukumu hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Viongozi wa juu wa NASACO wakaweka bayana kwamba, uamuzi huo wa serikali wa kuruhusu shirika hilo lipoteze biashara yake ya uwakala wa meli ulikuwa unaisababishia hasara ya shilingi bilioni tisa, kiwango ambacho ni mara tisa hivi ya kile ambacho wafanyakazi wangelipwa kama marupurupu yao ya kupunguzwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uamuzi huo wa serikali ukaonekana kuwa usio na maana kabisa na usiozingatia misingi ya uzalendo wa kweli miongoni mwa viongozi wa serikali. Iddi Simba akawekwa katikati ya lawama zote hizo. Akaonekana msaliti machoni mwa Watanzania wa kawaida, vyama vya siasa, wabunge wenzake na hasa hasa wafanyakazi wa NASACO, jamaa na ndugu zao pia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Julai mwaka 2001wafanyakazi hao wakaandamana hadi ofisini kwake wakitaka abatilishe uamuzi wa kutoa leseni kwa makampuni hayo binafsi. Yeye akaendelea kushikilia msimamo wake thabiti akisema hana uwezo wa kutengua uamuzi wa kisera wa serikali. Ikafikia hatua ya watu wakimtaka ajiuzulu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vyombo vya habari vilipomfuata ofisini kwake, akawa mkali kweli kweli, akaeleza kushangazwa na wafanyakazi hao kuandamana hadi kwake akisema yeye hakuwa akihusika katika kuwatafutia maslahi yao bali taasisi nyingine ambazo hatas hivyo alikuwa hataki kuziweka bayana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Agosti 2001 mwaka huo huo 2001, chama cha siasa cha Tanzania Labour (TLP) kikaongoza maandamano makubwa ya kushinikiza Simba ajiuzulu kutokana na uamuzi wake huo wa kuwatesa maelfu ya wafanyakazi wa NASACO, ndugu na wategemezi wao.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maandamano hayo yakaungwa mkono na kundi kubwa la watu, na hoja mpya ikatolewa hapo kwamba, uamuzi huo wa serikali ulikuwa ni mbovu kabisa kwani, udogo wa kodi ambazo ilikuwa ikitarajia kuyatoza makampuni hayo binafsi ya uwakala yangeikosesha serikali kiasi cha shilingi bilioni 30 kwa mwaka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakurudi nyuma, akaendelea na msimamo wake wa kutoa leseni kwa makampuni mengine na kilio cha NASACO kikabakia kuwa ni historia. Baada ya kuonekana kuwa shujaa katika suala lile la COMESA, hili la NASACO likamwaribia sifa yake ya kuwa kiongozi msomi, mchumi mzuri na mchapakazi hodari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika miaka minne leo hii baada ya mambo hayo, kivuli cha maamuzi yake hayo na serikali bado yanamuandama yeye. Jitihada zake za kuamua kujisafisha akijenga hoja kwamba alikuwa akitekeleza uamuzi wa pamoja wa baraza la mawaziri zinaonekana kugonga ukuta.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika mwaka 2001 ukazidi kuonekana kuwa ndiyo kilele cha mafanikio yake kisiasa kwani, wakati hilo la NASACO likiwa bado halijapatiwa jibu la uhakika, akaingizwa tena katika kile ambacho mwenyewe anakataa kukiita kashfa bali sakata ya sukari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sakata hii ilihusishwa na uamuzi wake wa kutoa vibali kwa makampuni kadhaa vya kuagiza sukari nje ya nchi, lengo likiwa kukidhi mahitaji makubwa ya sukari yaliyokuwa yakilikumba tatizo wakati huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uamuzi huu wa kutoa vibali kwa wafanyabiashara hao badala ya kuwa wa manufaa, ukaonekana kuwaumiza zaidi walaji, wananchi wa kawaida. vyombo vya habari vikamwandama Simba kwa kutoa vibali hivyo kwa namna ambayo wadadisi wa mambo wakaiona kuwa ni yenye harufu ya rushwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mara ya kwanza Simba akawekwa katika mazingira magumu ambayo huko nyuma yaliwahi kumlazimisha aliyekuwa Waziri wa Fedha, Prof Simon Mbilinyi alazimike kujiuzulu uwaziri wake kwa sakata la minofu ya sukari mwaka 1997.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kawaida yake, Simba akasema alitoa vibali hivyo kwa maelekezo ya Baraza la Mawaziri kwa hiyo hakuona kama alikuwa amefanya kosa lolote la kiutendaji kwa hiyo, akakataa kujiuzulu kama alivyokuwa akitakiwa na baadhi ya watu kupitia katika vyombo vya habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwezi huo huo wa Agosti 2001, sakata hilo la sukari likaingia bungeni, mbunge wa Kwela (CCM), Chrisant Mzindakaya akaja na hoja binafsi dhidi ya Simba. Akatoa taarifa kuhusu kile alichokiona kuwa ni kashfa kwa waziri huyo, serikali na hata Chama Cha Mapinduzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akaweka shinikizo la kutaka Simba, kwanza ajiuzulu nafasi yake ya uwaziri  na pili aliombe radhi bunge kwa kulidanganya wakati alipokuwa akiwasilisha makadirio na matumizi ya wizara yake pale alipolitafuna tafuna suala zima kuhusu sakata hiyo ya sukari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza Simba akalieleza bunge bayana kwamba hata jiuzulu kwani haoni kutenda kosa lolote. Kauli yake hiyo haikuweza kumuokoa na wala haikuweza kukiokoa chama chake. Upinzani mkali ukaendelea toka ndani ya CCM na nje wakimtaka ajiuzulu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miezi mitatu baada ya kuendelea kwa mashinikizo, hatimaye Simba akaamua kujiuzulu uwaziri, akisema bayana kwamba amelazimika kuchukua uamuzi huo kwa ajili ya kuinusuru serikali yake kusambaratika na chama chake kustawi. Huo ukaonekana kuwa ni ushindi kwa wapinzani wake, kuanzia wale wa COMESA, NASACO hadi akina Mzindakaya, wana CCM wenzake na wasiokuwa wana CCM wenzake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuondoka kwake serikalini kukachukuliwa na wapinzani wake kwamba huo ulikuwa ndiyo mwisho wa safari ya kisiasa ya Simba. Hata hivyo akawa amebakia kuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM, kwa nafasi yake ya Mwenyekiti wa Taifa wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM. Kwa kweli huo haukuwa mwisho wake. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wiki ijayo tutaendelea naye tukindelea kuiangalia safari yake kisiasa, falsafa yake ya uzawa, mchango wake katika masuala ya kitaifa na kimataifa na nafasi yake kwa jumla katika kuteuliwa kuwa mgombea wa chama chake.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-114603393866546528?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/114603393866546528/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=114603393866546528&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603393866546528'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603393866546528'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2006/04/iddi-simba-mchumi-jeuri-anayeutaka.html' title='Iddi Simba; Mchumi jeuri anayeutaka urais'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114603356932192060</id><published>2006-04-25T23:35:00.000-07:00</published><updated>2006-04-25T23:39:29.456-07:00</updated><title type='text'>Mwandosya, Msomi huyu ataiweza mikikimikiki ya urais?</title><content type='html'>NI wiki ya tatu sasa tangu gazeti hili la Mwananchi Wiki Hii lianze kuwachambua, japo kwa wagombea wetu waliojitokeza kugombea urais wa Tanzania. Ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), idadi ya wagombea imeongezeka na kufikia 10, baada ya Mbunge wa Sengerema na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Dk. William Shija kujiunga katika mbio hizo za urais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wiki iliyopita tuliwaangalia Frederick Sumaye na John Malecela. Kwa kutumia makala ile, mpembuzi yeyote makini wa masuala ya siasa, angeweza kuwaweka katika mizania ya ubora wagombea hao wawili wanapolinganishwa na Jakaya Kikwete, mgombea maarufu zaidi kuliko wote na Salim Ahmed Salim, mwanasiasa anayeweza kuwa mtu anayeheshimika  miongoni mwa wenzake waliojitokeza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunaendelea na tathmini ya wagombea wengine, wiki hii tukianzia na Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Profesa Mark Mwandosya mtu anayeonekana kuwa mwanasiasa msomi na mpya, ndani ya CCM kutokana na kutokuwapo kwake katika orodha ya makada viongozi wa chama hicho, ingawa mwenyewe anatamba kwamba amekuwa kada nje ya chama hicho kwa takriban miaka 28 sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno yake mwenyewe, siku alipojitosa na kuchukua fomu ya kugombea urais, alisema bayana kwamba, kutokuwapo kwake katika uongozi wa chama hicho kwa muda mrefu tofauti na ilivyo kwa wagombea wenzake kama, Jakaya Kikwete kwa mfano,  Salim Ahmed Salim, au hata Dk Abdallah Kigoda hakuwezi kukamfaya aonekane kuwa mtu mgeni ndani ya CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si rahisi kuelewa moja kwa moja sababu hasa zilizomsukuma Mwandosya, mwanasiasa msomi wa kweli kweli, kuamua  kuingia katika mpambano wa siasa za ndani ya chama chake, akianzia na ubunge mwaka 2000, ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) kupitia Mkoa wa Mbeya (2002) na hadi kufikia hatua ya kuutaka urais (2005).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kuonekena kuwa mwanasiasa mwenye nafasi finyu ya kushinda machoni mwa watu walio nje ya CCM na pengine hata ndani ya chama hicho, iwapo atafanikiwa na kuteuliwa na chama chake kuwa mgombea wa urais, anaweza akaweka historia ya kuwa mtu aliyepata mafanikio makubwa kabisa ya kisiasa, katika kipindi kifupi cha uongozi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nini kitu gani hasa kinaweza kikawa kimemsukuma kugombea urais msomi huyo? Kuna watu wanaufananisha ugeni wake katika siasa za ndani ya CCM, na ule aliokuwa nao Rais Benjamin Mkapa wakati alipoteuliwa kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho mwaka 1995, na hivyo kumpa moyo kwamba lolote linaweza likatokea mwaka huu pia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, kinachomtofautisha na Mkapa ni kwamba, ugeni wake (Mkapa) katika siasa za ndani ya CCM haukuwa kikwazo kikubwa kwake kwani tayari alishakuwa kwa kipindi kirefu katika nyadhifa za kiserikali, bunge na ubalozi zilizokuwa zikimweka katika mizania ya ukaribu kabisa ya kupimwa uwezo wake moja kwa moja na watu wenye hadhi kubwa kama Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza, wakati Mkapa alianza kupanda akiwa Mhariri Mtendaji wa magazeti ya serikali ya The Nationalist na baadaye Daily News na Sunday News, na akaendelea na kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Habari Tanzania (SHIHATA), Mwandishi wa Habari wa Rais, balozi katika nchi kadhaa, Waziri wa Mambo ya Nje ya Nchi, Waziri wa Habari na hata kufikia kuwa Waziri wa Sayansi, Tekinolojia na Elimu ya Juu kabla ya kuteuliwa kuwa mgombea urais, Mwandosya hana historia ya namna hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, Mkapa hakuwa mgeni sana katika chama, kwani hata kabla hajawa Rais wa Tanzania, alishakuwa mbunge mapema zaidi na wa muda mrefu kuliko Mwandosya. Tatu Mkapa alipata bahati tena ya kipekee kabisa ya kuungwa mkono na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na hivyo kuwa mgombea mwenye nguvu zaidi kuliko mwingine yeyote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo ni makosa kuhusisha kutojulikana sana kwa Mkapa na Mwandosya katika duru la kisiasa kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakifanya. Itakumbukwa kwamba Mkapa aliteuliwa kuwa mbunge kwa mara ya kwanza mwaka 1977 muda mfupi tu baada ya kurejea kutoka Nigeria alikokuwa balozi wa Tanzania huko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si hivyo tu, wakati Mwandosya aliingia bungeni kwa kuchaguliwa kwa mara vya kwanza mwaka 2000, Mkapa yeye wakati huo alikuwa na uzoefu wa shughuli za bunge kwa muda mrefu tu kwani miaka 10 kabla ya hapo tayari alikuwa ameshakuwa mbunge wa kuchaguliwa wa Masasi. Mwandosya amekuwa mbunge wa kuchaguliwa kwa miaka mitano tu hadi hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pengine Mwandosya anayo sifa ya ziada inayomtofautisha na wenzake wengine kwani, miongoni mwa wagombea wote 10 waliojitokeza, idadi inayojumuisha madaktari wa falsafa watatu (PhD), wakiwamo yeye mwenyewe, Dk. Shija na Dk. Abdallah Kigoda hakuna miongoni mwao anayeweza akatamba na kusimama kwamba anafikia kiwango cha kitaaluma cha Mwandosya. Udaktari wa Salim na Malecela ni wa heshima tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni yeye peke yake ambaye amevitumia ipasavyo vyeti vyake vya kitaaluma. Kwanza akianza kwa kuwa mhadhiri wa kawaida katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaa akapanda na kufikia daraja la uprofesa wa uhandisi wa umeme na elektroniki. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si hivyo tu, akiwa msomi wa dhati kabisa, amekuwa akijihusisha na uandishi wa kiwango cha kimataifa wa vitabu na mada za kisomi (academical papers) nyingi tu ambazo hivi sasa zinatumiwa kama rejea za kitaaluma katika nchi mbalimbali duniani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika Watanzania wengi hawaijui vizuri historia ya Profesa Mwandosya na ndiyo maana wanapomweka katika mizania na wana CCM wenzake wa kiwango cha Dk. Shija, Malecela, Salim, Kikwete na hata Sumaye ambao aghalab majina yao yamekuwa yakisikika kwa miaka mingi sasa, anaonekana kuwa mgeni mno katika siasa za ndani ya chama hicho.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, kumbukumbu zinaonyesha kwamba, Mwandosya ni mmoja wa wana sayansi wa mazingira wanaoheshimika duniani kutokana na mchango mkubwa alioutoa wakati wa Mkutano wa Mazingira wa Kimataifa wa Kyoto (Japan) mwaka 1997 ulioweka viwango vya utoaji wa gesi za sumu katika viwanda katika nchi tajiri duniani kwa kiwango cha kuwakera Wamarekani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkutano huo wa Kyoto ulifanyika Desemba mwaka 1997, ukijumuisha mataifa 166 duniani ukiwa na ajenda kuu ya kuangalia namna bora kabisa ya kuhakikisha viwanda katika nchi zilizoendelea na zinazoendelea zitakavyopunguza viwango vya utoaji wa gesi ya Carbon Dioxide na nyingine ambazo zinachangia katika ongezeko la joto duniani na kuleta madhara makubwa ya kiafya na kimazingira.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni moja ya mikutano mikubwa na ya kihistoria ambayo ilijenga misingi ya mustakabali wa matumaini kwa nchi maskini (kama Tanzania) ambazo kama si nguvu ya hoja zilizotolewa na wawakilishi wa nchi zinazoendelea, basi mitazamo ya viongozi wa nchi zilizoendelea kama ule uliotolewa na Bill Clinton aliyekuwa rais wa Marekani wakati huo, ndiyo ambayo ingeendelea kutawala dunia hadi hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alikuwa ni Mark Mwandosya aliyepewa jukumu la kuwa kiongozi na msemaji mkuu wa mataifa yote masikini duniani (China na India zikijumuishwa) katika mkutano huo aliyejenga hoja dhidi ya hadaa za nchi kubwa duniani zikiongozwa na Marekani, zilizokuwa zikijaribu kuzibana nchi maskini ili nazo ziwekewe viwango vya utoaji wa gesi hizo hatari. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli ya Clinton iliyosomwa katika mkutano huo na makamu wake Al-Gore, ilikuwa ikisema bayana kwamba, Marekani ingeshiriki kikamilifu katika kupunguza uzalishaji wa gesi hizo za sumu iwapo tu nchi zinazoendelea, zingeshiriki pia katika kufanya hivyo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Clinton ambaye hoja yake ilikuwa ikiungwa mkono pia na nchi tajiri za Ulaya Magharibi ilipingwa vikali na kwa nguvu kubwa ya hoja na Mark Mwandosya ambaye alisimama na kutoa hotuba ambayo ilichangia katika kufikiwa kwa Azimio la Kyoto ambalo hadi leo hii linaheshimika kimataifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aliposimama kujibu hoja za Clinton na matajiri wenzake, Mwandosya alitoa kauli hadi hivi sasa imewekwa katika kumbukumbu za kimataifa akasema; "Wengi wetu hivi sasa tunajibidisha kufikia kiwango bora cha maisha kwa watu wetu, halafu tena anakuja mtu na kuanza kutulazimisha tupunguze uzalishaji wa gesi za sumu ili nchi zenye viwanda vingi duniani ziendelee kunufaika na maisha yao ya kawaida ya uchafuzi."&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja hiyo ya Mwandosya iliwagusa washiriki wa mkutano huo. Lilipokuja Azimio la Kyoto, hoja yake ilikuwa imeshinda na ile ya Makamu wa Rais wa Marekani Al-Gore aliyoitoa kwa niaba ya Clinton na kuungwa mkono na matajiri wenzake wa Ulaya, ikagonga mwamba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Azimio la Kyoto likasema bayana kwamba, nchi zenye viwanda (nchi tajiri duniani) zitapaswa kupunguza utoaji wa gesi za sumu kama Carbon Dioxide na Methane kwa mfano kwa kiwango cha kati ya asilimia 6 hadi 8 ifikapo mwaka 2012. Marekani ikawekewa kupunguza kiwango cha asilimia 7; nchi za Ulaya zikatakiwa kupunguza kwa asilimia 8, Japan asilimia 6. Nchi maskini zikatakiwa kujiwekea viwango vyao kwa namna zitakavyoona inafaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufikiwa kwa azimio hilo ambalo lilikuwa ni ushindi kwa nchi maskini kulisababisha Al Gore aondoke Kyoto pasipo kutia saini makubaliano hayo. Clinton pamoja na kuonyesha kuliunga mkono kwa mdomo, hakuweka bayana msimamo wa wazi wa nchi yake kuhusu suala hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Azimio hilo likamjenga Mwandosya katika siasa za kimataifa, vyombo vya habari katika nchi mbalimbali maskini duniani vikamuona kuwa balozi shupavu wa nchi maskini. Gazeti la India Express linalochapishwa Bombay likamwagia sifa likimwita, mjenga hoja bora, mtu mwenye sauti nzito ya ushawishi na balozi wa nchi za kusini anayetokea Tanzania. Watanzania hatuzijui sifa hizo za Mwandosya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si rahisi kujua ni kwa nini hasa historia hii ya Mtanzania kuongoza kundi la nchi za kusini katika mkutano nyeti wa kimataifa kama huo wa Kyoto imewekwa kapuni na kulifanya tukio lenyewe lionekane kuwa ni la kawaida, wakati Watanzania wengine waliowahi kupewa nafasi za kama hizo za kimataifa wakiendelea kutukuzwa na kuonekana wenye haiba na sifa za kimataifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huenda hilo linatokana na hulka ya Mwandosya mwenyewe kutopenda makuu au pengine linachangiwa na ukomavu wake unaomfanya alione tukio hilo la Kyoto kuwa ni la kawaida kabisa na stahili ya msomi wa kariba yake. Kwa upande mwingine hilo linaweza kuwa ni kielelezo cha mwanasiasa ambaye kwa sababu ya uchanga wake katika mchezo huo, hajui kuzichanga vyema karata zake.      &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukirejea nyumbani, Mwandosya aliingia serikalini kwanza akiwa kamishna wa Nishati katika Wizara ya Maji, Nishati na Madini mwaka 1985 na akashikilia wadhifa huo hadi mwaka 1990 alipopandishwa cheo na kuwa Katibu Mkuu katika wizara hiyo hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo basi, mwaka 1988 wakati Mwinyi alipomteua Kikwete kuwa mbunge na Naibu Waziri wa Maji, Nishati na Madini alimkuta Mwandosya akiwa kamishna wizarani hapo kwa miaka mitatu tayari, na akafanya naye kazi kwa miaka miwili mingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwaka 1990, Mwandosya alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu, Kikwete naye akapandishwa na kuwa waziri kamili katika wizara hiyo hiyo  na wakafanya wote tena kazi kwa miaka miwili hadi mwaka 1992 wakati Rais Ali Hassan Mwinyi alipomwamishia yeye (Mwandosya) katika Wizara ya Viwanda na Biashara kuendelea kwa wadhifa huo huo wa ukatibu mkuu, aliokaa nao hadi mwaka 1993 alipoondoka na kurejea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kufundisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alipoondoka serikalini na kurejea Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam katika Kitivo cha Uhandisi alikokuwa ameazimwa, maneno mengi yalisikika. Miongoni mwa mashabiki zake, walikihusisha kitendo hicho na ubabaishaji uliokithiri serikalini ambao wasomi wa kariba yake walishindwa kuumudu. Kitendo hicho kilimuondoa katika siasa za wazi na utendaji serikalini na watu wakamsahau.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si hilo tu lililosemwa, kwani inaonekana alishajenga maadui kadhaa serikalini kwani, maneno mengine yalimhusisha na kushindwa kwake kutimiza wajibu wake na hivyo kumfanya Rais Mwinyi alazimike kumrejesha chuoni na nafasi yake kuchukuliwa na mtu mwingine. Nini hasa kilitokea, ni Mwandosya mwenyewe, Mwinyi na pengine uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ndiyo wanaolijua vizuri hilo.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo uzoefu alioupata serikalini akichanganya na usomi wake ambao mtu yeyote makini anayemfahamu vyema hawezi akautilia shaka hata kidogo, ulimfanya ajione akipwaya kuendelea na uprofesa wake chuoni peke yake, pasipo kufanya jambo jingine litakalomwezesha kulisaidia taifa na ulimwengu wa kisomi katika nyanja za nishati, mazingira, sayansi na maendeleo ya teknolojia kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwaka huo huo wa 1992, akishirikiana na msomi mwingine, Profesa Mathew Luhanga ambaye pia ni Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu, waliamua kuanzisha taasisi waliyoiita, Centre for Energy, Environment, Science and Technology (CEEST) kwa kiswahili cha haraka haraka, Taasisi ya Nishati, Mazingira, Sayansi na Tekinolojia iliyosajiliwa kama kampuni. Mwandosya akawa ndiye mwenyekiti wake hadi leo hii na Luhanga akiwa Mkurugenzi Mwenza. &lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Tangu wakati huo, amekuwa akiutumia muda wake mwingi kufanya tafiti, ameandaa 'papers' nyingi tu za kisomi akaandika vitabu akishirikiana na wasomi wenzake kadhaa katika masuala mbalimbali yanayohusu nishati, mazingira na mambo mengine na hivyo kuiwezesha taasisi hiyo ambayo sasa inajulikana kama CEEST (2000) Ltd anayoingoza, hadi leo kuwa na nakala zaidi ya 3,000 za rejea za kisomi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya kuwa Mwenyekiti na Mkurugenzi wa CEEST (2000) Ltd, Mwandosya hakuondoka katika utumishi wa umma, kwani kwa nyakati tofauti aliteuliwa katika nafasi kadha wa kadha. Kwanza akawa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) moja ya taasisi zilizokuwa na nguvu kubwa wakati dola ilipokuwa ikimiliki uchumi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadaye akateuliwa kuwa Kamishna katika Tume ya Rais ya Kurekebisha Mashirika ya Umma (PSRC), asasi inayofanya kazi chini ya rais ikiwa na majukumu ya kusimamia zoezi la ubinafsishaji wa mashirika ya umma. Vile vile amewahi kuwa Mkurugenzi (asiye mtendaji) wa Standard Chartered Bank (Tanzania).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mantiki hiyo, kwa kuwa kwake kamishna wa PSRC, kwa miaka mingi tu hadi alipoteuliwa kuwa Waziri mwaka 2000, Mwandosya amepata fursa nzuri ya kujua siri za zoezi zima la ubinafsishaji, nyufa zilizomo katika zoezi hilo na namna zoezi hilo zima linavyotekelezwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kuzingatia historia hiyo, pengine ni yeye tu na Abdallah Kigoda ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mipango na Ubinafsishaji) miongoni mwa wagombea wa urais kwa tiketi ya chama hicho, wanaofahamu kwa undani ni mambo gani hasa yanatokea kabla, wakati na baada ya mashirika kadhaa ya umma kubinafsishwa.   &lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Tukiachana na uzoefu wake katika siasa, kuna haja, tena ya lazima kulifanyia tathmini, japo fupi tu kuhusu hili la yeye kuamua kugombea urais na kuuhusisha uamuzi wake huo na masuala mawili au matatu hivi yaliyokuwa yakitokea kabla hajatangaza rasmi azma yake hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kwamba haijulikani ni kitu gani kimekuwa kikitokea katika siasa za Tanzania, ukweli ni kwamba, jina la Mwandosya limeanza kuhusishwa na ajenda nzima ya urais mapema kabisa, baada ya kuteuliwa na Rais Benjamin Mkapa kuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi mwaka 2000.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si rahisi hata kidogo kuelewa kwa haraka haraka ni sababu gani hasa zilichangia kuhusishwa kwake na urais, wakati katika baraza hilo jipya mwaka 2000 kulikuwa na mawaziri wengine ambao aghalab baadhi yao walionekana kuwa na uzoefu wa muda mrefu katika uongozi katika ngazi za kisiasa na kiserikali tofauti na alivyokuwa yeye.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, ni uwezo wake mkubwa wa kazi? Ni nyota yake ing'aayo? Ni uaminifu aliojijengea kwa Rais Mkapa hata kabla hajateuliwa kuwa waziri? Ni usomi wake uliotukuka? Ni utendaji wa kazi uliovuka mipaka ya ukawaida akiwa Katibu Mkuu au katika nafasi nyingine alizowahi kuzishika huko nyuma? Ni jambo gani hasa? Watanzania tunapaswa kukuna vichwa zaidi ili kumpima barabara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Itakumbukwa pia kwamba, muda mfupi tu baada ya yeye kushinda ubunge huko kwao Rungwe Mashariki mwaka 2000 tena kwa mbwembwe nyingi na Mkapa kujihakikishia muhula wa pili wa urais, jina la Mwandosya likaanza kutajwa zaidi kuwa mtu aliyekuwa akipewa nafasi kubwa na kuteuliwa kuwa Waziri Mkuu akichukua nafasi ya Frederick Sumaye.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutajwa-tajwa kwa jina la mtu huyo ambaye alikuwa mgeni kabisa ndani ya Bunge la Jamhuri, (akiingia kwa mara ya kwanza) lilikuwa ni jambo la kushangaza. Baadhi ya vyombo vya habari vikaandika habari hiyo. Gazeti moja la Tanzania Leo (sasa halipo tena) likawa na kichwa cha habari; Mwandosya kuwa Waziri Mkuu? Kwa hakika minong'ono hiyo ilionekana kufanana na ukweli, kwani iliwahusisha hata wanasiasa ambao walikuwa katika serikali ya muhula wa kwanza wa Mkapa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitendawili kiliteguliwa siku Rais Benjamin Mkapa alipotangaza rasmi baraza lake la mawaziri. Mwandosya hakuwa Waziri Mkuu, bali Sumaye akaendelea. Hata hivyo Rais hakumwacha kando, alimteua kuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, wadhifa alioendelea kuwa nao hadi leo hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa aliukosa uwaziri mkuu, kuingizwa kwake katika baraza la mawaziri kulitafsiriwa na baadhi ya wadadisi wa mambo kwamba, huenda kweli Mkapa alikuwa na mpango huo wa kumfanya Waziri Mkuu na hilo lilivurugwa na kuvuja kwa habari hizo mapema.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Habari hizo zinaweza zikawa za kweli ama la, ingawa ushawishi wake kwa kiwango kikubwa unachangiwa na hulka ya usiri uliokithiri ya rais Mkapa ambaye huwa hapendi kuona kile anachodhamiria kikiingiliwa na kutangazwa kabla yeye mwenyewe hajatoa tamko rasmi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna yoyote ile, taarifa hizo za kumtaja kuwa waziri mkuu mtarajiwa ambazo hazikutimia na kuingizwa kwake katika baraza la mawaziri tena katika muhula wake wa kwanza bungeni, ukichanganya na usomi wake, kulimfanya aingie katika orodha ya wanasiasa wenye nafasi kubwa ya kufanya vyema katika kipindi kifupi kijacho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu walio karibu na Mkapa wamewahi kusikika wakisema kwamba, uamuzi wa Rais Mkapa kumteua tena Sumaye kuendelea na wadhifa huo, haukutokana na uchapaji kazi wa mbunge huyo wa Hanang, bali ulilenga kulipunguzia taifa mzigo wa gharama za kuwalipa marupurupu mawaziri wakuu wastaafu zaidi ya wale waliokuwapo kama; Rashid Kawawa, Joseph Warioba, Cleopa Msuya, John Malecela, Salim Ahmed Salim na halafu Sumaye mwenyewe. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukichanganya masuala hayo na uamuzi wa sasa wa Mwandosya kuamua kuchukua fomu ya kugombea urais unaweza ukapata hitimisho moja rahisi kwamba, kuna mambo kadhaa ambayo yamemuhamasisha kugombea, moja kati ya hayo likiwa ni hilo la nyota yake kuonekana iking'ara hata kabla Mkapa hajatangaza baraza la mawaziri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo alipopata uwaziri, Mwandosya alijikuta akipata wakati mgumu wizarani kwake, kwani ile sura ya kuheshimika kama msomi makini iliyomjengea staha na haiba ya kipekee ikatoweka, na badala yake yakasemwa mambo ambayo hadi hivi leo yanamweka katika njia panda kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dosari hiyo ilianza miezi mitatu tu baada ya kuingia tena serikalini yaani Februari 2001 pale serikali ilipofikia makubaliano ya kuuza asilimia 35 ya hisa zake katika Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) kwa makampuni mawili ya Mobile System International (MSI) ya Uholanzi (sasa Celtel International) ikishirikiana na Detecon ya Ujerumani kwa Dola za Marekani milioni 120.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chini ya mkataba wa uuzaji huo, wawekezaji hao walitakiwa kulipa kianzio cha Dola za Marekani milioni 60 na wakapewa vile vile jukumu la kuunda menejimenti. Wakalipa kianzio hicho na wakaunda menejimenti. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati mzozo ukiendelea kufukuta na hata kufikia hatua ya menejimenti kushtakiwa mahakamani, wawekezaji hao wakaingia katika mzozo mwingine wa pili na serikali. Wakakataa kulipa nusu ya pili ya fedha zote za manunuzi ya kampuni hiyo, (Dola milioni 60 zilizobaki) wakidai kwamba ukaguzi wa mahesabu ya mwaka 2000 ulionyesha kulikuwa na matatizo makubwa ndani ya TTCL ambayo yalisababisha kushuka kwa thamani ya taasisi yenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hiyo ikamweka Mwandosya katika wakati mgumu. Wafanyakazi wakatoa madai makali dhidi yake, wakitaka ajiuzulu kwa kushindwa kazi na kuwaacha wawekezaji 'wakihujumu' taasisi muhimu ya umma. Suala hilo halikuishia kwa wafanyakazi tu, likaenda bungeni na wabunge wakamwandama Mwandosya kweli kweli. Kwa mara ya kwanza, uwezo wa Mwandosya kama msomi mzalendo na mwanasiasa makini ukawekwa rehani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbunge wa Karatu (CHADEMA), Daktari Wilbrod Slaa, na wenzake kama Frank Magoba (CUF-Kigamboni) kwa mfano, wakamtia tumbo joto Profesa Mwandosya, wakisema ubinafsishaji wa TTCL unanuka rushwa. Wakahoji iweze mwekezaji (MSI/Detecon) anayemiliki asilimia 35 tu ya hisa akapewa menejimenti nzima. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wabunge hao wakafikia hatua ya kuufananisha ubinafsishaji huo na mikataba mibovu kama ule wa kamba katika mto Rufiji, wa umeme wa  IPTL, ule wa Mradi wa ndege za AJAS na mradi wa kuchapisha vitambulisho vya kitaifa ambao mpaka sasa haijulikani lini vitakuwa tayari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati mzozo ukiwa haujapatiwa ufumbuzi bado, taarifa zikaandikwa katika gazeti moja (siyo Mwananchi wala Mwananchi/Wiki Hii) kwamba, mtoto wa Waziri Mwandosya alikuwa ameingia mkataba wa mafunzo kazini na mwekezaji huyo wa TTCL, mkataba ambao ulimpeleka hadi Afrika Kusini ambako alipangishiwa hoteli ya kifahari na mwekezaji huyo. Hilo likapata tafsiri rahisi kwamba, mwekezaji alikuwa amemhonga waziri, ili alainike na kuridhia mambo yake 'machafu' ndani ya TTCL.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya taarifa hizo kuandikwa, Mwandosya alitafutwa na mwishoe akakubali kulitolea kauli suala hilo. Kwanza alikiri kwamba hizo zilikuwa ni taarifa za kweli, ingawa mtoto wake huyo alikuwa shuleni na alikuwa akitakiwa kupata mafunzo kwa vitendo na akapata nafasi hiyo kama mwanafunzi msomi na si mtoto wa Mwandosya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Majibu hayo yakamfanya Mwandosya Mwandosya aonekane hakushiriki kwa namna yoyote katika suala hilo la Mwanae na hata kama alishiriki lilikuwa ni jambo la kitaaluma na si la kuhusishwa na uwaziri wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mtazamo wa pili kukaonekana kuwapo na ukinzani wa kimaslahi (conflict of interests). Swali likawa Je, Mwandosya hakuona kwamba kuna dosari kwa mtoto wake huyo kupata mafunzo ya kitaaluma katika kampuni ambayo inazozana na serikali, wakati yeye ndiye akiwa kwenye kitovu cha mzozo huo? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Iwapo ni kweli kwamba mtoto wa Mwandosya alikwenda huko kama msomi na si mtoto wa waziri, kwa kibali na mkono wa heri wa baba yake, basi jibu moja ni rahisi kabisa; nalo ni kwamba Profesa Mwandosya aliwarahisishia wapinzani wake kwamba yeye hakuwa mwanasiasa makini, anayepaswa kuchukua tahadhari mapema kwa kila hatari inayoweza kumsonga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu ya kosa hilo, ataka asitake, leo hii kuna watu ambao wanaposikia Mwandosya anagombea urais wanajiuliza; Je huyu mtu anaaminika kweli? Ni msafi kwa kiwango gani? na kwamba umakini wake katika maamuzi ya msingi ni wa kiasi gani?         &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na kwa kuzingatia mazingira hayo, jitihada zake (Mwandosya) za kujaribu kutoa ufafanuzi kuhusu suala zima la ubinafsishaji wa TTCL na hilo la mwanae lilionekana kutowaingia hata kidogo wabunge, wafanyakazi wa TTCL na hata wananchi wa kawaida. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwisho wa yote, lile la mzozo wake juu ya TTCL likachukuliwa na Ofisi ya Rais (Ikulu) ambayo ikalisimamia ili kulitafutia ufumbuzi wa mwisho na wa kudumu ambao ungewatoa mashaka wadau wote. Kimsingi Mwandosya alionekana kupwaya. &lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Mwaka jana mwanzoni, Katibu Mkuu Kiongozi, Martern Lumbanga akaitisha mkutano na waandishi wa habari Ikulu na akatangaza rasmi kwamba, mzozo kati ya serikali na wawekezaji (MSI/Detecon) ulikuwa umemalizwa baada ya mkaguzi huru, John Ellison, ambaye ni mshirika wa kibiashara wa kampuni ya kimataifa ya ukaguzi ya KPMG yenye makao yake London, Uingereza kukamilisha kazi yake ambayo matokeo yake yalikubaliwa na pande zote.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika makubaliano hayo, mwekezaji alitakiwa alipe nyongeza ya Dola milioni 4.96 tu badala ya Dola milioni 60 za awali na kwamba alitakiwa pia kulipa malimbikizo ya riba yanayofikia Dola za Marekani 321,000. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tamko la Lumbanga, likamsafisha Mwandosya kwani, suala zima likawekwa wazi kwamba kulikuwa hakuna njama yoyote kati yake na wawekezaji za kuihujumu taasisi hiyo ya umma, bali tatizo lilikuwa ni 'ufu wa TTCL yenyewe' uliohalalisha ubinafsishaji wake.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, wakati mzozo wa TTCL haujamalizika, katika kipindi kile kile cha kati ya mwaka 2001-2002, Mwandosya akaingizwa tena katika mzozo mwingine. Safari hii akatuhumiwa kwa kuanza kujiandaa kwa ajili ya urais mwaka 2005 (mwaka huu) mapema kabla ya wakati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mzozo huu wa pili ulitokana na uamuzi wa mwanasiasa huyo kujivisha joho la ukada wa kitaifa wa chama chake na kupita katika mikoa mbalimbali hapa nchini akiitisha harambee za kukichangia chama, kilichompa dhamana ya ubunge. Akakusanya mamilioni ya fedha kwa staili hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili kwa kweli likawakera washindani wake kisiasa, wakahoji iweje mtu ambaye si mjumbe wa Kamati Kuu wala Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM ajitwike jukumu la kukichangishia chama, tena bila kutumwa wazi wazi na kiongozi ye yote wa juu wa chama hicho? Gazeti moja likafikia hatua ya kuweka takwimu ya fedha zote alizokusanya. Kwa hakika, kampeni zilikuwa zimeshaanza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Shutuma hizo dhidi yake aliamua kuzijibu kwa staili ya aina yake. Tofauti na alipoamua kujibu mashambulizi dhidi ya TTCL na lile la mwanae 'kufadhiliwa' na wawekezaji wa kampuni hiyo, Mwandosya alikaa kimya kwa muda na wakati fulani akakariwa akiwaeleza watu wake wa karibu kwamba, mabaya yote dhidi yake yalikuwa yana uhusiano na uchaguzi mkuu ujao. Kwa mantiki hiyo alijizatiti kukabiliana na mambo hayo. Ni kwa kiasi gani alijiandaa, vikao vya uteuzi vya CCM vitathibitisha.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taswira hiyo ya kushambuliwa mara kwa mara na mahasidi wake kisiasa hatimaye kulimfanya afikie uamuzi wa kuingia katika Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) mwishoni mwa mwaka 2002. Hiyo ikawa hatua yake ya kwanza kujiimarisha. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na mashambulizi yote hayo bado Mwandosya alibakia kuwa kipenzi cha watu wake. Wakazi wa Jimbo lake na mkoa mzima wa Mbeya wakatoka kwa maelfu kumpa pole na kumuunga mkono dhidi ya kile kilichoonekana kuwa ni juhudi za wazi za kumpaka matope na kumchafua. Wakamchagua kuwa mjumbe wa NEC kupitia mkoa huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokana na kuthamini mchango wake mkubwa alioujenga jimboni mwake na mkoani kwake pia, alikowapa shule zaidi za sekondari, akasaidia maskini wengi, akashiriki katika matatizo yake na mkewe akafikia hatua ya kuanzisha asasi ya kusaidia yatima wa ukimwi huko akaendelea kutukuzwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii  wananchi wengi wa Mbeya wanamuona kuwa yeye ndiye kiongozi wa kizazi hiki, ambaye anastahili kubeba heshima kubwa na ya kipekee ya kiwango cha (au hata zaidi ya) akina John Mwakangale, Dk. Amon Nsekela, Jeremiah Kasambala,Wilfrem Mwakitwange na Esil Mwakyambiki ambao pamoja na kuvuma kwao enzi zao hawakuwahi kujaribu kuukwaa urais. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushahidi wa hili ni rahisi kabisa kwani, wakati ule kulipokuwa na tishio la kuwapo kwa shinikizo la kumtaka kujiuzulu uwaziri kwa sababu ya sakata hilo la TTCL, wazee kadhaa wa mkoa huo walijikusanya na wakakaribia kufanya jaribio la kuandamana kwa lengo la kumuokoa mwakilishi wao huyo ambaye pamoja na kuwa ni Mbunge wa jimbo moja tu la Rungwe Mashariki, anaonekana kuwa ndiye mbunge wa mkoa mzima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Upo ushahidi wa pili wa hili. Wakati fulani na kwa kuzingatia kasi ya maendeleo kati ya Jimbo la Rungwe Mashariki analoliongoza na lile la Rungwe Magharibi linaloongozwa na Profesa David Mwakyusa, mmoja wa watu ambao hivi majuzi alimsindikiza kuchukua fomu kule Dodoma  alidiriki kusema hadharani kwamba angependa kuona majimbo hayo mawili yakiunganishwa tena na kumfanya Mwandosya kuwa mbunge wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimsingi mtu yeyote anayezifahamu vyema siasa za sasa za mkoa wa Mbeya anaweza akakueleza bayana kwamba, umaarufu wa Mwandosya umewafunika kabisa wanasiasa wenzake, mmoja kati ya watu waliofunikwa na ambao pamoja na kufanya jitihada kubwa za kujijenga na kujiimarisha anakwama ni, Profesa Mwakyusa. Si yeye tu, hata Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Gideon Cheyo ambaye ni mbunge wa Ileje, mbali kabisa kutoka Rungwe Mashariki ni mtu mwingine ambaye kivuli cha Mwandosya kinamtesa pia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati hivi sasa mgombea kama Jakaya Kikwete, Salim Ahmed Salim, John Malecela na Frederick Sumaye wanaonekana kuwa ndiyo wagombea wenye mvuto wa kitaifa zaidi, Mwandosya ndiye mtu anayeonekana kuwa na umaarufu wa kiwango hicho katika mkoa wake wa Mbeya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umaarufu wake huo ambao mwaka 2002 ulimwezesha kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa kupitia mkoa huo, ndiyo huo huo ambao umekuwa ukisababisha baadhi ya wapinzani wake kumhusisha na ukabila, jambo ambalo amekuwa akilipinga kwa nguvu zake zote kila linapoibuka. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika baadhi ya mikoa aliyokwenda kuomba wadhamini kwa mfano, ameongozana na baadhi ya watu ambao walimsindikiza kuchukua fomu Dodoma. Kwa bahati mbaya, watu hao wanatoka kule kule kwao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata kile kichotokea Moshi Mjini siku aliyokwenda kutafuta wadhamini na kuvuna mamia ya watu na kuwashangaza wengi, kina uhusiano mkubwa na nguvu zake mkoani Mbeya. Hivi nani hajui kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Hilda Ngoye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Rungwe hivi majuzi tu kabla ya kupanda cheo na kuwa mkuu wa mkoa? Uhusiano wa kikazi kati ya Mwandosya na mama huyo wakati akiwa Rungwe, umewajenga wote wawili. Kila mmoja amekuwa akimsaidia mwenzake. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo basi, Mwandosya atapata wakati mgumu kukabiliana na hoja za ukabila katika vikao vya Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na pengine Mkutano mkuu. Kimsingi akichaguliwa kuwa mgombea atalazimika kupigwa msasa mkali wa siasa za kitaifa na kuachana na sera za "mcheza kwao hutuzwa."  &lt;br /&gt;  &lt;br /&gt;Si rahisi kufahamu kwa takwimu ni kwa kiasi gani shutuma ambazo zimekuwa zikielekezwa dhidi yake zimemharibia kisiasa. Hata hivyo jambo moja ni dhahiri kwamba, ana wakati mgumu kupenya na kuteuliwa. Wanasema hakuna lisilowezekana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Atapaswa kufanya kazi ya ziada kuyashinda majina makubwa ndani ya CCM, Atalazimika kuwahakikishia mashabiki wake na wapinzani wake kwamba yeye ni mwanasiasa msomi ambaye iwapo atapewa fursa ya kuongoza anaweza akamzidi kwa ubora Benjamin Mkapa katika medani ya kitaifa na kimataifa.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-114603356932192060?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/114603356932192060/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=114603356932192060&amp;isPopup=true' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603356932192060'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603356932192060'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2006/04/mwandosya-msomi-huyu-ataiweza.html' title='Mwandosya, Msomi huyu ataiweza mikikimikiki ya urais?'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114603306831154929</id><published>2006-04-25T23:23:00.000-07:00</published><updated>2006-04-25T23:31:08.586-07:00</updated><title type='text'>Wajua ni kwa nini Sumaye na Malecela wanagombea, wanagombewa?</title><content type='html'>Hii si ajenda mpya. Tunawajadili wagombea wa urais waliojitokeza. Sasa wamefikia tisa baada ya Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Patrick Chokala kuuangana na wenzake wanane wa awali. Jumapili iliyopita tuliwachambua japo kwa muhtasari, Salim Ahmed Salim, Jakaya Kikwete na John Samwel Malecela kama majina makuu matatu yanayochuana kuwania urais wa Tanzania hivi sasa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukaangalia uwezekano wa Dk. Ali Mohammed Shein kugombea na kubadili mwelekeo mzima wa mambo. Kwa nahati mbaya au njema bado hajachukua fomu hadi hivi sasa. Tukamdurusu  Frederick Tluway Sumaye ambaye kuingia kwake katika kinyang'anyiro hiki kunafanya uwanja wa mapambano kuwa na majina makubwa manne yenye nguvu ndani na nje ya chama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wagombea hao wanne, Salim, Kikwete, Malecela na Sumaye wanajivunia historia zao. Kila mmoja kwa wakati wake, ukimwacha Jakaya Kikwete amewahi kushika nafasi za juu serikalini. Wote kwa nyakati tofauti, wamewahi kuwa mawaziri wakuu wa Tanzania, Salim (1984-85), Malecela (1990-1994), Sumaye (1995-hadi sasa).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nafasi zao kitaifa ama za kimataifa za sasa na zile walizowahi kuzishika huko nyuma, ndizo msingi uliowapa jeuri ya kuamua kujaribu bahati za kukipata kiti kitukufu cha urais ambacho kinyang'anyiro chake tena ndani ya chama kimoja kinaonekana kutokuwa ni ushindani tu wa kawaida, bali wa kweli kweli unaohusisha watu kukabana makoo na pengine kulifanya kuwa zoezi la kufa na kupona.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pengine kikubwa ni kwamba, wagombea kama Sumaye na John Malecela ambao ni wajumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho kwa nyadhifa zao, wameipata jeuri ya kupigania nafasi ndani ya chama chao, kwa sababu wanayo matumaini makubwa kutoka kwa wapiga kura wao ambao ni, wajumbe wenzao wa Kamati Kuu, Halmashauri Kuu ya Taifa na wale wa Mkutano Mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matumaini ya Malecela na Sumaye kwa mfano yanachangiwa na mambo kadhaa, moja kati ya hilo ni namna walivyoshinda 'kwa kishindo' nafasi walizogombea mwaka 2002 wakati uchaguzi wa ndani ya chama hicho uliofanyika Dodoma. Malecela alivuna maelfu ya kura za umakamu uenyekiti wa CCM-Bara wakati Sumaye akaongoza kundi la wagombea wa nafasi 20 za ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) akiwapiku makada wenzake wote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miongoni mwa watu ambao waliachwa kwa mbali na Sumaye ni Jakaya Kikwete. Matokeo hayo yalizusha majadala mkubwa miongoni mwa wana CCM na wasio wana CCM. Wengine waliyaita matokeo hayo kuwa ni "Kura za Kiitifaki" huku baadhi ya watu wakiyaona kuwa ni daraja muhimu la kuwapeleka akina Sumaye na Malecela katika nuru ya kutwaa nafasi ya kuteuliwa na chama hicho kugombea urais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika sehemu ya jeuri ya sasa ya Sumaye kugombea pasipo kutishwa na yeyote, inachangiwa na matokeo hayo. Hana wa kumhofia tena, kwani mtu pekee miongoni mwa wagombea ambaye angeweza kumtia joto ni huyo Kikwete ambaye vikao hivyo hivyo mwaka 1995 vilimkubali kwa kiwango kikubwa na kukaribia kabisa kumwezesha kuteuliwa kuwa mgombea wa urais wa CCM.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande wa Malecela itakumbukwa kwamba, kabla matokeo hayo hayajatangazwa, minong'ono iliyokuwa nje ya ukumbi wa Chimwaga ulioko nje kidogo ya mji wa Dodoma ulikofanyika uchaguzi huo mwaka 2002 ilikuwa ikidai kwamba, kulikuwa na mipango mahususi ya kumuangusha katika nafasi yake hiyo ya umakamu wa uenyekiti na kumpa mwana CCM kijana kuchukua nafasi yake. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hilo kwa hakika halikutokea. Malecela alishinda kwa kishindo. Pamoja na kwamba hakupata asilimia 100 ya kura zilizopigwa kama ilivyokuwa kwa Makamu mwenzake wa upande wa Zanzibar, Amani Abeid Karume bado aliwathibitishia wapinzani wake kwamba, yeye bado ni jemedari wa mapambano ndani ya CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kabla ya uchaguzi kufanyika, kampeni za waziwazi kati ya makundi ya vijana na wazee zilisikika zikipigwa. Baada ya matokeo kutangazwa na Malecela kuibuka mshindi, huku Mwenyekiti wa Taifa wa Vijana,Emmanuel Nchimbi akianguka katika kupata ujumbe wa NEC, wazee walipata ahueni na matokeo hayo yakaonekana kuwa ni fundisho kwa vijana walioonekana kuwa na ari kubwa. Vita hata hivyo haikuisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mara baada ya matokeo yote kutangazwa, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na kada mkongwe wa chama hicho, Kingunge Ngombale Mwiru alitoa hotuba nzito. Alisema bayana kuhusu kuwapo kwa mgawanyiko wa kimakundi kati ya wazee na vijana na akayaasa makundi hayo mawili kufanya kazi kwa kwa pamoja na kwa kutegemeana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna yoyote ile, matokeo hayo ya mwaka 2002, ndiyo yaliyowapa jeuri Sumaye na Malecela kila mmoja kuingia katika kusaka ili ateuliwe kuwa mgombea urais kupitia CCM, wote wakijua kwamba wajumbe waliowapa kura nyingi takriban miaka mitatu iliyopita ndiyo hao ambao watakuwa na jukumu la kupitisha jina moja la mgombea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo hayo kimsingi yalimtembeza kifua mbele Sumaye na hata wasaidizi wake walisikika wakitamba bayana kwamba, 'mzee (Sumaye) hatadharauriwa tena, kwa kuwabwaga wapinzani wake na kuthibitisha kwamba kashfa alizokuwa akizushiwa za kuwa kiongozi legelege na anayebebwa tu zilishindwa kumbomoa ndani ya  chama hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vita hiyo ya uzee na ujana haikumalizika na hata leo hii bado inaonekana kumwandama Malecela hii. Kwa namna mambo yanavyokwenda hoja hiyo inaonekana kukosa nguvu na kinachobaki ni kumchambua mgombea huyo kwa hulka yake kama mwanasiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Malecela ameamua kufa au kupona kukabiliana na hoja hiyo ya uzee kwa hoja. Anawashangaa wanaomwita mzee wakati wakijua vyema kwamba ameshawathibitishia kwa vitendo kama yeye ni mwanasiasa mpambanaji, anayefanya kazi mchana na usiku kukabiliana na wapinzani na maadui zake wa ndani na nje. Amekuja na hoja nyingi za kuikabili, amejifananisha na embe bivu na sasa anataka atambulike kama Mzee Ushindi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo suala moja ni dhahiri hivi sasa kwamba, kuna wazee na vijana wanaomuunga mkono na kuna watu wa makundi hayo hayo wanaompinga. Kimsingi hoja hii iwe ni ya maana au la ina athari zake. Ama itamjenga na atapigiwa kura za kuipuuza hoja yenyewe, au atapata zile za huruma na za kuwahukumu wapinzani wake au itatumika kumnyima kura yeye na kuwapa vijana wake.    &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapinzani wake ndani ya CCM wamebakiza hoja kuu moja. Wanapaswa kumpima kwa vigezo vingine. Wanatakiwa kurejea maandiko ya Baba wa Taifa dhidi yake na kuhoji iwapo kweli Malecela ni kiongozi ambaye hana msimamo thabiti katika masuala ya msingi. Wanapaswa kumwangalia iwapo mawazo na hoja zake ni vitu vinavyokwenda sambamba na mabadiliko ya dunia ya sasa ya utandawazi, vita dhidi ya ugaidi, ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara na nchi jirani au la!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanalazimika kumpima Malecela kwa mantiki ya uwezo wake katika kuimarisha mahusiano mema kitaifa na kimataifa, kushamirisha demokrasia na kwa jumla wanatakiwa kumweka katika tanuru moja na wagombea wenzake na kuwachambua kwa kuzingatia vigezo 13 vilivyowekwa na chama hicho ambavyo vyote havisemi iwapo umri ni sifa ya ziada au kikwazo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Malecela ana nguvu ya pili ambayo inampa jeuri, hii imejengwa si kwa sababu nyingine bali na hulka na uzito wa majukumu ya kazi ya mwenyekiti wake, Rais Mkapa. Nguvu hii ya mwenendo wa mambo unaweza ukaiita 'Coincidental Strength' ndiyo aliyoitumia kujijenga na sasa anaifanya silaha yake ya kutwaa urais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kipindi cha miaka 10 ya utawala wake, Rais Benjamin Mkapa ameutumia vyema utaratibu wa mgawanyo wa madaraka. Muda wake mwingi  ameutumia kujenga misingi imara ya utawala bora katika serikali yake, kwa kurejesha nidhamu ya kazi na matumizi ya fedha za umma, kuimarisha ukusanyaji wa mapato, kupunguza mfumuko wa bei, kuimarisha huduma za kijamii kama elimu na kurejesha heshima ya Tanzania katika jumuiya ya kimataifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati akifanya hayo akamwacha Philip Mangula ambaye ndiye mtendaji mkuu wa chama asimamie shughuli zote za kila siku za chama na Malecela akawa ndiye mpiga debe wake mkuu. Ni Malecela aliyepewa jukumu la kuongoza kampeni za ubunge na udiwani za chama hicho katika maeneo mbalimbali. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akautumia upiga debe wake huo kujijengea ukaribu mkubwa zaidi na wanachama wa chama hicho na viongozi wenzake ndani ya CCM, kwa akawa karibu zaidi na wajumbe wenzake wa Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na hata mkutano mkuu. Hilo likamwezesha kujitwalia jeuri ya ujemedari katika mapambano ya kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yeye mwenyewe tayari ameshaanza kuutumia upiga debe wake huo kama silaha yake kubwa ya ushindi. Amewahoji wale wanampinga wakidai yeye ni mzee ni kwa nini wanampa sifa hiyo sasa wakati wamekuwa wakimuunga mkono kila alikokwenda kuimarisha chama au kuongoza mapambano yawe ni ya ubunge au udiwani. Kwa maneno yake mwenyewe mara kadhaa tangu achukue fomu ya urais amesikika akisema; "Mbona alipokuwa dalali katika kampeni za chama chake alizozifanya usiku na mchana hakuna aliyejitokeza na kumwita mzee!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya sana, baadhi ya vyombo vya habari vimeingia katika mtego wa wapinzani wa Malecela na kujikuta wakiitumia hoja za uzee kumpinga. Kwa sababu ya kuibeba juu juu hoja hiyo, wanashindwa kuitumia dhidi ya wagombea wengine kama Iddi Simba (71) ambaye wanapishana na 'mzee mwenzake' huyo mwaka mmoja tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kinachooneka kuwashinda wanaompinga Malecela ni kushindwa kwao kutambua kwamba tatizo lale si uzee wake, bali  hulka yake kukosa uvumilivu, kutoa kauli za ajabu ajabu na kukaa madarakani muda mrefu kiasi cha jina lake kukinai masikio yao. Lakini ukizungumza na wapinzani wake hao watakueleza wasiwasi mkubwa walionayo juu yake. Wanasema yeye ni mtu asiyesamehe na mwenye kisasi. Hajamsamehe nani au ni yupi aliyemlipiza kisasi ni mambo yasiyowekwa bayana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na yote hayo, wanaomuunga mkono ndani ya CCM wanasema, Malecela anaonekana kuwa na nguvu kubwa ndani ya CCM kwa miaka mingi sasa. Huenda ni wasiwasi huo wa yeye kuwa na nguvu hizo ndiko kulikomtisha hata Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere mwaka 1994 na akatumia kosa lake la kucheza na muungano kumwadhibu na kuhakikisha kwamba haupati urais. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapambe hao wa Malecela wanasema kwamba nguvu kubwa ya mwanasiasa huyo ndiyo iliyosababisha wapinzani wake wakatafuta kila aina ya hoja, iwe ni ya maana au la kumshambulia, kumchafua na kumwondoa kabisa katika orodha ya rais mtarajiwa. Kwa sababu hiyo wakamwita mzee, mtu asiye na msimamo katika masuala ya msingi, mwanasiasa aliyechukiwa zaidi na Mwalimu Nyerere ilimradi tu apoteze ari ya kuendelea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huyu si mtu wa kumpuuza hata kidogo, anaweza akafanya lolote. Anayo nafasi kubwa ya kuteuliwa ingawa kabla hajafikia hatua hiyo anapaswa kuwathibitishia wana CCM wenzake wanaomuunga mkono na wanaompinga kwamba yeye ni mtu makini, wa kauli na matendo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli zake za hivi karibuni zimemweka katika sura kuu mbili, upande mmoja zimethibitisha kwamba yeye ni gwiji la siasa za ndani ya CCM. Alipokuwa akichukua fomu aliwathibitishia wana CCM wenzake kwamba kweli yeye ni mwanasiasa mwenye uwezo wa kupambana pasipo kukata tamaa, mpiganaji asiyechoka na mwanaharakati asiyekata tamaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande mwingine Malecela baada ya kutoa kauli nzito zilizompa heshima wakati akichukua fomu akarejea kule kule kwa awali, akaja tena na kauli za kitatanishi. Akamponda waziwazi mmoja wa wagombea wenzake wa urais bila ya kumtaja kwamba anatafuta umaarufu kupitia katika vyombo vya habari. Akaeleza kukerwa na namna mgombea huyo anavyofananishwa na tsunami. Akairejesha taswira ile tuliyoizungumzia wiki iliyopita ya kauli za kitatanishi ambazo aghalab zimekuwa kero kwa wana CCM wenzake.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-114603306831154929?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/114603306831154929/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=114603306831154929&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603306831154929'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603306831154929'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2006/04/wajua-ni-kwa-nini-sumaye-na-malecela.html' title='Wajua ni kwa nini Sumaye na Malecela wanagombea, wanagombewa?'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114603248761859954</id><published>2006-04-25T23:09:00.000-07:00</published><updated>2006-04-25T23:21:27.650-07:00</updated><title type='text'>Urais: Sifa, uwezo, hoja au haiba?</title><content type='html'>Makala hii ni sehemu ya mfululizo wa makala nilizoandika wakati wa mchakato wa ndani ya CCM wa kumtafuta Rais wa Nne wa Tanzania mwaka 2005 na ambazo kwa kiwango kikubwa zilionyesha namna kila mgombea alivyokuwa na nafasi yake katika kushinda nafasi hiyo ambayo hatimaye ilimwangukia Kikwete&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;MAJINA makubwa yamejitokeza kuwania urais wa Tanzania. Salim Ahmed Salim, Jakaya Mrisho Kikwete , John Samwel Malecela na Frederick Tluway Sumaye. Bado jina moja kubwa linasubiriwa, nalo ni la Dk. Mohammed Ali Shein kukamilisha orodha ya 'mabwana wa vita'&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wagombea hao wanaingia wakijivunia rekodi zao za utendaji wa kazi, nyadhifa walizowahi kushika, hadhi walizojijengea, staha walizopata maishani na kikubwa namna kila mmoja wao alivyotoa mchango wake kwa ajili ya maendeleo ya taifa lake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dk. Salim (63) anaingia katika kinyang'anyiro hicho akijivunia uzoefu wake wa takriban miaka 41 ya utumishi uliotukuka, unaojumuishwa na uongozi wa kitaifa uliompandisha kwa kiwango cha kufikia kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania na ule wa kimataifa uliomfikisha Umoja wa Mataifa na akakaribia kabisa kuutwaa ukatibu mkuu wa umoja huo, kabla hajachaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa uliokuwa Umoja wa Nchi za Afrika (OAU) mwaka 1989. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uzoefu huo ambao kwa miaka mingi umemuweka nje ya Tanzania, aghalab ndiyo uliomjengea pia heshima nyumbani na kumuwezesha vile vile kushika nyadhifa kubwa za Uwaziri Mkuu wa Tanzania, Naibu Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Nje na Waziri wa Ulinzi kwa nyakati tofauti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu wanaomuunga mkono wanaamini kwamba, Dk. Salim mwenye umri wa miaka 63 sasa  ndiye mtu anayestahili kuchukua nafasi ya Mkapa Oktoba mwaka huu, kwani ndiye mtu pekee wa daraja la juu kabisa kitaifa ambaye haiba yake inamfanya aheshimike Tanzania, Afrika na duniani kote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mujibu wa watu hao, hata kabla ya enzi za uhai wa Baba wa Taifa, akiwa Rais wa Tanzania na baada ya hapo, Salim ndiye aliyekuwa mtu wake nambari moja, akiwazidi watu kama, Benjamin Mkapa, John Malecela ukimwacha Waziri Mkuu wa zamani, Hayati Edward Moringe Sokoine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Duru za kisiasa ndani ya CCM zinasema kwamba, mara mbili, mwaka 1985 na 1995, yeye ndiye aliyekuwa chaguo la kwanza la Mwalimu kwa nafasi ya urais wa Tanzania na mara zote nafasi hizo zilichukuliwa na watu tofauti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwaka 1985, Salim alijikuta akiuokosa urais 'kwa bahati mbaya' baada ya Mwinyi aliyekuwa Rais wa Zanzibar wakati huo na Makamu wa Rais kumpiku baada ya makundi kadhaa ya ndani ya chama hicho kumpinga na kumuunga mkono mpinzani wake huyo (Mwinyi). &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mambo hayakuishia hapo, mwaka 1995 tena wakati akiwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi za Kiafrika (OAU), inasemekana Mwalimu Nyerere alitaka tena kuona taifa hili likiongozwa na Salim. Ujumbe wa watu ulikwenda Adis Ababa kumshawishi. Yeye akataa kurejea nyumbani kugombea nafasi hiyo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapambe hao wa Salim ambao baadhi yao walimfuata hadi Addis Ababa kumshauri arejee ili kugombea wanaamini kwamba yeye ndiye aliyekuwa chaguo nambari moja la Mwalimu akiwatangulia Rais Benjamin Mkapa na Jakaya Mrisho Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mantiki hiyo basi, ukimwondoa Mkapa ambaye tayari ameshamaliza muhula wake wa vipindi viwili vya miaka mitano mitano, ni Dk. Salim na Kikwete pekee ambao wanaingia katika kinyang'anyiro hicho cha urais wakiwa na historia hiyo ya kuwahi 'kunusa harufu'  ya kuteuliwa kupitia CCM.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Turufu na pengine kikwazo kwake anachoonekana kubeba Dk. Salim safari hii ni Uzanzibari. Kauli aliyoitoa Dodoma juzi wakati akichukua fomu kwamba alisita kugombea mwaka 1995 kwa sababu alikuwa akiamini ilikuwa ni zamu ya Watanzania Bara ina maana kubwa moja kuwa, sasa hivi ni zamu yao Wazanzibari kwani rais anayeondoka ni wa Tanzania Bara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli hii ya Dk. Salim huko nyuma ilishawahi kuzua maneno ndani ya CCM kiasi cha kumlazimisha Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Rais Benjamin Mkapa kuitolea kauli pale alipotamka bayana kwamba, hakuna mahali popote katika Katiba ya CCM na ile ya nchi panaposema kwamba urais ndani ya chama hicho utakuwa ni wa kupokezana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa misingi hiyo, ni yakini kwamba, hoja ya zamu itakuwa ni moja ya mijadala ndani ya chama hicho, Wazanzibari wakiamini ni zamu yao, huku wale kutoka Tanzania Bara wakiungana na mwenyekiti wao kuupinga msimamo huo ambao ama kwa bahati mbaya, au desturi umefanya kazi katika awamu tatu zilizotangulia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo hoja hiyo ya zamu au urais wa kupokezana kwa maana ya Bara na Visiwani, inapata nguvu unapoiangalia CCM kama chama pekee kisicho na ushindani na pengine ingeendelea kuwa na nguvu kama mfumo wa vyama vingi ungekuwa haujaanza bado. Tayari vyama vya CUF na TLP kwa mfano vimetangaza majina ya wagombea wake ambao wote ni Wabara. Iwapo itatokea kimoja kati ya vyama hivyo kikashinda, kutakuwa na mantiki ya zamu za Uzanzibari na Utanzania Bara kwa CCM?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pengine hoja hiyo ya Salim inaweza ikaonekana kuwa na kasoro moja kubwa. Hivi leo Watanzania wengi wanamuona Rais wa Jamhuri ya Muungano kuwa mtawala wa bara zaidi kuliko visiwani, pamoja na kwamba anachaguliwa kwa kura za pande zote mbili za muungano. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mantiki hiyo basi wanaona kwamba Mbara ndiye mwenye nafasi kubwa zaidi ya kupewa urais wa muungano na Wazanzibari wakaachia ile ya umakamu wa rais na pia ya Rais wa Zanzibar wanayoipata moja kwa moja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja hizo hata hivyo zinaweza zikaonekana kuwa nzuri tu kimantiki ingawa kwa maana ya umadhubuti wa muungano zinaweza zikawa chachu kuu ya kuendelea kumomonyoka kwa ukuta wa mshikamano kati ya Tanzania Bara na Zanzibar, ukuta ambao katika miaka ya hivi karibuni unaonekana kubomoka pole pole. Kwa maana hiyo hata ile kauli ya Mkapa kupinga ajenda ya zamu inaweza ikaonekana kukosa nguvu.      &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, pamoja na kuonyesha mwelekeo huo, Dk. Salim ameeleza bayana kupinga ubaguzi katika zama hizi za utandawazi na akawaita wajinga wale wanaojaribu kuwabagua, Wazanzibari katika misingi ya Uunguja na Upemba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alisema huwezi kumkuta mzaliwa wa Unguja asiye na mchanganyiko wa Pemba wala Mpemba&lt;br /&gt;asiye na mchanganyiko wa Unguja. Akitoa mfano alisema, yeye binafsi alizaliwa Unguja na kukulia Pemba, kutokana na mama yake kuwa Muunguja na baba Mpemba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mujibu wa hoja ya Salim kigezo na sifa kuu ya kugombea uwe ni Utanzania wa mgombea, uwezo wake na sifa 13 zilizoandaliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) mwaka jana na siyo Uzanzibari, Uzanzibara, Uunguja, Upemba au pengine Utanzania Bara. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huyo ndiye Dk. Salim mwenye mke mmoja, Amne na watoto watatu, Maryam, Ali na Ahmed ambaye amesema bayana kwamba, iwapo atashinda, suala la msingi kuliko yote, litakuwa ni kuimarisha mshikamano, udugu na umoja wa Watanzania na muungano wa Tanganyika na Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alizaliwa Januari 23, mwaka 1942, aliteuliwa kuwa balozi akiwa na umri wa miaka 22. Tangu wakati huo akawa balozi katika nchi mbalimbali kabla ya kurejea nyumbani na kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kuanzia mwaka 1980 hadi 1984.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwaka 1970, Dk. Salim aliteuliwa kuwa Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, nafasi ambayo aliishikilia kwa karibu miaka 10. Baada ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Moringe Sokoine Aprili 12, 1984, Mwalimu Nyerere alimteua kuwa Waziri Mkuu, nafasi ambayo aliishikilia hadi mwaka 1985.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aliteuliwa kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, mara baada ya Mwinyi kuingia madarakani nafasi ambayo aliishikilia hadi alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa OAU mwaka 1989. Alimaliza muda wake kuwa Katibu Mkuu wa OAU Septemba mwaka 2001 baada ya kutumikia kwa miaka 12. Hivi sasa Dk. Salim ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Hubert Kairuki. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanaomuunga mkono wanaamini kwamba, Salim anaweza akakabiliwa na ushindani wa kweli na wa dhati kwa mantiki ya sifa, uwezo, staha, uzoefu na haiba ya kisiasa ndani ya chama hicho na mgombea mmoja au wawili tu ambao ni Malecela na hasa hasa, Jakaya Kikwete, kada wa muda mrefu wa TANU na baadaye CCM, mtu aliyeshika wadhifa wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano kwa muda mrefu kuliko mwanasiasa mwingine yoyote hapa nchini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati Dk. Salim akijivunia uzoefu mkubwa wa kidiplomasia, Kikwete anamzidi kwa kuwa mwanasiasa kada wa kukulia ndani ya chama chake akianzia TANU na baadaye CCM kabla hajaingia serikalini na kushika nyadhifa za unaibu waziri wa Maji, Nishati na Madini na baadaye akaupata uwaziri kamili katika wizara hiyo hiyo kabla hajahamishiwa Wizara ya Fedha na akawa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa tangu mwaka 1995.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati Kikwete anaweza akaonekana kuwa mwana TANU na CCM kwa kuzaliwa, Salim yeye analikosa hilo kwani, huwezi ukamuweka katika kundi la waasisi au vijana wa Afro Shiraz Party (ASP), chama kilichopigania ukombozi wa Mwafrika Zanzibar na kuleta mapinduzi, kabla hakijaungana na TANU na kuzaa CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siasa za chuki za kihistoria za Zanzibar zinazojieleza hadi hivi leo kati ya CCM na chama cha CUF, ni ushahidi mmoja tu kwamba ni rahisi kwa Wazanzibari wenzake kumuweka katika kundi la wapinzani wa asili wa Hizbu. Sababu ya kufanya hivyo ni rahisi kwamba alikuwa mwanachama wa chama cha UMMA kabla hajajiunga na ASP. Mahusiano ya kihistoria ya awali yanakiweka pamoja UMMA Party na U-HIZBU (chama cha Ki-sultani).        &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya hilo, Dk. Salim ambaye amekuwa kiongozi ndani ya nchi kati ya mwaka 1980 na 1989 anaonekana kuwa mwanadiplomasia zaidi kuliko alivyo mwanasiasa totauti na Kikwete ambaye amekuwa ndani ya nchi kama kiongozi wa chama na serikali kwa takriban miaka yote 30 ya utumishi wake na 10 kati ya hiyo akipata uzoefu wa masuala ya mahusiano ya kimataifa ambayo kimsingi ndiyo nguzo kuu kabisa ya mafanikio na heshima aliyojijengea Dk Salim.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Fursa aliyopata ya kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kwa miaka 23, kuwa kwake mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho kwa miaka tisa, moja ya vikao vyenye nguvu kubwa ya maamuzi ndani ya chama hicho ambacho muundo wake unatokana na miundo ya vyama vya kisoshalisti duniani ni silaha nyingine muhimu ya ushindi wa Kikwete dhidi ya wagombea wengine wa chama hicho, ukimwacha John Samwel Malecela.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hiyo haitoshi, kuwamo kwake katika Baraza la Mawaziri kwa takriban miaka 17 sasa ni changamoto nyingine kubwa ya ufahamu wa namna serikali inavyofanya kazi katika kipindi hiki cha mabadiliko makubwa ya kisera, kitaifa na kimataifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno yake mwenyewe Kikwete anasema; "Miaka 10 ya kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi yetu, kumeniwezesha kujifunza kwa nini baadhi ya nchi zinapata mafanikio na wengine kushindwa," kauli ambayo inaonyesha namna alivyo na kile ambacho Salim na yeye kinawafanya wawe tofauti na wagombea wengine wote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na ukweli kwamba, John Malecela anao pia uzoefu huo wa masuala ya kidiplomasia ambao aliupata kwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na balozi wa Tanzania katika nchi kadhaa wakati wa uongozi wa Awamu ya Kwanza, bado hawezi kuwafikia washindani wake hao wawili ambao mahitaji ya kimataifa ya wakati huu wa dunia ya utandawazi yanatofautiana sana na yale ya Zama za Vita Baridi na Ubaguzi wa Rangi ambazo yeye (Malecela) alionekana kuwa mwanadiplomasia mahiri na anayeheshimika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tofauti hiyo ya kisera ya vita baridi na ya sasa ya soko huria, ndiyo inayomweka Salim juu zaidi ya Kikwete, Malecela, Iddi Simba na wagombea wote wengine kutokana na ukweli kwamba, yeye ndiye mtu pekee kati yao, aliyepata fursa kuliko mwingine yoyote, kufahamu kwa undani sera za kimataifa za dunia ya sasa na ile ya kabla ya hapo ambayo falsafa kuu mbili za mrengo wa kushoto na kulia zilikuwa zikisigana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiacha uzoefu wa kisiasa na kidiplomasia, Kikwete anaonekana kuwa na sifa nyingine ambayo pengine wengine hawana, sifa ambayo kimsingi ndiyo inayomfanya awe mgombea maarufu zaidi kuliko wengine wote, umaarufu unaoonekana kuwa heri na kero vile vile. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni  jambo la wazi kwamba, watu ambao wamekuwa wakimuunga mkono Kikwete, tangu mwaka 1995 wamekuwa wakimuona kama mgombea anayewakilisha mawazo ya kizazi kipya cha Watanzania na mtu anayeweza akawa daraja la mahusiano kati ya wazee wastaafu na vijana wenye uchu wa kutaka kupewa nafasi ya kuongoza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na ukweli kwamba, Kikwete anapogombea hivi sasa ana umri wa miaka 55, vijana na wana CCM wanaoungana na falsafa ya Baba wa Taifa ya kuwataka wazee wang'atuke madarakani wanamuona kuwa ndiye chaguo lao sahihi kabisa la 'wakati huu' pamoja na ukweli kwamba, watu wa rika lake kama vile Frederick Sumaye (55) na Mark Mwandosya (57) wanaonekana kuwa ni wa kizazi kingine na tena waliochomoza kwa bahati mbaya tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mzee Peter Kisumo (71), mmoja wa watu wanaomuunga mkono Kikwete na mtu aliyekuwa kiongozi wa hadi kufikia ngazi ya ukuu wa mkoa na uwaziri katika serikali ya awamu ya kwanza na ambaye sasa ni mdhamini wa CCM anaamini kwamba watu wa umri wake kama walivyo akina Iddi Simba (70) na John Malecela (71) wamechoka na wanapaswa kupumzika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali moja hadi hivi sasa linaonekana kutojibiwa sawasawa. Ni kwa nini basi miaka 10 baada ya kugombea urais kwa mara ya kwanza mwaka 1995, Kikwete bado anaonekana ndiye mwakilishi wa Watanzania wa kizazi hiki na mtu anayeonekana kufaa zaidi kuongoza taifa katika karne ya 21 zaidi kuliko ilivyo kwa wengine kama hao akina Sumaye, Mwandosya kwa upande mmoja na hata akina Malecela, Salim, Iddi Simba kwa upande mwingine. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je ni hulka yake ya kujichanganya na watu wa rika tofauti? Ni haiba yake ya ujana aliyodumu nayo kwa miaka yote 10 tangu mwaka 1995? Ni upofu wa mashabiki zake? Ni upeo wake mkubwa wa kuona mambo? Ni hoja zake za kisasa? Ni uzalendo wake? Ni mapungufu waliyonayo washindani wake? Ni kitu gani hasa? Watanzania wanapaswa kuliangalia hilo na kulitafutia majibu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi karibuni taasisi mbili tofauti moja ya vyombo vya habari na nyingine ya kitaaluma zilifanya tafiti zake na zote zilipata majibu yanayolingana kwamba Kikwete ndiye aliyekuwa mwanasiasa maarufu zaidi kwa ajili ya kugombea nafasi ya urais akifuatiwa na akina Prof. Haruna Lipumba, Dk. Salim Ahmed Salim na wengine kadhaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwingine ni John Samwel Malecela, mkongwe huyu wa siasa. Anajivunia rekodi yake na ni rekodi hiyo hiyo inayomtia katika hatihati ya kumfanya ateuliwe kuwa mgombea wa CCM dhidi ya wagombea wengine kama Dk. Salim na Kikwete kwa mfano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anayo rekodi nzuri ya utendaji wa kazi serikalini na katika chama na pia ana rekodi ya kuonekana kukosa msimamo thabiti katika masuala ya msingi (rejea Kitabu cha Mwalimu Nyerere cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika Malecela ni 'mwanadiplomasia wa kihistoria' wa kiwango cha Salim Ahmed Salim pengine na ndiyo maana  aliteuliwa na Jumuiya ya Madola kuunda timu ya wanadiplomasia mashuhuri duniani waliopewa jukumu la kuushawishi uliokuwa utawala wa kibaguzi nchini Afrika Kusini kuachana na sera zake za kikandamizaji, akiwa miongoni mwa watu maarufu duniani kama rais wa sasa wa Nigeria Olusegun Obasanjo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si hilo tu, tangu mapema kabisa mwa miaka ya 1970, Malecela amekuwa mmoja wa wanasiasa waliokuwa wakiunda baraza la mawaziri katika wizara mbalimbali zikiwamo za Mawasiliano na Uchukuzi hadi ile ya Mambo ya Nje. Ameiwakilisha Tanzania nje ya nchi kwa muda, amekuwa mkuu wa mkoa na akapanda hadi kufikia kuwa Waziri Mkuu na baadaye Makamu wa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM (Tanzania Bara).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya kwake au nzuri, tofauti na ilivyo kwa wagombea kama Salim na Kikwete, uongozi wake umekuwa ni wa misukosuko mingi. Wakati fulani wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere, katika hali ya kushangaza Malecela aliondolewa serikalini akarejea mtaani kwa miaka kadhaa akiwa hana madaraka yoyote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Malecela ambaye kabla ya kuondolewa katika Baraza la Mawaziri na Mwalimu mwanzoni mwa miaka ya 1980 alikuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi alijikuta akiingia katika wakati mgumu kutokana na kauli yake ya 'You can Go to Hell' (tafsiri isiyo rasmi 'Nendeni hata Kuzimu) aliyoitoa dhidi ya watu walioanzisha upinzani wa hoja dhidi yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli za kitatanishi mara kadhaa zimekuwa zikimweka mwanasiasa huyo matatani. Kauli za namna hiyo ndiyo zinazohusishwa sana na kukosa urais kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Cleopa Msuya mwaka 1995 ambaye wakati akiwa Waziri wa Fedha huko nyuma aliwahi kuwaambia Watanzania kuwa; "Kila Mtu Atabeba Mzigo wake."&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Iwapo CCM italazimika kuwapima wagombea wake, kwa mantiki ya ustahimilivu wa kauli zao, basi wagombea kama Malecela, Iddi Simba na Frederick Sumaye wanaweza wakajikuta katika wakati mgumu kwani 'jeuri ya kauli' zao inaweza ikawa kaburi la wao kushindwa kuteuliwa wagombea urais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akiwa Makamu Mwenyekiti wa CCM, machoni mwa wapinzani wa chama hicho na hata wana CCM wenzake Malecela anaonekana kuwa ni mtu anayeweza kutoa kauli zisizotarajiwa na kutatanisha ambazo mara kadhaa zimekuwa vigumu kuelezwa kuwa ni za chama au zake binafsi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hiyo haitoshi, Malecela pengine kutokana na kuwa na kauli tata, kulimfanya hata Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kumlazimisha Rais Mwinyi amuondoe katika nafasi ya uwaziri mkuu kutokana na kutokuwa na msimamo katika suala la muungano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kutumia falsafa hiyo ya Mwalimu, Salim na Kikwete wameshaweka bayana suala hilo kwamba wao watadumisha muungano iwapo watateuliwa kuwa wagombea urais huku Kikwete akienda mb&lt;br /&gt;ali zaidi kwa kusema; "Kiongozi bora ni yule aliye na msimamo thabiti katika mambo ya msingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya wagombea Dk. Salim, Kikwete na Malecela, yuko Frederick Sumaye ambaye kikubwa anachojivunia ni kukaa kwake muda mrefu katika nafasi ya uwaziri mkuu kuliko mwanasiasa mwingine yoyote katika historia ya taifa hili tangu mwaka 1961. Sambamba na hilo, Sumaye anaringia mafanikio ya serikali ya Mkapa, na mwenyewe anajijumuisha kuwa sehemu ya mafanikio hayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jambo la tatu, kama ilivyo kwa Malecela pengine, Sumaye ndiye kiongozi ambaye katika kipindi cha miaka 10 sasa jina lake limekuwa likisikika zaidi kuliko mtu mwingine yoyote. Amesikika kwa mabaya na mema. Amekuwa katika ziara mikoani, amepigwa picha akiwa katika shughuli mbalimbali ziwe ni za kuweka jiwe la msingi au kuchangisha fedha. Amekuwa kiongozi wa shughuli za bunge kwa miaka yote hiyo. Kukisika kusikokoma ndiyo sifa yake kuu, amejenga wapambe na maadui, na sasa anagombea urais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sumaye ameingia katika orodha ya mawaziri wakuu waliowahi kugombea urais huko nyuma; Amefanya kile alichofanya, Rashid Kawawa (alitajwa 1985), Cleopa Msuya (1995), Joseph Warioba (1995) na John Malecela (1995). Wote hao walishindwa, yeye anaweza akabadili historia. Asingegombea watu wangemshangaa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya sana kwake, yeye ndiye mgombea mwenye tuhuma nyingi dhidi yake. Anafuatiwa kituhuma na Iddi Simba, Mark Mwandosya na baadaye John Malecela. Kama walivyofanya wenzake hao, Sumaye amezikanusha tuhuma zote hizo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Iwapo wana CCM wataamua kuzingatia sifa za mtu wa kuteuliwa kuwa Rais kwa tiketi ya chama hicho zilizotolewa na Mwalimu Nyerere mwaka 1995 aliposema "Mke wa Mfalme aliachwa kwa tuhuma tu" basi nafasi ya Sumaye na wenzake hao kuteuliwa kugombea wakati kuna wengine wenye sifa na wanaoonekana kuwa safi itakuwa finyu kweli kweli. Hata hivyo hilo si la kulitilia maanani sana, kwani CCM imempuuza Mwalimu katika mengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kapu moja watawekwa wagombea wengine. Wa daraja la juu atakuwa Dk. Abdallah Kigoda, mwanasiasa asiyeeleweka sana nje ya CCM, ingawa ndani ya chama hicho anaonekana kuwa na historia ndefu, akianzia katika Umoja wa Vijana na kuwa miongoni mwa wajumbe wa sekretarieti ya chama hicho kwa miaka kadhaa sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Usomi wake unamweka katika kundi la wasomi wengine kama, Prof Mark Mwandosya, wanataaluma waliojitosa katika siasa, ingawa uzoefu wake unaonekana kumwacha mbali kiasi mwenzake ambaye anaonekana kuwa mgeni sana ndani ya CCM.           &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anamwacha mbali sana Mwandosya ambaye amekuwa mbunge kwa takriban miaka 10 sasa, na mjumbe wa NEC kwa miaka isiyozidi mitano. Iwapo falsafa ya huyu ni mwenzetu itafanya kazi kama ilivyokuwa ikifanya kazi zama zile, wahafidhina wa ndani ya chama hicho watahoji; 'ametokea wapi mtu huyu?' Hata hivyo alichosema Mwinyi miaka kadhaa iliyopita kwamba; 'Kila Zama na Mambo Yake' kinaweza kikatokea, na lile lililoshindikana siku zilizopita likawezekana leo. Tusubiri tuone. Itaendelea Jumapili ijayo kwa kuangalia nafasi za wagombea wengine.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-114603248761859954?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/114603248761859954/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=114603248761859954&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603248761859954'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114603248761859954'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2006/04/urais-sifa-uwezo-hoja-au-haiba.html' title='Urais: Sifa, uwezo, hoja au haiba?'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114596812829747860</id><published>2006-04-25T05:04:00.000-07:00</published><updated>2006-04-25T05:28:48.320-07:00</updated><title type='text'>Rushwa yamweka Kikwete katika mtego uliomnasa Mkapa</title><content type='html'>KWA mara ya kwanza tangu aingie madarakani Desemba 21 mwaka jana, Serikali ya Awamu ya Nne inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete imeingizwa katika mtihani mkubwa wa kuamua suala la kimsingi linaloweza likatoa taswira halisi ya mustakabali wake wa kiuongozi katika kipindi cha miaka minne na ushee ijayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa namna yoyote ile habari kwamba, viongozi waandamizi katika serikali hiyo, wakiwamo mawaziri watatu na naibu waziri mmoja ni mmoja wa vigogo wanaohusishwa kutajwa katika ripoti ya siri inayowahusisha watu 30 iliyowasilishwa serikalini mwaka 1996, ni suala litakalomuumiza kichwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kikubwa katika ripoti hiyo ambayo imetokana na vyanzo vya kuaminika, watu wanaotuhumiwa kujihusisha na ufisadi si tu kwamba wametajwa kwa majina, bali pia tuhuma zao zimekwenda sambamba na vielelezo vingine kadhaa vinavyohusisha akaunti zao za fedha katika benki za ndani na nje ya nchi na watu waliohusika na uingizaji wa fedha hizo chafu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya mawaziri, wengine wanaotajwa kuhusika katika tuhuma mbalimbali za ufisadi ambazo iwapo vyombo vya sheria vitathibitisha kuwa ni za kweli zinaweza kubadili kabisa sura ya vita dhidi ya rushwa ni makatibu wakuu, watendaji wengine wakuu katika asasi za umma na wafanyabiashara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika ripoti hiyo ya siri ambayo taarifa zinaihusisha na kazi iliyofanywa na Tume ya Rais ya Kuchunguza Mianya ya Rushwa iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba, inawataja pia baadhi ya viongozi wa juu wastaafu katika serikali zote mbili za Tanzania na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar na makada maarufu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao miongoni mwao bado ni maafisa wa juu wa chama hicho tawala.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo habari hizo zilipoanza kuandikwa na gazeti la Mwananchi, Jaji Warioba mwenyewe alikana kuwasilisha majina ya watuhumiwa wa rushwa serikalini, ingawa katika barua ya kuwasilisha ripoti yake kwa rais anakiri kuwasilisha majina ya watuhumiwa waliotajwa na wananchi kwenye vyombo vya dola. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na Serikali ya Awamu ya Nne na hususan Rais Kikwete mwenyewe kutamka mara kadhaa kuhusu dhamira yake ya dhati ya kupambana na rushwa kubwa inayohusisha wakubwa, hakuna kiongozi yoyote wa ngazi ya juu serikalini aliyetoa taarifa rasmi ya ama kukiri kuwapo kwa taarifa ya namna hiyo au la.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukimya huo wa serikali hata hivyo hauwezi hata kidogo ukafuta maneno yenye ujumbe mzito ambayo yamekuwa yakitolewa na Rais Kikwete kuhusu rushwa tangu alipoingia madarakani zaidi ya siku 100 zilizopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mara ya kwanza katika kauli rasmi akiwa madarakani, Kikwete aliahidi kupambana na rushwa Desemba 30, wakati alipolihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano mjini Dodoma, akirejea kile alichokisema mwanzoni mwa mwaka jana, siku alipotangaza azma yake ya kugombea urais kupitia CCM huko Kibaha mkoani Pwani alipokaririwa akisema: "Tutapambana na rushwa kwa Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya."&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akizungumza kuhusu tatizo hilo, katika hotuba yake hiyo, Rais Kikwete alisema: “Tutaongeza kasi ya kupambana na rushwa kisayansi kwa kushambulia kiini chake na kuziba mianya yake.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mara kadhaa baadaye, Kikwete amekuwa akiendelea kuahidi kukabiliana na rushwa kwa nguvu mpya hata kufikia hatua ya kusema kwamba ameitaka Taasisi ya Kupambana na Rushwa (PCB) kuwasilisha kwake majina ya vigogo ambao wataonekana kuwa ni wazito kwao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sehemu pekee ambayo Kikwete alionyesha kupatwa na kigugumizi katika vita dhidi ya rushwa ilikuwa ni wakati alipohutubia Mjini Sumbawanga, mkoani Rukwa siku moja tu baada ya kufungua mkutano wa PCB iliofanyika Mbeya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siku hiyo Kikwete alitamka hadharani kuwajua kwa majina walarushwa na akasema ameamua kutochukua hatua yoyote dhidi yao lengo lake likiwa ni kuwapa muda zaidi wa kujirekebisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kauli yake hiyo, Kikwete kwa maneno mengine alithibitisha kuwa na orodha ya siri ya majina ya walarushwa, ingawa hadi hivi sasa si rahisi kujua iwapo majina hayo ndiyo yale yale yanayojumuisha vigogo 30 ambao Mwananchi Jumapili imeyaona majina yao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo hadi hivi sasa, si rahisi kusema kwa uhakika kabisa ni hatua gani Rais Kikwete atachukua dhidi ya watuhumiwa wa rushwa hasa baada ya kubaini kwamba baadhi yao wako ndani ya serikali yake na wengine ndani ya chama ambacho anatarajia kuchukua jukumu la uenyekiti wa chama hicho kuanzia Juni mwaka huu wakati Mwenyekiti wa sasa, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, atakaostaafu rasmi wadhifa huo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jambo pekee ambalo limeanza kujenga mazingira ya wasiwasi kuhusu kuwapo kwa uwezekano wa kukwama kwa vita dhidi ya rushwa hivi sasa ni yale madai ya viongozi wa serikali kutaka ushahidi kabla ya kuwawajibisha watuhumiwa, jambo ambalo ndilo lililokwamisha kwa kiwango kikubwa vita ya namna hiyo iliyotangazwa na Mkapa wakati alipoingia madarakani mwaka 1995.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Philip Marmo bungeni mjini Dodoma Aprili 4, mwaka huu kuhusu suala hilo la ushahidi ni kielelezo kingine kinachotia doa vita dhidi ya rushwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akijibu swali la Mbunge Hamad Rashi Mohamed (Wawi-CUF) aliyetaka kujua hatua ambazo serikali itazichukua dhidi ya watu ambao majina yao yalitolewa na Tume ya Jaji Warioba, Waziri Marmo alisema: &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;"Ni kweli Serikali ya Awamu ya Tatu iliundwa tume inayojulikana kama Tume ya Joseph Warioba na Serikali iliifanyia kazi ripoti ya tume hiyo kikamilifu na ndiyo maana leo tunaongea kuhusu miaka 10 ya jinsi ambavyo Tume ya Kuzuia Rushwa imejipanga vizuri.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;"Orodha ya waliokuwa wakishukiwa ni wapokea rushwa wakubwa ilipokewa na hata sasa bado kuna orodha kama hiyo. Mheshimiwa Spika, lakini ni kitu kimoja kuwa na orodha na kutia mashaka watu wanaopokea rushwa, lakini ni kitu kingine kabisa kujenga hoja ya kufungua kesi mahakamani, kesi ambayo una hakika utashinda.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;"Utaratibu wetu wa kisheria ni kwamba anayeshitaki lazima athibitishe kweli kweli ili kumtia mtu hatiani na masuala haya ya rushwa mnavyofahamu siyo rahisi kuthibitisha kabisa kabisa kwamba mtu ana hatia. Ndiyo maana  pamoja na kuwa orodha inaonekana, ni vigumu kuwapeleka mahakamani  watu kama hao. Kwa wale ambao Serikali ina uwezo nao huwa inachukua hatua za kinidhamu kama vile kuwastaafisha kwa manufaa ya umma..." alisema Waziri Marmo katika majibu yake ambayo yanapatikana katika kumbukumbu za Hansard za Bunge.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-114596812829747860?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/114596812829747860/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=114596812829747860&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114596812829747860'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114596812829747860'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2006/04/rushwa-yamweka-kikwete-katika-mtego.html' title='Rushwa yamweka Kikwete katika mtego uliomnasa Mkapa'/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114502389737481053</id><published>2006-04-14T07:01:00.000-07:00</published><updated>2006-04-14T07:11:37.390-07:00</updated><title type='text'></title><content type='html'>&lt;a href="http://photos1.blogger.com/blogger/4909/992/1600/KIbanda%20Pics%20new.0.jpg"&gt;&lt;img style="float:right; margin:0 0 10px 10px;cursor:pointer; cursor:hand;" src="http://photos1.blogger.com/blogger/4909/992/200/KIbanda%20Pics%20new.jpg" border="0" alt="" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/11968291-114502389737481053?l=absalomkibanda.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/feeds/114502389737481053/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=11968291&amp;postID=114502389737481053&amp;isPopup=true' title='4 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114502389737481053'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/11968291/posts/default/114502389737481053'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://absalomkibanda.blogspot.com/2006/04/blog-post_114502389737481053.html' title=''/><author><name>Absalom Kibanda</name><uri>http://www.blogger.com/profile/17995968711079164378</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='21' src='http://2.bp.blogspot.com/_1lNMnqlahLM/SSGHhPKW7QI/AAAAAAAAAAo/_dNVzUSb2Gk/S220/DSC_0396.JPG'/></author><thr:total>4</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-11968291.post-114449020770045348</id><published>2006-04-08T02:51:00.000-07:00</published><updated>2006-04-08T02:56:47.716-07:00</updated><title type='text'>Mbona polisi wanashindwa kukamatana?</title><content type='html'>JESHI la Polisi limeanzisha mkakati kabambe wa kukabiliana na watu wanaotuhumiwa kuhusika na vitendo vya kufadhili na kuwalinda majambazi likiwalenga wafanyabiashara wakubwa huku kukiwa hakuna afisa yeyote wa juu wa polisi aliyetajwa waziwazi kuhusika katika vitendo hivyo vya uhalifu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uchunguzi uliofanywa unaonyesha kwamba, tangu jeshi hilo lianze kamatakamata ya vigogo wanaotuhumiwa kuwafadhili na kuwalinda majambazi kwa siku kadhaa sasa, walengwa wakuu wamekuwa ni wafanyabiashara tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kamatakamata hiyo ya wafanyabiashara ambayo tayari imekwisha kutolewa maelezo katika mikoa ya Kilimanjaro, Dar es Salaam na Manyara haijawahusisha maafisa wa jeshi la polisi ambao kwa muda mrefu ndiyo wamekuwa wakilalamikiwa kuwalinda hao wanaoonekana kuwa ni wafadhili wa majambazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitendo cha kutokuwapo kwa taarifa zozote za ama kuhojiwa au kusimamishwa kazi kwa afisa yeyote wa juu wa polisi hadi hivi sasa ni moja ya ushahidi wa wazi kwamba, jeshi hilo limeamua kujisafisha machoni mwa jamii kwa kuwageuzia 'kibao' wafanyabiashara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya hilo hata mabadiliko makubwa ya Makamanda wa Polisi wa Mikoa (Ma-RPC) yaliyotangazwa jana na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Saidi Mwema bado hayajatoa jibu la iwapo wale waliotajwa katika tuhuma za ujambazi watachukuliwa hatua zozote za kisheria au watakwenda makao makuu ya jeshi hilo kama ambavyo imekuwa ada ya miaka nenda miaka rudi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukio la hivi karibuni kabisa la kumhamishia aliyekuwa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar es Salaam,  Abdallah Zombe baada ya polisi wake kadhaa kutuhumiwa kuua raia wasio na hatia wakati akiwa madarakani, ni ushahidi mmoja unaoondoa matumaini yoyote ya kuchukuliwa kwa hatua zozote kwa wengine watakaokutwa na tuhuma mbalimbali.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikumbukwe kwamba, tangu kuanza kwa kamata kamata hiyo viongozi wakuu wa kiserikali na wale wa polisi wakiwamo Rais Jakaya Kikwete, Waziri wa Usalama wa Raia, Bakari Mwapachu na Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Alfred Tibaigana, wamekiri kwamba hatua za kuwakamata baadhi ya watu kwa tuhuma za ujambazi zimetokana na majina ambayo yamekuwa yakiwasilishwa kwao kwa siku kadhaa sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Februari Mosi mwaka huu, Waziri Mwapachu alithibitisha kwamba, alikuwa amepokea majina ya vigogo 20 wa polisi ambao walikuwa wakitajwa kuwalinda majambazi na wengine wakituhumiwa kuhusika na mtandao wa ujambazi nchini na nchi za jirani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tangu Mwapachu ambaye katika maelezo yake hayo aliahidi kulifanyia kazi suala hilo, ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua vigogo hao atoe ufafanuzi huo, hakuna dalili zozote ambazo zimeonyesha bayana kuwako kwa ofisa yeyote wa juu wa polisi aliyekamatwa, kusimamishwa kazi au hata kuhojiwa kwa sababu hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakizungumza hivi karibuni Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Zelothe Stephen na mwenzake wa Mbeya, Suleiman Kova, walieleza kwamba walikuwa hawajapata maelekezo kutoka makao makuu yaliyokuwa yakiwaelekeza kuwafanyia uchunguzi polisi waliokuwa wakihusishwa na vitendo hivyo vya uhalifu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata baada ya gazeti hili kumweleza Zelothe kwamba, kulikuwa na taarifa za mmoja wa maafisa wake wa juu kutajwa kuhusika katika vitendo vya kuwalinda majambazi, kamanda huyo alisema alikuwa anasubiri maelekezo kabla ya kuchukua hatua yoyote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande wake, Kova alifikia hatua ya kusisitiza kwamba, katika mkoa wake, tayari operesheni ya kuwashughulikia na kuwachukulia hatua za kinidhamu polisi wote waliokuwa wakienda kinyume cha maadili ya kazi zao zilikuwa zimechukuliwa muda mrefu na hivyo kutokuwapo kwa polisi yeyote aliyekuwa akikabiliwa na tuhuma za namna hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya hilo, kuanza kutoweka kwa matumaini ya kuchukuliwa kwa hatua zozote dhidi ya maafisa wa juu wa polisi kwa hivi sasa kumetiwa chachu na kauli ambazo zimetolewa na Rais Kikwete mwenyewe hivi karibuni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akizungumza katika hafla maalum ya kumuaga aliyekuwa Mkuu wa jeshi hilo, Omari Mahita na kumkaribisha mrithi wake, Saidi Mwema, Rais Kikwete alilisifu jeshi hilo kwa kusema alikuwa na imani nalo na kwamba kulikuwa hakuna jeshi mbadala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya hilo, Kikwete alitumia muda mrefu kumsifu na kumfariji Mahita kwa kile alichokielezea kuwa ni utumishi wake mzuri na akaahidi kuendelea kuwatumia polisi hao hao katika kuliongoza jeshi hilo na si vinginevyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli ya Kikwete ambayo iliitoa siku chache tu baada ya kuwapo kwa mawazo kwamba, angemteua mkuu mpya wa jeshi hilo kutoka nje ya polisi kama ilivyofanyika katika nchi za Uganda na Kenya ambako wakuu wa polisi ni wanajeshi, kwa namna moja ilionyesha kuwapa nguvu zaidi maafisa wa juu wa jeshi hilo ambao tuhuma dhidi yao zilionekana kuwalemea. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mara ya kwanza Kikwete 'aliwalinda' polisi wakati alipozungumza na wazee wa Dar es Salaam mwishoni mwa Januari mwaka huu, alipoeleza bayana kwamba alikuwa na imani na jeshi hilo na hivyo kuthibitisha kwa mara ya kwanza kwamba, kulikuwa na uwezekano mdogo kwa serikali kuwachukulia hatua za kinidhamu baadhi ya maafisa wa juu wa jeshi hilo wanaohusishwa na vitendo vichafu vya uhalifu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali ya hilo, Kikwete mwenyewe na Mwapachu kwa nyakati tofauti walipokutana na maafisa wa juu wa jeshi hilo wamekuwa wakiwaasa kulifanya marekebisho jeshi hilo kwa lengo la kuwarejeshea imani wananchi, kauli ambazo aghalab zinaonyesha kwamba, serikali imenawa mikono kwa polisi na kuwaacha wenyewe wajisafishe. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati polisi wakifanya kile waswahili wanasema "funika kombe mwanaharamu apite", hivi karibuni baadhi ya askari polisi kutoka mkoani Mwanza walimwandikia b
